Dilunga
JF-Expert Member
- Apr 8, 2009
- 679
- 52
- Unaona ulivyo nje ya mstari yaani mtu anayeliwpa dola elfu 20 bongo eti hawezi kwenda tibiwa majuu, mkuu sometimes unachekesha sana, watu wanalipwa dola elfu tatu tu kwa mwezi na wanakwenda kutibiwa majuu, itakwua $ 20,000?
Angalia sasa ulivyo changanya data. Nimeongelea mshahara wa 20,000 kwa mwaka, wewe unanichanganyia habari za $3,000 kwa mwezi.
Yule mchangiaji Icadon amedhani mshahara wa $ 20,000 unatosha kumudu gharama za matibabu Marekani. Haku specify $ 20,000 kwa wiki, mwezi, saa, wiki mbili, siku, hivyo huwa inachukuliwa kwamba unaongelea kwa mwaka. Sasa mshahara wa $ 20,000 kwa mwaka utamudu matibabu Marekani? Marekani ya wapi hiyo? Kama unalipwa $ 20,000 kwa mwaka na una familia basi unahitaji pango la serikali, sehemu ya nane, na lishe ya serikali, stempu ya chakula. Achilia mbali gharama za afya.
Na hiyo hoja ya kwamba umeishi maisha ya mipakani mwa nchi duniani haimaanishi kwamba ulikaa ukaelewa maisha yanavyokwenda huko. Umeharibu vibaya vibaya kutoa ushauri potofu kwamba atakae rudi Bongo ahakikishe amechonga channel za kwenda kutibiwa nje. Channel gani, kutumia kadi za bima za watu? Si wote wanaweza au kutaka kuwa Mponjoli au Escobar. Yana umri wake yale mambo mzee, utaenda utaisha.
Unaandika kwenye kurasa zinazosomwa na watu kila pande ya dunia, unachosema kihakiki. Afya si rahisi kule.