Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
Sisi ni waoga sana wa kujijenga kifikra na kutafakari mambo. Hatupendi kujiuliza maswali mpaka tufike mwisho wa kuuliza na balbu ituwakie tujitambue.
Tunapenda kufanya delegation ya kila kitu.
Tuna wachumi wakutosha wanaoweza kutuliangalia taifa na kufanya mipango inayoendana na Sera na hata Ilani. W anachohitaji ni motisha na changamoto kubuni mfumo mizuri wa uchumi iwe ni kwenye kilimo, ufugaji, uvuvi, viwanda vidogo na hata vikubwa: processing and manufaturing na kwa sekta zote, binafsi na zilizo chini ya serikali.
Lakini badala ya kufanya empowerment na hata kutoa imani na kuwaamini wachumi wetu, tunathamini tafiti, tathmini na mapendekezo ya watu wasio Watanzania, wasio na mahusiano ya karibu na jamii kwa kuelewa kwa mapana na marefu maisha, tabia na mifumo yetu ya asili.
HIi peke yake inaweza kuwa ni Sera ya kuwawezesha wazawa.
Lakini kwa kuwa tafsiri na mtazamo wetu uko kwenye kumpa mtu cheo, fedha au dili, hatuoni sababu ya kuanza kuangalia ni jinsi gani wataaluma na wataalamu wa nyumbani wanavyoweza kutumika kujenga mfumo imara wa uchumi, uzalishaji, elimu, afya bila usiasasiasa na kujuanajuana.
Leo tukikaa chini na kufunguka na kuanza kuulizana the 6 to 8 why's on why Ujamaa na Kujitegemea vilitushinda au Azimio la Arusha, utakuta wengi wataishia why ya 2 au 3, na kuanza kunyoosha vidole vya lawama au kutoa sababu na si kurudi kwa undani mpaka tuweke orodha nono ya mambo yaliyosababisha Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea ishindwe na tukaleta mapinduzi mapya ya Azimio la Zanzibar ambalo kipaumbele kimekuwa ni kujenga uchumi kwa kutegemea FDI na mikopo.
Kwa upinzani, wanachoweza kuhubiri mpaka waingie ikulu na kupimwa ni Sera na ahadi ambazo ni mpaka wazifanyie kazi, ndipo wananchi tunaweza kusema sera zao hazikuleta manufaa.
Lakini kutokuwa madarakani , hakuunyimi ukawa kujiandaa vizuri kuwa wepesi kuingia madarakani na kuanza implementation.
I would hope kuwa sasa hivi regardless ya matokeo, kuna jopo la wataaluma na wataalamu wa kila sekta na nyanja katika ukawa wakisuka vizuri sera zao collectively na kuonyesha mshikamano wa kuongoza nchi kwa ufanisi na si kuanza kubabaika tena kama suala la mgombea urais na wagombea udiwani na ubunge lilivyokuwa.
Tunapenda kufanya delegation ya kila kitu.
Tuna wachumi wakutosha wanaoweza kutuliangalia taifa na kufanya mipango inayoendana na Sera na hata Ilani. W anachohitaji ni motisha na changamoto kubuni mfumo mizuri wa uchumi iwe ni kwenye kilimo, ufugaji, uvuvi, viwanda vidogo na hata vikubwa: processing and manufaturing na kwa sekta zote, binafsi na zilizo chini ya serikali.
Lakini badala ya kufanya empowerment na hata kutoa imani na kuwaamini wachumi wetu, tunathamini tafiti, tathmini na mapendekezo ya watu wasio Watanzania, wasio na mahusiano ya karibu na jamii kwa kuelewa kwa mapana na marefu maisha, tabia na mifumo yetu ya asili.
HIi peke yake inaweza kuwa ni Sera ya kuwawezesha wazawa.
Lakini kwa kuwa tafsiri na mtazamo wetu uko kwenye kumpa mtu cheo, fedha au dili, hatuoni sababu ya kuanza kuangalia ni jinsi gani wataaluma na wataalamu wa nyumbani wanavyoweza kutumika kujenga mfumo imara wa uchumi, uzalishaji, elimu, afya bila usiasasiasa na kujuanajuana.
Leo tukikaa chini na kufunguka na kuanza kuulizana the 6 to 8 why's on why Ujamaa na Kujitegemea vilitushinda au Azimio la Arusha, utakuta wengi wataishia why ya 2 au 3, na kuanza kunyoosha vidole vya lawama au kutoa sababu na si kurudi kwa undani mpaka tuweke orodha nono ya mambo yaliyosababisha Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea ishindwe na tukaleta mapinduzi mapya ya Azimio la Zanzibar ambalo kipaumbele kimekuwa ni kujenga uchumi kwa kutegemea FDI na mikopo.
Kwa upinzani, wanachoweza kuhubiri mpaka waingie ikulu na kupimwa ni Sera na ahadi ambazo ni mpaka wazifanyie kazi, ndipo wananchi tunaweza kusema sera zao hazikuleta manufaa.
Lakini kutokuwa madarakani , hakuunyimi ukawa kujiandaa vizuri kuwa wepesi kuingia madarakani na kuanza implementation.
I would hope kuwa sasa hivi regardless ya matokeo, kuna jopo la wataaluma na wataalamu wa kila sekta na nyanja katika ukawa wakisuka vizuri sera zao collectively na kuonyesha mshikamano wa kuongoza nchi kwa ufanisi na si kuanza kubabaika tena kama suala la mgombea urais na wagombea udiwani na ubunge lilivyokuwa.