Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,410
- 31,395
UTANGULIZI
Uchaguzi ni tukio la kidemokarasia la kuchagua au kuchaguliwa kupata watakaokupewa madaraka
Si tukio la kupata ''watawala'' bali viongozi watakaotumikia wananchi
Ni muhimu kuwajua wenye madaraka kwa hulka na tabia ,maono, na wanachosimamia kupitia vyama vyao tu
Ni haki kwa wananchi kuwajua wagombea nafasi mbali mbali kwa hulka, tabia,na wasifu .
Ni muhimu kujua ilani/sera walizopewa si kwa maandishi bali wanavyozitafsiri na kuzijengea hoja. Tutalitolea mfano mbele
Nchi masikini zinazokumbatia demokrasia ya kujfiunza tunachagua viongozi kama watu, kwa muonekano na ubabaishaji wao
Tawala za kiasili za machifu zilizingatia mrithi wa kiti kwa tabia, maono , unyenyekevu na sifa za uongozi.
Aghalabu, mrithi mtaraJiwa angeweza kuachwa kwasababu tu hakidhi vigezo na si kuwa ndiye mrithi anayefuata
Na wala si kwa Afrika tu, Uingereza ilishatokea mfalme ‘akaachia ngazi' (King Edward VIII 1936-Abdication)
Kwa Waafrika limekuwa tatizo. Tunaangalia mambo yasiyo na umuhimu kuliko tunayopaswa kuyatolea uamuzi kweye kura
Nchini, mijadala imetawaliwa na hisia, fitna, majungu n.k.
Tumeusahau ilani/sera zitakazotumika ‘kutusaidia au kutuhukumu' Mwisho tunavuta viti na majamvi tukilalamika.
Tuliowapa madaraka kwa upuuzi wetu wa ‘homeboy' au kabila,kanda na dini wanajilimbikizia
Mwishowe kutuporomoshea mitusi wanapo mnadi mlinzi wa malimbikizo anayefuata. Si wao ni sisi wajinga, hatukuangalia
Ni kwa msingi huo, tunaona umuhimu wa majadiliano kuhusu wagombea na ilanisera.
Bila kufanya hivyo tutarudi kujiuliza inakuwaje tuliwachagua wakiwa hawajui kwanini sisi ni masikini.
Tutajiuliza kwanini umasikini unatopea badala ya kupungua.
Tutabaki taifa mahiri la walalamikaji, na la wazembe wa kufikiri
Tunaangalia kwa fikra katika mabandiko yajayo
Inaendelea….
Uchaguzi ni tukio la kidemokarasia la kuchagua au kuchaguliwa kupata watakaokupewa madaraka
Si tukio la kupata ''watawala'' bali viongozi watakaotumikia wananchi
Ni muhimu kuwajua wenye madaraka kwa hulka na tabia ,maono, na wanachosimamia kupitia vyama vyao tu
Ni haki kwa wananchi kuwajua wagombea nafasi mbali mbali kwa hulka, tabia,na wasifu .
Ni muhimu kujua ilani/sera walizopewa si kwa maandishi bali wanavyozitafsiri na kuzijengea hoja. Tutalitolea mfano mbele
Nchi masikini zinazokumbatia demokrasia ya kujfiunza tunachagua viongozi kama watu, kwa muonekano na ubabaishaji wao
Tawala za kiasili za machifu zilizingatia mrithi wa kiti kwa tabia, maono , unyenyekevu na sifa za uongozi.
Aghalabu, mrithi mtaraJiwa angeweza kuachwa kwasababu tu hakidhi vigezo na si kuwa ndiye mrithi anayefuata
Na wala si kwa Afrika tu, Uingereza ilishatokea mfalme ‘akaachia ngazi' (King Edward VIII 1936-Abdication)
Kwa Waafrika limekuwa tatizo. Tunaangalia mambo yasiyo na umuhimu kuliko tunayopaswa kuyatolea uamuzi kweye kura
Nchini, mijadala imetawaliwa na hisia, fitna, majungu n.k.
Tumeusahau ilani/sera zitakazotumika ‘kutusaidia au kutuhukumu' Mwisho tunavuta viti na majamvi tukilalamika.
Tuliowapa madaraka kwa upuuzi wetu wa ‘homeboy' au kabila,kanda na dini wanajilimbikizia
Mwishowe kutuporomoshea mitusi wanapo mnadi mlinzi wa malimbikizo anayefuata. Si wao ni sisi wajinga, hatukuangalia
Ni kwa msingi huo, tunaona umuhimu wa majadiliano kuhusu wagombea na ilanisera.
Bila kufanya hivyo tutarudi kujiuliza inakuwaje tuliwachagua wakiwa hawajui kwanini sisi ni masikini.
Tutajiuliza kwanini umasikini unatopea badala ya kupungua.
Tutabaki taifa mahiri la walalamikaji, na la wazembe wa kufikiri
Tunaangalia kwa fikra katika mabandiko yajayo
Inaendelea….