Duru za siasa: Uchaguzi Mkuu USA

MJADALA WA emails UNAENDELEA KATIKA VYOMBO VYA HABARI

JE, DIR. COMEY AMEKIUKA HATCH ACT YA 1939?

Mjadala mpana kuhusu barua ya Dir Comey kwa bunge unaendelea.

Kinachojulikana ni FBI kupitia emails na kuona kama watufungua uchunguzi tena kwa maana kama kuna connections kati ya email hizo na zingine

Barua ya Comey haikueleza tatizo bali uwezekano emails hizo zikawa na uhusiano na uchunguzi alioufunga July. Tuweke series of events kwani kuna kuchanganya mambo

Baada ya FBI kufunga mjadala mwezi July kwa kusema kulikuwa na 'uzembe mkubwa' katika handling ya emails, Republican walikuja juu kwa kusema kwanini hakushtakiwa. Hili likazaa kauli ya 'rigged system'

Mwezi Sept kakawa na uchunguzi unaomhusu Anthony Weiner(congressman) ambaye alikuwa mume wa Huma Abiden. Huma amefanya kazi na Clinton kwa miaka 20 na huitwa 'mtoto' wa pili wa familia ya Clinton

Uchunguzi wa Weiner ulihusisha ufuska wake kwa binti wa miaka 16.

Kwa mantiki hiyo uchunguzi huo haukuhusu emails za Clinton au Huma.

Wachunguzi walichukua Laptop na kubaini emails za Huma,mkewe Anthony zinazohusiana na zile za Clinton kwa maana huenda hazikupitiwa wakati wa uchunguzi
au ni duplicate ya zile zilizopitiwa

Wachunguzi wakamtaarifu Dir ambaye taarifa hizo kuanzia October mwanzoni.

Dir Aliwasiliana na idara ya sheria (DOJ) kuhusu kuandika barua kwa congress , jambo aliloshauriwa si jema

Majuzi kaandika barua ambayo haina details ikisema kuna au kutokuwa na tatizo

Democrat wamekuja juu kwasababu uchunguzi wa awali ulifanyika ili usivunje kanuni kuwa ndani ya siku 60 kusiwepo na uongiliaji wa uchaguzi.

Republican wanasema uchunguzi uwekwe wazi wakimsifu Comey

Katika kanuni hiyo, kuna sheria ya mwaka 1939 inayojulikana kama Hatch Act,

Sheria hiyo inazuia wafanyakazi wa 'executive branch' ya serikali kutoingilia uchaguzi kwa misaada, ahadi n.k.

Sheria hii imefanyiwa amendment lakini huo ndio msingi wa kuanzishwa kwake.

Wapo watakouliza, kwanini Obama, Biden na viongozi wengine wanapiga kampeni?

Well, Hatch Act imewasemehe Rais , Makamu na baadhi ya viongozi wa executive branch

Ikumbukwe first lady hana role yoyote katika federal au chama!!!

Sheria inawabana wafanyakazi wa federal wanaoweza kutumia ushawishi ku influence uchaguzi!
Utaona mawaziri wa serikali akiwemo secretary of state wamekaa mbali.

Swali linakuja katika timbwili Hatch act imekuwa violated AU Comey yupo sahihi?

Tunatajadili bandiko lifuatalo
 
Mwalimu wangu kuna issue nyingine mbich imeingia, Kumbe 'mama' alipewa majibu ya mtihani ili afaulu kwa alama za juu kwenye debate. Kutokana na hili CNN wamelazimika kumtimua aliyevujisha mtihani...! Obama yawezekana alikuwa sahihi kipindi kile cha 2008 kuwa huyu mama ni weak, na dhani hata Trump anaweza kuwa sahihi kuwa HRC ni 'krukudi'.

Brazile out at CNN after WikiLeaks reveals she gave debate questions to Clinton camp
 
COMEY NA HATCH ACT

Ipo hoja kuwa FBI kama federal bureau ipo huru, lakini pia ni chombo kilichopo chini ya DOJ(Dept of justice)
DOJ wameomba search warrant ya emails za Huma.

Kumbuka, wanaomba search warrant kwasababu uchunguzi haukuwa kwa Huma bali Weiner, na wamepata

Hatch act ukiisoma kwa undani inaeleza kinachotazamwa si maadili ya mtumishi wa federal kuhusu kuingilia uchaguzi bali nia au kusudio 'intent' ya kutenda hivyo

Kama Comey alilenga kuitaarifu kamati ya bunge bila madhumuni mengine, hapo hajakiuka sharia ya Hatch act.

Tatizo lililopo ni kuwa kuna kanuni ya kutoingilia uchaguzi katika muda fulani je, kanuni hiyo imesimamiwa?

Na itawezekanaje kwa upande wa Dem kuamini kuwa hakuna nia au kusudio baya ili hali wanaona jinsi inavyoleta madhara kwa upande wao, au itakavyoathiri uchaguzi kwa upande wao?

Nia na kusudio haviwezi kujulikana kwasababu aliyefanya ni Comey na ndiye anajua kama ilikuwa kwa nia njema au nia njema inayotafsiriwa vibaya au nia mbaya

Issue inakuwa ngumu pale ambapo barua hiyo inaonekana kutokuwa na details za nini kimeonekana.

Hoja inayotawala hapa ni kuwa Comey kavunja kanuni nyingine ya FBI ambayo inatamka uchunguzi kutowekwa wazi hadi pale panapokuwa na hitimisho

Barua ya Comey haina hitimisho, je, ilikuwa sahihi kuitoa hadharani ikieleweka inaweza kubadili mwenendo wa uchaguzi katika siku 10 zilizobaki?

Dir Comey anajikuta mahali pagumu kwani anatakiwa , kwanza, aeleze kama hajakiuka kanuni ya siku 60 kutoingilia uchaguzi. Pili, kama hajawa na kusudio baya au alikuwa na kusudio jema katika siku 10 za uchaguzi

Tatu, Dem na GOP kwa pamoja wamemtaka aweke wazi nini alichoona. Hapa kuna sehemu kadhaa
1. Je, ataweza kufanya hivyo siku 8 zilizobaki? Kwamba itakuwa ni sahihi kufanya hivyo hata kama ana ushahidi?
2. Matokeo yakionyesha Clinton ana makosa, uchaguzi ulioanza utafutwa?
Au Ataliacha suala hili hadi uchaguzi uishe? T
rump akishinda, Comey atahusishwa na kushindwa Dem. Clinton akishinda Comey atahusishwa na 'rigged system''

3. Kwa assumption kuwa Clinton atashinda, je, kitakachofuata ni impeachment? ikibainika kuna makosa?

4. Kama ikitokea emaila hazina kitu kigeni kuliko kilichoelezwa July, Comey ataeleza nini kuhusu 'interference'?

Huu ndio mtazamo kwa sasa na huenda mambo yakabadilika kutokana na muda

Tutaendelea kufuatilia
 
Mkuu nguruvi3 me nashangaa unapata shida ya nn hapa..! James comey yuko sahihi kwa sababu bi clinton akipatikana na makosa,kosa lake ni la kijinai. Hiyo sheria ya hatch act ingawa sijaisoma lkn kwa vyovyote haiwezi kuzuia makosa ya kijinai kuchunguzwa hata km ni ndani ya siku 60 zilizotajwa.

Lkn lingine mkuu Nguruvi3 HC hatakiwi marekani, hili limefanyika ili kupunguza hayo makali yake ili iwe Rahisi kwa trump kushinda bila mizengwe! National poll kwa sasa ni :Clinton 46%+1 na trump 45. Mpaka jtano naamini trump ataongoza mpaka siku ya uchaguzi yenyewe!!!
 
Mkuu nguruvi3 me nashangaa unapata shida ya nn hapa..! James comey yuko sahihi kwa sababu bi clinton akipatikana na makosa,kosa lake ni la kijinai. Hiyo sheria ya hatch act ingawa sijaisoma lkn kwa vyovyote haiwezi kuzuia makosa ya kijinai kuchunguzwa hata km ni ndani ya siku 60 zilizotajwa.

Lkn lingine mkuu Nguruvi3 HC hatakiwi marekani, hili limefanyika ili kupunguza hayo makali yake ili iwe Rahisi kwa trump kushinda bila mizengwe! National poll kwa sasa ni :Clinton 46%+1 na trump 45. Mpaka jtano naamini trump ataongoza mpaka siku ya uchaguzi yenyewe!!!
Mkuu suala la kupata tabu linatoka wapi?

Nimeeleza tangu mwanzo, hatuna influence yoyote kwa uchaguzi wa Marekani na tupo takribani km 13,000 kutoka sanduku la kura, kwanini unadhani tunapata tabu na ili iweje!

Nadhani hujafuatilia nyuzi hii kwa undani na nyingine zilizotangulia.

Dhima yetu si jingine bali kujadiliana katika upana na kuweka scenario na perspective mbali mbali ili wasomaji waokote kimoja au viwili. Hilo tu

Mathalan, hukujua Hatch act na sasa unaweza kufuatilia na kuijua ili kesho ukija utupe kile tusichokiona au kile unachokiona tofauti. Hivyo ndivyo mijadala inavyokuwa.

Mbona hatukupata tabu kueleza process nzima ya uchaguzi wa Marekani kuanzia primaries hadi sasa?

Pengine kwa kutoangalia mambo kwa upeo mpana, na kuongozwa kwa ushabiki kuliko hoja, tayari unasema kuna 'criminal offense' Hebu tueleze chombo gani kimesema hayo?

Lini investigation ikawa 'crime' na hayo ndiyo aliyosema Comey?

Jiulize kama ni simple hivyo, kwanini vyombo vyote Marekani vimegeuza Comey kuwa subject?

Sasa kama Trump au Clinton hatakiwi US hayo ni maoni yako na tunayaheshimu, siyo facts

Ukisoma mabandiko mawili hapo juu, hakuna mahali nimesema Comey yupo wrong.
Zipo sehemu nimeuliza, na hiyo ni njia ya kuleta fikra kwa msomaji bila kumwekea maoni.

Ni vema kama ungalikuja na 'rebuttal' ukishambulia hoja moja hadi nyingi kwa mtazamo na faida yetu sote

Sipendi kabisa kusema haya baadhi wameeleza kwa lugha laini, lakini tulipofikia pengine ni muhimu kusema. Nadhani upo katika wrong forum

Ahsante
 
FBI HAWATATOA TAARIFA YA UCHUNGUZI KARIBUNI

Duru za habari zinaeleza kuwa Dir Comey hataongea kuhusu suala la email hadi hitimisho la uchunguzi
Hili nalo limezidi kutengeneza mazingira ya mjadala kwa maana kuwa kwanini alitoa taarifa na sasa hawezi

Barua aliyoandika imeleta mjadala mkubwa kwa umma. Mwanasheria wa zamani wakati wa G.Bush Jr Bw Gonzalez amekaririwa na kituo cha TV akisema hilo halikuwa sahihi kama ambavyo Eric Holder naye alivyosema

Hawa hawakuzungumzia hatua za Comey, walichosema barua ipo 'vague' kwani haina details zozote
Barua ya Comey ilipelekwa kwa house comm Republican huku Minority leader akisikia katika vyombo vya habari

Duru zinaseama uchunguzi hauwezi kukamilika hadi uchaguzi upite. Kinachofanyika sasa na FBI Virginia ni kwanza, kupata access na hilo linmeshapata ufumbuzi wa search Warrant.

Pili, FBI itabidi iwasiliane na wataalam wengine watakaoweza kuchuja emails takribani 6500 ili waweze kutenga kati ya Clinton, Huma na Weiner na zipi zimeingia katika seva gani

Ili kufaninikiwa kwa hilo FBI wanatarajiwa kutumia soft ware maalumu na si search engine
Email zitkapopatikana zitahitaji kufanyiwa tathmini kama zina classified material

Kazi ya ku sort classified and non itashirikisha vyombo vingine na si FBI peke yao

Hilo linaifanya kazi isiweze kukamilika kwa siku 7, watu wataenda uchaguzi bila undani wa nini kimetokea.

Hakuna uhakika kwasababu FBI hawakeleza kilitokea nini Zaidi ya kushuku kuwa email zilizopatikana zinaweza kuwa na uhusiano na zile za awali

Na katka waathirika wa tukio hili kuwepo au kutokuwepo kwa matikeo ni Democrat

Tusemezane
 
Nguruvi3 mbona umepanic mkuu!!? Nilichosema umekielewa kweli!? Me nilimaanisha clinton akipatikana na kosa baada ya uchunguzi hilo kosa ni jinai! Kwa kawaida makosa ya jinai hayana mpaka na kwa kuzingatia hilo,bila kujali matokeo ya uchunguzi km yatamtia hatiani au la,lkn uchunguzi hauwezi kusubiri kutokana na uzito wa suala lenyewe.

Ndo maana sijamuona James comey na kosa lolote na viongozi wa Democrat wanaomlalamikia,wanajaribu tu kuokoa kampeni ya mama ambayo inadorora hatua za lala salama lkn ukweli wanaujua.

Nimesikitika sana jinsi ulivyotafsiri andiko langu,sikuwa na nia yoyote mbaya mkuu ya kukukera. Nakuhakikishia km ujumbe wangu umekuumiza halikuwa lengo langu na itakuwa imetokea kwa bahati mbaya sana. Nisamehe mkuu nguruvi3. Makosa ni sehemu ya ukamilifu wangu km binadamu...!! Tupo pamoja mkuu.
 
ELECTION NIGHT IN US

Kama tulivyosema utakuwepo uzi maalumu siku ya Jumanne tarehe 8 tukiwaletea matoke state kwa state
Itakuwa state kwa state kwasababu US Rais hachaguliwi na wingi wa watu kitaifa bali viti 'electoral college''

Hii ina maana gani? Kwamba, kampeni zinazofanywa na poll zinategemea eneo na si jumla
Kwa mfano, 'popular vote' ya nchi nzima inaweza kuonyesha mgombea A anaongoza dhidi ya B

Jambo hilo linatokana na ukweli kuwa kila state ina mambo yake ya kisiasa, kiuchumi, kijamii n.k.
Kwa mfano, mgombea akienda Arizona, Utah au Colarado likely atasikilizwa akiongelea immigration kuliko jingine. Mgombea akienda Pen au Ohio au Michigan ataeleweka akiongelea uchumi kuliko immigration
Likewise, mgombe akienda New York, Washington ataeleweka akizungumzi ulinzi na usalama
Mgombea akienda Illinois, Lousiana ataeleweka Zaidi akiongelea race na employment kuliko engine

Hii ni baadhi ya mifano, na hivyo popular vote inayotengeneza survey ya nationawide haitoi picha halisi kuliko kwenda state by state.

Uchaguzi wa Marekani unathiriwa na vigezo vingi sana.

Leo Wagombea wamejikita Florida, Ohio, Pen state, North Carolina, Utah, Arizona, Nevada, New Hampshire , Ohio n.k. Kwanini basi isiwe California, Texas, New York n.k.?

Jibu ni moja , kuwa wanagombea electoral college na hiyo ndiyo inayotoa Rais wa Marekani
Florida ina EV (Electoral vote 29), Ohio ina 18 , NC 15, NH 4, IO 4, NV 6, UT 6 ,CO 9, AZ 11,PA 20

Hizi ni state zikazoangaliwa na wachambuzi na wana habari kwa wingi wiki ijayo.
Ndizo zinaamua nani atakuwa Rais wa Marekani.

Nationa survey haielezi electoral vote, inaeleza kwa ujumla mtazamo wa watu
Na inategemea imefanyika kuhusu suala gani kama tulivyoainisha hapo juu

Wagombea wanajikkita katika maeneo yenye matarajio na mavuno makubwa na si kila mahali.
Kila mgombea kabla ya uchaguzi anajua atashinda majimbo gani, siyo suala la rigged kama wengi wanavyodhani

Ni suala la hesabu. Kwamba Clinton ana EV 55 za California, Trump ana 38 za Texas n.k. hiyo ndiyo inatoa lile neno la Red and Blue states.

Hesabu za Wagombea. Kwa kuzingatia Red States Trump anatakiwa ashinde, FL,OH, NC
Kwa baseline ya Red states (193?) Trump anahitaji EV 77 ili kufikia magic number ya 270.
FL,OH, PA vinampa viti 67 akishinda, na EV 10 anaweza kuzipata kwa NH 4,NV 6 na atafikia 270

Challenge ni kuwa UT yenye EV 6 ni battleground kutokana na uwepo wa Eval McMullin. Colorado ni battle ground ikiwa na EV 9.

Jumla ya hizi mbili ni viti 15 ambavyo lazima uvitoe katika GOP base number ya 193.
Hilo litamwacha na upungufu wa viti 15.

Kwa maana nyingine ushindi wa EV 15 za NC utakuwa umezibwa na kushindwa Utah na Colarado.

Hii maana yake ni kuwa he has to sweep the board across.

Tujadili Dem na Challenge zake. Inaendelea...
 
..ila huyu Comey kamharibia sana Hillary Clinton.

..Comey has basically thrown a lifeline to Donald Trump.

..halafu nimesikia kwamba nafasi( Dir FBI) yake ni ya mkataba wa miaka 10. Kwa hiyo hata kama Hillary atashinda huyu bwana ataendelea kutumikia kama Dir wa FBI.
 
..kuna ukweli wowote kwamba Tax records za Donald Trump zimevujishwa?
Yes NY times wameandika kuhusu Taj Mahal na NY Plaza
Jamaa alichukua mkopo,alipofahamu miradi ina feli akawauzia creditor share.

Mwisho wa siku akakwepa karibia 425M achilia mbali zile 916M na madudu mengine

Lawyers walimuonya kuhusu mambo kadhaa yanayohusiana na hilo na kwamba IRS watafanya audit

Basically, hakuna sheria inayomzuia kutoa tax returns hata kama yupo katika audit
Tatizo ni kuwa lenders/Creditors/contractors n.k watabaini mengi
 
..ila huyu Comey kamharibia sana Hillary Clinton.

..Comey has basically thrown a lifeline to Donald Trump.

..halafu nimesikia kwamba nafasi( Dir FBI) yake ni ya mkataba wa miaka 10. Kwa hiyo hata kama Hillary atashinda huyu bwana ataendelea kutumikia kama Dir wa FBI.
Juzi FBI walitoa habari za Baba yake Trump na leo wametoa zinazomhusu Billy Clinton 2001

Wanasema wametoa katika hali ya freedom of information request

Alichokifanya Comey kinaangaliwa kwa macho tofauti sana na wanasheria wakiwemo wa GOP

Uchunguzi ni jambo moja, timing ya kuzungumza ni jambo jingine, kinazungumzwa nini jingine pia na wakati gani

Barua haina details za nini kinachunguzwa. Hilo limeacha kila mtu na tafsiri katika wakati huu. Sasa anasema matokeo hayawezekani kabla ya uchaguzi

Wachambuzi wanasema kama ilikuwa ni hivyo, alikuwa na sababu gani za kupeleka hiyo barua Republican? Na lini FBI wameanza kutoa taarifa za uchunguzi ukiendelea?
 
Kuna tetesi kuhusu kura zilizopigwa mpaka sasa (early votes) huko Florida ambazo hazijathibitishwa rasmi. Ukweli ni kwamba pamoja na kuonesha idadi karibu sawa ya wapiga kura kutoka vyama vyote viwili, uchunguzi umeonesha kwamba asilimia 28% ya Republicans hawakumpigia kura Trump. Inasemekana Clinton mpaka sasa anaongoza kwa kupata asilimia 53% ya kura zote za awali.

Picha inayopatikana hapa ni tofauti kabisa na polls zinavyoonesha kwamba wagombea hao wawili wanakaribiana kwa kura walizopata, zingine zikidai tofauti ndogo ya asilimia moja tu. Hii ni kwa sababu ingawa rekodi zinaonesha kuwa waliojitokeza idadi yao inakaribiana kwa vyama vyote ni makosa kuchukulia kwamba Republicans wote wamempigia kura Trump wakati mambo ni tofauti.
 
Hii kashfa ya emai ya Hillary Clinton ina impact kubwa sana hvyo usijaribu kumtetea hata kidogo, maana ninajua kabisa wewe unampigia kampeni HC mitandaoni.
Japo unajifanya mchambuzi lakini hauko fair

Swali;
Hivi unalipwa sh. Ngapi na HC?
Mnakuja jukwaa hili kufanya nini kama uwezo wa kuchangia ni mdogo,kwanini usikae kimya tu na kuwa msomaji zaidi ili ujifunze kwa wengine.Unatia aibu,rudi kwenye Jukwaa la siasa ukachangie kwa style hiyo ya vijimaswali vya "unalipwa shilingi ngapi?" Huku waachie real GT .
 
Back
Top Bottom