Dunia haina usawa

Dunia haina usawa

SEHEMU YA 88

Hakusubiri kusikilizia suala hilo tu bali pia alitaka kufahamu kilichokuwa kimeendelea kati ya kijana wake aliyemtuma kuzungumza na Rosemary, kijana mtanashati aliyeitwa kwa jina la Juma.

Alitaka kupata taarifa juu ya kila kitu. Hakutaka kuona Rosemary akionewa kisa tu mumewe alifariki dunia, alitaka kuona akimsaidia kwa kuwa alikuwa mke wa mwanaume aliyekuwa na nguvu sana nchini Tanzania hivyo hakuona kama kulikuwa na sababu ya kumuacha mwanamke huyo pasipo kumpa msaada.

Alikuwa akimsubiri Juma, kijana aliyemtuma kwa ajili ya kuzungumza na Rosemary na kumwambia kila kitu kilichokuwa kimepangwa lakini cha kushangaza, kijana huyo hakupiga simu, na hata alipompigia haikupokelewa.

Matiku akakasirika mno, alitaka kusikia kila kitu hata kabla mnada haujamalizika na watu kuondoka mahali hapo. Alipoona kimya sana ndipo akampigia simu mwanaume aliyekuwa amemtuma kununua nyumba hiyo, Othman ambaye alimwambia kwamba alimuona Juma kipindi fulani akizungumza na Rosemary, baada ya hapo, akaondoka zake.

“Hujajua ameelekea wapi?” alimuuliza.
“Hapana! Ila aliondoka!”
Matiku hakutulia, muda wote alikuwa akimpigia simu kijana huyo lakini hali haikubadilika, iliendelea kuwa vilevile kwamba simu haikuwa ikipokelewa na baada ya kupiga sana, ikaisha chaji, alipoendelea kumpigia, haikuwa ikipatikana.

Akashikwa na hofu, akahisi kulikuwa na jambo baya lilikuwa limemtokea Juma, akawasiliana na vijana wake wengine ili wachunguze na kujua kilichokuwa kimetokea, walipoingia mitaani, wakarudi na taarifa kusema kwamba Juma alitekwa na watu wasiojulikana.

“Alitekwa?” aliuliza Matiku kwa mshtuko.
“Ndiyo mkuu! Ametekwa, waliomteka wala hawajulikani,” alijibu kijana wake.
“Wapi?”
“Namanga!”

Hilo likamchanganya zaidi, hakujua ni watu gani waliokuwa wamemteka, hakugundua kwamba watu hao walitumwa, alihisi kwamba baada ya kumuona na gari la kifahari wakadhani kwamba alitoka kwenye familia ya kitajiri na ndiyo maana walimteka kwa kuitaka familia yake kutoa kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya kumuokoa ndugu yao.
 
SEHEMU YA 89

Akawapigia simu polisi na kuwaambia kilichotokea, polisi walishangaa kwani mazingira ya utekaji hayakuonyesha kama watekaji walitoka sehemu ya mbali au walihitaji gari lake kwani kama ingekuwa hivyo ilikuwa ni lazima kulichukua na kuondoka nalo.

“Waliomteka walimtaka yeye na ndiyo maana wameacha gari,” alisema polisi mmoja.
“Sawa. Ila kwa nini wamemteka?”
“Labda wamejua kwamba ametoka katika familia ya kitajiri! Kuendesha V8 kwa nchi kama yetu si jambo la kitoto mkuu,” alisema polisi mmoja.

“Hebu fuatilieni! Watu walioshuhudia tukio wamesema kwamba watekaji waliondoka na huyo kijana njia ya kwenda Mikocheni, sasa kwa jinsi ninavyowajua, inawezekana wamekwenda naye Kawe. Fuatilieni huko,” aliagiza mkuu wa polisi katika Kituo cha Polisi cha Osterbay.
Hilo ndilo lililofanyika, gari moja la polisi likaondoka kituoni hapo huku kukiwa na polisi watano waliokuwa na bunduki, waliunganisha na kuanza kwenda Mikocheni na Kawe huku wakiwasiliana na wenzao na kuwataarifu tukio lililokuwa limetokea.

Mbali na watu waliokuwa wameshuhudia tukio hilo pale Namanga hakukuwa na watu wengine waliojua kwamba gari lililoondoka mahali hapo lilikuwa na mateka kwa ndani hivyo watu wengi kutokujua jambo lolote lile.

“Twendeni ufukweni! Ni lazima tuhakikishe huyu mateka anapatikana vinginevyo Matiku akiamua kuwaambia ngazi ya juu, halitokuwa jambo jema,” alisema polisi mmoja huku tayari gari hilo likiwa linakata kulia kwenye Kituo cha Sanaa kuelekea ufukweni.

Je, nini kitaendelea?
 
SEHEMU YA 87

Wakati Juma akiondoka, wanaume wale hawakutaka kumfuatilia kwa ukaribu, walichokifanya ni kutulia ndani ya gari lao kisha kumwacha mpaka atakapoingia ndani ya gari lake, alipofanya hivyo, wakaanza kumfuata.

“Kuna kitu!” alisema jamaa mmoja.
“Hata mimi nahisi! Hebu tumfuatilie, atatuambia ni kitu gani kinaendelea!” alisema jamaa mwingine.
Juma hakuwa na habari kama alikuwa akifuatiliwa kwa nyuma, akaingia kwenye barabara ya lami na kuondoka huku akielekea maeneo ya Namanga huku lengo lake likiwa ni kutaka kuelekea Kinondoni alipokuwa akiishi.

Wakati akiwa amekwishafika maeneo hayo ya Namanga, karibu na kona ya kuelekea ubalozi wa Marekani, akashtukia gari moja aina ya Range SUV jekundu likija na kusimama mbele yake.

“Kuna nini?’ alijiuliza lakini hata kabla hajajijibu, milango miwili ya gari lile ikafunguliwa, wanaume wawili waliokuwa na bastola mikononi mwao wakateremka na kumfuata Juma.
“Shuka chini,” alisema jamaa mmoja huku akiwa amevunja kioo.

“Nimefanya nini?”
“Paaa…” risasi ikapigwa hewani, watu wote waliokuwa wakishangaa huku wakitamani kujua kitu gani kinaendelea, wakaanza kukimbia.
“Jamani msiniue!”
“Basi teremka.”

“Sawa!” alisema Juma huku akitetemeka.
Akateremka, wakamchukua, wakamuingiza ndani ya gari lao na kuondoka naye mahali hapo. Watu wote waliokuwa wamejificha, wakaanza kujitokeza huku wengine wakilaumu kwamba kwa nini polisi wa Kituo cha Osterbay hawakutokea na wakati hawakuwa mbali na mahali ambapo risasi ilipigwa?

“Wale sio majambazi?” aliuliza jamaa mmoja.
“Majambazi! Majambazi gani wanavaa suti?” aliuliza jamaa mwingine, wakati huo gari lile lilifika ubalozini, likakata kulia na kuanza kuelekea Mikocheni huku muda wote huo Juma akilia kuomba msamaha japokuwa hakujua alifanya nini.

*** Bilionea Adam Matiku alikuwa nyumbani kwake ametulia, alichokuwa akikisubiri ni ripoti kutoka nyumbani kwa Mapoto ambapo nyumba ya marehemu huyo ilikuwa ikipigwa mnada huku akiwa amemuandaa rafiki yake, Othman Ngolisho kwa ajili ya kuinunua nyumba hiyo.
Mbona hamna sehemu ya 87?!

Barikiwa
Mh Dada unataka nikutafunie kabisa mbona ipo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom