Dr. W. Slaa anaondoka CHADEMA

Dr. W. Slaa anaondoka CHADEMA

Maombi yanahitajika, mtumishi wa Mungu Joseph Gwajima tafadhari sana ongea na mke wa daktari huyu, moyo umesononeka sana lakini Mungu ana makusudi na Tanzania, this is a very trying moment to chadema.

Likitokea hili MBOWE ana kesi ya kujibu

Watu wamekufa kwa ajili ya chadema yeye anakuja kuiua kwa siku moja just for Lowasa
 
Alikuwa kajiandaa kuchukua nchi sasa amezinguliwa kwann asiondoke

Dr. hajazinguliwa kwa kunyimwa fursa ya "kuchukua nchi". Sio mbinafsi kihivyo. Akiondoka basi itakuwa ni kwa sababu ya kukiukwa au kupindishwa kwa kanuni ya/za misingi anazoziamini. Bila shaka, hata yeye anao ufahamu mzuri kuwa kushinda u-rais kwake si jambo rahisi.
 
Slaa kachoka kuendeshwa na mbowe, mbowe ndo dereva wa ukawa
 
napenda sana jinsi CHADEMa inavyoweza kucheza na kuiyumbisha media kwanza ku-frustrate ccm , pili kupotezea weakness za kumpoke Lowasssa Ku-win sympathy za waliotaka Dr. Slaa awe president na kumtoa Magufuli katika media completely

Hongera CDM think tanks
 
kama slaa ni mtu wa principle hawezi kukaa chama kimoja na lowasa,kwajinsi alivyokua akisema lowasa fisadi,haiwezekani unless awe mnafiki....


ndo maana ccm wako kimyaaaa,wanasubiri tu hatima itakua vipi hapa
 
Moderators na wanajukwaa wote,NAWASALIMU!
Ninaomba kutoa hoja kuhusu uzi wa ndugu Manyerere Jackton kuwa Dr.Slaa anakabidhi ofisi usiku wa leo.
Humu jukwaani tupo wafuasi wa KUFA na Dr Slaa na hii habari imeleta mfadhaiko mkubwa miongoni mwetu.
Natoa hoja kuwa ,endapo itafika kesho saa moja (1) asubuhi bila ndugu Manyerere au mtu mwingine kuthibitisha kuwa Dr Slaa amekabidhi ofisi,basi ndugu Manyerere apewa adhabu kali ikiwa ni pamoja na kupewa kifungo cha maisha.
Ndugu moderators,Naomba kutoa hoja!
 
KAULI MBIU NI MADILIKO TU, ATA HUYO Dr. SLAA AONDOKE AU ABAKI.

INA MAANA YEYE ATAIBADILISHA HII NCHI? CCM IMEJAA Maprofesa ila ni Madudu tu vyachwani mwao.

TUKO PALE PALE MAGEUZI MBELE.

Thamani ya Dr. Slaa ni zaidi ya elimu yake au vyeo alivyokuwa navyo. Hajakashifu mtu. Mpe heshima yake hata kama anaondoka. Tujifunze kutambua na kuheshimu watu wa maana hata kama maamuzi yao mengine yatatupa taabu. Na bado hatujaujua ukweli wenyewe.
 
Maombi yanahitajika, mtumishi wa Mungu Joseph Gwajima tafadhari sana ongea na mke wa daktari huyu, moyo umesononeka sana lakini Mungu ana makusudi na Tanzania, this is a very trying moment to chadema.

Unataka Gwajima Aongee na Mke wa Mtu. We hujamjua Gwajima Kwa wake za watu?
Hebu mpeleke mkeo aombewe uone Balaa.
Km hakurudi na katoto ka Ufufuo na uzima nyumbani.
 
Jamani mimi nauliza tu,hivi mirembe kutakuwa salama kweli?makufuli ya huko hayajavunjwa kweli?au pengine walinzi wamekacha shift zao?maana yake hali iliopo leo siyo hali ya kawaida,jukwaa limevamiwa nyuzi zote zinazoletwa hapa utafikiri zinaletwa na wale waliopuruchuka kutoka mirembe.
 
Tujipe muda kwani kipindi hiki wakukurupuka ni wengi sana.........
 
Mi sioni ajabu Slaa kuondoka, kama ameona hawezi kwenda na speed hii nimtakie kila la heri tu.. aliikuta chadema na ataiacha
 
Sasa usiku huu anakwenda kumkabidhi nani hivyo vitu? Kwanini asiende mchana? Au anakwenda kuvitelekeza hivyo vitu maana ofisi zitakuwa zimefungwa.Hebu jipange basi mleta maada!

Labda atakabidhi walinzi..
 
Nawaaambia, ijumaa ya kesho haitapita bila kukubaliana na mimi. Dk. Slaa anajiengua.
Km tukio linafanyika kesho haraka ya nini mkuu!? Hapa si umejitafutia ban ya bure! Hivi hata kwa akili ya kawaida tu ya darasa la 7,dr.slaa anaweza kufanya wenda wazimu km huu!!?
 
Najua wapo watakaobeza na hata kutukana lakini napata ushujaa wa kuyasema haya. Dk. Slaa usiku huu anaingia makao makuu kukabidhi gari, kadi, walinzi na cheo. Anajitoa CHADEMA. Naomba uzi huu uachwe hapa hapa ili baadaye nihukumiwe kwa haki.

Chanzo: Mimi mwenyewe.

hakuna jinsi,wacha aondoke tu,you must accept to loose so as to gain,ni lazima kurudi nyuma ili kwenda mbele kwa mshindo. ahsante dr slaa kwa utumishi wako uliotukuka na kukijenga kuwa chama bora,binafsi nakutakia kila kheri katika maisha mapya utakayoyachagua,kwa heri dr slaa,sisi tunaendelea na mapambano na tutaendeleza ulioachia.
 
Kama slaa akiondoka CHADEMA mimi binafsi sitajiingiza tena kwenye siasa..nitabaki mtazamaji maisha yangu yote..
 
Back
Top Bottom