Dr. W. Slaa anaondoka CHADEMA

Dr. W. Slaa anaondoka CHADEMA

Na wewe umeanza kuwa muhuni au mabange umeanza kuvuta

Msimuamini hizi ni habari za uongo. Slaa aende wapi muda na umri wake kaumalizia chadema sio kirahisi hivi. Wapuuzeni waongo wapuuzi.
 
Thamani ya Dr. Slaa ni zaidi ya elimu yake au vyeo alivyokuwa navyo. Hajakashifu mtu. Mpe heshima yake hata kama anaondoka. Tujifunze kutambua na kuheshimu watu wa maana hata kama maamuzi yao mengine yatatupa taabu. Na bado hatujaujua ukweli wenyewe.

Ni sawa ila tusiaminishwe kwamba hatuwezi kuleta mabadiliko bila ya Slaa.. Hicho kitu sio sawa kwamba tunamtegemea mtu mmoja katika watu 45milion.. We can do it with or without him
 
Najua wapo watakaobeza na hata kutukana lakini napata ushujaa wa kuyasema haya. Dk. Slaa usiku huu anaingia makao makuu kukabidhi gari, kadi, walinzi na cheo. Anajitoa CHADEMA. Naomba uzi huu uachwe hapa hapa ili baadaye nihukumiwe kwa haki.

Chanzo: Mimi mwenyewe.

Bado hajarudisha tu? Au anavizia usiku wa manane asionekane na mtu?
 
kwa jinsi ninavyomfahamu Dr Slaa kamwe hawezi kuchukua hatua za kuondoka Chadema eti kwa sababu hatagombea Urais
acheni kumpakazia hasa wewe Manyerere Jackton wewe ni mtu usiye eleweka misimamo yako,kaa mbali na process zote zinazoendelea kwenye nchi yetu hufai hata kidogo kuwa mtoa taarifa za muhimu
Dr Slaa siyo mtu mjinga kiasi hicho ni mtu smart nimekuwa naye karibu kwa muda mrefu na namwamini sana

shida kubwa sana hapa sio urais tu,,, shida ni kula matapishi ujue wanachadema wote walau wanaweza kufumba macho wakampokea huyu jamaa ila scenario ya mzee slaa na lowasa ni special case ambayo inahitaji special treatment manake huyu mzee ndo alimtaja jamaa kwenye ile list of "fame" halafu eti leo slaa ambae ni presidency favorite wa ukawa ampishe mtu huyo huyo ambae alimshupalia kua fisadi-papa kwenye kiti cha ugombea ili kesho akishinda awe bosi wake... najua slaa kujiengua chadema ni ngum sana ila kwa situation ya sasa ilivo akibaki chadema atakua ndo mtanzania wa kwanza kua na moyo mpana unaoweza kuhimili presha kuliko wote
 
Hakuna kitu kama hicho wanajamvi hizi habari zilisemwa tangu jana na Dr Slaa amezikanusha kwa nguvu zote tusihadaiwe na prop za ccm.
 
Mtu aitwae #Manyerere Jackton ameandika mambo yasiyofanana na chembe ya ukweli kuhusu KM Dk. Slaa.

Bado tuko Ofisini. Kazi zinaendelea.

Hicho alichokiandika labda kama kinatokea kwenye ofisi ya chama kingine anachokijua Manyerere na kwa mtu mwingine tofauti na Dk. Slaa, Katibu Mkuu wa CHADEMA.

Nimuombe Jackton Manyerere, mpiganaji ambaye anapaswa kuwa na heshima yake kwenye tasnia ya habari afanye atimize wajibu wa kitaaluma katika kukusanya na kupasha habari badala ya uzushi na maneno haya yasiyo ya kweli.

Labda kama wameanza tena kufanya Kazi ile ile waliyokuwa mwaka 2010 ambako walimzushia Katibu Mkuu Dk. Slaa kila aina ya uzushi ambao Watanzania waliukataa.

Habari hizi za kuzusha na kutengeneza ndizo zilizotumika pia katika kampeni za mwaka 2005 ambapo hawa wanaozizusha leo mitandaoni walikuwa ndiyo timu ya utawala huu ulioshindwa. Wakimpamba mfalme kuwa amevaa nguo wakati yu mtupu. Kwa kila mapambo kuficha uvundo uliokuwa ndani ambao hatimaye leo unanuka (kushindwa) kila mahali.

Makene
 
Asante kwa taarifa,ila Tumaini Makene, CHADEMA mtu wa Media/Msemaji wa CHAMA kuna mapungufu,habari hizi znazagaa tangu jioni na mpo kimya,unless ni part ya vita dhidi ya mkoloni mweusi!!
 
Last edited by a moderator:
Ni aibu sana kwa mtu kama Manyerere kuandika habari ambazo hajathibitisha
 
Hebu tunahitaji dokta kesho azungumze na vyombo vya habari roho zetu zitulie
 
Asante sna kamanda Makene,hapa sasa walau napumuwa,Tulianza na Mungu na tutamaliza na Mungu.Mungu nakuomba siku nikiipa ccm kura na iwe mwisho hapo hapo kwwnye sanduku la kura amina
 
Back
Top Bottom