Dr. Slaa Receives A State Reception In Alabama Capitol !

Dr. Slaa Receives A State Reception In Alabama Capitol !

Hivi hiyo ilikuwa ziara binafsi au ziara ya kichama? Nauliza kwa sababu naona kwenye meza ya mazungumzo yupo Dr. Slaa na Mama Josephine lakini upande mwingine naambiwa kuna Gavana na Mawaziri. Kwa hiyo ujumbe wa CHADEMA uliongozwa na Dr. Slaa na Mama Josephine peke yao? Inakuwa kama Mseto vile; kwa upande wa Alabama State uwakilishi ni wa viongozi wa Jimbo lakini kwa upande wa CHADEMA uwakilishi unakuwa wa familia zaidi!


Swali la msingi sana,mipaka lazima ichorwe.
Huyu mama angebaki hotelini tu mda wote wa official visits,au kama akienda aende sehemu
zingine sio kunusa nusa kama watch d'x#%^///
 
Wine kwa kitoweo karatasi! unanchekesha!

Looh! hata haya hamuoni?

Wasiwe na makaratasi kwa vile walitoka kwenye disco na kupembea au walitoka kwenye majadiliano mambo muhimu yaliyowafanya wakutane? Just think twice before you ink on a piece of paper or hands on key board kwenye tofuti pakato, au kwenye mobile phone.
 
Mkuu upo sahihi kwa upande mmoja haswa unaposema Mkuu wa Kaya ajifunze kupitia kwa Dr. Slaa, yaani apunguze msururu wa watu anaoongozana nao anapokuwa safarini. Na nilivyokuelewa hapo mkuu hoja yako ni ili kupunguza gharama.
Swali: Uwezo wa kudadavua mambo kwa upana zaidi kati ya Mkuu wa Kaya na Dr. Slaa unalingana?
Jibu utanipa mkuu, ila maoni yangu Mkuu wa Kaya aendelee na misururu yake kwani inatufichia aibu sana watanzania na pia aendelee na hotuba za kusoma maana siku akianza kuutubia pasipo kuandikiwa nadhani watanzania tutaaibika sana.

Mimi naomba nikusaidie kujibu swali lako, kiukweli tofauti kati ya mkuu wa kaya na Dr. Slaa upo mkubwa sana tena katika nyanja mbali mbali hasa katika suala zima la kudadavua mambo. Dr. Slaa anauwezo mkubwa sana katika kudadavua mambo kuliko mkuu wa kaya na hii pia inachangiwa zaidi uwezo wa kitaaluma mkuu wa kaya udokta wake kapewa zawadi hasa baada ya kugawa rasilimali zetu kwa anao penda kuwaita wakubwa lakini Dr. Slaa ni Dr. Original so hapo unaweza kungudua kuwa kuna Dr. wakichina na Dr. Original hivyo hata utendaji wao lazima utofautiane kwa kiasi kikubwa sana.
 
Nimefarijika sana sana.Shujaa na Rais wa mioyo ya watu!

Hizi kauli ndizo zinazo mvimbisha Slaa kichwa hadi anakua na dharau.,
Kwa sasa ni katibu mkuu wa chadema,haja teuliwa hata kugombea uraisi.

Over expecting is harmful. Mtamuita raisi weeee,asipo teuliwa na chama atakufa kwa presha.
 
Wasiwe na makaratasi kwa vile walitoka kwenye disco na kupembea au walitoka kwenye majadiliano mambo muhimu yaliyowafanya wakutane? Just think twice before you ink on a piece of paper or hands on key board kwenye tofuti pakato, au kwenye mobile phone.

Mnazidi kujidhihirisha usukule wenu, si afadhali mngesema yuko kwenye mazungumzo na wasaidizi wa gavana kuliko kujidai wanakula chakula cha mchana wakati hakuna chakula hapo wala kijiko wa umma wala kisu.

Hivi mnazo haswa?
 
Unaonesha hata haya maneno chini ya picha hujayaona, unatumia mchina nini? "Uongozi wa jimbo na Dr. Wakila chakula cha mchana iliyotayarishwa kwa ajili yake"

Rudi juu kajiridhishe kwa kigezo chako na uje tena utueleze umeona umma na kisu juu ya hiyo meza? au kimchina kako hakioneshi picha pia?
Mnazidi kujidhihirisha usukule wenu, si afadhali mngesema yuko kwenye mazungumzo na wasaidizi wa gavana kuliko kujidai wanakula chakula cha mchana wakati hakuna chakula hapo wala kijiko wa umma wala kisu.

Hivi mnazo haswa?

Nimeamini mtu wa jikoni niwa jikoni tu issue muhimu uliyoiona wewe ni uwepo wa umma na kijiko mezani,

try to look in a broad picture.
 
Mkuu mimi sipingi Kiongozi kuambatana na mwenza wake; tatizo ni kwamba hapa kuna Serikali ya Jimbo, Gavana na Mawaziri wake, wakiwa wamempokea Kiongozi wa Chama cha Siasa. Lakini Kiongozi wa Chama cha Siasa yuko yeye na mke wake tu bila kuwa na ujumbe wa chama. Ningemuona kiongozi mwingine wa CHADEMA akiwa ameongozana na Katibu Mkuu kwenye hayo mazungumzo wala nisingekuwa na cha kuuliaza; lakini yeye na mke wake peke yao mbele ya ujumbe wa seruikali ya jimbo inabidi nijiulize. Sijawahi kumuona JK na Salma peke yao wakiwa kwenye mazungumzo ya kiuwakilishi labda iwe wamekaribishwa wao kama familia ama wamekaribisha kama familia.


Najiuliza,mda wote wa mazungumzo alikua kimya au alichangia point?
Kama alichangia,ali changia kama nani?
 
Nilichopendea ziara hii ni namna viongozi wetu wanaweza kujifunza wanapotembelea nchi zingine na uwazi uliomo kwenye ziara yenyewe. Si suala la bora ziara na mikutano mingine kufichwafichwa kana kwamba kuna kipande cha ardhi kinauzwa kinyemela. Hii nimeipenda japo mtoa taarifa anaonekana Mmasai kwa kiswahili chake. Big Up Dr. Slaa, big up mleta taarifa
 
Nyie tianeni ujinga tu lakini itabaki historia tu kuwa alishawahi kumsindikiza ikulu JK 2010.

Kikwete mwenyewe anafahamu kuwa alisukumizwa tu kuingia ikulu, ndo maana imempwaya sana, kabaki kufanya biashara ya malori na mwanae.
 
Dr Slaa ana potezea hao viongozi wa hilo jimbo muda wao tu; hivi kiongozi wa chama kwenda kujikomba komba kwa Wamarekani ina faida gani kwa CHADEMA?

Hajaenda kuomba misaada ya chadema,hata ziara yake haito titled "vision chadema" ni "VISION TANZANIA"
Man up and use ur brain damn it.
 
Swali la msingi sana,mipaka lazima ichorwe.
Huyu mama angebaki hotelini tu mda wote wa official visits,au kama akienda aende sehemu
zingine sio kunusa nusa kama watch d'x#%^///

Hili wala halina mjadala hata JK na udhaifu wake wote pale kwenye official talks Salma hatii mguu.

Dr Slaa ni dhaifu kwa Josephine na wala halihitaji degree kulitambuwa, nitaendelea kumfanyia vetting binafsi Dr Slaa mpaka pale nitakapojiridhisha ameweza kumdhibiti huyu Mwanamke.

Wale wenye mahaba ya kupitiliza endeleeni tu kunifuata pm lakini kwenye sitayumba na msimamo wangu ni mkali sana na hauwezi kubadilishwa na yeyote zaidi ya Dr Slaa na Josephine.
 
Ni kawaida kwa kiongozi yeyote kuambatana na mwenza wake ziarani, wewe unatolea mfano wa Ridhiwani, hivi Ridhiwani ni Mwenza wa Rais?
Msipotoshe mambo. JK aliambatana na kijana wake Kenya kwenye sherehe za kuapishwa rais wa Kenya. Tulipiga kelele sana Ridhwan alipopiga picha akiwa mbele ya viongozi wa serikali kwani tuliona kama protokali haikuzingatiwa. Ujinga tunaolaani unapofanywa na ccm hatuwezi kukaa kimya kwa kuwa tu ujinga huohuo umefanywa na Slaa au na CDM.

Wengi tunamfahamu Dr Slaa kama mtu makini, lakini anapokaa kwenye kikao rasmi na gavana wa jimbo na mawaziri wake huku akiwa na mkewe, huyo mkewe anamwakilisha nani, au ni nani CDM? Tumeyaona Anna aliyomfanyia Mkapa, hatutaki yajirudie kwa Josephine na Slaa, na kwa vyovyote mstibue imani ambayo wananchi wameanza kuijenga kwa CDM.

Mliopo karibu na huyu mzee msaidieni. Inawezekana amezidiwa na nshutama.
 
Mnazidi kujidhihirisha usukule wenu, si afadhali mngesema yuko kwenye mazungumzo na wasaidizi wa gavana kuliko kujidai wanakula chakula cha mchana wakati hakuna chakula hapo wala kijiko wa umma wala kisu.

Hivi mnazo haswa?

Faiza Fox: Hii ni ndogo sana kwako ku-comment negatively. Hata kama huwapendi CDM kiasi hicho hebu jaribu na uungwana kidogo. Appreciate mahali panapostahili na kisha toa constructive criticisms. Mimi nadhani unaweza kufanya vizuri zaidi ya comments hizo
 
Hili wala halina mjadala hata JK na udhaifu wake wote pale kwenye official talks Salma hatii mguu.

Dr Slaa ni dhaifu kwa Josephine na wala halihitaji degree kulitambuwa, nitaendelea kumfanyia vetting binafsi Dr Slaa mpaka pale nitakapojiridhisha ameweza kumdhibiti huyu Mwanamke.

Wale wenye mahaba ya kupitiliza endeleeni tu kunifuata pm lakini kwenye sitayumba na msimamo wangu ni mkali sana na hauwezi kubadilishwa na yeyote zaidi ya Dr Slaa na Josephine.

"Honey twende na mimi nikaone,nipige na picha pia,kule bukoba watajuaje niko kwa Obama?"
 
Sasa hiyo ndio "state reception" au kaomba appointment apeleke makaratasi yake ya ufataani?

Mijitu minngine mna mnana mtu ambae hanangiki.

Alipewa dakika ngapi na Gavana?

Utakufa kwa kijiba cha roho wa "mjane mweusi"
 
Hizi kauli ndizo zinazo mvimbisha Slaa kichwa hadi anakua na dharau.,
Kwa sasa ni katibu mkuu wa chadema,haja teuliwa hata kugombea uraisi.

Over expecting is harmful. Mtamuita raisi weeee,asipo teuliwa na chama atakufa kwa presha.

Ni ujinga huu huu ndio ulimwaribu Zitto Kabwe akavimba kichwa akadhani wote sisi ni Wannabe matokeo yake ameshapotea hata aeleweki anahitaji nini pamoja na usomi wake wote.

Mtu mmoja alidiriki kutaka kugombea majimbo matano ya Ubunge hizi si akili za kawaida.
 
Hili wala halina mjadala hata JK na udhaifu wake wote pale kwenye official talks Salma hatii mguu.

Dr Slaa ni dhaifu kwa Josephine na wala halihitaji degree kulitambuwa, nitaendelea kumfanyia vetting binafsi Dr Slaa mpaka pale nitakapojiridhisha ameweza kumdhibiti huyu Mwanamke.

Wale wenye mahaba ya kupitiliza endeleeni tu kunifuata pm lakini kwenye sitayumba na msimamo wangu ni mkali sana na hauwezi kubadilishwa na yeyote zaidi ya Dr Slaa na Josephine.

Salma hawezi kutia mguu si kwa sababu hatakiwi,ila ni kwa sababu ya tatizo la lugha ya watu,Josephine
ni msomi mwenye uwezo mzuri,lugha ya kiingereza inapanda na anajiamini.Tujifunze kwa wazungu wanavyothamini wake zao na tuache vijiba vya roho na chuki binafsi
 
Mnazidi kujidhihirisha usukule wenu, si afadhali mngesema yuko kwenye mazungumzo na wasaidizi wa gavana kuliko kujidai wanakula chakula cha mchana wakati hakuna chakula hapo wala kijiko wa umma wala kisu.

Hivi mnazo haswa?

Ukiona meli inaanza kupigwa na mawimbi kisha kuyumba huku na kule waliomo ndani ya meli hukazana kujishikiza kwenye milingoti na kuta za meli hiyo inayoyumba wakifikiria kujishikiza usalama wao wakati chombo kizima kipo hatarini kutumbukia baharini.

Tunahangaika na kukaza mishipa usoni kuwa mbona umma, kisu nk havionekanai, mara makaratasi, hatujadili ya maana aliyojadili Slaa kwa manufaa ya watanzania. UCCM, UChadema, UCUF nk unatupofusha mno. Tuelewe mtanzania anapokuwa katika anga za kimataifa huko hawamji Faiza Foxy, wanalijua taifa la Tanzania. Wenzetu wanachagua mtu mwenye ukweli katika anachokisema si itikadi za kichama.
 
Back
Top Bottom