Rugemeleza
JF-Expert Member
- Oct 26, 2009
- 668
- 136
Wanamapinduzi, hoja kama hizi hakuna haja ya kuhangaika nazo. Ni taaHira tu au fisadi au asiyejua mbele na nyuma anamchagua JK na CCM.
Leo bei zinapaa na mtajua Dr. Slaa alikuwa anasema nini. Mafuta ya kula ndani ya wiki 2 yamepanda toka elf 2 hadi 3 kwa lita. Na bado mtajuta. Haya ni maafa. Dr anachosema ni kwamba matokeo ya NEC hayana uhusiano na kura zilizopigwa.
Amefanya vyema kutohalalisha huu uhuni na mzaha wa JK na watu wake.
Hoja yenye nguvu. Makame na Kiravu wanajua jinsi ambavyo miaka yote wamekuwa wakishiriki kuiba kura na kuvuruga uchaguzi.
Inakuwaje kila kasoro ambayo washindani utoa iwe ni kasoro ndogo ambayo isingeweza kubadilisha matokeo? Wakati kasoro hizo zinaingilia ndani ya utendaji mzima wa Tume na kuonyesha jinsi gani ilivyokuwa ni chombo cha kupika kura kwa manufaa ya CCM. Halafu bila aibu, soni, wala haya anasema eti kuwaambia watu walinde kura ni kuchochea ghasia na kuleta mashaka yasiyo na msingi.
Kwa taarifa yako Kiravu kila mchaguaji ana haki ya kupiga kura na kuilinda kwani hana wakala wa kura yake. Kama huelewi hilo basi ni uthibitisho tosha wa uwezo wako mdogo wa kufikiri na jinsi dhamira yako ilivyokufa.
Jiuzuluni Makame na Kiravu nyie ni aibu kwa nchi yetu.