Dr Slaa na njama ya kukwepa kodi

Dr Slaa na njama ya kukwepa kodi

Status
Not open for further replies.
Acha ujinga wewe issues zotebzinazomhusu Slaa hata kama zinaonesha kuwa na ukweli unaleta ujinga ujinga wako,kws nn tusichambue hili kwanza na kujua ukweli wake,usipende kutukana wakati hujapata ukweli,

Zinaonyesha wapi wewe pimbi? Kwenye karai la maji au kwemye kioo? Unatetea mvuke huna hata haya. Majambazi wakubwa na chama chenu.

Kigumu chama cha Mapuuzi.

 
Ritz,
Utabwabwaja na propaganda mpaka utachoka. Basi angalau ungelikuwa hata na Taarifa
Sahihi.
1. Kwanza hoja ya kukutana na Wajapani nyumbani, pamoja na kuwa Dr Slaa hazuiwi na sheria au utaratibu wowote kukutana na yeyote anayetaka nyumbani kwake au mahali popote, siyo ya kweli. Hakuna siku hata mmoja, siyo mwezi Juni tu, wajapani 20 walipofika na kula nyumbani kwangu. Kama ni hivyo, mbona unawake picha za Mama Slaa alipokuwa Japan basi. Isitoshe picha za safari ya Mama Slaa hazikuwa siri zilikuwa kwenye FB yake. Mtihani wa kwanza umefeli vibaya sana. Fanya mwingine tuone.

2. Ah! Kumbe ujenzi wa Hospitali! Pamoja na kuwa sina mpango huo, labda Kama utakuwepo baadaye tatizo ni nini. Dr. Slaa nimeasisi taasisi ya CCBRT mwaka 1994 na kujenga, pamoja na programs zingine, Hospitali kubwa kuliko zote hasa kwa performance( look at statistics) Afrika South of Sahara inayoshughulikia disagbilities under one roof, ten a katika Ardhi tuliyopewa na Serikali ya JMT. Sasa hivi, tunajenga Hospitali kubwa ya Mama na Mtoto itakayokuwa tayari 2014/15, nayo pia katika nyongeza ya ardhi tuliyopewa na Serikali. hospitali zote ziko exempted. Ukwepaji kodi uko wapi. Kama CCBRT imepata cheti cha TRA, Kama stori yako ungekuwa kweli, si ni utaratibu huo huo ungelifuatwa! Tatizo liko wapi hapo? ritz una akili ya ajabu, ningetaka kufanya biashara ningeshindwa kufanya hivyo kupitia CCBRT. Nadhani mnatafuta pa kushikiza, piga ramble zaidi labda itakusaidia!



Hakiyamungu Nchi Ngumu sana hii,
Anyway yetu ni macho na maskio,uhai na afya tunamuachia muumba,ila kadiri muda unavozid kwenda mbele ndivo mambo yanavozid kuwa MATAMU,tunaomba uhai 2015 tuweze kuiona na kujionea KIVUMBI...!!
 
Naomba ipagwa siku maalumu ambayo hata tajwa rais wangu Dr.W.Slaa humu. Hata mbili kwa wiki
 
Last edited by a moderator:
Kweli nimeamini kah*ba ni k*haba tu hata akiwa mtawa hawezi kuficha tabia yake...

Hapa mdada umeonyesha tabia yako ya ndani kabisa,,, tamaa mbaya sana,, naamini buku saba ya Lumumba kwa nyie wenye tamaa ni ngumu sana kuwatosha.

Huyu maza kanisikitisha sana kumbe ni gamba lililo kubuhu


Sijaona picha inayoonyesha Dk. Slaa akikwepa kodi. Natamani sana niione picha hiyo.

Hata mie nasubiri picha hizo eti ushahidi picha na maelezo haviendani picha ya 2012 maelezo anasema 2013

Sasa nimeona hiyo picha ambayo Dk. Slaa anakwepa kodi. Kumbe huku ndiyo kukwepa kodi. Sasa nimeelewa.

Atupe huo ushahidi unao onyesha Dr. Slaa anakwepa kodi, picha alizo weka kachukua FB ya mke wa Dr. Slaa.
 
DR Slaa, acha kutufanya wana JF kuwa ni watoto. Ungekuwa muungwana ungejibu hoja za Ritz badala ya kubwabwaja tu. umejibu hoja moja tu kuwa hujawahi kufanya kikao na wajapani nyumbani kwako tena kwa vile tu Ritz hajaweka picha za hicho kikao cha nyumbani kwako na badala yake kaweka picha za Josephine akiwa Japani

badala ya kujibu hoja za msingi, wewe unakmbilia kucheza na akili za watu tu kudanganya. Ni kiongozi gan kama wewe anakuwa na ndoto ya kuwa Rais wa nchi lakni ni mdanganyifu na mjanjamjanja namna hii. Ni aibu kwako binafsi, chama unachoongoza na familia yako. Hapa kuna hoja nyingi zimeibuliwa na Ritz ambazo hujajibu na badala yake umetumia muda mwingi kuelezea mafanikio ya Taasisi ya CCBRT ambayo nayo inaendeshwa kiujanjaujanja. Ile Taaasisi ipo kimaslahi zaidi lakini wanatumia kigezo cha kutoa huduma ili kupata upendeleo kwa serikali. Hoja za Ritz ambazo ulipaswa kuzijibu ni hizi zifuatazo;
  1. Dr Slaa pamoja na Mchumba wako Josephine mlitembelewa na Wajapan 20 nyumbani kwenu na kula chakula cha jioni. Hiyo ilikuwa ni Juni 2013. Hoja hiyo umejibu kisanii sana eti hujawahi kutembelewa na wajapani nyumbani kwako. Kanusho lako limekuja tu kwa vile Ritz ameweka picha za Josephine akiwa Japan ambazo umesema kuwa hazikuwa ni za siri. Naamini kuwa endapo Ritz asingeweka picha yoyote, ni wazi kuwa hata ziara hiyo ya mchumba wako ungeikataa
  2. Ritz amesema kuwa CHADEMA mna mpango wa kujenga Hospitali huko mlalakuwa. Je hoja hiyo imekaa vipi? Si dhambi kwa CHADEMA kujenga hospitali. Hoja ya msingi hapo ni huo ulaghai unaowafanyia wajapani kuwa wewe ndiye Rais mtarajiwa 2015 na kwamba kama ukiwa Rais, makampuni ya Japani yatapata upendeleo kwa kile kinachodaiwa kulipa fadhila. Hilo unasemaje?
  3. Mahusiano ya Dr SLaa, familia yako, chadema na Askofu mmoja ambaye licha ya kuwa Ritz hajamtaja, lakini wadau wametusaidia kuwa ni Gwajima yapoje? Je ni kweli kuwa hospitali hiyo tarajiwa inajengwa kwa ubia yaani Dr Slaa na familia yako, CHADEMA na Gwajima? Kama ni hivyo, ubia huo una malengo gani? Ninachokiona hapo ni ukwepaji wa kodi ambao ni dhahiri Gwajima anahusika
  4. kama hospitali hiyo ni ya CHADEMA, iweje Mchumba wako Josephine ndiye anayefuatilia kwa karibu na si organs za chama chako? Katika hilo, hapo hapana harufu ya ufisadi?

Nawatahadhalisha sana CHADEMA kuacha ushabiki usio na manufaa na badala yake mnapaswa kufuatilia kwa karibu nyenendo za Dr Slaa na mchumba wake kwani wana mambo mengi ya siri wanayafanya kwa kutumia jina la chama na kanisa ila kwa manufaa yao.
Mkuu Lizaboni,

Nashukuru sana kwa kudadavua hizi bayana.

Dr. Slaa kashindwa kukataa kama wana uwanja Mlalakuwa ambao wanataka kujengea hospitali na Wajapani yeye na Josephine.
 
Last edited by a moderator:
Ritz,
Pamoja na kuwa nakuheshimu, lakini unazungumza utumbo bila utafiti. CCBRT Dr Slaa siyo " kateuliwa tu..." Kama unavyotaka kuonyesha. Dr Slaa " Founder" wa CCBRT na ni mwenyekiti wa Board. Pamoja na Disability Hospital CCBRT ina programs nyingi ikiwa ni pamoja na maboresho ya Vituo 14 vya Afya Jijini Dar na Maboresho ya Hospitali za Amana, Temeke na Mwananyamala kabla ya kufungua Hospitali ya Mama na Mtoto. Kazi hizo zote zinafanyika bila siasa kwa kuwa kwenye Maendeleo hakuna siasa. Wakuu, nimekwisha kuweka msingi wa ukweli, sitajibizana ten a na Ritz. Hata hivyo nimalizie kwa kumwambia Ritz kuwa huo ndio uzalendo, kuhudumia Watanzania bila kuchoka, na bila kuwabagua kwa rangi, itikadi, dini au wanakotoka. Kielelezo cha uzalendo ni matendo na siyo maneno wala propaganda.


QUOTE=Ritz;7283094]Kamanda mbona unataka kulazimisha CCBRT siyo mali ya Dr.Slaa ameteuliwa tu mjumbe wa bodi.
[/QUOTE]
Dr slaa tumsifu yesu kristo nadhani utakuwa umeitikia,

hili swala la familia yako kushirikiana na mchungaji husika kujenga hospili kwa mgongo wa kanisa upo wazi sana tena mchungaji mwenyewe ni gwajima hakuna haja ya kujificha sana wakati swala liko wazi,

Kabula sijaenda mbali sana siku moja niliuliza swala hapa hukunijibu naomba kuuliza tena kwa nia njema kabisa yule baba askofu wa kwanza wa jimbo la katoliki karatu ni nani yako kunatarifa zimezagaa sana kuhusu wewe na baba askofu,kama ukitaka nifunguke zaidi ntafunguka mkuu.
 
Ritz,
Pamoja na kuwa nakuheshimu, lakini unazungumza utumbo bila utafiti. CCBRT Dr Slaa siyo " kateuliwa tu..." Kama unavyotaka kuonyesha. Dr Slaa " Founder" wa CCBRT na ni mwenyekiti wa Board. Pamoja na Disability Hospital CCBRT ina programs nyingi ikiwa ni pamoja na maboresho ya Vituo 14 vya Afya Jijini Dar na Maboresho ya Hospitali za Amana, Temeke na Mwananyamala kabla ya kufungua Hospitali ya Mama na Mtoto. Kazi hizo zote zinafanyika bila siasa kwa kuwa kwenye Maendeleo hakuna siasa. Wakuu, nimekwisha kuweka msingi wa ukweli, sitajibizana ten a na Ritz. Hata hivyo nimalizie kwa kumwambia Ritz kuwa huo ndio uzalendo, kuhudumia Watanzania bila kuchoka, na bila kuwabagua kwa rangi, itikadi, dini au wanakotoka. Kielelezo cha uzalendo ni matendo na siyo maneno wala propaganda.


QUOTE=Ritz;7283094]Kamanda mbona unataka kulazimisha CCBRT siyo mali ya Dr.Slaa ameteuliwa tu mjumbe wa bodi.
[/QUOTE]

Dr endelea na majukumu mazito achana na hawa vijana ambao hii kwao uwaingizia kipato na mkono kwenda kinywani!!!!!
 
Dr.W.Slaa,

Jibu hoja siyo kuzunguka, CCBRT ni mali ya familia ya Dr.Slaa?

Acha umburula, rudi kwenye mada uliyoisisi uko wapi ushahidi wa dk slaa kuanzisha hospitali na kukwepa kodi? Kama unahamu ya kuwafaahamu wamiliki wa CCBRT anzisha uzi au muulize akupe orodha ya wamiliki na yeye atakuambia kuwa ni nani pale....come back to the point usianzishe mada ndani ya mada.....uthibitisho meeeen.....

 
Dr slaa tumsifu yesu kristo nadhani utakuwa umeitikia,

hili swala la familia yako kushirikiana na mchungaji husika kujenga hospili kwa mgongo wa kanisa upo wazi sana tena mchungaji mwenyewe ni gwajima hakuna haja ya kujificha sana wakati swala liko wazi,

Kabula sijaenda mbali sana siku moja niliuliza swala hapa hukunijibu naomba kuuliza tena kwa nia njema kabisa yule baba askofu wa kwanza wa jimbo la katoliki karatu ni nani yako kunatarifa zimezagaa sana kuhusu wewe na baba askofu,kama ukitaka nifunguke zaidi ntafunguka mkuu.
[/QUOTE]
Acheni bange na kuvuta cocaine nyie maccm wekeni ushahidi hapa
 
Mbona wewe umeandika pumba kwa kutumia nguvu nyingi.
Mkuu, kama wewe unatumia nguvu kujibu pumba, usifananishe na kila mtu. Huo nilioandika ndo uhalisia na nina hakika kuwa hata Dr Slaa mwenyewe hawezi kujibu. Dr slaa akikamatwa kisawasawa anakimbilia kwa mods ili waondoe uzi
 
kiukweli slaa hana uadilifu wowote kwenye jamii hii naye ni fisdi tu kama mafisadi wengine kama akina mengi.
 
Kilichonifurahisha kwenye hii thread ni jinsi magamba walivyokuwa wamejipanga kuchafua hali ya hewa!! Wakati nashangaa issue gani ya maana hapa Pasco akafunga thread kwa post yake ya kwanza kabisa.
 
Last edited by a moderator:
Rits kabla hujapost kitu njoo na data za uhakika
amekwepa kodi kivipi? kwa namna gani? hospitali hiyo inamilikiwa na nani?
nani shareholder? who are the directors? imesajiliwa Brela lini?
njoo na vielelezo vinavoonyesha kakwepaje kodi na kodi kiasi gani?
Mke wa Dr Sla kwenda Japan sio ishu? na wala wajapan kuja sio ishu hapa
Kama askofu ndio mmiliki wana misamaha ya kodi,
na kwa hili kama linahusu Mke wa Sla,utamtaje Dr Sla kama ndio mkwepaji wa Kodi?
njoo na data za uhakika tumuumbue Dr Slaa. la sivo
ni sawa na unapost udaku unaongolewa kwenye vijiwe vya kahawa.
 
Inabidi upigwe ban we gamba kwa kudanganya umma
Mkuu, si kla kitu ban zinafaa. Mambo mangapi tunasoma humu ni uongo mtupu lakini hakina ban? Hapa anayestahili kupigwa ban ni Dr Slaa kwa vile anatoa majibu mepesi na yasiyolingana na maswali aliyoulizwa. Haina maana sasa ya kutumia ID as a verified user
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom