Dr Slaa na Kuhalalisha Gongo: Kwanini Yupo Sahihi

Status
Not open for further replies.
Mchambuzi maoni yako ni sahihi. Njia sahihi ni kudhibiti kwa mtindo tofauti na si kuzuia. Mpaka sasa kuzuia huko kumefeli pamoja na wanao piga kelele kwamba si maadili kuruhusu gongo. Watu wanakunywa kidicho bora. Kuna watu serikalini wamesomeshwa kwa pombe hii 'chafu'. Kwahiyo pamoja na burudani, gongo pia ni source of income ya watu wengi vijijini. Ruhusa itakayoweka viwango na mfumo wa utengenezaji mzuri utaleta mapinduzi ya aina yake na kuibua wazalishaji 'John walker' wa kitanzania.
 
Gongo ni Pombe Haramu, serikali ilishafanya utafiti na kujiridhisha kuwa ni hatari kwa Mtanzania kutumia Pombe hii kali inayotengenezwa kienyeji, Serikali kwa kuwapenda wananchi wake ikapiga marufuku kinywaji hiki.

Umenena vyema ilipigwa marufuku kwa sababu ni hatari kwa kutengenezwa 'kienyeji'. Je mazingira ya kienyeji yakibadilishwa yakawa ya kistaarabu na kisasa, inaweza kuruhusiwa?
 
Ifike mahali tuwaze mambo ya msingi zaidi. Kama vinywaji vikali vipo varieties za kutosha kabisa, watanzania hawana shida ya vilevi. Changamoto zinazomkabili Mtanzania, hili la kukosa kilevi cha bei rahisi halipo.

kwahiyo hoja ya msingi ni kwamba variety ya vinywaji imetosha; Fine, tukibakia kwenye hoja ya variety kwa sasa, gongo ni kinywaji ambacho kimekuwepo nchini kwa miaka hamsini au zaidi, huku vilevi vingine, hasa vya kigeni (imported) lakini pia hivi vipya vinavyozalishwa na TBL, Serengeti n.k (hata konyagi imeikuta gongo) vikizidi kumiminika sokoni kila kukicha, na vyote hivi vimeikuta gongo. Kwanini suala la variety zinatosha liwe applicable kwa gongo tu, tena ambayo imetangulia sokoni siku nyingi, lakini hivi vilezi vingine vipya hamsemi vinatosha na badala yake mnakimbilia kukaba kodi huko kupata fedha za to run the bureaucracy? Hoja yako ingekuwa na mashiko iwapo:

1. Serikali ingekuwa haitegemei kwa kiwango cha kupitiliza, utozaji wa kodi kwenye vilevi;
2. Serikali ya TANU (CCM) ingekuwa haijawahi kuja na hoja hii kama nilivyojadili.
3. Serikali ingesema kwanini Mbege na Chibuku ni halali lakini sio gongo.

Na hakuna sehemu nimejadili kwamba watanzania wana shida ya vilevi, na hiyo sio hoja ya msingi, naona unajaribu kuja na political spinning (pengine ni mtumwa wa Lumumba, kama sio niwie radhi);

Hoja ya msingi hapa ni the economics and health issues nilizojadili ambazo kwa ustadi mkubwa, unazikwepa;
 
Imeruhusu pombe zipi ambazo ni Salama? wajua Gongo haina tofauti na Konyagi? na konyagi ukinywa nyingi unakufa! ndio na gongo vile vile nyingi una ndei

Ndio haya haya ya double standards ya serikali ninayoijadili; Mwezi uliopita, ndugu zangu kijijini Singida wamezika mtu ambae alipata fedha za mavuno, akanunua konyagi kubwa tatu na kuanza kuzinywa kwa sifa kavu kavu kwa mtindo wa 'tarumbeta' moja baada ya nyingine ndani ya dakika tano. Alipofikia chupa ya pili na nusu, akaanguka na kufariki hapo hapo; Na taarifa kama hizi zipo nyingi; Konyagi (sio zote) pia zina matatizo ya viwango;
 
Mchambuzi,

maomba uipandishe hii post ili wafuatiliaji waweze kujua exactly kile alichosema dr slaa na hiki unalichoweka wewe ili tuwe tunajua kwa usahihi tunachokijadili.

Dr. Slaa: Tukishika Dola tutaruhusu utengenezaji wa pombe ya gongo kisheria
Saturday, 14 December 2013 ·


Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimetoa mpya baada ya kueleza kuwa kitakapofanikiwa kushika dola kitaruhu Shirika la Viwanda Vidogo Vidogo (SIDO) kutengeneza mitambo ya kutengenezea pombe aina ya gongo. Katibu Mkuu wa Chadema, Dk.Willbroad Slaa, akizungumza na wananchi wa Jimbo la Kasulu Vijijini alisema kama gongo itatengenezwa kwa mitambo maalum itaondoa mianya ya rushwa kwa polisi ambao wamekuwa wakiwakamata wanaotengeneza kwa kificho na kuwafanya vitega uchumi vyao.


"Gongo sasa hivi ni haramu sababu inatengenezwa kwa kificho katika mazingira machafu, tukishika dola tutataka SIDO itengeneze mitambo ya kutengeneza gongo ili iwe katika hali ya usafi," alisema.


Mitambo hiyo itakayotengenezwa na SIDO itakapouzwa itaiingizia mapato serikali pia wauzaji wa gongo watafanya biashara hiyo kwa amani tofauti na sasa ambapo wanaifanya kwa kificho na wakikamatwa fedha zote wananufaika polisi.


Dk. Slaa alisema hata suala la kukamata watu wanaotengeneza silaha linapaswa kuangaliwa upya kwani wanaokamatwa wakifanya kazi hiyo wangekuwa wanashikiliwa kwa muda na baadaye wanapelekwa katika kiwanda cha serikali cha kutengenezea silaha ili watuhumiwa hao wapeleke ujuzi huo huko badala ya kuwafunga jela.


Dk. Slaa alisema matatizo yote yanatokana na wasomi kutofikiri namna ya kuisogea nchi mbele kimaendeleo.


"Nchi hii imelala, imechoka sababu waliopewa madaraka wamelala, wamejisahau hawatambui kuwa wamepewa nafasi hizo ili kuwatumikia wananchi," alisema.


MTAMBO WA KUPIKIA GONGO KATIKA PICHA.


CHANZO: NIPASHE
 
Mkuu ZeMarcopolo,

All that said and done, suala la msingi hapa ni jinsi gani Dr. Slaa has stimulated my thinking; Swali linalofuatia kwako ni je:
· Kuna haja ya kuhalalisha gongo au hakuna haja?

Binafsi naamini kwamba kuna haja ya kuhalalisha gongo, na nikaenda mbali na kujadili kwanini nafikiri hivyo na nipo katika maandalizo ya sehemu ya pili ya mada yangu. Tumuache Dr. Slaa kwa sasa, badala yake, mimi na wewe tuingie katika mjadala ambao umekuja baada ya Dr. Slaa kusema neno moja tu la msingi kwamba kuna haja ya kuhalalisha gongo, hoja ambayo nimeiendeleza kama ulivyokwisha soma #1 . Nadhani kwa mtindo huo, tutaacha kujadili personality (DR. Slaa) na kujadili ISSUE (whether to legalize or continue to ban Gongo).

Nimejadili kwamba ndio ipo haja, na kwa ufupi (rejea kwa kirefu bandiko namba moja), nimejikita zaidi katika kuchambua juu ya umuhimu wa serikali kuhalalisha gongo kwa manufaa ya uchumi wa mtengenezaji, afya ya mnywaji, pamoja na multiplier effect ya kuhalalisha pombe za namna hii katika uchumi wa taifa, hasa katika nchi ambayo serikali yake inatambua vilezi vingine vya kienyeji kama kama vile mbege, chibuku, chimpumu, lakini vile vile vinywaji vya kigeni ambavyo ni moja ya vyanzo vikuu vya kodi ya serikali. Tanzania ingekuwa ni nchi ambayo imepiga marufuku vilevi vyote kwa mujibu wa sheria, hoja yangu na ile ya Dr. Slaa zingekosa mashiko.

What are your counter arguments katika hili? Kumbuka hata Serikali ya TANU chini ya Nyerere ilifikiria kuhalalisha pombe hii kwa hoja inayofanana sana na ya Dr. Slaa miaka 30 baadae; Kilichoikwamisha TANU ni gharama kwa mnywaji kutokana na regulation and licensing effects on the producer. Kwa vile suala hili ni more socio-economic, huku siasa ikiwa ni daraja tu la kuitekeleza au kutoitekeleza kupitia sera na udhibiti, political spinning haina nafasi hapa, tulijadili bila ya kujali itikadi za vyama.

Mkuu,

Kwenye kichwa cha habari yako unasema "Dr. Slaa na kuhalalisha gongo..". Unaosema hutaki kujadili alichosema Dr. Slaa badala yake twende moja kwa moja kwenye kile ulichoandika unakuwa unakimbia mjadala ambao umeuanzisha wewe mwenyewe.

Kwa vile umetaka twende kwenye kile ulichosema hapa na kuacha mjadala uliouanzisha, mimi pia nitakubaliana na wewe. Tujadili kuhalalishwa kwa gongo, bila kumhusisha Dr. Slaa or personalities.

Here I come,

Gongo maana yake ni pombe kali inayotengenezwa kiholela ambayo pamoja na vitu vingine huwa na sumu inayoathiri afya ya binaadamu.

Pombe hii ina madhara ya kibaiolojia, kisaikolojia, kiuchumi, na kijamii. Ili kufuisha urefu wa post hii nitagusa kila madhara kwa juu juu tu na nitakuwa nikiingia deeper kadri mjdala utakavyoendelea.

Madhara ya kibaiolojia: Yapo madhara ya muda mfupi na muda mrefu kwa afya ya binaadamu kama upofu, magonjwa ya ini, kudhoofisha kinga ya mwili, magonjwa ya moyo na mishipa ya damu, kuunguza uwezo wa kuconcentrate.

Kisaikolojia: Matumizi ya gongo ya muda mrefu yanamjengea mtu hali ya kutokujiamini na hivyo kupunguza uwezo wake wa kufanya kazi.

Kiuchumi: Ni dhahiri kwamba watu wanaokunywa gongo wanashiriki kidogo katika GDP kuliko wale wasiokunywa gongo.

Kijamii: Gongo imekuwa sababu ya mahusiano mabaya katika jamii. Wanandoa kuachana, vijana kujifunza tabia ya wizi.

Kwanini gongo haipaswi kuruhusiwa kisheria?

Pamoja na kwamba gongo ina madhara mengi, lakini sababu kuu ya gongo kutokuruhusiwa kisheria ni moja, ambayo ni kutokukidhi viwango vya ubora unaohakikisha usalama wa wanywaji wake.

Leo hii iwapo mpika gongo atahakikisha kuwa anachouza ni salama kwa matumizi ya binaadamu, basi hatakatazwa kukiuza. Taratibu za yeye kupewa kibali cha kutengeneza, kusambaza na kuuza pombe salama zipo.

Unaposema gongo iruhusiwe ni kwamba unasema pombe kali inayoweza kupofua watu macho iruhusiwe kuuzwa. This is exactly what you just said in your post.

Je, unadhani ni sahihi kurusu pombe inayopofua macho kuuzwa just because tunataka muuzaji apate kipato?
 
Mkuu,

Kwenye kichwa cha habari yako unasema "Dr. Slaa na kuhalalisha gongo..". Unaosema hutaki kujadili alichosema Dr. Slaa badala yake twende moja kwa moja kwenye kile ulichoandika unakuwa unakimbia mjadala ambao umeuanzisha wewe mwenyewe.

Kwa vile umetaka twende kwenye kile ulichosema hapa na kuacha mjadala uliouanzisha, mimi pia nitakubaliana na wewe. Tujadili kuhalalishwa kwa gongo, bila kumhusisha Dr. Slaa or personalities.

Tutazunguka zunguka bila maana, lakini la msingi ni kwamba ujumbe wa Dr. Slaa ni kwamba gongo ihalalishwe.

Here I come,

Gongo maana yake ni pombe kali inayotengenezwa kiholela ambayo pamoja na vitu vingine huwa na sumu inayoathiri afya ya binaadamu.

Pombe hii ina madhara ya kibaiolojia, kisaikolojia, kiuchumi, na kijamii. Ili kufuisha urefu wa post hii nitagusa kila madhara kwa juu juu tu na nitakuwa nikiingia deeper kadri mjdala utakavyoendelea.

Madhara ya kibaiolojia: Yapo madhara ya muda mfupi na muda mrefu kwa afya ya binaadamu kama upofu, magonjwa ya ini, kudhoofisha kinga ya mwili, magonjwa ya moyo na mishipa ya damu, kuunguza uwezo wa kuconcentrate.

Kisaikolojia: Matumizi ya gongo ya muda mrefu yanamjengea mtu hali ya kutokujiamini na hivyo kupunguza uwezo wake wa kufanya kazi.

Kiuchumi: Ni dhahiri kwamba watu wanaokunywa gongo wanashiriki kidogo katika GDP kuliko wale wasiokunywa gongo.

Kijamii: Gongo imekuwa sababu ya mahusiano mabaya katika jamii. Wanandoa kuachana, vijana kujifunza tabia ya wizi.

Kwanini gongo haipaswi kuruhusiwa kisheria?

Pamoja na kwamba gongo ina madhara mengi, lakini sababu kuu ya gongo kutokuruhusiwa kisheria ni moja, ambayo ni kutokukidhi viwango vya ubora unaohakikisha usalama wa wanywaji wake.

Leo hii iwapo mpika gongo atahakikisha kuwa anachouza ni salama kwa matumizi ya binaadamu, basi hatakatazwa kukiuza. Taratibu za yeye kupewa kibali cha kutengeneza, kusambaza na kuuza pombe salama zipo.

Unaposema gongo iruhusiwe ni kwamba unasema pombe kali inayoweza kupofua watu macho iruhusiwe kuuzwa. This is exactly what you just said in your post.

Je, unadhani ni sahihi kurusu pombe inayopofua macho kuuzwa just because tunataka muuzaji apate kipato?
Nitakurudia kupitia bandiko langu la sehemu ya pili ambalo litajibu hoja zako hizi muhimu;
 
Ndio haya haya ya double standards ya serikali ninayoijadili; Mwezi uliopita, ndugu zangu kijijini Singida wamezika mtu ambae alipata fedha za mavuno, akanunua konyagi kubwa tatu na kuanza kuzinywa kwa sifa kavu kavu kwa mtindo wa 'tarumbeta' moja baada ya nyingine ndani ya dakika tano. Alipofikia chupa ya pili na nusu, akaanguka na kufariki hapo hapo; Na taarifa kama hizi zipo nyingi; Konyagi (sio zote) pia zina matatizo ya viwango;

Hapa unakosea. Thinking ya namna hii haiwezi kutufikisha popote.

Unajua mtu anaweza kufa hata kwa kula ugali iwapo ataula hovyo.

Au soda, hivi mtu akinywa soda non stop, atakuwa salama? Tukiuendesha mjadala kwa design hii tutapoteza mwelekeo.

Kama unataka gongo iruhusiwe kwa sababu unadhani gongo na konyaji ni vinywaji sawa, basi inabidi turudi hatua nyingi sana nyuma kabla hatujaanza kujadili kuhalalishwa au kutokuhalalishwa kwa gongo.
 
Tutazunguka zunguka bila maana, lakini la msingi ni kwamba ujumbe wa Dr. Slaa ni kwamba gongo ihalalishwe.


Nitakurudia kupitia bandiko langu la sehemu ya pili ambalo litajibu hoja zako hizi muhimu;


Mkuu Mchambuzi,

Naona na wewe umeana mchezo kama wa Mwanakijiji!

Huna sababu ya kuleta hoja nusu nusu. Summarize na ulete kitu kilichokamilika.

Hii ya kuandika maneno marefu inafaa kwenye zile essays wanazosema andika maneno 800 au idadi fulani. Hapa JF lets try to be as brief as possible, ili tunapojadili tusiache mianya kama hii ya kungoja sehemu ya pili etc.

Kama unashindwa kabisa kuwa brief, basi andika abstract halafu ndio uendelee na maelezo marefu ili kutoa picha kamili ya ujumbe uliotaka kuufikisha.
 
Ndugu Mchambuzi Mimi jambo hili naliangalia zaidi katika muktadha wa kisiasa kuliko muktadha wa kiuchumi kwa mazingira ya Tanzania. Dr.Slaa ni kiongozi wa kisiasa, Lengo lake kuu ni kupata uungwaji mkono na jamii ya walio wengi kabla ya kitu chochote kile.

Ndugu Mchambuzi unapotaja neno gongo katika mazingira ya tanzania kutokana na kanuni za kimaadili na kiutamaduni ni neno lisilo na mvuto kwa jamii ya walio wengi. Kwa hiyo jambo hilo likishupaliwa, watu hawataliangalia katika misingi ya kiuchumi nakiafya bali kimaadili na hivyo kufanya mwanasiasa anayesimamia hiyo ajenda kupotezakukubalika.Anayekataa na ajaribu aone.Ni sawa na concept ya kuhalalisha ukahaba (kumradhi) anayetaka na ajaribu kuja na ajenda hii aone kama atapata uungwaji mkono na jamii ya kitanzania.Suala kwa hoja za aina hii si uchumi wala Afya; ni kanuni za kimaadili za jamii.
betlehem

kasome tena ndugu nadhani hujamsoma Mchambuzi.

1. sio kila kitu mwanasiasa anahitaji kungwa mkono, kuna vitu vingine vikifanyika hakukna atakaye kuunga mkono, wengi watapinga lakini mwisho wasiku ukisisimama kidete watakuja kukubali. Mfano MKAPA alisimamaia ulipaji wa madeni nje ya nchi na tukafunga mkanda na hakika hakuna aliyekubali yale, lakini baada ya mika si chini ya 3/4 Tulisamehewa madeni kwa nia yetu nzuri ya kulipa na misaada zaidi tukapa, na dr.dr.dr.dr.dr. kikwete alivyo ingia alipata nafasi ya kukopa zaidi na zaidi hadi leo mnajivunia kukopa lakini ukweli ni kutokana na uamuzi wa kijasiri wa Mkapa wa kulipa madeni.

2. Mchambuzi amekuambia kinachosababisha GONGO haramu ni huko kwenu kuuiita haramu lakini zaiid ya hapo, haina tofauti na Kibuku, mbege, jackdaniel, henken an nyingine.
 
Last edited by a moderator:
Tutazunguka zunguka bila maana, lakini la msingi ni kwamba ujumbe wa Dr. Slaa ni kwamba gongo ihalalishwe.

Ujumbe wa Slaa kumbe hujauelewa.

Ujumbe wake sio gongo ihalalishwe. Ujumbe wake ni kwamba polisi wasiwabughudhi wauza gongo. Njia aliyopendekeza ya kuondoa bughudha hiyo ni kuhalalisha gongo.

Problem aliyokuwa anaadress Slaa ni polisi kuwakamata na kuwaomba rushwa wauza gongo.
 
gongo ikiruhusiwa, kwanza, naamini gharama yake itakuwa juu may be sawa sawa na konyagi, pili naamini hata watengenezaji wake watabadilika, mtanzania wa kipato cha chini hatakuwa na uwezo wa kuitengeneza tena (kumbuka lengo ni kuinua kipato cha mtanzania wa chini), tatu, hata watumiaji watabadilika, naamini watanzania wa kipato cha chini hawatakuwa na uwezo wa kuinunua.
kama gongo ikiruhusiwa naamini haitamsaidia mtanzania wa hali duni moja kwa moja labda in indirect way!
Mwisho, zitaibuka aina mbili za gongo, gongo haramu (ambayo itakuwa na madhara yale yale iliyonayo gongo ya sasa, itaendelea kutengeneza nafasi za askari kuomba rushwa n.k) aina ya pili itakuwa gongo halali ambayo itakuwa haina tofauti na Tanzania konyagi (kumbuka inatengenezwa Tanzania hii), viroba, vodka n.k
 
Ujumbe wa Slaa kumbe hujauelewa.

Ujumbe wake sio gongo ihalalishwe. Ujumbe wake ni kwamba polisi wasiwabughudhi wauza gongo. Njia aliyopendekeza ya kuondoa bughudha hiyo ni kuhalalisha gongo.

Problem aliyokuwa anaadress Slaa ni polisi kuwakamata na kuwaomba rushwa wauza gongo.

Msipindishe mambo,Dr slaa amesema hivi

Gongo sasahivi ni haramu kwa sababu inatengenezwa katika mazingira machafu, tukishika dola, tutataka SIDO itengeneza mitambo ya kutengeneza gongo ili iwe katika hali ya usafi


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
2. Mchambuzi amekuambia kinachosababisha GONGO haramu ni huko kwenu kuuiita haramu lakini zaiid ya hapo, haina tofauti na Kibuku, mbege, jackdaniel, henken an nyingine.

Kwanza, sio ukweli kwamba gongo haina tofauti na heineken. Tofauti ya kwanza kubwa ni kwamba heineken ukichukuan kopo lake unaona vitu vyote vilivyomo vimeandikwa na unajua unakunywa nini. Gongo hata aliyetengeneza hajui composition yake.

Lakini pili, kufanana na haineken au mbege haimaanishi vyote vimove towards kuhalalishwa. Kwanini usiseme Mbege, Kibugu, Jack Daniels na Heineken zipigwe marufuku badala yake unataka gongo ihalalishwe? Kama wewe ni raia unayoitakia mema nchi yako na umegundua kuwa hizo pombe nyingine zina madhara kama ya gongo, nilitegemea move yako iwe kutaka hizo pombe zipigwe marufuku kama gongo, sio kutaka gongo ihalalishwe.

Ni sawa na kijana mwizi anadunda mitaani. Kijana mwingine mwizi amefungwa jela. Halafu wewe unalalamika yule mwizi aliye jela atolewe kwa sababu huyu mwingine yuko mtaani! Nilitegemea kama raia mwema utoe taarifa ili huyu mwizi mwingine naye afikishwe kwenye vyombo vya sheria badala ya kutumia nguvu nyingi kutaka yule aliye jela atolewe.
 
Msipindishe mambo,Dr slaa amesema hivi

"Gongo sasahivi ni haramu kwa sababu inatengenezwa katika mazingira machafu, tukishika dola, tutataka SIDO itengeneza mitambo ya kutengeneza gongo ili iwe katika hali ya usafi"

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Kwahiyo wewe Mchambuzi unaamini kuwa tatizo la gongo ni uchafu?

Tukitengeneza kinywaji chenye composition ileile ya gongo pale MovenPick unadhani ni sahihi kusambazwa kwa wanywaji?

Je, SIDO wanaleta vipi usafi? Usafi unakuwaje swala la SIDO?

Soma habari hii ya Nipashe kuona alichokuwa anaadress Slaa
Katibu Mkuu wa Chadema, Dk.Willbroad Slaa, akizungumza na wananchi wa Jimbo la Kasulu Vijijini alisema kama gongo itatengenezwa kwa mitambo maalum itaondoa mianya ya rushwa kwa polisi ambao wamekuwa wakiwakamata wanaotengeneza kwa kificho na kuwafanya vitega uchumi vyao.
 
Kwahiyo wewe Mchambuzi unaamini kuwa tatizo la gongo ni uchafu?

Tukitengeneza kinywaji chenye composition ileile ya gongo pale MovenPick unadhani ni sahihi kusambazwa kwa wanywaji?

Je, SIDO wanaleta vipi usafi? Usafi unakuwaje swala la SIDO?

Kabla ya sijajibu swali lako, je unakubali kwamba hilo ndilo alilosema dr slaa?


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Sema sahihi, hi hi hi, sio sahii
Natambua hilo, lakini it was too late, only moderators ndio wanaweza rekebisha;asante kwa kukumbushia;


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Nakupongeza sana Mchambuzi kwa mjadala huu na uchambuzi ulioufanya kwa mtazamo wa kitaifa zaidi badala ya kiitikadi.

Tumejifunza historia jinsi mengi ambayo yalishaasisiwa na wazee wetu yamekuja kupigwa vita na wakoloni kwa kuhalalisha bidhaa zao ambazo zilichukua nafasi ya soko mbadala, jitihada za wazee wetu zilitokana na mianzo hali kadhalika njia hizo hizo, iwe imani, uundwaji wa vitu mbalimbali na utamaduni.

Narejea kwenye uchambuzi wa
Mchambuzi kwamba alichokisema Dr. Slaa ndio uzalendo ambao utatufikisha kuwa na uwezekano wa kubuni kinywaji hicho ambacho kwa sasa tunavyo vingi vya kiwango cha alcohol hiyo kinachozalishwa toka nje au kuzalishwa nchini na makampuni ya nje. Kwa nini sisi wenyewe tusiendeleze kile ambacho tayari kinafanyika na kinachotakiwa ni tu kuboresha mazingira, vitendea kazi na nafasi ya soko? Hivi vinywaji vya kutoka nje vilianza kwa njia za kienyeji hivi hivi, nimeshuhudia mwenyewe nilipotembelea maonyesho ya makampuni yao yalivyoanza huko kwao.

Naweza kutamka wazi kwamba ni ujinga tunapopinga kila kitu hata kiwe chema kwa manufaa ya watanzania kwa vile tu kimetoka upande wa upinzani, hayo ndiyo yanayotuangusha na kudidimiza juhudi za kujenga misingi ya maendeleo nchini.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom