Dr Slaa kutikisa Same Jumanne

Dr Slaa kutikisa Same Jumanne

Yule mama yake wa kambo wa LEMUTUZ atakuwa keshatia timu kutengeneza mambo,mama mchawi sana yule

Mchawi wake yupo sehemu inaitwa MSARANGA kule Kihurio. Unavuka ziwa Karamba, halafu unakwenda ndani kidogo kama unaelekea Mkundi ya Mnazi. Watu walisha wahi muona akigagula mtupu. Uongozi kaaaazi kweli kweli.
 
Mchawi wake yupo sehemu inaitwa MSARANGA kule Kihurio. Unavuka ziwa Karamba, halafu unakwenda ndani kidogo kama unaelekea Mkundi ya Mnazi. Watu walisha wahi muona akigagula mtupu. Uongozi kaaaazi kweli kweli.

Mkuu Kanundu acha kuvua watu nguo.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Communist watu wanaoimba migogoro na makundi ni mawakala wa Magamba wanaotumwa hapa JF kuchochea mambo ambayo hayapo.

Nimeshangaa kuna mtu mmoja anajiita mwanachadema anaitwa Tuko kaanza kuleta mambo ya CCM hapa eti Chadema ina makundi.

Wao wakipika majungu mtandaoni Dr Slaa yuko busy kuimarisha chama vijijini.

C.c Mwita Maranya, SEBM, Shardcole, Crashwise, Mungi, Ben Saanane.

Mkuu Wangu
PHP:
Molemo

Huyu tunamjua na hatupi shida.historia ya post zake za nyuma ukiijua hata thread yake utajua muelekeo na malengo yake
 
Mkuu Communist watu wanaoimba migogoro na makundi ni mawakala wa Magamba wanaotumwa hapa JF kuchochea mambo ambayo hayapo.

Nimeshangaa kuna mtu mmoja anajiita mwanachadema anaitwa Tuko kaanza kuleta mambo ya CCM hapa eti Chadema ina makundi.

Wao wakipika majungu mtandaoni Dr Slaa yuko busy kuimarisha chama vijijini.

C.c Mwita Maranya, SEBM, Shardcole, Crashwise, Mungi, Ben Saanane.

Mkuu Molemo!

Kazi iliyoko mbele ya CHADEMA ni kukoboa na kusaga. Hii habari ya hao walio zoea mipasho ya TOT kama Mwenyekiti wao tuachane nao Mkuu. Kwanza kuchangia mada zao ni kuwapa ujiko. Tukizi puuza watakosa la kuzusha na kuandika.

Tafadhali Mkuu, tunaomba utupatie yaliyo makini na ya kujenga chama. Mengine acha "WAFU WAZIKE WAFU WAO".
 
kwa sasa hakuna mwanasiasa anaemkaribia Dr.slaa, huyu ndo rais wa awamu ya 4 ambae hajaapishwa.
ila awamu ya 5 tutamuapisha kwa lazima....
 
wana Same tunamuomba Dr.W.Slaa atembelee eneo la Chome ambako kuna uharibifu mkubwa wa mazingira kutokana na mradi wa uchimbaji wa madini ya bauxite. tunaiomba Chadema iliangalie suala hili kwa umakini zaidi kwasababu mazingira ya msitu wa Shengena ambao ndiyo chanzo cha maji kwa wilaya nzima ya Same yanaathiriwa kwa kiasi kikubwa. athari za uharibifu huo wa mazingira umeanza kuonekana katika mto Saseni.

tunawaomba CHADEMA waliwasilishe tena suala hili BUNGENI, pamoja na kwa wanaharakati wa mazingira ndani na nje ya nchi. suala hili lilifika bungeni ambapo mbunge wa Same Mashariki, Mama Kilango Malecela alidai ana video zinazoonyesha uharibifu wa mazingira msitu wa Chome. WAZIRI MKUU alitoa amri bungeni kwamba uchimbaji wa bauxite usimamishwe, kitu ambacho kilifanyika. Muda mfupi baada ya kikao cha bunge kuisha, mwekezaji amekwenda baraza la mazingira na kupata barua ya kutengua agizo la Waziri Mkuu, na sasa hivi uchimbaji unaendelea kwa kasi ya kutisha.

Wananchi tunataka kujua huyu mwekezaji ametoa wapi kiburi cha kutengua amri na maagizo ya Waziri Mkuu? Je, kwanini Waziri Mkuu, Waziri wa Mazingira, pamoja na wabunge wa Same[Malecela, Mathayo] wote wamekaa kimya huku maisha ya wananchi yakiathirika kiasi hiki? Je, viongozi hao wamenunuliwa?? Serikali iko wapi? CCM iko wapi?

Kwasababu wabunge wa CCM wameshindwa kutusaidia wananchi wa Same sasa tunaomba msaada wa Chadema tuone na nyinyi mtatusaidia vipi.

nakala: Zitto, John Mnyika, Mikael P Aweda, Josephine, Molemo, Mwita Maranya, Edwin Mtei, MTENGETI, Nape Nnauye

Nimefanikiwa kuongea na wana Same wawili watatu na kuna kila dalili kuwa hili suala la uchimbaji madini lina mkono wa mtu mzito sana serekalini. Kwa taarifa nilizozipata ni kwamba mwanzoni Mkuu wa wilaya pamoja na mbunge walikua wakali sana na walitoa mchango mkubwa sana hadi uchimbaji huo kusitishwa. Baada ya mchimbaji kuruhusiwa tena, si mkuu wa wilaya wala mbunge ambaye amethubutu tena kunyanyua mdomo wake, wanaonekana wameingia woga! wametulia tuliii!!

Anyway tukiachana na hilo la uharibifu wa mazingira, naamini kabisa kuwa wakati umefika sasa kwa ndugu zangu wapare wa Mwanga na Same kufanya mabadiliko. Mkoa mzima wa Kilimanjaro hizi ndizo wilaya pekee ambazo zimegoma kuitupa CCM lakini madhara yake yanaonekana wazi kwa kuwa ndizo zinazoshika mkia kwa maendeleo mkoani humo. Shule zao ndo zinashika mkia kila mwaka, wao ndio wana njaa kila mwaka, wagonjwa wanapelekwa wilaya nyingine kutibiwa, hakuna ajira, shida kubwa ya maji na barabara zisizopitika kipindi cha mvua japo zina umuhimu mkubwa.

Wana Same mna option ya kuacha mambo kama yalivyo muendelee kudidimia kwenye umaskini au kuamua kufanya mabadiliko na kuboresha maisha yenu ya kila siku.
 
Kiongozi Mkuu wa Upinzani Nchini ambaye ni Katibu Mkuu wa Chadema Dr Wilbroad Peter Slaa anatarajiwa kuhutubia mkutano mkubwa wa hadhara mjini Hedaru-Same Jumanne tarehe 15 January 2013.

Mbali na kuhutubia mkutano wa hadhara Dr Slaa anatarajiwa pia kupokea wanachama wapya wa Chadema,kufungua ofisi za Chadema kata ya Hedaru na kuzindua matawi ya Chadema maeneo ya Hedaru,Makanya na Same.

Tayari mji wote wa Same na vitongoji vyake kuna gumzo kubwa kuhusu Ujio huo wa Dr Slaa ambaye anaonekana kama kiongozi aliyevuka vizingiti vingi vya mahasimu wake huku nyota yake ikizidi kung'aa kila siku kuelekea mwaka 2015

Kwa sasa Katibu Mkuu huyo amejichimbia mkoani Kilimanjaro akiongoza vikao vizito vya Sekretariati yake ikiwa ni maandalizi ya operesheni kubwa ya kuimarisha chama chake kwa mwaka huu.


Hivi nani anachagua Kiongozi Mkuu wa Upinzani? Hivi vyeo vinatoka wapi? Kama kuna Kiongozi Mkuu wa Upinzani je naweza kuruhusiwa kusema Kiongozi Mkuu wa Utawala ambaye ni Rais wa Jamuhuri anatembelea China?
 
hakuna kulala mpaka kieleweke, amsha amsha kwa kwenda mbele. Hawa "jamaa" wametunyonya vya kutosha sasa tuseme ccm basi tena, let it perish completely.
 
Hivi nani anachagua Kiongozi Mkuu wa Upinzani? Hivi vyeo vinatoka wapi? Kama kuna Kiongozi Mkuu wa Upinzani je naweza kuruhusiwa kusema Kiongozi Mkuu wa Utawala ambaye ni Rais wa Jamuhuri anatembelea China?

Kama imekuuma mkuu wangu kanywe mataputapu ulale
 
Kama imekuuma mkuu wangu kanywe mataputapu ulale

Dr. Slaa hawezi kuwa na cheo cha kufikirika (imaginary). Hakuna cheo au nafasi inayoitwa KIONGOZI MKUU WA UPINZANI. Vilevile Same Jumanne ni jina la mtu.
 
ImageUploadedByJamiiForums1358051483.849574.jpg

Hali sio nzuri hospitali ya wilaya, hapo ni maternity ward kina mama wanalala mzungu wa nne kwenye single bed.
 
Dr. Slaa hawezi kuwa na cheo cha kufikirika (imaginary). Hakuna cheo au nafasi inayoitwa KIONGOZI MKUU WA UPINZANI. Vilevile Same Jumanne ni jina la mtu.

Usikasirike sana mkuu wangu Zakumi unaweza kupata BP bure..! Relax man...!
 
Last edited by a moderator:
Kanundu; Hapo unapopita na kunitenga usirudie tena!


Mkuu Molemo!

Kazi iliyoko mbele ya CHADEMA ni kukoboa na kusaga. Hii habari ya hao walio zoea mipasho ya TOT kama Mwenyekiti wao tuachane nao Mkuu. Kwanza kuchangia mada zao ni kuwapa ujiko. Tukizi puuza watakosa la kuzusha na kuandika.

Tafadhali Mkuu, tunaomba utupatie yaliyo makini na ya kujenga chama. Mengine acha "WAFU WAZIKE WAFU WAO".
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom