Dr Slaa kutikisa Same Jumanne

Dr Slaa kutikisa Same Jumanne

Gogo la Choo,
kwa kweli wilaya ya same inasikitisha sana. Same ndiyo tunashika mkia mkoani kilimanjaro katika masuala ya elimu, afya, maji, kilimo, na mazingira. wananchi wana hamasa ya kutafuta maendeleo ila inachokosekana ni uongozi.

aisee ni kweli kabisaa..ukijaribu kupita maeneo ya vijijini utaona huruma jinsi Same ilivyo nyuma kielimu lakin watu wa thame saivi wameshamjua adui yao..asante sn Dr.kwa kufanikisha hili!!daahh!
 
Imetikisika, sasa tunahamia wapi? Na hamu na jimbo la mwigilu.
 
Kiongozi Mkuu wa Upinzani Nchini ambaye ni Katibu Mkuu wa Chadema Dr Wilbroad Peter Slaa anatarajiwa kuhutubia mkutano mkubwa wa hadhara mjini Hedaru-Same Jumanne tarehe 15 January 2013.

Mbali na kuhutubia mkutano wa hadhara Dr Slaa anatarajiwa pia kupokea wanachama wapya wa Chadema,kufungua ofisi za Chadema kata ya Hedaru na kuzindua matawi ya Chadema maeneo ya Hedaru,Makanya na Same.

Tayari mji wote wa Same na vitongoji vyake kuna gumzo kubwa kuhusu Ujio huo wa Dr Slaa ambaye anaonekana kama kiongozi aliyevuka vizingiti vingi vya mahasimu wake huku nyota yake ikizidi kung'aa kila siku kuelekea mwaka 2015

Kwa sasa Katibu Mkuu huyo amejichimbia mkoani Kilimanjaro akiongoza vikao vizito vya Sekretariati yake ikiwa ni maandalizi ya operesheni kubwa ya kuimarisha chama chake kwa mwaka huu.

Dr. Slaa tunakuomba ufike mpaka KIHURIO na pitia kutoka hapo Hedaru urudi mpaka kwenye kona mkono wa kulia UANZE KUPITA BARA BARA YENYE CHANGARAO HAKUNA LAMI TANGU NIZALIWE MPAKA LEO NINA MIAKA 53. JE NI KWANINI NJIA PANDA KWENDA MPKA KIHURIO HAKUNA LAMI? MBUNGE WETU ANNA MALECELA TULIDHANI BAADA YA KUPATA UBUNGE ATATUGOMBOA LAKINI MPAKA LEO HAKUNA LAMI? SHIDA NINI JAMANI?

DR. SLAA INGIA HAPO NA FANYA JAMBO
ASANTE
 
Chadema inabidi wajipange kweli kweli wawe na mikakati kamili ya nini cha kufanya iwapo wataongoza nchi 2015, maana nchi hii imeshageuzwa kichwa chini miguu juu, ndani nje, mbele nyuma na sasa inacharangwa mapanga....
 
Back
Top Bottom