Dr. Slaa hatimaye aibuka

Dr. Slaa hatimaye aibuka

Chadema aliondoka Zito Kabwe, madiwaniwa arusha mjini,na wengine wengi na inakwenda mbele
kwa hiyo dr. slaa akikosa hekima ya kutulia, na akaamua kuondoka, chadema bado itaendelea kama ni
MUNGU amewapa kibali, slaa ni mtu muhimu sana, ila anaweza asiwe na umuhimu kama akihamua kuondoka
MUNGU NAOMBA UIBARIKI CHADEMA. AAAMEN
 
Huyu mzee apunzike tu kwa amani asitake kutuchanganya watz kwa kauli zake banaa! yeye atuachie sisi wananchi tudili na ccm wenyewe. Au aende vocation Rwanda kama Lipumba ama nene!
 
Mi nilchojua slaa hakufurahishwa na ujio Wa lowasa yeye alkuwa anataka agombee urais yeye na ukawa hawakufanya kosa kumchagua lowasa kwa sbbu anauzika na anaushawishi Wa watu ningemshauri slaa arudi tuendelee kujenga chama

Kwa kuongezea ana sehemu yake kubwa tu ya kukamilisha mabadiliko tunayosubiri. Naamini ukimya wake una maslahi kwa taifa na chama chake.
 
Dr s. Anamaadili na anajitambua..... Kama 2010 mbowe na wabunge wa chadema walitoka bungeni wakidai dr silaa alishinda uchaguzi ila akaibiwa kuraa kwanini safariii hiii asiweze kushindaaa amaa walitudanganyaaa au deal la billion 10 ni la ukweli kwa kamanda wa angaa. Mzee wa mabisinessss

Uwezo wako wa siasa ni mdogo mno kutoa michango jukwaa hili sana sana ni za kichochezi zaidi kwani ushahidi wa hizo billion kumi huna na ushukuru ungeyaandika haya baada ya tarehe moja Sept. ungeizoea mahakama.Siasa sio msahafu au bibilia kwamba huwezi kuongeza au kupunguza yaliyoandikwa. Siasa hubadilika kufuatana na nyakati.Mikakati uliyoitumia miaka mitano nyuma na kukupa matokeo uliyoyapata sio lazima kuyatumia tena kwa uchaguzi unaofuata.Unaweza kufuata michache na kuongeza na inayoendana na kipindi ulicho nacho kwa wakati uliopo. Pia sio lazima umsimamishe mgombea yule yule aliezoeleka kwenye chama.Ndio maana serikali huhamisha watumishi ngazi mbali mbali hadi mawaziri sio kwamba hawawapendi au hawakufanya vizuri. Ni kwa kuwa wamezoeleka na wengine ni ili wakaendeleze maeneo mengine.Mwisho ukawa na washirika wake ni taasisi na sio mtu. Vyama na hata ukawa wana taratibu za kuwapata wagombea wao na mara nyingi kamati kuu za vyama hivyo hushirikishwa na kuridhia au kubadilisha.Hata huyo unaemtuhumu kutoa hizo billion kumi alipitishwa kwenye vikao hivyo na mwisho kuridhiwa na ukawa.Upepo umeshavuma na sasa nyeti za kuku zinaonekana.
 
CCM wakikuamulia hata kama Ulikuwa na msimamo mkali lazma utalegeza tu. Haya maviongozi makubwa yanataka kuharibu mambo saa za ukombozi kwa sababu kuna dili yanakula na CCM. ama kweli ukombozi Tanzania itatuchukua mda
 
Slaa asiwe na wasiwasi, Lowasa akiingia madarakani
tutamjengea Ikulu yake pale Karatu ataishi yeye na
first lady josefin mushumbusi kwa sababu tayari ni
rais wa mioyo yetu.
 
Nasikia CCM wameshampitisha kugombea ubunge karatu ... Huyu Mzee amejidhalilisha sana ... anatumiwa na waaidika wa mfumo ... Hivi pengo ni nani hadi Slaa ajiharibie kiasi hiki?

Acheni habari za kusikia vijiweni.
 
Dr. Slaa, asicheze na nguvu ya UMMA...!!

Akienda against UKAWA, atakuwa ktk hali mbaya sana...i hope kashaisoma namba...!!

He is NOT SPECIAL...period..!!!

Slaa sio MAARUFU kuliko Lowassa....!!!

Slaa hata angegombea UKAWA, asingeshinda...hili nina uhakika 100%...!!!

Mbowe is very GENIUS POLITICIAN... he knows exactly upepo unavuma wapi... na historia ya nchi hii itamkumbuka MBOWE milele... anajua siasa, Dr. Slaa kama alidhania siasa ni DINI arudi kanisani...kapotea...!!! Alishagombea urais akashindwa vibaya...aache uchu wa madaraka...anakera sana sasa, anajiona mtakatifu...? kwa lipi..?

Mtu anasusa kama demu...tupa kuleeeeeeee, hafai kwa ukombozi...tupa kuleeeeeeee...arudi upadre...!!

Team Lowassa @ work (mwagia majitaka tishio lolote...)
 
Nasikia CCM wameshampitisha kugombea ubunge karatu ... Huyu Mzee amejidhalilisha sana ... anatumiwa na waaidika wa mfumo ... Hivi pengo ni nani hadi Slaa ajiharibie kiasi hiki?

Ndugu yangu uelewe hakuna anaekataa uwezo wa Slaa kwenye siasa na wote tunakubali kuwa yeye ni muhimu sana chadema ila nae anaelewa chadema ni taasisi na sio mtu. Kugombea kwa Slaa 2010 ni baada ya kuombwa sana na chama na haikuwa utashi wake.Ukawa ni muungano wa vyama vinne kwa malengo makuu mawili.Kwanza kutetea katiba bora bunge la katiba na pili kuiondoa ccm madarakani kwa kumsimamisha mgombea mmoja kama ukawa ili kuweza kuiondoa.Tena nikizidi kukumbuka walikubaliana pia mapungufu ya takayajitokeza katika vyama wakati wa utekelezaji wa zoezi la kuiondoa ccm madarakani yatarekebishwa baada ya zoezi. Kwa hapa tukiwasema viongozi wa ukawa ni pamoja na wenyeviti na makatibu wa vyama washirika. Sasa mara hii yupo mwenzetu aliyeona pungufu tena kwake tu na kusahau dhamira nzima ya ukawa? Kwanini nalo hilo halikusubiri zoezi likamilike na bado tumwelewe ana nia nzuri?Hivi ni nani mwenye kuzijua siasa za nchi hii asiejua ukaribu wa askofu Pengo na ikulu ya magogoni na kuwa Slaa hawezi kutenda nje na maagizo ya kanisa lake?Hivi kakuaminisha nani kuwa mkristo ni mkristo tu kwa utawala wa Roma? Hapana utaungwa mkono tu kama ni mroma na tayari wanae huko ccm. Ya Lipumba siyazungumzii kwani mimi na hata Maalim Seif alimwelewa siku nyingi na madhaifu yake. Chukulia uchaguzi wa 2010 alimpigia debe JK misikitini eti kwa kuona anazidiwa na anaweza kushindwa na akakiri mwenyewe msikiti wa Idrissa Dar. Aliwahi kuitisha mkutano wa cuf huko Songea na kumwalika swahiba wake wa Act kuhutubia nae huku akijua hakuwa mwenza wa ukawa n.k.
 
CHANZO: NIPASHE


Mytake: Kauli hizi za Dr. Slaa zinazidi kuonesha namna gani baadhi ya viongozi na wasemaji wa CHADEMA wanavyojribu kuwahadaa Watanzania kuhusu Sakata la Mwanasiasa huyu tegemeo kabisa katika CHADEMA. Sote tunaothamini mchango wa Dr. Katika kukijenga chama hatuna budi sasa tuachane na habari za hawa watu na tusubiri kauli ya Dr. Slaa mwenyewe.

Kauli ya Dr. Slaa imekuja wakati tayari zilishatolewa taarifa mbalimbali na viongozi na wasemaji wa Chadema kuhusiana na sakata hili, taarifa ambazo kwa kauli hii ya Slaa ni wazi zilikuwa ni za kuwahadaa watanzania. Kauli hizo ni pamoja na:

1. Dr. Slaa ameamua kupmzika, akiwa tayari atajiunga nasi-FREEMAN MBOWE

2. Dr. Slaa kukutana na Secretarieti ili kupanga mikakati ya ushindi ya UKAWA-YERIKO NYERERE

3. DR. SLAA atazindua Kampeni za UKAWA-JOHN MNYIKA n.k

Am tuned
 
unanishtaki,kwani hujui tofauti kati ya tofali la block na la udongo?
Wepi ni imara zaidi (cement blocks), kati ya (a)wana chadema halisi
(b)wahamiaji haramu(ccm)
jibu linaweza kuwa(b)?
Miye sikubali kuwa
C+O2=C badala ya CO2
au 2+3=2
NB KWA SASA HATUNA CHADEMA BALI tuna LOTION

ha ha ha kuna uwezekano mkubwa hilo jumba lenye msingi wa tofali za udongo na ukuta wa sementi likaporomoka hata kabla ya uchaguzi
 
unanishtaki,kwani hujui tofauti kati ya tofali la block na la udongo?
Wepi ni imara zaidi (cement blocks), kati ya (a)wana chadema halisi
(b)wahamiaji haramu(ccm)
jibu linaweza kuwa(b)?
Miye sikubali kuwa
C+O2=C badala ya CO2
au 2+3=2
NB KWA SASA HATUNA CHADEMA BALI tuna LOTION

Umekuwa lini mtetezi wa chadema? Hata ikifa wewe unaumia kwa lipi. Magamba bana.
 
Chadema ni sawa na msukule unaonyonya watu damu yafaa kuogopwa zaidi ya Kansa ndio maana sie wenye akili zetu timamu tulishasepa mdaaaaaa

Hivi wewe unaweza kujiaminisha kuwa ulisepa kwa ridhaa yako mwenyewe au ndio wale mlifukuzwa kwa kufungashiwa virago na mwenzako mtela?una ubavu wa kusepa wewe?
 
hahahhahhaaa mnazidi kuipaisha Chadema hahahhaaaa

Unajua hawa ccm ni wa ajabu sana! Ni sawa na wacheza mdundiko harusini.
Usiku mzima wanakesha nje wanacheza wakati maharusi wako ndani wanaburudishana na hizo kelele za Ngoma zao nje kwao ni burudani
 
Back
Top Bottom