Dr. Slaa hatimaye aibuka

Dr. Slaa hatimaye aibuka

Nilishawaambia lakini hamtaki kuelewa

Dr Slaa hana Mpango wa kurejea CHADEMA

Kafulila alienda kuongea nae kumwomba ajiunge ACT na agombee Uraisi huko

Kafulila atajiunga na ACT hivi karibuni

Dr hajakubaliana bado na ACT...Ila maongezi yako kwenye hatua nzuri

Pia Its Confirmed Kuwa Lipumba atajiunga na ACT.

Haki ya nani hizi siasa ni kizunguzungu kitupu.
 
Tuwe makini katika mambo tunayoandika, tunapaswa kukumbuka kuwa Dr. amefanya kazi kubwa sana ndani ya CDM. Kutokukubaliana katika maisha ni jambo la kawaida, anazo hoja ambazo kwa maoni yangu alikuwa sahihi. Isipokuwa watu kwa wakati huu wanataka mabadiliko kutokana na fursa iliyopo na mara nyingi haziji mara mbili. Hawa jamaa wakiachiwa wakati huu watajipanga na hawatafanya makosa .

Ni vizuri Dr. akaliangalia hilo na kutafuta suluhu badala ya kuwa na misimamo mikali ambayo itapunguza fursa hii muhimu kwa wakati huu. Suala la wizi wa kura hata mwaka huu huwezi kulikwepa, ikiwa wanaibiana wenyewe ndani ya chama chao sembuse za wapinzani? Lakini wizi unakuwa mgumu iwapo kunakuwa na ushindi mkubwa. Hivyo tunamhitaji Dr. sasa hivi kuliko wakati mwingine wowote, yeyote anayeweza kusaidia hilo na alifanye kwa moyo wote.

Mwacheni Dr Slaa apumzike ajitafakari alipo na alikotoka ajipime. Nina imani hawezi kuwa msaliti naelewa ni mkweli wala hanunuliki nategemea atatu suprise kwa ujio wake ili kuipa ushindi Ukawa. Hapo ndio ccm wote mwili utawalegea kwa mshangao.
 
Ukombozi hauwezi kusubili mtu mmoja mmoja akubaliane na wengi chadema inamhitaji dr slaa lakini watanzania wanamhitaji zaidi lowasa awe raisi wao ..............
 
Kuzungumzia chadema ni nafuu uzungumzie ACT, Mambo waloyafanya ni ya ajabu sana sana, Dr. Hawezi kukubaliana na ujinga wa namna hiyo, ww umtukane mtu na ufanye hadi kapoteza uwaziri mkuu wake na unao ushahidi wa kutosha na unathibitishia watanzania na unasema kama Lowasa anabisha na aende mahakamani kwa kuwa ni kweli Lowasa hakuwahi kwenda mahakani. Maana yake kulikuwa na ukweli, Jana ulikuwa unasema Lowasa mwizi fisadi, leo unasema mwenye ushahidi na aende mahakamani, hivi wanaona ss mabwege sana na hatuna ufahamu kabisa.

Mimi nimesikia viongozi wakubwa wa ukawa wanasema kwamba ccm hawakumtedea haki Lowasa hadi walimkata na imekuwa ni ajenda kubwa sana sana, swali langu kwao je uchaguzi wa kumpata Mgombea wa UKAWA ulikuwa wa kidemokrasia? Kwani nn nasema hivyo sijaona wagombea wa vyama washirika ambao walipata nafasi kwenye vyama vyao wakichuana na Lowasa, kilichofanyika ni kumpachika Lowasa kugombea nafasi hiyo, na kama wao wanademokrasia kiasi hicho mbona hawajafanya mazungumzo na waasisi wa ukawa? Ss Lipumba kaondoka na Dr. Slaa pia. Tena Mbowe anawaaminisha wajumbe kuwa mzee tumeamua kumpumzisha, maana yake tu ni kwamba watu wasihoji, kuhusu Dr. Slaa.

Wenye ufahamu tayari nao wameondoka kimya kimya wala wao hawatangazi, ila mwaka huu UKAWA mlikuwa na bahati sana ya kuingia ikulu ss mtabakia kuitazama tu kwa ajili ya tamaa zenu za ajabu ajabu, mimi nawapa pole sana sana, watanzania tulio waengi tunatizama picha inavyokwenda japo kusoma hatujui.

Mkuu wanaopiga kelele humu ni wale team El eti kwamba watavuna members humu jf, ila kwa jinsi nnavyowajua wana jf hawashawishiki na maneno ya juujuu , matusimatusi, zomea zomea ,,, kuponda,, kejeli vinavyotumiwa na team el ili mradi tumuunge mkono bwana wao,
Wanawezaga kuwarubuni watu wasiofikiria hata kidogo lakini humu wanapiga kelele tu.

Nawaambia team El acheni tamaa, fanyeni kazi mpate kipato halali ,,,,, mmeitolea macho TZ yetu ,,,mnataka kuitafuna bila huruma.
Tutakuja kuwanasa tu..au mnadhani hela zitawaokoa?
 
"DK SLAA amefunguka kwamba dakika za mwisho MBOWE aliwaburuza na kulazimisha tumpokee LOWASA , hapo nikaona nikae pembeni. muda si mrefu nitaitisha press confrence kwani watu wanapotosha sana kuhusu mimi DK SLAA."
 
Kaka mkubwa tuwaache hao majirani hebu tuangalie maisha yetu yanavyokuwa magumu..maana ukiamka ni Lowasa Dr
. Slaa wakati hali zetu ni mbaya ktk mikakati yetu kushinda tena na tenaa
 
"DK SLAA amefunguka kwamba dakika za mwisho MBOWE aliwaburuza na kulazimisha tumpokee LOWASA , hapo nikaona nikae pembeni. muda si mrefu nitaitisha press confrence kwani watu wanapotosha sana kuhusu mimi DK SLAA."
Yeye aende anakoenda na ataenda yeye na familia yake. Sisi ni wafuasi wa chama siyo wa mtu , nafikiri majibu mmeyapata kwa LIPUMBA. Wasaidieni hao watu kiuchumi lakini sisi malengo yetu yako palepale kumwondoa mkoloni mweusi CCM oktoba.
 
yeye aende anakoenda na ataenda yeye na familia yake. Sisi ni wafuasi wa chama siyo wa mtu , nafikiri majibu mmeyapata kwa lipumba. Wasaidieni hao watu kiuchumi lakini sisi malengo yetu yako palepale kumwondoa mkoloni mweusi ccm oktoba.

leo unamkana dk
 
leo unamkana dk
Mimi siku zote ni mfuasi wa chama si mtu. Ukiwa mfuasi wa mtu je akifa utafanyaje? Kama yeye kachoka aende anakoenda au apumzike kama afanyavyo kwani umeona kazi zimesimama kwa yeye kutokuwapo? Kufa kufaana.
 
Chama kwanza mtu baadaye! Hakuna mtu maarufu zaidi ya chama! Akitaka afuate nyayo za Lipumba!
 
dr.slaa hebu shusha pumzi urudi tukijenge chama,hasa kipindi hiki cha uchaguzi.
 
"DK SLAA amefunguka kwamba dakika za mwisho MBOWE aliwaburuza na kulazimisha tumpokee LOWASA , hapo nikaona nikae pembeni. muda si mrefu nitaitisha press confrence kwani watu wanapotosha sana kuhusu mimi DK SLAA."

Kwahiyo?
 
Kadi yangu ya CDM imekuwa mzigo mzito sana kwangu kwa sasa, tokea gia ilipobadilishiwa angani, in the name of politics is the game of dynamics.
 
Back
Top Bottom