Dr. Slaa anastahili kuheshimiwa

Dr. Slaa anastahili kuheshimiwa

mkuu ni misisiem inayojiandaa kuwa mipinzaji, inakula tizi ya kutukana serikali ya ukawa after october
 
Wengi wanaomkashifu Dr.Slaa ni wale walijiunga Chadema kwa mafuriko ya Lowassa.

Hivyo Lowassa akihama Chadema nao wanahama...... Kuna mdau mmoja humu amesema wapo kama Nyumbu.
 
Atimaye gamba umerudi nyumbani hongera naona sasa n wazee mtakiona cha mtema kuni

Bila CCM madhubuti nchi hii itayumba

CCM ni chama dume

CCM ni chama kinachopendwa Tanzania

Kidumu chama tawala
 
Wandugu,

Nimeanza kuona kejeli, uzushi, kashfa, matusi, mipasho ya kila aina juu ya Dr Slaa ambaye alikuwa Katibu Mkuu wa CHADEMA. Dr Slaa alikuwa muhimili mkuu wa CHADEMA na kupambwa kwa kila afanyalo Lakini leo amekuwa Si chochote si lolote.

Ushauri Wangu Kwenu Ni kuwa na subra na stara kwake Kwani hata kama humpendi katika Siasa tena ki umri ni Mzee Wako hivyo anastahili Sana heshima!

Vijana wa Bavicha acheni uzandiki kuweni na mitazamo ya kukubaliana kutofautiana na sio matusi na kejeli.

Nawasilisha!

ushauri huu ungemfaa sana mbunge wako mwigulu ncheemba, manake ndiye kinara wa kumsakama Dr. Slaa Kwa matusi.

Tutoke kwenye mada kidogo:-
hivi home boy wako Jairo alizidiwaje kete/dau ya kutoa rushwa na Mwigulu, tuambie walikuwa wanatoa bei gani na Kilimba nini kilimpata. Nini kinaendelea hapo mampanta na Kinambeu kwa ujumla.
 
Last edited by a moderator:
Rekebisha isomeke "Dr. Slaa katibu mkuu wa chadema"
 
Hakuna mwanaChedema anayeweza kumkandya Dr.Slaa.
Wote tunamkubali kwa kazi yake aliyoifanya haiwezi kufutika na itabaki miyoni mwa wanaChadema wote.
Ila inapofika wakati wa kusonga mbele inabidi safari iendelee with or without him.
 
una uhakika gani kuwa hizo post za kumchafua zinatoka BAVICHA? Nyie maCCM mnamtukana, halafu mnajifanya huo uozo wenu unatoka BAVICHA... We are not as stupid as....
 
Bado ni Katibu mkuu wa Chadema na atarudi kazini baada ya likizo.
 
Bila CCM madhubuti nchi hii itayumba

CCM ni chama dume

CCM ni chama kinachopendwa Tanzania

Kidumu chama tawala

Pole sana! Mtapigwa vibaya sana mwaka huu, tafiti zinaonesha ukawa watapata 60% na ccm na washirika wake akina Zitto wataambulia 40% .sasa tafuta asilimia ya ccm kwenye 40% baada ya kutoa za ACT, TLP, na vibaraka wengine.
 
wengi ya wanamtukana ni pro lowasa na pro mbowe
 
Hutakiwi kumponda Slaa, Slaa amefanya makubwa chadema Yule Mzee amepigwa sana mabomu! He deserve more and full respect, yeye ni binaadamu tu Kama wengine,, isipokua kwa wimbi hili la kuitoa ccm madarakani sio Dr Slaa peke yake anahitajika Hadi Zitto Kabwe tunamuhitaji kuongeza nguvu!!

Kwanza nakubaliana na mleta posti lakini sikuungi mkono kwa kushauri viongozi wa CHADEMA kupoteza muda kumbembeleza Slaa ama Zitto. Mtu pekee wa kuwapeleka mchakamchaka CCM ni Lowassa pekee. Ni dhahiri Slaa kachukizwa kupokonywa kugombea uraisi na hata kama UKAWA wangempitisha Lipumba bado Slaa angesusa.
 
Nguvu ya dr slaa inaonekana dhahiri kwa nyinyi mnaopinga maamuzi yake.na hili linaonekana wazi chadema bado inamhitaji sana kuliko anavyo ihitaji kwa sasa
 
Hutakiwi kumponda Slaa, Slaa amefanya makubwa chadema Yule Mzee amepigwa sana mabomu! He deserve more and full respect, yeye ni binaadamu tu Kama wengine,, isipokua kwa wimbi hili la kuitoa ccm madarakani sio Dr Slaa peke yake anahitajika Hadi Zitto Kabwe tunamuhitaji kuongeza nguvu!!

Kumuita Dr slaa mnafiki ni kumkosea adabu na kutojua nini maana ya uhuru wa maoni na mchango wake katika kuijenga chadema. Kusema au kutosema ni uamuzi binafsi, bila shaka kukaa kwake kimya ni ishara ya busara iliyo tukuka na dalili nzuri zaidi kwa upande wa ukawa kwani hakuna miongoni mwetu anaejua kama akisema atasema nini na itakuwa na faida au hasara gani kwa ukawa. Matendo yanaonyesha wazi kuwa hakubaliani na ujio wa Lowasa ndani ya chadema,nadhani hii inatosha kuwa sababu ya msingi na sio kuanza kutunga uongo ili kumchafua.Unafiki ni kuficha hisia zako kwa kuonyesha upendo au umoja wa bandia ambao ni sumu mbaya sana kwa afya ya demokrasia.
Kuhusu Zitto nadhani utakuwa unaongelea swala usilolijua kwani Chama cha ACT kiliandika barua kuomba kujumuishwa katika ukawa na mpaka leo hii hakuna jibu na iliishia kwa Mh John Mnyika kupanda majukwaani na kusema kuwa adui yao mkubwa ni Zitto na ACT. Propaganda za kuwa ACT ni CCM "B" zimekuwa zikiendeshwa katika mitandao ya kijamii ikiwa kama njia ya kuikataa ACT kuingia katika UKAWA. Sasa iweje leo useme ZItto anastahili kujiunga na UkAWA ilihali hata ombi la kujiunga na UKAWA limekataliwa? Na wewe unaesema ajiunge na UKAWA unasema kama nani ikiwa Mwenyekiti Mbowe hajatoa ufafanuzi wowote juu ya maombo hili?
 
Kusamehe ni agizo shariti uwasamehe adui zako ili upunguze adui na kuongeza marafiki, hiyo ndio kanuni ya Mungu. Wote wanaotoka ccm tushawasamehe kilichobaki ni kupambana kuliondoa zimwi ccm
kwa hiyo wakihama ccm wote myawapokea akiwemo Kinana na JK? Kwa hiyo kwenu tatizo ni jina CCM? Watu wote walioko CCM wakihamia CDM si itakuwa ni ccm ileile. Tusiteteee ujinga kwa kushindwa kuishi na kutetea principles. Mnasema sauti ya wengi wakati ni wazi ujio wa Lowasa ni wazo la Mbowe mwenyewe. Kama angetaka liwe la sauti ya wengi angehusisha mkutano mkuu na kuruhusu mjadala mpana juu ya hilo.wanachama wanatakiwa kuchagua mgombea na sikupitisha chaguo moja la familia moja. Binadamu lazima uheshimu dhamiri yako. Lini Lowasa aliacha dili zake? Kama alikuwa na uchungu na mkataba Richmond as a premier alitakiwa kugomea ili kulinda maslahi ya umma na taifa? Lakini akakaa kimya na kuacha taiga likipata hasara kubwa. Hata kama hakupata mgao kwa MTU aliyejua ubovu wa wa mkataba ule kutokusimamia maslahi ya umma kunaacha mashaka uadilifu wake? Wala haikuhitaji ajiuzulu yeye angegoma waliopanga dili wangeogopa kuendelea kwa dili kubumburuka. Lakini pia MTU Huyu bado anaurafiki na Rostam ambaye kwa Maelezo ya Richmond ndo alikuwa na haki ya kisheria. Ukitafakari kwa undani utagundua kuwa ni kweli Lowassa peke yake kama waziri mkuu asingeweza kupitisha mkataba kwa influence yake pasi bosi wake kujua yaaan rais. Hivyo wote walipiga dili lile. Anachokifanya nikumuingiza rais kama mfaidika ili kumtisha kutokuendelea kumsema hili alilitumia Prof. mahalu kwenye kesi yake na Takukuru juu ya jengo la ubalozi Canada. Hiki wanakijua akina Lissu na Marando kuwa serikali ikijitia kwenda mahakamani watamuuingiza rais kama shahidi. Tafakari sana
 
Back
Top Bottom