SiimaK
JF-Expert Member
- Jan 12, 2015
- 340
- 158
Kuongoza ni Pamoja na kumwambia kipi ni Kibaya na Kipi ni Kizuri.Ndio maana wanatuambia Hadharani USIIBE.Na hapa wametuambia hadharani tupige KURA YA HAPANA kwa sababu Katiba inayopendekezwa inaenda tofauti na Matakwa ya Mungu aliye Hai.
Mbona umeenda nje ya mada, USIIBE ipo kwenye amri kumi za Mungu kwa hiyo kama viongozi wa Dini wanahaki kutuambia tusiibe kutokana na maandiko yanavyotuambia na kufuata biblia.
Nikuulize swali kwani kwenye biblia kuna kipengele kinachozungumzia KATIBA na Mungu akasema tuseme hapana? Kama kipo Pengo atakuwa amefanya kosa kwenda kinyume na maandiko, na kama hamna Gwajima amefanya kosa kubwa kumtukana Pengo kama amepindisha maandiko kwa kuwaambia waumini wachague wenyewe kadri Roho Mtakatifu atakavyowashauri kama ndio au hapana.
Gwajima ana Roho Mtakafujo ndani yake na Pengo ana Roho Mtakatifu ndani yake.