Boss, kwani sisi tuna waasi? System tulizonazo inclusion iko automatic, tunga Bunge! Wapinzani na chama tawala wanajadiliana. Tuna taasisi ile ya vyama vienye wabunge bungeni inayoongozwa na Mh. Mbatia kote huko vyama vyote vinashiriki vinavyotaka.
Tuna majukwaa ya kisiasa ambapo kila mtu au chama viko huru kuongea lolote?
Tuko kwenye mchakato wa Katiba vyama vyote vinashiriki na CDM ifika mahali ikaenda ikulu...
Swali: Mnamtuhumu Kikwete kwamba haongei au hashirikishi wapinzani, niambieni mnatakiwa kufanyiwa nini?
Hapa ndio huwa nafika naona nchi hii ina wapumbavu kupitiliza, hivi mateso wanayopata watanzania huyaoni chini ya uongozi wa huyo baba yako;
Kwa taarifa nilimpigia kura mwaka 2005 kwa upendo mkubwa sana nikiwa si mwanachama wa chama chochote cha siasa, nilisafiri umbali mrefu kumpigia kura kwa gharama zangu mwenyewe nikitegemea makubwa sana toka kwake lakini akili yake na ile yako haina tofauti hivi huoni kwamba watanzania wanauwawa yuko kimya, watu wanatekwa kimya, watu wanamwagiwa tindi kali kimya, Mwigulu anachezea uvumilivu wa watanzania munao uita amani kimya, wabunge wake wanachezea maisha ya watanzania kwa kupiga kura ya ndiooooooooooooooooooooooo kimya(ulisha wahi kusikia wanapiga kura ya hapana nikupe zawadi? au serikali ni malaika haikosei) kimya, watu wanapigwa na mabomu kimya, unasema majukwaa ya siasa na bunge sehemu zilizojaa matusi na vijembe ndio unajivunia chinin ya uongozi wa baba yako pole sana!
Ndg yako asipo kaa kimya huwa anaonya sasa anashauri wenzie kukaa na waasi haoni matatizo ya hapa kwetu ya watu kufa na kupigwa na mabomu?
kuna tofauti gani ya mtu anaye uwawa Rwanda na bomu lililorushwa na waasi na anayekufa hapa kwetu kwenye mkutana wa hadhara kwa kurushiwa bomu na mtu asiyejulikana vyombo vyote vya usalama vipo nchini na vinatumia kodinzetu mbona hakukaa na watuhumiwa aongee nao(cdm, ccm,polisi,dini,n.k)
Acheni ushabiki usio kuwa na tija. Unatetea mtu ambaye tunaapa kumshitaki baada ya kustaafu kwa vifo na vilema alivyowaachia watanzania, kuuza mali za watanzania kwa watu weupe(wachina, wamarekani n.k) kila mwezi viongozi wastaafu wa marekani wako hapa nchini! watu wamepoteza maisha Mtwara kisa gesi!
Ngoja nikwambie ujue toka leo achana na maoni ya wana siasa, JK anatukosea sana mimi, wewe na vizazi vyetu amini usiamini tutakuja kuchekwa na vizazi vijavyo kuwa hatukuwa na uwezo wa kufikiri!
Mtu tuliyempa dhamana hata uteuzi wa mawaziri ana bahatisha kuwa huyu labuda anafaa mawaziri wake wakuu wote kichefu chefu mara mwingine mwizi alijiuzuru sasa anasaka uraisi kwa udi na uvumba anatumia fedha nyingi kujinadi kila mtu aone anakubalika anahonga watu kusambaza ujumbe kuwa anafaa kila kona iwe fb, jf hukosi sura yake kisa muone anapendeka watu tunaujua ukweli akiwa raisi ntaishi ukimbizini mpaka anasitaafu!, mwingine ni mtu wa piga tuuuuuuuuuuuu!
Sasa watanzania wanapigwa tuuuuuuuuuuu!!!!!!!!!! Ponda nasikia kapigwa tu! mawaziri ndo usiseme hicho kizazi mimi nasema wote uchaguzi ujao watanzania wangewapiga chini wote waliowahi kuwa mawaziri wa JK. maana hawana jipya wizi mtupu!
Mimi najua JK nafasi yake anapwaya na kwa kuwa mawaziri na wateule wake ni watu wa karibu naye sasa hawana tofauti maana watu wako wa karibu lazima mshabiane karibia asilimia 75, Tunasubiri waichezee nchi hasa kupitia katiba mpya mwisho wa siku tunawapeleka kizimbani!!!! kila kukicha mapya wameanzisha mchakato wa katiba sasa tena wanalazimisha mawazo yapite matakwa yao!
Hii nchi ni yetu sote tunasikitika kuona madawa ya kulevya yanatuchafua na Raisi anasema anawajua kwa nini sasa huchukui hatua? raisi anaonya i hadmajambazi kuwa nawapa wiki mbili mjisalimishe!!!!!!!!!! Raisi unaonya lini sasa unachukuwa hatua!
Kodi yetu ya kumpeleka Adis Ababa hatukumpeleka akatatue matatizo ya Rwanda au atugombanisha na nchi yeyote ile bali tulimpeleka ahakikishe watanzania tuko salama, masilahi yetu yanalindwa lakini pia tunanufaika kiuchumi, kisiasa,kitechnologia n.k siyo kutuingiza kwenye migogoro!!
Unauliza kama tuna waasi, kama watanzania wanafanyiwa matendo sawa na wanayo fanyiwa wananchi wa nchi zilizo na waasi unaulizaje swali la kijinga kama hilo?
Hujui wandishi wa habari wanatekwa na wengine kuawa?, hujui watu wanamwagiwa tindikali? hujui watu wanapigwa tu mabomu na risasi za moto? hujui watu wanatuhumiana kwa ugaidi hadi wanarumbana bungeni na Mwigulu anasema ana ushahidi na magaidi anawajua?