Dr. Slaa amkosoa Rais Kikwete kuhusu Rwanda

Dr. Slaa amkosoa Rais Kikwete kuhusu Rwanda

....


The Banyamulenge is a term historically describing the ethnic
Tutsi concentrated on the High Plateau of South Kivu, in the eastern region of the Democratic Republic of the Congo, close to the Burundi-Congo-Rwanda border. The ambiguous political and social position of the Banyamulenge has been a point of contention in the province, leading to the Banyamulenge playing a key role in the run-up to the First Congo War in 1996-7 and Second Congo War of 1998-2003
.....

The M23 was formed on 4 April 2012 when nearly 300 soldiers, a majority of then former members of the National Congress for the Defence of the People (CNDP), turned against the DRC government, citing poor conditions in the army and the government's unwillingness to implement the 23 March 2009 peace deal. General Bosco Ntaganda, also known as "The Terminator", was accused by the Government of Kinshasa of leading the group,[SUP][8][/SUP] and President Kabila called for his arrest on 11 April 2012.[SUP][9][/SUP] The government had threatened to redeploy former CNDP soldiers away from North Kivu before the full implementation of the peace agreement, which prompted many of them to defect from the army and create the M23.[SUP][10]

unganisha na hapachini:
[/SUP]

The M23 is made up primarily of Tutsis and opposes the Hutu Power militia Democratic Forces for the Liberation of Rwanda (FDLR) as well as area Mai-Mai (community militias).[SUP][11]

[/SUP]

Following military successes, M23 rebels have made additional demands, citing issues of human rights, democracy, as well as good governance. They have accused President Kabila of cheating in the November 2011 elections.[SUP][12][/SUP] The rebels have threatened to march on Kinshasa and depose the president.[SUP][13]

[/SUP]
......TAFAKARI
 
Kwenye hili sakata, kwa hali ilivyo, ccm hakuna mwanasiasa makini anayeweza kushughulika na Kagame. Kikwete haliwezi! Tena wasijefanya makosa kumkabidhi mwigulu au nape, hawa ndo kabisa, ni vilaza tu. Hili swala wawakabidhi makamanda tu, kina Dr Slaa na Mbowe, uone kashikashi lake.

Hao uliowapendekeza hawajui hata maana ya diplomasia, ni nani asiejua kuwa Dr Slaa ni mwanasiasa mbabe na jeuri?, ukimkabidhi hili sakata kikubwa atakacho fanya ni kuitisha vita tu kumbe room ya mazungumzo ipo wazi.
 
Sijawahi ona Padri mzandiki kama Dr Slaa! Anataka kutusahaulisha kuwa Rais Kikwete hakai na wapinzani wakati yeye dr slaa na viongozi wa chadema waliwahi kukaa ikulu kwa masaa 6 wakijadili namna ya kuunda mfumo wa kukusanya maoni ya kuunda katiba mpya kwa uwazi! Leo anasema Rais hawasikilizi wapinzani! Ee Mungu tuepushe kiongozi huyu asije akashika madaraka makubwa ya Taifa letu kwa mapenzi yako Mungu! Amen



Mlengo wa Kati hebu eleweni concern ya Slaa kwanza

Wewe baba mwenye nyumba haukuwepo umesafiri umerudi umekuta nyumbani kwako kuna matatizo yaliyotokea ukiwa haupo si ni lazima utahitaji kuelewa ilikuwaje? Kuna watoto wameumia si utawajulia hali jamani wanangu hamjambo?

Kwa Rais wetu hakuwepo nchini wakati bomu limetupwa na ccm kwenye mkutano wa Cdm Arusha alivyorudi angeonyesha kuguswa na tatizo lile,lakini hakulichukulia uzito wowote aliona kama waliopoteza maisha pale sio binadamu bali ni kuku,simply ni chama cha upinzani,ingekuwa limetokea kwa ccm si angetoa hata kauli kulaani tukio hilo? Hapo ndipo anaambiwa ataachaje kwake kunaungua unaenda kuzima nyumba ya jirani? Wapinzani CUF wameteswa na jeshi Mtwara na Lindi hakutoa kauli,Daudi Mwangosi ameuawa na polisi katulia,Soweto Arusha bomu limerishwa na polisi katulia hajataka hata kukaa na wapinzani kubadilishana nao mawazo lazima wanamuona kama anafurahia madhila yanayowapata,sasa utaendaje kushauri mwenzako akae na wapinzani wake wakati wewe haukai na wapinzani wako? Huo ushauri unakusaidia nini

Ndio maana Slaa anaona huo ushauri haumsaidii,hivyo tuache kukurupuka kujibu usichokielewa,unapotoa ushauri wewe unautumia?
 
MziziMkavu.
nilikuwa nakuheshimu sana sikuwai kujuwa wewe ni mtu wa kujenga chuki kwa propaganda za siasa majitaka. heading thread yako imeonyesha ulivyo.
 
Yaani naipenda chadema lakini katika hili naanza kuamini huyu mzee anazeeka vibaya.....Huwezi kumkosoa Rais wa nchi yako na kumuegemea foreigner katika jambo linalohusu maslahi ya nchi...naona nakosa imani naye iwapo atakuja kuwa kama Rais.....katika hili amechemka sana

Mgogoro wa JK na PK hauna maslahi kwa nchi?kama yapo,ni yapi?

watz wana maslahi na mgogoro na Malawi,nayo ni ziwa Nyasa

maslahi yapo mgogoro kati ya Kenya na Uganda,nayo ni kisiwa Migingo

huu si mgogoro wa watz na warwanda,hauna nationals interest

ndio maana PK au JK mmoja wao au wote wakiondoka madarakani namgogoro unaisha,sababu hauna faida kwa kiongozi atakaefata au wananchi

either pk or jk leaves office,goes away with it
 
Tena Ajabu Dr Slaa kajibu vema na kuweka sawa,
kinachomfanya yy kuja juu kwa lugha za matusi na hasira utadhani katukanwa au kakashifiwa yeye nini?
Kuna vijana wanajipendekeza ndan ya chadema na kwa viongoz utadhani waungu wao,tena kwa sababu zisizo za msingi na maana,
kichefu chefu sana

Yani hata hawapimi kauli zao kila kitu atakachosema slaa wao wanaona sawa! Hivi ni lini dr slaa ameomba kukutana na kikwete kakataliwa kama sio unafiki tu!
 
Dr. Slaa sio kosa lake.
Uwezo wake wa kufikiri umekuwa wa kiwango cha Josephine Mushumbusi.

Anasema Kikwete haongei na wapinzani wakati Slaa ameonekana mara kadhaa
Ikulu akinywa juice. Sasa sijui walikuwa wanakunywa juice kimyakimya!!!

View attachment 105628

Ikulu kitu gani wewe muazimisha akili? mbona baada ya juice wababe wakasema Nchi haitatawalika!!!!
 
Mzizimkavu,

This is too cheap. Kumbe kukosoa udhaifu ni kuunga mkono upande wa pili! Wenye kujua principles watanielewa. Ukifanya makosa lazima tutakuambia, ndio maana wakati wa EPA tuliwasema hadharani, bila kumumunya maneno. Wangapi wakati ule walituunga mkono! Tusingelikuwa majasiri tungekata tamaa. Tulishikilia, na hata sasa ninaamini kauli ya JK haina uhusiano na kuunga mkono upande wa pili! Hata wakati wa EPA tuliambiwa hatuna uzalendo, tunaaibisha Taifa, oh tutakosa misaada, oh! Oh! Oh, Taifa lisilo na watu wenye principle au misimamo linaenda kaburini.



QUOTE=MziziMkavu;6999416]

Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbroad Slaa, amemkosoa Rais Jakaya Kikwete, kuhusu kauli yake ya kumshauri Rais wa Rwanda, Paul Kagame, kuzungumza na waasi wa serikali yake ...


Dk. Slaa amesema haoni busara kwa Rais Kikwete kuwaambia viongozi wa Rwanda, akiwamo Rais Kagame, kuzungumza na wafuasi wa chama cha FDRL walioko Congo.

Slaa aliyasema hayo wakati akizungumza katika kongamano la vijana wa Chadema (BAVICHA) la uchumi na ajira lililofanyika jana jijini Dar es Salaam.

“Rais Kikwete hapa nyumbani hawezi kuzungumza na wapinzani na hajachukua hatua dhidi ya wauaji wa mwandishi Daudi Mwangosi...


"Alishauriwa amuwajibishe Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa Michael Kamuhanda na badala yake amempandisha cheo,” alisema Slaa.


Kauli Dk Slaa imekuja siku moja baada ya Rais Jakaya Kikwete kueleza kuwa Tanzania haina mgogoro na nchi ya Rwanda, kutokana na kauli za kejeli na matusi zilizokuwa zikitolewa na viongozi wa nchi hiyo dhidi yake na Tanzania.



Kumezuka sitofahamu ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Rwanda, baada ya Rais Kikwete kuitaka Rwanza imalize ugomvi na waasi kwa njia ya mazungumzo ya amani...

Rais Kikwete aliutoa ushauri huo wakati wa mkutano wa Umoja wa Afrika (AU) uliofanyika Addis Ababa, Ethiopia hivi karibuni.

Ushauri huo ulionekana kumchukiza Rais Kagame, anayedaiwa kuhutubia mikutano kadhaa nchini kwake na kutumia lugha ya matusi, kejeli na dhihaka dhidi ya Rais Kikwete na Tanzania.


Kitendo cha Dr Slaa kumkingia kifua Kagame kinatia shaka uzalendo wake na chama chake kwa taifa hili ...

Sote tumekuwa tukishuhudia matusi ya Kagame dhidi ya Tanzania.Iwaje Rais Kikwete aonekane mbaya kwa kumjibu Kagame, tena kwa lugha ya kizalendo??


Kagame amekuwa akituhumiwa na jumuiya mbalimbali za kimataifa kwa kutoa misaada ya kivita kwa waasi wa M23 ambao wamekuwa wakiua raia na kuwabaka wanawake....


Kauli ya Dr Slaa ina mambo mengi yaliyojificha na huenda yeye na chama chake ni wafuasi wa karibu wa M23 kama ilivyo kwa Kagame.

Kuwa mpinzani, haimaanishi ukosoe kila kitu.

chanzo.
WANYARWANDA WAANZA KUREJEA MAKWAO BAADA YA RAIS KIKWETE KUWAPA SIKU 14 ZA KUONDOKA
[/QUOTE]

Dr. Kwa hili sioni upeo wako juu ya masuala ya kitaifa. Ninavyofahamu charity begins at home. Kikwete hawezi kuanza kupatanisha kama hakuna political will baina ya Wanyarwanda wenyewe. Ushauri wa Kikwete ulilenga kuamsha utayari wa serikali ya Rwanda kujadiliana na waasi. Na huo ndio ungekuwa mwanzo wa yote. Kisha wangesema tunataka mpatanishi wa nje hapo ndipo ushauri wako ungeonekana muafaka. Tanzania inahistoria ya kupatanisha makundi hasimu katika nchi za Rwanda na Burundi. Hata Nyerere alifanya hivyo kwa Burundi. Lakini unapokuja na cheap politics kwenye suala hili sisi tunaona kama umekosea. Masuala ya siasa za kimataifa zina complication nyingi. Sioni tatizo kwenye ushauri wa Kikwete kama unavyotaka kutuaminisha. Lakini vilivile huwezi kulinganisha masuala haya na yale ya EPA. Tunashindwa kukuelewa kama kwa kufananisha na EPA unataka cheap popularity au political gain au vipi? Tunaamini kwamba hapo Dr wetu umeteleza. Kukiri ni njia tu ya kujiimarisha aala siyo kujidhalilisha. Asante.
 
Mkuu, kama umeisoma hii story kwa urefu wake, basi tuwekee story nzima. Nimesoma habari hizi kwenye title ya gazeti la Tanzania Daima, but sijajua undani wa habari yenyewe. Tafadhari tusaidie kwa kutuwekea story nzima ili tujue kwa undani hayo aliyoyasema Slaa.

Acha kushusha hadhi watu wewee...
Sema ujue nini alisema Rais wa Mioyo yetu Dr,Slaa
 
Mlengo wa Kati hebu eleweni concern ya Slaa kwanza

Wewe baba mwenye nyumba haukuwepo umesafiri umerudi umekuta nyumbani kwako kuna matatizo yaliyotokea ukiwa haupo si ni lazima utahitaji kuelewa ilikuwaje? Kuna watoto wameumia si utawajulia hali jamani wanangu hamjambo?

Kwa Rais wetu hakuwepo nchini wakati bomu limetupwa na ccm kwenye mkutano wa Cdm Arusha alivyorudi angeonyesha kuguswa na tatizo lile,lakini hakulichukulia uzito wowote aliona kama waliopoteza maisha pale sio binadamu bali ni kuku,simply ni chama cha upinzani,ingekuwa limetokea kwa ccm si angetoa hata kauli kulaani tukio hilo? Hapo ndipo anaambiwa ataachaje kwake kunaungua unaenda kuzima nyumba ya jirani? Wapinzani CUF wameteswa na jeshi Mtwara na Lindi hakutoa kauli,Daudi Mwangosi ameuawa na polisi katulia,Soweto Arusha bomu limerishwa na polisi katulia hajataka hata kukaa na wapinzani kubadilishana nao mawazo lazima wanamuona kama anafurahia madhila yanayowapata,sasa utaendaje kushauri mwenzako akae na wapinzani wake wakati wewe haukai na wapinzani wako? Huo ushauri unakusaidia nini

Ndio maana Slaa anaona huo ushauri haumsaidii,hivyo tuache kukurupuka kujibu usichokielewa,unapotoa ushauri wewe unautumia?

Kwa maaana hiyo Kikwete hakuwa na sifa ya kuhudhulia ule mkutano wa Great lakes? Lakini nikuulize ni lini Wapinzani wa Tanzania wameomba kukutana na Rais Kikwete kuzungumza meza moja aka kataankuonana nao????? Kwa hili mimi naona Dr slaa hajamtendea haki Kikwete!
 
Hao uliowapendekeza hawajui hata maana ya diplomasia, ni nani asiejua kuwa Dr Slaa ni mwanasiasa mbabe na jeuri?, ukimkabidhi hili sakata kikubwa atakacho fanya ni kuitisha vita tu kumbe room ya mazungumzo ipo wazi.

Hili swala ni dogo sana, lakini kwa jinsi linavyomtikisa huyu Mheshimiwa Rais, kwa kweli nashindwa kuelewa! Kulikuwa hakuna sababu yeyote ya kujieleza kiasi hicho mbele ya taifa as if unajipendekeza kwa Kagame. Inasikitisha sana. Kagame is in frustration, wao na M7 wanakimbiakimbia tu hovyohovyo maporini huko, sasa hivi wamempata Uhuru wakumvuta masikio basi, wamepata jeuri ya kutishia watu. Yeye Kagame kam anauwezo adhubutu basi tumwone.

Rais alitakiwa amwite tu Kagame, akigoma, tuma watu wakazungumze basi! Rwanda hawana ujanja wowote kivita au kiintelligenisia kupambana na watanzania. Yaani we have so many options kuwa maliza bila hata kushika mtutu!!

Tatizo letu watz ni ccm basi!!
 
Rangi halisi ya Dr. Slaa imeanza kuonekana.

Mara awaambie watu kuomba Mungu sio jambo zuri. Sasa anaunga mkono waasi na kuside na Kagame agaist Rais wa Tanzania!!!

umekuwa mvivu wa kusoma na kufukiri na hadi unajichanganya. yani Dr slaa ka side na kagame alaf papo hapo kaunga mkono waasi?
 
Mzizimkavu,

This is too cheap. Kumbe kukosoa udhaifu ni kuunga mkono upande wa pili! Wenye kujua principles watanielewa. Ukifanya makosa lazima tutakuambia, ndio maana wakati wa EPA tuliwasema hadharani, bila kumumunya maneno. Wangapi wakati ule walituunga mkono! Tusingelikuwa majasiri tungekata tamaa. Tulishikilia, na hata sasa ninaamini kauli ya JK haina uhusiano na kuunga mkono upande wa pili! Hata wakati wa EPA tuliambiwa hatuna uzalendo, tunaaibisha Taifa, oh tutakosa misaada, oh! Oh! Oh, Taifa lisilo na watu wenye principle au misimamo linaenda kaburini.

Well done,Rais na Tumaini letu kwa Taifa Teule Tanganyika..
Hakika sikukosea kukupatia kura ya NDIO ..
Tuko pamoja na tuna imani utalifikisha salama Jahazi hili... God bless u always..
 
===>> As of this moment, day... NAMTOA KABISA . SLAA ktk viongozi wenye uelewa na weledi na uzalendo wa nchi yangu....

===He can't differentiate among many things.... he is attacking JK personally na kuchanganya vitu hovyo hovyo.... he is poor analyst...

... hajui siasa za CHAMA NA CHAMA...NCHI YAKE NA NCHI ZA NJE... he is mixed up himself...with cdm politics (internal) na external politics hajui asumame wapi..... SLAA CHOCHOTE JK ASEME YEYE KUPINGA TU.... HATA RAIS ATUKANWE NA KUTISHIWA MAISHA...SLAA KAZI KUMPINGA JK TU....NA HATA KAFIKIA HATUA YA KUSEMA JK AOMBE MSAMAHA HUMU JF.....poor Slaa.... Josephine kakuharibu kwa tabia na umekuwa little minded... u can*t compete with anybody.... na usijaribu eti kuutaka Urais wa nchi yangu.... poor leader....

=== Sikujua utasema uongo hivyo eti JK hajawahi kukutana na wapinzani kuongea nanyi....

=== NIKUANIKE WW SLAA UNAZEEKA VIBAYA....WW NDIO ULIKUWA HUTAKI KATA KATA KUONANA NA JK.... nakumbuka hata siku ya KUAPISHWA JK UWANJA WA TAIFA ULISUSA....that time sijakuelewa...kumbe ww una uchu sana wa madaraka hadi umeusahau UZALENDO WA TANZANIA.....

===>> I declare HUFAI HATA KIDOGO WW....hv ulikuwaje padri na roho ya hivyo....

== Mungu wa ajabu kweli....HIVI WW NA JK nani aombe msamaha...¡¿¿¿ NILIFIKIRI UNGESEMA UMEKOSEA.....na kuomba radhi.... instead... ur useless kabisa....

====>> JK made a right decision..... go ahead achanana haka kazee .... Slaa ur brain is desintegrating rapidly.... take action...

===> Na koma kutufanya wapuuzi ukifikiri kila usemacho uko sahihi.... hufai -100%
 
WE DON'T WANT WARS AGAINST OUR NEIGHBOURS AND FRIENDS!!!. Kama Rais wenu JK anataka kupambana na PK basi watafutiwe ULINGO,WAVAE GLOVES wazichape. On the other side,mimi naona hii ishu inakuzwa bure tu na VYOMBO VYA HABARI na MITANDAO ya kijamii kama hii kwa watu kutoa tafsiri zao tu za kauli za viongozi hawa. na matokeo yake wanawavimbisha vichwa kila mmoja kuanza kujiona kama vile anadhauliwa na mwenzake!!

Kwa hili JK alichemka, hakupaswa kuropoka ktk swala sensitive kama hili linalowahusu Rwanda na Wanyarwanda wenyewe hata kama kwa kiwango flani mgogoro wao unatuathiri na sisi.Alipaswa kufanya kama walivyofanya Kenya, Zimbabwe kama kweli alikuwa na nia njema kwa sababu hapa pana pande mbili zinazogombana sasa ili kuleta maelewano lazima awepo mtu wa katikati na kwa sababu ameamua kuwa yeye basi aweke ROAD MAP ya kuwapatanisha hawa na si KUFANYA MAMBO NYETI YANAYOHUSU TAIFA HURU LA WATU WENGINE KIMIPASHOPASHO na KWA MZAHA (otherwise awe na persoal interests ktk) kama vile tu anavyofanya katika mambo ya ndani ya nchi yake . Matokeo yake ndiyo haya sasa anatukanwa na wengine mnaunga tela bila kujua motives za mgogoro huu!!

Sio kila linalo semwa na RAIS wetu tunalikubali tu na kuliunga mkono bila kujali ni jema au baya eti ukilipinga au ukipingana naye wewe unakuwa si mzalendo.Katika hili mimi SIKO NAYE hadi pale atakapotoa genuine reasons za kusababisha mgogoro usio na lazima na jirani zetu!!!.........LET EVERY ONE OF US THINK BIG and INDEPENDENTLY......!!
 
Wewe ni mpuuzi na wakupuuzwa kama wahuni wenzio tu wanaoganga njaa hapa mtandaoni,

Umehama MMU sasa unadandia jukwa la siasa kijana?

Mods

Unganisheni ----- huu na uzi halisi wa "Dr Slaa ampinga jk",
Hivi wewe akitajwa Dr slaa unachanganyikiwa eehhh kijana unamawazo mgando

au unatafuta "sympathy" pale makao makuu kinondoni poleeee
 
Ok! Vipi kuhusu mabomu?? Hakuona umuhimu wa kuongea na hasimu wake kabla ya kutuma kikosi cha mauaji??haya ya mazungumzo yana fit upande wa rwanda tu? Mwangosi aliuliwa na polisi mbele ya kamanda wao!au sio? Dialogue haikuwepo miaka hiyo? Mtwara wanataka tu kujua manufaa ya gesi itakayopatikana kwao!jibu ni mazungumzo rahisi tu ya kuwaelewesha wana mtwara A B c ,badala ya majibu wamepelekewa jeshi la wabakaji wauaji!!! Na wewe umeona ni sawa tu?????eti?

Mwangosi aliuwawa na polisi ndio, lakini mwenye uwezo wa kutoa hukumu ni mahakama na siyo Kikwete. Kama mahakama itaona Kamuhanda anahusika basi itampa hukumu. Huo ndio utawala wa sheria. Rais hawezi kufanya maamuzi kwa sababu tu eti Chadema mmesema. Mahakama zipo zitafanya kazi yake. Ni upuuzi kusema Kikwete katuma kikosi cha mauaji kurusha bomu bila kuwa na ushahidi. Ningewashauri wewe na Chadema kama mna ushahidi fuateni misingi ya kisheria mpeleke huko ushahidi wenu ili wahusika wachukuliwe hatua za kisheria. Hizo porojo zenu za kusema tume ya kijaji hazina maana wala tija kwa taifa. Kabla hujailaumu serikali kuhusu Mtwara, jiulize kwanza ni uharibifu kiasi gani uliofanywa na vijana wa Mtwara kabla ya polisi na jeshi kuamua kutumia nguvu. Kudai haki hakukupi ruhusa ya wewe kuvunja haki ya mwingine. Yawezekana wananchi wa Mtwara walikuwa sahihi kudai haki yao ila njia waliyotumia siyo sahihi na ndio maana nguvu iliyowekwa kisheria imetumika.[/QUOTE]

Swali linabaki hapo hapo!! Hakukuwa na nafasi ya mazungumzo?? Hakukuwa na chance ya kujiuliza kulikoni wana mtwara ku react kwa kiasi kile?? Kama ni kweli mwangosi aliuliwa na polisi chini ya kamanda wao,je ni lini rais kikwete aliwahi kuwashauri polisi au kamanda wao kukaa mezani na wananchi kumaliza tofauti zilizotokana na tukio hilo??au tunaosha chombo kwa nje huku tukiacha uozo ndani?
 
Back
Top Bottom