Mimi sio shabiki wa vyama vya siasa, ni mshabiki wa watu makini wenye kujali maslahi ya taifa....kipindi kidogo cha nyuma cdm ilikuwa moto wa kuotea mbali sababu ya umakini uliokuwepo,, mikutano ilikuwa na hamasa kubwa na vilikuwa vinashushwa vitu vya maana ndani ya mikutano ya cdm....mfano tu hii escrow saga ati mpaka sasa hivi hatuwajui wanufaika kupitia bank ya stanbic, kipindi kile tayari tumeshayajua kupitia dr slaa.Kipindi hiko Zitto kashika kanda ya magharibi, Mbowe anapasua kaskazini wakati dr slaa shaaaa mwembe yanga ndani ya daresalama.Ilikuwa ni combination ya hataree tofauti na hawa vijana wa sasa hivi mara kaeni kwenye tv muone nitakachofanya bunge likianza, kubali ukatae speed imepungua.
Inawezekana unazunguuka mbuyu
1. Unaweza kutueleza kwa data na ushahidi malumu kushuka kwa chadema? tumia dhana hii
a) Uchaguzi Serikali za mitaa imepanda imeshuka, imepata asilimia ngapi ukilinganisha na hapo awali au imepoteza ngapi
2. Nimikutano ipi ya chadema imekosa hamasa, unaweza itaja kwa majina ikibidi picha
3. Escrow, unataka nini zaid, kama jambo limeenda mpaka bungeni, rais kapewa maazimio na bunge nk unataka chadema ifanye nini? Iulize serikali kwanini haitaki wezi kupitia Stanbic waeleweke, inamechanism zote, cdm unailaum kwa lipi
4. Hoja hii kwa uzushi tu inamjadili Dr Slaa kwa uwongo na uchafuzi, Zitto unamtowa wapi? unataka kusema ZZK ndiyo chadema? huu nao niuzushi mwingine.
Elewa wazi tunaelekea uchaguzi mkuu 2015, kila chama kina
-Mikakati yake
-Agenda zake
-Mipangilio nk
Huwezi leta hoja hapa chadema imeshuka bila takwimu za
a) serikali za mitaa
b) kuongezeka au kupunguwa kwa wanachama
c) Kupoteza majimbo ya ubunge, udiwani nk
Hebu wewe mwenye hoja jadili sasa kwa hoja na takwimu tuone huo ukweli wa kuporomoka kwa chadema na Dr Slaa.
Tafadhali shusha takwim