Mark Francis
JF-Expert Member
- Nov 19, 2010
- 605
- 310
Kama utetezi huu ni kweli ameundika Dr.Slaa(siamini), basi utetezi wake ni wakifisadi.
1. Kusema kuwa watumishi wa vyama hawaruhusiwi kukopa ni uwongo mtupu na uzushi.Hakuna sheria inayomzuia mtu kukopa. Kukopa na kukopeshwa ni makubaliano ya kimkataba kati ya mtu na mtu au mtu na taasisi kadiri wanavyoaminiana. Unabisha wewe ni benki? Benki nyingi hazina utaratibu wa kukopesha wafanyakazi hasa wa private, kuwakopesha wafanyakazi wa vyama vya siasa ni risk sana na hivyo benki nyingi zinakwepa.
2. Je lengo msingi la fedha ya ruzuku ni kwaajili ya kukopeshana? Hata kama lengo kuu sio kukopesha lakini organisation nyingi hukopesha ili kuboresha maisha ya wafanyakazi wao, maana kwa kufanya hivyo wanakua wanawa-motivate kufanya kazi kwa bidii na kwa kujituma zaidi.
3. Yeye kama mtendaji mkuu wa chama, je haoni kujikopesha fedha za ruzuku kuna conflict of interests? Je haoni kwamba kitendo hiki kinajenga mashaka makubwa dhidi yake juu ya accountability, credibility,transparency? Chama sio Dr Slaa, hata kama yeye ndio mtendaji mkuu wa chama. Chama kina NEC, CC na baraza la wadhamini, hao wote ni zaidi ya Dr Slaa. Kungekua na tatizo, NEC, CC na baraza la wadhamini wangelishughulikia
4. Je haoni kuwa tendo hili la kujikopesha fedha za ruzuku ni tendo la kifisadi? Sio tendo la kifisadi, kukopeshwa ni kitendo halali na haivunji sheria ya nchi wala sheria za vyama vya siasa. Kumbuka mkopo sio wizi.
5. Je huku siyo kutumia vibaya madaraka? Mpaka Mwampamba akajua maana yake haikua SIRI, lilikua suala la wazi. Kama ni suala la wazi, maana yake utaratibu wa kupata mkopo huo ulifuatwa kikamilifu na hivyo hakuna matumizi mabaya ya madaraka.
6. Je haoni kuwa akiwa Ikulu kuna uwezekano mkubwa akajikopesha bajeti yote ya ikulu? Hilo ni swali la kitoto, kwa unataka kusema bajeti ya Chadema ni milioni 20 tu, kama ni zaidi mbona hakukopeshwa yote?
Tamko: Dr. Slaa hafai kuwa raisi.
Mkopo ulitolewa na ukarudishwa, tatizo lenu nini? Mbona mnawashwa pasipo sababu!!