Dr Slaa ajibu tuhuma dhidi yake

Dr Slaa ajibu tuhuma dhidi yake

Status
Not open for further replies.
Mosi, Tupe kipengele cha katiba ya Chadema kinachosema ni marufuku kumkopesha katibu mkuu.
Pili, kama sisi baraza kuu ambao ndo wenye mamlaka ya kuhoji hilo tunajua kinachoendelea na tumeridhika wewe mwanaccm inakuuma nini?
Well said!wamezidi vihere here kama mashoga.
 
Options
Willibrod Slaa


Hoja ya kujikopesha kwa sura ya ufisadi ni "mfu" nimetamka nilikopa 20 kwa kuwa watumishi wa vyama hawawezi kukopa kwingine. Aidha siyo 140 Million. Zote 20 m zililipwa awamu ya mwisho June 2012. Hivyo hakuna deni la chama tena.
2. Josephine hajawahi kulipwa hata senti mmoja na chama kwa ziara za Mikoani, wala kwa shughuli yeyote ile isipokuwa wakati wa kesi Arusha alipokuwa na mtoto wa miezi 3 na tulihitaji yaya
Mwambieni Dr Slaa the damage done is collosal and permanent, credibility ya uaminifu kwa hela ya chama ina dondoka kwa kasi kubwa.
CHADEMA inatumiwa kama kampuni binafsi

Maswali mengi kuliko majibu hapa.
Tutajuaje alikopa 20mil na si 140mil
Mkopo uliidhinishwa na nani?
Je CHADEMA kina utaratibu wa kukopesha wanachama wake
Slaa anasema hawezi kukopa kwingi -si ni uongo huu?
Hana hati ya nyumba kukopea benki?
Na kukmbukumbu za pay -in slips zipo?

Nani mwingine " kajikopesha " hela ya chama?

Something fishy around here!
 
I dought kama kauli hii ni ya babu. Haina vionjo tulivyozoea.

Kwanini mwamuhita babu? Hizi ni kauli za Nape ndo anapenda kumuhita hivi....Dr Slaa bado ana maswali ya kujibu kwa mujibu wa Masalia kuna issue kadhaa za kujibu...
 
Kama utetezi huu ni kweli ameundika Dr.Slaa(siamini), basi utetezi wake ni wakifisadi.

1. Kusema kuwa watumishi wa vyama hawaruhusiwi kukopa ni uwongo mtupu na uzushi.Hakuna sheria inayomzuia mtu kukopa. Kukopa na kukopeshwa ni makubaliano ya kimkataba kati ya mtu na mtu au mtu na taasisi kadiri wanavyoaminiana.
2. Je lengo msingi la fedha ya ruzuku ni kwaajili ya kukopeshana?
3. Yeye kama mtendaji mkuu wa chama, je haoni kujikopesha fedha za ruzuku kuna conflict of interests? Je haoni kwamba kitendo hiki kinajenga mashaka makubwa dhidi yake juu ya accountability, credibility,transparency?
4. Je haoni kuwa tendo hili la kujikopesha fedha za ruzuku ni tendo la kifisadi?
5. Je huku siyo kutumia vibaya madaraka?
6. Je haoni kuwa akiwa Ikulu kuna uwezekano mkubwa akajikopesha bajeti yote ya ikulu?

Tamko: Dr. Slaa hafai kuwa raisi.
 
Sasa Mwita Maranya, na wale wanaopata mgao wa zile bil 3 zilizotengwa kwa ajili ya kumchafua Dr Slaa na Chadema nao hawana cha kuandika kweli kama wewe??

Kweli kamanda Aweda umenikumbusha jambo la msingi sana, kuna watu hawawezi kupeleka mkono kinywani hadi walitaje mara nyingi sana jina la Dr. Slaa hapa JF.
 
Maswali mengi kuliko majibu hapa.
Mkopo uliidhinishwa na nani
Je CHADEMA kina utaratibu wa kukopesha wanachama wake
Slaa anasema hawezi kukopa kwingi -si ni uongo huu?
Hana hati ya nyumba kukopea benki?
Na kukmbukumbu za pay -in slips zipo?

Nani mwingine " kajikopesha " hela ya chama?

Something fishy around here!
Tatizo la hawa viongozi ni kujiingiza kwenye siasa kwa manufaa binafsi,leo Dr Slaa ameshakuwa mbunge na alipwa kiinua mgongo,ni board member CCBRT,analipwa mil 7 kwa mwezi Chadema plus posho za vikao na safari,bado anatolea macho ruzuku? Halafu bila aibu anasema akakope wapi kama sio kwenye chama.Inasikitisha kwa kweli yaani natamani hata kulia halafu ndio anajiita mkombozi???
 
1. Kusema kuwa watumishi wa vyama hawaruhusiwi kukopa ni uwongo mtupu na uzushi.

Una mfano hai wa mwanasiasa aliyewahi kukopeshwa na taasisi za kifedha based on malipo/mshahara anaopata kutokana na utumishi wake katika chama cha siasa? Kwamba amekopeshwa kwa dhamana ya chama anachokitumikia. Usinitajie wafanyabiashara ambao ni wanasiasa.
 
Una mfano hai wa mwanasiasa aliyewahi kukopeshwa na taasisi za kifedha based on malipo/mshahara anaopata kutokana na utumishi wake katika chama cha siasa? Kwamba amekopeshwa kwa dhamana ya chama anachokitumikia. Usinitajie wafanyabiashara ambao ni wanasiasa.
Sasa huko alikokopa ni SACCOS au Vikoba? huu ni huuni na matumizi mabaya ya ruzuku kama anaona hawezi kuufanya kazi ya siasa si akatafute kazi itakayomlipa vizuri na si kuja kula pesa za ruzuku.

 
Ni bora kiongozi anayekopa na kurudisha kuliko mafisadi wanaojikwapulia mali za umma na kutokomea kusiko julikana! Hata wakiambiwa wamekwapua hakuna anayekiri utafikiri wao ni malaika hawakosei! Mimi na muona Dr. Slaa kama mtu anayeishi maisha ya kawaida anaishiwa kama sisi na anahitaji msaada wa kifedha kwa njia halali kama sisi! Nazidi kumwani kama kiongozi anayelifaa hili taifa!
 
Mosi, Tupe kipengele cha katiba ya Chadema kinachosema ni marufuku kumkopesha katibu mkuu.

Baraza kuu ndo tunaweza kuhoji hilo siyo wewe.
Acheni hoja dhaifu za kutetea ufisadi>
Ficheni nyuso zenu kwa unafiki mnaouonyesha hadharani.

Mnapata ujasiri wapi kukemea ufisadi serikali wakati nyie wenyewe mna mizizi ya ufisadi na kutetea ufisadi?

Mtumishi wa serikali "akijikopesha" fedha ya umma mtakuwa na uhalali gani wa kuhoji kama suala hilo vile vile litaishia vikao husika?

Kweli wezi hawana aibu!
 
Mwambieni Dr Slaa the damage done is collosal and permanent, credibility ya uaminifu kwa hela ya chama ina dondoka kwa kasi kubwa.
CHADEMA inatumiwa kama kampuni binafsi

Maswali mengi kuliko majibu hapa.
Tutajuaje alikopa 20mil na si 140mil
Mkopo uliidhinishwa na nani?
Je CHADEMA kina utaratibu wa kukopesha wanachama wake
Slaa anasema hawezi kukopa kwingi -si ni uongo huu?
Hana hati ya nyumba kukopea benki?
Na kukmbukumbu za pay -in slips zipo?

Nani mwingine " kajikopesha " hela ya chama?

Something fishy around here!
Acha Kiherehere Mkuu!Mambo ya CDM waachie CDM,vinginevyo utafananishwa na wanawake wa uswahilini(Wambea),wanaopenda kufuatilia mambo ya watu.
 
Humu Jf mammuluki wa CCM ni mburura kweli kweli. Hoja ya Dr. kukopesheka haina mashiko kama ilivyokuwa ya kumiliki kadi ya magamba. Nyie mngetwambia Slaa kashikwa na contena la meno ya Tembo kama msimali KINANA katibu mkuu wenu hapo tungeshake. Badala ya kujadili yale makontena ya pembe za ndovu mnakomaa na ruzuku za CDM. Huoni huo ni ujinga. Haya tupeni CCM mnapata ruzuku kiasi gani kwa mwezi na matumizi yake kama hamjakimbia humu jukwaani. Kwa vyovyote vile slaa ni muiba kwenu. T2015 CDM lazima iwamalize. kama vipi panda twende au hamia CDM.
 
pesa zilishalipwa kwahiyo tunabishania deni ambalo ni non exist watanzania sisi kwanini tunapenda kubishana vitu vya kijinga na kuacha mambo msingi utakuta mtu anabishana mpaka mishipa inamtoka kubishania simba na yanga wakati mali za taifa zinapotea hata habari hana halafu anashangaa kwanini huduma za jamii zinadidimia.
nilisha sema kuhangaika na vichwa maji ni kuumiza kichwa,magamba hawana akili vichwa vimejaa maji machafu.
 
Una mfano hai wa mwanasiasa aliyewahi kukopeshwa na taasisi za kifedha based on malipo/mshahara anaopata kutokana na utumishi wake katika chama cha siasa? Kwamba amekopeshwa kwa dhamana ya chama anachokitumikia. Usinitajie wafanyabiashara ambao ni wanasiasa.
Mtoto wa Mkulima.Nilimsikia ktk 1 of his speech.For more ref p'se mtafute mwenyewe.
 
pesa zilishalipwa kwahiyo tunabishania deni ambalo ni non exist watanzania sisi kwanini tunapenda kubishana vitu vya kijinga na kuacha mambo msingi utakuta mtu anabishana mpaka mishipa inamtoka kubishania simba na yanga wakati mali za taifa zinapotea hata habari hana halafu anashangaa kwanini huduma za jamii zinadidimia.
mkuu tatizo lenu hamtuelewi sisi ccm hatuna tatizo na mkopo wa slaa, tatizo letu sisi ni slaa kugombea uraisi mwaka 2015! Tunataka kummaliza kabisa!na kuimaliza chadema.
 
Una mfano hai wa mwanasiasa aliyewahi kukopeshwa na taasisi za kifedha based on malipo/mshahara anaopata kutokana na utumishi wake katika chama cha siasa? Kwamba amekopeshwa kwa dhamana ya chama anachokitumikia. Usinitajie wafanyabiashara ambao ni wanasiasa.
Let us be principled. Kwa kitendo cha katibu mkuu wa chama(Dr.Slaa) kukopa fedha ya ruzuku ni uthibitisho tosha kuwa huyu ana uroho mkubwa wa fedha na mali za umma. Ni dhahiri kwamba chama kinahitaji fedha hizi kwaajili ya kujiimarisha ya aina yoyote ile. Wanafanya kazi kwa kujitolea. Dr. Slaa analipwa kila mwezi mshahara wa sh.mil.7 plus other benefits. Huyo huyo anakopa fedha ya walalahoi ya ruzuku. Kitendo hiki alichofanya Dr. slaa ni cha kihuni, amepoteza moral authority ya kuwa kiongozi anayeweza kuaminika ktk nchi yoyote ile.Kama alikuwa na shida Je hakukuwa na namna nyingine ya kupata fedha, mpaka akope za ruzuku?
Watu wanaropoka majukwaani kuwa wanapigania haki za wananchi, kumbe wanapigania matumbo yao.
This is very bad, it is double standards.Dr. Slaa sasa awaachie vijana kazi ya ukatibu mkuu. Wakpo wengi wenye uwezo mkubwa sana zaidi yake.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom