Dr Slaa ajibu tuhuma dhidi yake

Dr Slaa ajibu tuhuma dhidi yake

Status
Not open for further replies.
Sijawahi changia thread za kijinga kama hii ila ngoja nifanye once and last. Kwani kama unafanya kazi sehemu ya kwanza kukopa ni kazini kwako au bank? Na je unapoishi utaanza kuulizia wakukukopesha jirani wa karibu au utatafuta mtaa wa tatu......Caritas peribus
Hoja hapa siyo kukopa hoja kubwa ni kwamba mbona habari hii ilipotolewa miezi saba iliyopita Dr. Slaa hakuja kutoa ufafanuzi huu anaoutoa leo kwani hii si habari mpya
 
hapo kwenye sumu mnajidanganya, mumemshindwa mwaki... na mwando..wenye jeshi dogo mtamuweza Dr. mwenye jeshi hadi korido za Ikulu?

si ndo nakuambia kwa kuwa tumechemka nikumuua kwa maneno tuu mpaka umaarufu wake uishe kabisaa!
 
Kwahiyo ulitaka riba iende taasisi ya fedha na wala tusiipate CDM. Haya basi mwenzio kaangalia penye riba nafuu akaona ni kazini kwake kwake kimeharibika nini?
Sasa mbona hakusema alikopeshwa kwa riba ya asilimia ngapi?
 
Dr. Slaa ni mbumbu wa sheria. Kukaa kimpya maana yake umekubali, siyo umepuuza.Silence presuposes concerned.
Kama mnautaratibu wa viongozi wakuu wa chama kukopeshana fedha za ruzuku(fedha za umma, siyo za kibiashara), basi utaratibu huo ni mbovu, na hauna uhalali wowote kimaadili.Kwasababu hilo siyo lengo la ruzuku. Ruzuku ya fedha ya walipa kodi kwaajili ya kuimalisha demokrasia nchini. Pia, kwanini utarajibu wa kukopeshana ruzuku anufaike nao katibu mkuu tuu wa chama na si mlalahoi mwingine wa chama hichohicho? Dr. Slaa hapa umechemka. Huna mlango wa kutokea. Huu ni ufisadi wa kimkakati!

We ndio MBUMBUMBU wa sheria, sio kila wakati kukaa kimya ni kukubali wakati mwingine kukaa kimya ni kutokubaliana na kile kinachosemwa hasa kama yale yanayosemwa hayajatolewa mahali panapostahili. Tuhuma hizo zingekua zilitolewa kwenye vikao halali, ukimya wake ungemaanisha kukubaliana lakn kwa vile tuhuma zimetolewa mitaani, kukaa kimya ni busara na kutokubaliana na kilichosemwa.

Katibu mkuu wa chama ni mwajiriwa kama waajiriwa wengine na ana haki zote zinazopaswa kutolewa kwa mwajiriwa ikiwepo kukopeshwa ili kuboresha maisha yake. Dr Slaa kama mwajiriwa wa CHADEMA ana haki ya kukopa na kukopeshwa ili kuboresha maisha yake. Chama cha siasa ni organisation kama zilivyo organisation nyingine ziwe za kibiashara, 'club' au 'charity', ina mapato na matumizi kama zilivyo organisation nyingne, suala la mkopo kwa mwajiriwa halijalishi mapato ya organisation yanatoka wapi. Ruzuku na ada za wanachama haizuii fedha hizo kukopeshwa kwa waajiriwa, hata kama kukopesha sio lengo la organisation hiyo.

Tuache siasa/hoja za kitoto wakati wengi wetu ni waajiriwa na tunajua ukweli kuhusu hilo swala la mikopo kwa waajiriwa.
 
Hakuna kubishana watu wanataka kujua. Kwa hiyo hata nyie mnalalamika humu JF serikali imejaa mafisadi ni machizi. Kwa nini msipeleke malalamiko yenu serikalini.
si tukipeleka tunaambiwa tunash ngapi haaaa milushwa tuu imejaaa!
 
hapo kwenye sumu mnajidanganya, mumemshindwa mwaki... na mwando..wenye jeshi dogo mtamuweza Dr. mwenye jeshi hadi korido za Ikulu?

Seifu yupo wapi mkuu saizi analamba matak yetu tuuu ccm si mchezo mkuu!
 
Katika hili Dr Slaa kachemka,bora angeendelea kukaa kimya kwani majibu yake utasema kamtuma Le Mutuz kumjibia.
 
Mkuu, issue ni kwamba swala hili lililetwa hapa JF kwa mara ya kwanza na TUNTEMEKE ambaye alipigwa ban kwa kosa la kuleta "taarifa ya uongo". More than 14 months later, ndio babu anajitokeza kukubali kuwa alichukua pesa za chama.
Mbaya zaidi, babu anakuja na porojo kuwa watumishi wa vyama vya siasa hawaruhusiwi kukopa. Halafu babu huyuhuyu anataka aaminiwe kuachiwa Ikulu. Bado huoni issue ilipo Jasusi?

Bora kukopa kuriko kuiba
 
Last edited by a moderator:
Utaratibu gani ulitumika kumkopesha? Je, viongozi wengine pia wanaruhusiwa kukopeshwa? kwa utaratibu upi?
Kwanini TUNTEMEKE alivyotoa tuhuma hizi kwa mara ya kwanza mwaka 2011 alipigwa ban wakati inaonekana kweli wakati huo deni lilikuwepo? - Tuntemeke aombwe radhi, to be fair...
Tuhuma zimeendelea kuwepo kwa sababu hazikujibiwa.

Tuhuma zozote zile nilazima zithibitishwe beyond easonable doubt, if his allegation is lacking impecable evidence itachukuliwa mojakwamoja ni uzushi hatakama ni kweli kosa limetendeka.usisahau uongo na uzushi unastahili adhabu.
 
WanaJF,
Nilidhani walioko humu ni great Thinkers. Nilisema hakuna hoja ya kujibiwa hivo sina muda wa kupoteza kujibu hoja za kufikkirika. Ni jukumu la mwenye kuleta hoja kutoa ushahidi si jukumu la mtuhumiwa. Ndio maana wakati wa EPA/B0T. Nilitoa account no, bank husika, majina ya wahusika, tarehe ya transaction na kadhalika. Kama ni kutamka anybody anaweza kutamka chochote hat a kichaa. Hivyo watanzania, nikikaa kimya maana yake nimepuuza kwa kuwa hakuna hoja ila wanaoleta wanadhamira tu ya kutuondoa kwenye hoja za msingi. Nagpenda kwa Mara ya mwisho niwahakikishie woe wenyewe mapenzi MEma Chadema iko makini, yote tunayofanya ni kwa mujibu wa taratibu zetu tulizojiwekea. Iwapo mwenye nia Njema anahitaji kufahamu jambo milango ya makao makuu yako wazi saa zote alimradi unafuata taratibu za kawaida za kiofisi.
..Ni vizuri sana Dr.umekuja kujibu hizi hoja za kizushi dhidi yako....Mimi najua wewe ni mtu safi na maadui zako wako ndani na nje ya chadema....na wanatumia mahusiano yako na Bi Mshumbushi kutaka kukuangamiza kisiasa...hasa baada ya kukosa hoja za msingi dhidi yako....That said, nikupe tu angalizo la msingi: Kwa kuwa bi Mshumbusi anakuwa kama target wanayotumia maadui zako dhidi yako...basi cha msingi jitahidini kumweka mbali na majukwaa ya kisiasa....kama ni kazi za chama...well afanyie huko mahofisini....maana yaonekana anafuatiliwa kwa karibu sana na maadui wenu(mapandikizi ya ccm)walio ndani ya chadema....haya tumeyaona na tutaendelea kuyaona.....na wanaweza hata kumbambikiza mambo ya kipuuzi humo humo ndani ya mahofisi yenu ya chama.....kuweni makini na mnayofanya ndani ya chama....Ni angalizo tu toka kwa ngosha.....
 
Dr.W.Slaa,

Wewe umesema CCM wameingiza mtambo wa kuiba kura wamenunua bilioni 2 bila kuweka ushahidi wowote. Watu kuhoji mkopo wako unasema walete ushahidi.
Mkuu Ritz,mwachie kidogo babu apumue kwanza ameshakimbia mjadala.Siku hizi Chadema wamekuja na style mpya "njoo makao makuu upate ufafanuzi zaidi na ufuate utaratibu" nina kila sababu ya kuamini kila atakaenda kufuata ufafanuzi hatorudi salama.

 
Dr.Slaa .

Kwanza nikupongeze kwa kutolea maelezo tuhuma hizi zilizokuwa zinaelekezwa kwako japo hazikuwa na mikono wala miguu. Nasema hazikuwa na mikono wala miguu maana hata waliokuwa wanazitoa walikuwa wanashindwa kutushawishi kama kukopa ni dhambi au kosa la jinai. Ni ajabu na aibu katika nchi yenye massive scandals na corruption ambazo zinatufanya tuwe na huduma duni za jamii kuanzia tiba mpaka elimu na miundo mbinu mibovu, chakafu na substandard tunapoteza muda kutunga vitu ambavyo kavyo havina damage kwa maisha yetu lakini tunaangalia nani kakopa nini na wapi. Asante kwa kulitolea maelezo.

Ushauri wangu ni kwamba kitengo cha mawasiliano cha CDM kinabidi kiwe kinatembelea JF and other social networks so as to clear the atmosphere when polluted by shortsighted CCM cadres and their disciples planted in CDM. Itasaidia sana kuliko kukuamisha au kuwaamisha viongozi wetu wa juu katika core issues ambazo ni constructive si kwa chama tu bali Taifa kwa ujumla. Taifa wala sio chama tu kinawahitaji nyie viongozi sio at party level even intra and inter party mkaongee na kuleta suluhu kwenye maswala nyeti yanayorudisha mstakabali wa Taifa hili kwa sasa na kwa vizazi vijavyo. Majibu yako yamewafanya propagandists kuwa tragic hero. Yanahitaji kuendelezwa na kitengo cha mawasiliano cha chama.
 
Dr. Slaa ni mbumbu wa sheria. Kukaa kimpya maana yake umekubali, siyo umepuuza.Silence presuposes concerned.
Kama mnautaratibu wa viongozi wakuu wa chama kukopeshana fedha za ruzuku(fedha za umma, siyo za kibiashara), basi utaratibu huo ni mbovu, na hauna uhalali wowote kimaadili.Kwasababu hilo siyo lengo la ruzuku. Ruzuku ya fedha ya walipa kodi kwaajili ya kuimalisha demokrasia nchini. Pia, kwanini utarajibu wa kukopeshana ruzuku anufaike nao katibu mkuu tuu wa chama na si mlalahoi mwingine wa chama hichohicho? Dr. Slaa hapa umechemka. Huna mlango wa kutokea. Huu ni ufisadi wa kimkakati!

Moma naona macho yamekutoka km moma mwenyewe,bahati mbaya doctor anatetewa na wanyonge humu na wala sio nyie mnaonufaika na mfumo kandamizi maccm,watu wenye roho mbaya mnapenda kuungwa mkono tu bila kuwa challenged ,mnaiba kila kitu,mmefilisi mashirika ya umma na bado mnaendelea kumalizia tanesco na bandari. Acheni siasa za kijinga,waacheni wanachama wa chadema waamue. Eti mnaleta hoja za kuzusha mnataka kuungwa mkono nendeni uhuru ,mzalendo na habari leo. Mnabore maccccccm na mtaendelea kuzomewa kila kona
 
Kwa nini kumfuata mtu mpaka kwenye nguo zake.Issue hapa ni kukopa hajaiba,haijalishi anakopa bank au kwa mtu binafsi.Hata serikalini mfanyakazi anaruhusiwa kukopa, sasa kama sheria ya kazi ya Chadema inaruhusu mfanyakazi wake kukopa ubaya uko wapi?Kama Dr.Slaa ni muajiriwa wa CHADEMA basi kuna haki alizonazo ukilinganisha na mwanachama wa kawaida.Tusikuze mambo bila sababu.Hata Tuntemeke hakuwa na haki ya kutoa siri za maisha ya wtu hadharani je anajua kwa uhakika haki alizonazo Dr.Slaa kama muajiriwa wa CHADEMA?Kama anazijua alipata wapi contract ya Dr.Slaa,kama alipewa na afisa uajiri basi afisa uajiri wa CHADEMA anapaswa kufukuzwa kazi sababu ameshindwa kuweka siri za muajiriwa wake vyema.
 
Kwa Taratibu za Kiiutumishi ,Sheria Mama ya Tanzania Mtumishi akiwa nje ya Kituo analipwa Posho ya Kujikimu. Nimeshuhudia akina Mama wanalipwa Yeye ,Mtoto na Yaya na hata safari zake. Pia anapohamia mahali furani analipwa Yeye Mke/Mume na Watoto wanne akiwasilisha Cheti cha Ndoa na vyeti vya kuzaliwa watoto,Pia bima za afya n.k, CHADEMA lazima iki comply na sheria mama kwa kuwa siyo exception. Josephine alikuwa Kichama kwenye kesi ya Arusha.
Weka ushahidi kuonyesha kwamba sio 140 ni 20, na ushahidi kwamba zimelipwa zote...kwa hiyo yaya analipwa na chama?
 
...""Kama sio juhudi zake Shonza, haya yote tungepata wapi... kama sio, Kama sio juhudi zake TUNTEMEKE, haya yote angejua nani? x 3"" huu wimbo umebamba na ni mtamu ukisindikizwa na vigelegele vingiii vya masalia na miluzi. I looooove this song!!!!
 
Viongozi wa vyama vya siasa wangekuwa hawawezi kukopa Mbowe angekuwa hadaiwi na NSSF. Yaani na wewe unadanganyika haraka na kirahisi namna hiyo?! au ndio ile mtu akipenda chongo huita kengeza? Mikopo ipo kwa watu wote wanaokopesheka.Kama hakopesheki basi tatizo ni lingine lakini siyo kwa kuwa ni mwanasiasa. By the way, Slaa na mshahara wa milioni 7 alikuwa na ulazima gani wa kuchukua tena milioni 20 za chama?

Mkuu,
Hata majibu yake yanazua maswali mengine mengi;
-Pesa zilikopwa lini?
-kwa utaratibu upi
-Kwa kanuni zipi za chama
-utaratibu wa kukopa ndani ya chama ulianza lini na ulipitishws na kikao kipi cha chama

-Chama kinasemaje kwenye vitabu juu ya malipo ya nani wa girlfriend wa katibu mkuu wa chama.

Maswali ni mengi tu
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom