Dr Slaa ajibu tuhuma dhidi yake

Dr Slaa ajibu tuhuma dhidi yake

Status
Not open for further replies.
Unachokisema ni kweli lakini ndani ya CHADEMA hakijawahi kuwepo. Sera za CHADEMA ziko wazi na Kila kukicha zinaongewa kwenye jamii. Hakuna kipengele chochote kinachosema kama chama kinatoa unsecured loan kwa wanachama wake, ndiyo maana haijawahi kusikika kwa kiongozi yeyote akisema hivyo.Uungwana ni kukubali makosa pale yanapogundulika. CLOSED
Kanuni za ajira za chama sio sera.. hapo umechemka mzee, waajiriwa wana kanuni zao za ajira na zinabadilika kulingana na wakati, mfano mishahara hubadilika kulingana na kupanda kwa gharama za maisha, ajira hubadilika kulingana na teknolojia na uhitaji hivyo sera hazihusiki hapo ila kuna kanuni za watumishi na mahali popote penye ajira kuna mshahara na kama ndivyo kuna advances na loan kulingana na makubaliano na mwajiri, mikopo ya ajira sio unsecured kwamaana ajira yako ndio dhamana yenyewe ndugu au wewe upo dunia ipi hujui hayo?
 
Chama makini ni CCM ambacho wanakwiba pesa za Umma. mtueleze kwanza assets zote za viwanja vya mipira na majengo ambayo Watanzania wote tulishiriki kuvijenga pesa zake ziko wapi?

Hivi unafikilia kwa kuleta hoja kama hii ndiyo itaiua hoja ya msingi kwenye hii thread.

Kwani si inaaminika CHADEMA ni chama makini zaidi ya CCM. Sasa comparison ya nini wakati jibu unalo.

Achana na 'madudu' ya CCM, hoja iliyopo hapa ni uadilifu wa uongozi ndani ya chama katika macho ya katiba, kanuni, miongozo ya chama.

By the way, Mimi siyo mwanaCCM
 
Public figure 1008 friends only, loved by many JF users..... Napata shaka kama jamaa hakubaliki kiivo kama tunavodhani
 
Tatzo ni kukopa au tatzo n kulipa? mbna selikal ye2 imekopa more thn 20 tillions au imelipwa? na walipokopa walitujuza km wanaenda kukopa? mbna 2mekuja kufaham baada ya kuwa walishakopa au nyie mliambiwa kwamba 2naenda kukopa?
 
Kanuni za ajira za chama sio sera.. hapo umechemka mzee, waajiriwa wana kanuni zao za ajira na zinabadilika kulingana na wakati, mfano mishahara hubadilika kulingana na kupanda kwa gharama za maisha, ajira hubadilika kulingana na teknolojia na uhitaji hivyo sera hazihusiki hapo ila kuna kanuni za watumishi na mahali popote penye ajira kuna mshahara na kama ndivyo kuna advances na loan kulingana na makubaliano na mwajiri, mikopo ya ajira sio unsecured kwamaana ajira yako ndio dhamana yenyewe ndugu au wewe upo dunia ipi hujui hayo?

Mkuu,
Mimi nilichofanya ni kuweka muendelezo wa hoja hii
chama ni kama organisation nyingine tu. kina haki ya kutoa mikopo kwa wafanyakazi wake kulingana na sera zilizowekwa na chama husika. Huwezi chukua mkopo wa Mbowe ambao ni secured ukaanza kusema mbona yeye kakopeshwa? huo utakua uendaw.... .
Wewe tuambie ni taratibu zipi zinawakataza kutoa sababu hilo ni suala la sera tu( Policy). Kila chama kama taasisi zingine kina sera zake za fendha (Financial Policies) ambazo zina baraka ya msajili wa vyama So tusikurupuke kama hatujui za CDM zipo vipi. CLOSED

CHADEMA ni unique (political party), siyo kama organisation nyingine ambazo umetolea mifano kwa sababu hata formation na uendeshaji wake ni tofauti. Ni makosa kutaka kuharalisha jambo kwa kuweka mifano ili iendane na kilichotendeka.

Tatizo Watanzania hatuna mazoea ya kukili makosa na kuomba msamaha na yakaisha. Ustaarabu ni pamoja na kufanya hivyo ukichukulia kama wasemavyo kuwa mkopo umeisha lipwa.
 
Viongozi wa vyama vya siasa wangekuwa hawawezi kukopa Mbowe angekuwa hadaiwi na NSSF. Yaani na wewe unadanganyika haraka na kirahisi namna hiyo?! au ndio ile mtu akipenda chongo huita kengeza? Mikopo ipo kwa watu wote wanaokopesheka.Kama hakopesheki basi tatizo ni lingine lakini siyo kwa kuwa ni mwanasiasa. By the way, Slaa na mshahara wa milioni 7 alikuwa na ulazima gani wa kuchukua tena milioni 20 za chama?

Zemarcopolo, umeshaambiwa Rais wa mioyo ya watanzania alikopa na amesharejesha tatito liko wapi? Kwa position yake ana majukumu yanayohitaji pesa zaidi ya milioni 7 za mshahara wake. Wewe kama ungekuwa na akili timamu ungefuatilia raslimali na mabilioni ya fedha za watanzania zinazoibwa na magamba wenzako. Tatizo la magamba mkienda chooni mnakunya akili
 
Mbona hoja zote hizi zilishajibiwa na hata waasisi wa hizi propaganda walishahama huko ndio maana kila kukicha wanakuja kwa staili mpya, wewe bado umebaki huko? Go back and read sidhani kama utabaki ulivyo.


ondoa ukungu kwenye ubongo wako. ondoa tongo kwenye macho yako. sipendi majibu ya kijiweni. jibu hoja zangu 3 hapo juu. la sivyo kaa kimya!
 
Tatizo siyo kurudishwa kwa mkopo tu, tatizo ni kanuni, mwongozo na taratibu zipi ndani ya chama zilitumika kumpatia huo mkopo na malipo ya nan wa girlfriend wake

Huoni kama kuna hoja ya kujibiwa ukizingatoa CHADEMA inataka kuudhihilishia uuma wa Watanzania kama ni chama makini katika utendaji wake

Suala la msingi kwanza sio kujua kanuni, mwongozo na taratibu gani zilitumika, bali inabidi mtueleze taratibu gani zilivunjwa katika kutoa huo mkopo kwa sababu mkopo ni suala la kawaida kwa waajiriwa. Dr Slaa kama mwajiriwa wa Chadema ana haki zote wanazostahili waajiriwa wengine, ikiwemo haki ya kupewa mkopo ili kuboresha maisha yake.
 
Hebu tupe kwanza kwa ufupi personal affairs za Rais wetu aliyepo Madarakani JK, maana Ridhiwani ana Mama yake, Miraji ana Mama Yake na Salma Kikwete ana watoto wake, halafu tumalizie na masaibu ya Babu Seya huenda ukafanikiwa kuniondowa Wazimu wa kumpenda Dr Slaa, kiasi kwamba nimeshamuandalia kura yangu.

ondoa ukungu kwenye ubongo. ondoa tongo machoni. amka!!!!!!!!!!!! acha mambo ya kijiweni hapa. jibu kwanza hoja zangu 3 kama ni kweli au uongo. hapa ni nyumbani kwa great thinkers. kama unaona ubongo wako hauwezi kujenga hoja, kaa kimya
 
Wewe Kijana hoja hapa siyo hayo unayosema hoja hapa ni UADILIFU. Kama ameshindwa kuwa mwadilifu akiwa Kiongozi wa Upinzani matokeo yake KAPORA MKE WA MTU, KACHUKUA PESA BILA KUZINGATIA TARATIBU unategemea akiwa Kiongozi wa Nchi atafanya nini kwa wake za watu na watoto za watu wa kike watakaokuwa miongozi mwa wasaidizi wake? Hoja siyo mwadilifu kwa masuala ya mapenzi.

Pili kama ameweza kuchukua pesa kwenye Chama bila kuwepo utaratibu wa aina hiyo atashindwa nini akiwa Kiongozi wa Nchi kuchukua mijipesa pale BoT na kuipeleka kwa kina Josephine wengine?

Hakuna anayetaka kuiua CDM bali tunataka na wao wajisafishe vile vile wanavyowasema wengine wajisafishe. Siyo unatazama kibanzi jichoni mwa mwenzako wakati wewe una Boroti jichoni mwako.
wajisafishe kwa nani sasa???wewe na magamba wenzio au?and then mtafanya nini?poleka hukooo
 
ondoa ukungu kwenye ubongo. ondoa tongo machoni. amka!!!!!!!!!!!! acha mambo ya kijiweni hapa. jibu kwanza hoja zangu 3 kama ni kweli au uongo. hapa ni nyumbani kwa great thinkers. kama unaona ubongo wako hauwezi kujenga hoja, kaa kimya
Wewe ni Great Stinker, usijipe jina ambalo ushabihiani nalo, best option kwangu ni kukuignore, mwaka huu sina muda wa kudebate na wajinga.
 
Tuna tatizo kubwa kwa vijana katika nchi yetu, wengi wao siyo wabunifu, siyo watafiti, siyo jasiri, na wengi wao wanapenda umbea. Uongozi wa sasa wa wazee una kasoro lakini kama vijana wengi tulio nao ni wa namna hii ya msalia, au ZeMarcopolo, Tanzania hakuna nuru inayoweza kuonekana hata kwa mbali.

Hata ndani ya serikali ya CCM, vijana ndiyo wameonesha uwezo wa chini kabisa katika uongozi, mtazame Ngeleja, Malima, Masele, na yule aliyekuwa wa utalii jina nimelisahau, all of them were and some of them are still the most hopeless Ministers this country has witnessed.

BAVICHA masalia, nao ni hovyo kabisa. Ukiwasikiliza tu unaona upungufu wa wazi katika logical analysis, na hata kutambua tu niseme nini kwaajili ya kupeleka ujumbe gani.[

ZeMarcopolo, hivi mkopo huwa anastahili kupata mwenye mshahara kiasi gani? Hivi hujui hata wakitafutwa watanzania wenye madeni makubwa, wote watakuwa ni watu wenye mapato makubwa? Kama WADHAMINI WA CHADEMA waliamua kumkopesha katibu mkuu wa chama ni lazima walizingatia uwezo wa mkopaji wa kulipa deni, definately mwenye mshahara wa milioni 7 ana uhakika wa kulipa deni la milioni 20 kuliko mwenye mshahara wa laki 2 kwa mwezi.

QUOTE=ZeMarcopolo;5511110]Viongozi wa vyama vya siasa wangekuwa hawawezi kukopa Mbowe angekuwa hadaiwi na NSSF. Yaani na wewe unadanganyika haraka na kirahisi namna hiyo?! au ndio ile mtu akipenda chongo huita kengeza? Mikopo ipo kwa watu wote wanaokopesheka.Kama hakopesheki basi tatizo ni lingine lakini siyo kwa kuwa ni mwanasiasa. By the way, Slaa na mshahara wa milioni 7 alikuwa na ulazima gani wa kuchukua tena milioni 20 za chama?[/QUOTE]
 
Wewe ni Great Stinker, usijipe jina ambalo ushabihiani nalo, best option kwangu ni kukuignore, mwaka huu sina muda wa kudebate na wajinga.


nashukuru kwa kuni ignore. umenipunguzia mzigo wa kukuelimisha. kazi ipo kwa mtu yeyote kukuelimisha coz unatanguliza mapenzi ili kuficha ukweli. ubarikiwe sana ili pazia iliyokufunika iondoke. unahitaji maombi
 
Kwanini hataki kujibu hoja zote zilizoelekezwa kwake na masalia? Kuanzia za magafu wa mwanza, mwampamba wa mbozi, juliana na kisandu? Kwanini anachagua anayopenda yeye? Nadhani katibu mkuu anapaswa kuufahamisha umma kwa uwazi zaidi kuhusu haya mambo..

Majibu yalishatolewa siku nyingi kwa hawa wote maana walikuwa wanatumia ID moja ya
TUNTEMEKE.
 
we mbona ujatuwekea ushahidi wa uyo unaesema anaiba mali za umma?!au babu tu ndio anatakiwa kusikilizwa wengine wanahukumiwa bila ushahidi ! Don't play double standard

Ushahidi gani unataka ndugu yangu? Hujasikia hoja za Richmond, na Dowans? Huo ulikuwa mtaji wa Kikwete. Kamuulize Lowassa.
 
Kanuni huwezi kuzijua wewe maana siyo mjumbe wa baraza la Wadhamini la CHADEMA. Tunaamini kanuni zilifuatwa na kama hazikufuatwa basi mlezi wa vyama vya siasa angekuwa amekwishalichukulia hatua baraza la wadhamini kwa mujibu wa sheria. Dr. Slaa siyo mtunza fedha wa chama, na wala siye anayeweza kuidhinisha bajeti ya chama. Mamlaka yote ya mali za chama pamoja na matumizi yake, yapo kwenye baraza la wadhamini, Katibu Mkuu ni Mwajiriwa wa chama.

Haya maswali yanaonesha watanzania tulivyo wepesi wa kutoa hoja. Tunapenda kuishi kwa hisia, ni wavivu wa kutafiti na kuchungua. Kama una mashaka kuwa taratibu hazikufuatwa ilitakiwa ufanye utafi, utafute na uzijue hizo hatua, na kisha uje hapa useme kuwa kuna hatua ambazo hazikufuatwa, nazo ni hizi hapa.

Jukwaa hili linaitwa la Great thinkers, lakini great thinkers sitarajii watazidi 5%. Unaweza kuhesabu michango inayotolewa humu, itakuwa ni bahati sana kama utapata hata 5% ya michango ya maana, walio wengi, wameifeuza JF ni kijiwe cha mipasho.

Tatizo siyo kurudishwa kwa mkopo tu, tatizo ni kanuni, mwongozo na taratibu zipi ndani ya chama zilitumika kumpatia huo mkopo na malipo ya nan wa girlfriend wake

Huoni kama kuna hoja ya kujibiwa ukizingatoa CHADEMA inataka kuudhihilishia uuma wa Watanzania kama ni chama makini katika utendaji wake
 
ondoa ukungu kwenye ubongo. ondoa tongo machoni. amka!!!!!!!!!!!! acha mambo ya kijiweni hapa. jibu kwanza hoja zangu 3 kama ni kweli au uongo. hapa ni nyumbani kwa great thinkers. kama unaona ubongo wako hauwezi kujenga hoja, kaa kimya

sramble,

Maneno yako yanalingana kabisa na jina lako-scramble. Kwa watu wa data na microwave signals wanajua maana ya scrambled signal kuwa ni signal ambayo imevurugwa au kuchafuliwa ili usiweze kujua kilichoko ndani.Ni uchafu au takataka tu hakuna kinachoeleweka.

Baada ya kusema haya nakuja kwenye hoja. Wazungu siku zote wanasema intelligent mind discuss issues while foolish mind discuss people.Msemo huu unaenda moja kwa moja kwa mijtu yote ya Magamba-CCM na mishabiki yake. Kwamba ni jambo la kusikitisha na kushangaza mijtu mizima na kengele zao inaacha KUJADILI ISSUES ZA KITAIFA BADALA YAKE INAKAAA KUMZUNGUMZIA MTU-DR.WILBROAD PETER SLAA!!!Shame on you bastards. Kuna issue za kitaifa ambazo ni very hot kwa sasa kama hii ya GESI ASILIA YA MTWARA/LINDI ilivyo kaa vibaya! Badala ya mijitu ya CCM inayojidai kuwa imeshika dola kukaa na kutafakari namna ya kuuzima moto wa Gesi asilia ya Mtwara imekalia kumjadili Dr. Slaa!!!

What is 20 million Tshs. hata kama zingelikuwa hizo 140m! Mbona kama nyie CCM mna uchungu na hela ya walipa kodi wa Tanzania hamuhoji kuhusu Ufisadi uliopo serikalini kuanzia maswala ya EPA,DEEP Green,Meremeta na Mabilioni ya Shillingi yaliyoko kwenye offshore accounts huko Uswiss???Kuna watu wanadaiwa mabilioni lakini hakuna anayepiga kelele.

Sijui ni kipi cha ajabu kwa mtu kukopa fedha ya chama na baadaye kuirudisha! Kama mtu anaweza kukopeshwa na Kanisa na baadaye akarudisha hiyo pesa kuna tatizo gani?? Mbona hata wafanyakazi wa serikali na mashirika ya umma hukopeshwa na waajiri wao mishahara 3,2 au 1 kutegemea na mhitaji na baadaye akakatwa polepole kutoka kwenye mshahara wake na deni likaisha!!

Watanzania tunatakiwa kubadilika. Huu ushabiki wa kishenzi wa kushabikia kitu cha kipuuzi ili kumchafua mtu na ilhali hakina tija yoyote kwa jamii na Watanzania kwa ujumla wake ni ufisadi wa aina yake. Hivi kuna viongozi wangapi wa Serikali ya CCM wanaofanya madudu kila kukicha???Lakini kwa vile wao wameshika patamu mambo huwa wanayafunika kwa kutumia njia za kibabe ili wasiumbuliwe. Napenda niwahakikishie enyi wanafiki na wazushi wa chama Twawala siku inakuja muda si mrefu ambapo halitasalia jiwe juu ya jiwe. Mbona kila jambo litawekwa hadharani na sijui mtaficha wapi nyuso zenu!!

Pole sana Dr. Slaa. Kwa Watanzania na all Great Thinkers wenye akili timamu wanajua ukweli kuhusu wewe na wana Imani kubwa na wewe hadi 2015. CCM wanalijua hili na ndiyo maana kwa sasa majeshi yao yote yamehamishiwa CDM na nia ni kummaliza Slaa ili kwenye GE 2015 washinde kiulaini. Wanajua ulivyowapa tabu wakti wa GE 2010 ambapo ilibidi watumie UWT,Polisi na NEC kuvuruga matokeo ili kuinusuru CCM. Wanajua kuwa wasipofanya hivi kwa sasa ili kukuchafua na wakijua kuwa 2015 tutakuwa na Katiba mpya na Tume Huru ya Uchaguzi hawataingia Ikulu!!!

Nina amini Mungu yuko pamoja na wewe na Mungu atakuwa amekwisha kuwaandalia Rais aliye bora kabisa kutoka CHADEMA come 2015. Tusubiri.
 
Weka ushahidi kuonyesha kwamba sio 140 ni 20, na ushahidi kwamba zimelipwa zote...kwa hiyo yaya analipwa na chama?


Tuhuma makini hupingwa kwa ushahidi makini zaidi wote waliotoa madai haya hakuna hata mmoja aliyekuja na ushahidi wa kudhibitisha tuhuma hizi dhidi ya Dr. zaidi ya malalamiko ya majukwaani na mitandaoni,binafsi nadhani njia aliyoitumia Dr.ni sawa.
 
Suala la msingi kwanza sio kujua kanuni, mwongozo na taratibu gani zilitumika, bali inabidi mtueleze taratibu gani zilivunjwa katika kutoa huo mkopo kwa sababu mkopo ni suala la kawaida kwa waajiriwa. Dr Slaa kama mwajiriwa wa Chadema ana haki zote wanazostahili waajiriwa wengine, ikiwemo haki ya kupewa mkopo ili kuboresha maisha yake.

Mkuu,
Dr. Slaa amekubali kama amepewa mkopo, tatizo letu ni kwa njia zipi alipata huo mkopo kwa sababu hakuna kipengele katika uendeshaji wa CHADEMA kinachoainisha na kururuhusu ofisa wa fedha wa chama kutoa mkopo kwa wanachama na kama kipo kama unavyodai basi kisemwe. Kama hilo nalo haliwezekani basi hakuna haja ya kuendelea kuliongelea kwa sababu limeeleweka katika macho ya watu wenye fikra pana.

Nafikili tukubali kutokubaliana kwa sababu badala ya kunijibu swali langu la msingi, unachofanya ni kuniuliza tena.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom