Dr. Ramadhan Dau aunguruma darajani Kigamboni

Dr. Ramadhan Dau aunguruma darajani Kigamboni

swali kama hili kamuulize balozi Ombeni ndie mwenye jibu zuuuuri zaidi ya dr. Dau
Haya bwana, tuishie hapo maana ukienda kumuuliza Ombeni atakwambia 'ni maelekezo kutoka juu' na unajua kuna sheria inayozuia kuhoji chochote hiyo ngazi ya juu hata kama ni kwa ajili ya kujifunza, hivyo sitaki kuvunja sheria!
 
Nimesikiliza voice note ambayo Dau katamka kuwa anamshukuru mheshimiwa raisi kwa kutambua uwepo wake cause hata kwenye ratiba alikuwa hajawekwa na hivyo alikuwa hajajiandaa kwa speech!

Naam..

Huwez kuzima nyota ya mtu kwa fitna na majungu...

Magufuli pia yuko smart
 
hahahaha!! hii picha hii kuna watu wanatamani wavunje simu zao wakiingalia ...

cc Ritz FaizaFoxy



13051531_1129481750426638_1956601341495157194_n.jpg

Kwi Kwi kwi kwi Leo WAMEUMBUKA! MIDOMO INANUKA KWA KUNUNA! hawana la kusema Dr Magufuli kawafunga midomo!
 
By the way maisha yenyewe ni mafupi.Yu wapi Nyerere wa Butiama.
  • Julius Nyerere International Airport
  • Mwalimu Nyerere University
  • Mwalimu Nyerere Foundation
  • Kigoda cha Mwalimu Nyerere
  • Uwanja wa Kambarage Shinyanga
  • Mwenye Heri Nyerere
  • Daraja la Nyerere
 
Kikwete alimyanyua Mramba mkono kule Rombo akawaomba wapiga kura wamrejeshe jembe lake baada ya muda akamfunga siku hizi nasikia anafanya usafi Mwananyamala hospital.

Halafu Ustaadhi Mohamed Said kanichanganya kweli kweli katuaminisha daraja la Kigamboni ni daraja la Dau leo Dr Majipu kalibatiza rasmi daraja la Mwl Nyerere mtu kutoka bara asiyejua kula chapati wala kufunga tai kafunzwa na wazee wa Kariakoo leo kila kitu kizuri kinaitwa kwa jina lake na kuwaacha wazee wetu wa Dar es Salaam bila hadhi wala kumbukumbu wakati jiji hili lao.Mzee Mohamed Said anatuchanganya sana sijui tumfuate nani sasa duh vyovyote mimi nitaliita daraja la Dau potelea mbali ubwabwa na juice za NSSF zimetutia upofu.
Prof Ngongo,

Vipi unayo ile ripoti ya feki ya CAG inayosema Dr.Dau alinunua ardhi heka moja milioni 800 Karatu utuwekee hapa.
 
Kumtegemea mtu akufanikishie mambo yako ni shiriki. Na dhambi kubwa Mungu anahekima yake kwa binadamu. Mnashangaa Dau kutokukumbukwa katika uzinduzi wa daraja alolisimamia, mbona hamkumbuki hata Uhuru wa Tanganyika mambo ni hayohayo ,kikubwa hilo daraja watakuwa wanapita viumbe wake Mwenyemungu waovu na wachamungu. By the way maisha yenyewe ni mafupi.Yu wapi Nyerere wa Butiama.
Dream Boy,
Abdulwahid Sykes
hakualikwa sherehe za uhuru.
Alizisikiliza sherehe za uhuru akiwa nyumbani kwake.

Wazee wa TANU waliompeleka Nyerere UNO 1955
walikuja Uwanja wa Uhuru wakakaa majanini.

Mzee Haidari Mwinyimvua anasema tulimuona Nyerere
amekaa jukwaa kuu na wale ambao wakati tunajenga TANU
wao walikuwa bega kwa bega na mkoloni wakitucheka.
 
Basi kila kitu Nyerere? Kwa nini lisiitwe kwa jina la mtu mwingine aliyetoa mchango wa maana usio wa kisiasa? Watu kama Shaaban Robert, Walter Rodney (Najua si Mtanzania lakini...), Mathias E. Mnyampala, Sheikh Kaluta Amri Abeid, John Stephen Akhwari.... au hata kwa kuvutia zaidi tungeweza kuwaenzi watu waliopigania heshima ya mtu mweusi kwa jumla: Steve Biko, Alhajj Shabbaaz, Mori Kante etc Ila sitegemei kama JPM anawajua hawa!
 
Mie mkazi wa Kigamboni hapa nilipo kichwa kinaniuma nikifiria kama nitaweza kumudu kuvusha kitoyota corolla DX changu hapo darajani, maana hizo gharama za ujenzi na hiyo mishahara ya watendaji wote hapo yooote nitabeba mie,duh!
Pantoni bado lipo wewe
 
Hujamsoma THE BIG SHOW? RUDIA:

Magufuli anasema siwez kuongea bila kumwita mtu alietoa mchango mkubwa kabisa katika daraja hiliii.
Hebu Dr Dau Njoo hapa mara mojaaa uongee kidogoo....


Mkuu F.F...mimi nawaambia hawa jamaa kuwa ni Rahis sana kuongea uongo lakin ni vigumu kuutetea uongo huo...

Leo wanashindwa wapi pa kuweka sura zaooo...
 
Kikwete alimyanyua Mramba mkono kule Rombo akawaomba wapiga kura wamrejeshe jembe lake baada ya muda akamfunga siku hizi nasikia anafanya usafi Mwananyamala hospital.

Halafu Ustaadhi Mohamed Said kanichanganya kweli kweli katuaminisha daraja la Kigamboni ni daraja la Dau leo Dr Majipu kalibatiza rasmi daraja la Mwl Nyerere mtu kutoka bara asiyejua kula chapati wala kufunga tai kafunzwa na wazee wa Kariakoo leo kila kitu kizuri kinaitwa kwa jina lake na kuwaacha wazee wetu wa Dar es Salaam bila hadhi wala kumbukumbu wakati jiji hili lao.Mzee Mohamed Said anatuchanganya sana sijui tumfuate nani sasa duh vyovyote mimi nitaliita daraja la Dau potelea mbali ubwabwa na juice za NSSF zimetutia upofu.
Ngongo,
Waingereza wangesema, ''You are making a mountain out of a mole hill.''
Soma bandiko langu.

Sijasemapo kuwa daraja jina lake ni Dau ila nimesema kila nikikutana
na vijana wa Kidaresalaam basi ikija habari za daraja utawasikia wao
wakisema, ''Daraja la Dau.''

Hebu ingia hapa:
Mohamed Said: DR. DAU AUNGURUMA DARAJANI KWAKE
 
Haya wale wenye roho ya husda angalieni kiduchu hii matumbo ya kuhara yawakate.


Hivi wameisikia hiyo "Bismillahi" aliyoanza nayo. Sitaki ugomvi na mtu.
 
Back
Top Bottom