Dr. Mwakyembe: Rais hajavunja sheria wala Katiba

Dr. Mwakyembe: Rais hajavunja sheria wala Katiba

kalou (naamini wewe siye yule mchezaji wa mpira): sijakuelewa mwizi ni yupi na mwizi mwingine ni nani, wameiba nini? Kama kweli ni wezi basi watakuwa wakiitina wezi huko gerezani. Pia huyo "Kaka Jesika" ni nani!

Mstaarabu hujibu hoja kwa hoja, au ndugu "kalou"!
Ukimuona mwizi gerezani ujue amekamatwa,wako wengine hawajakamatwa

Kalou ni jina, yule mchezaji Mpira Hana hati miliki nalo.

Mwakyembe alitakiwa kujibu hoja ya uvunjaji wa katiba wa Mtukufu Raisi na sio kuleta attacks za kipuuzi ,kwa kuwa ameamua kutojibu hoja kwa hoja maana yake amefungua uwanja wa kujibiwa kipuuzi pia,Mzee wa mabehewa feki

Huyu Jesika ni MTU wa muhimu hapa nchini, hebu jaribu kumgoogle Dada Jesika mtoto wa mtukufu utajua mambo makuu anayoifanyia nchi hii.
 
kwa kweli huku tunapoenda ni kubaya mpaka sasa raiya wanatamani bora asingekuwa mtanzania Maana ni aibu sasa.
Hta uzalendo unapungua, mtu akiona watu wanageuza nchi kuwa ya kwao binafsi sidhani kama watakuwa wanajali chochote kuhusu nchi hii, badala yake ni kukaa na kuwasubiria wafeli kisha kuwazomea, ndio wananchi wamekuwa hivyo siku hizi, kwa kuwa watu wanafanya wanachotaka na ukiwahoji wanakupuuza pengine hata kukufunga
 
Profesa nchi hii utegemea unapata kitu gani na sio fikra huru tena aksanteni hakuna sheria iliyovunjwa.

Hivyo hakuna haja ya mazungumzo sababu mko sawa kikatiba kisheria pia, wengine mtasubiri sana kuona ukweli.
Walah tuko mahali pagumu sana kiitikadi kama nchi, tutavurugana bila sababu kuna jambo moja tuu nalo ni majeshi yetu yasipokuwa makini wakti huu ni dhahama inakuja kwa taifa letu.
 
Sasa nyie CCM nawashangaa sana, nyie mnataka msihojiwe kuvunja katiba ya nchi kisa Chadema wamevunja katiba yao? kwa hiyo tuseme hata chadema wakifanya jambo lolote baya nyie mtalifanya pia kwa kuwa chadema wamelifanya?

Mkuu uko sahihi kabisa.

Mheshimiwa badala ya kujibu hoja anaelekeza mashambulizi kwa watoa hoja!
 
tatizo kwa nafasi yake hakupaswa kuweka mipasho bali fact. huyu ni wa kupuuzwa...

Hana facts zozote huyo mnafiki tu. Ni liability kwa watu wa jimbo lake na taifa. Poleni watu wa Kyela. Hamna mwakilishi kwa miaka 5.
 
Ukimuona mwizi gerezani ujue amekamatwa,wako wengine hawajakamatwa

Kalou ni jina, yule mchezaji Mpira Hana hati miliki nalo.

Mwakyembe alitakiwa kujibu hoja ya uvunjaji wa katiba wa Mtukufu Raisi na sio kuleta attacks za kipuuzi ,kwa kuwa ameamua kutojibu hoja kwa hoja maana yake amefungua uwanja wa kujibiwa kipuuzi pia,Mzee wa mabehewa feki

Huyu Jesika ni MTU wa muhimu hapa nchini, hebu jaribu kumgoogle Dada Jesika mtoto wa mtukufu utajua mambo makuu anayoifanyia nchi hii.

Kweli "kalou" ni jina ila kila jina analochagua mtu, au kupewa na wazazi huwa na maana kubwa likiwakikisha uhalisia fulani.

Mwakyembe hatakiwi kujibu hoja ya uvunjaji wa Katiba, kwa kuwa yeye kama mwanasheria anajua sheria inamtaka mtuhumu kuthibitisha tuhuma za mtuhumiwa. Kwa hivyo basi:
1) Ni ukweli mtupu kwamba vyama vya upinzani vina wanasheria tena nguri, wameshindwaje kuandaa shauri la kimahakama lililosheheni vifungu vya Katiba vinavyodaiwa kuvunjwa!
2) Viongozi wa vyama vya upinzani vimeshindwaje kutumia wanasheria wake kuandaa Tamko la UKUTA, likinukuu vifungu vya Katiba vinavyodaiwa vimefunjwa, ili kuthibitisha ukweli huo! Au "kalou" kama unavijua hivyo vifungu, viainishe humu jamvini, tuvijadili!

Tuachane na mawazo yanayotawaliwa na kusukumwa na matamko ya "wanasiasa uchwara" ambao kila kukicha watafuta na kutumia njia za kujipatia umaarufu kisiasa.
 
Safi sana Mh mwakyembe kwa maelezo yako ,maana kuna watu wanatokwa na povu Oooo Rais anavunja katiba bila kufafanua kwa kina amevunja katiba ibara ya ngapi tatizo wanaishi maisha ya kukalilishwa na ****** wa pande zile.
mwakyembe hana ubavu wowote wa kumsaidia rais wetu kwenye mambo ya katiba na sheria. hatak
ikitokea kesho rais akasema chama kinachopaswa kupokea ruzuku ni ccm tu mwakyembe atasema rais yuko sahihi na hajavunja katiba wala sheria. kiufupi wasomi wetu ni majanga.
 
Profesa nchi hii utegemea unapata kitu gani na sio fikra huru tena aksanteni hakuna sheria iliyovunjwa.

Hivyo hakuna haja ya mazungumzo sababu mko sawa kikatiba kisheria pia, wengine mtasubiri sana kuona ukweli.
Walah tuko mahali pagumu sana kiitikadi kama nchi, tutavurugana bila sababu kuna jambo moja tuu nalo ni majeshi yetu yasipokuwa makini wakti huu ni dhahama inakuja kwa taifa letu.

Tusijenge hofu za kufikirika. Tudharau maneno na harakati za kisiasa. Tuache kushabikia viongozi wa kisasa wanataka "kiki" za kujipatia umaarufu.

Mimi kama mimi ni ukweli mtupu niko huru wa kila aina, kwa jinsi ulivyoainishwa kwenye Katiba ya JMT, Sura ya Tatu, nikinukuu kifungu cha 29(1): "Kila mtu katika Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kufaidi haki za msingi za binadamu, na matokeo ya kila mtu kutekeleza wajibu wake kwa jamii, kama zilzivyofafanuliwa katika ibara ya 12 hadi ya 28 za sehemu hii ya Sura hii ya Katiba".

Iki mifano mingi kama hii ya uhuru wa kutoa mawazo yangu humu jamvini bila kuvunja sheria yoyote ya nchi.
 
Ma doctor uchwara, wasomi wetu wanateseka sana, na wenyewe wanajitahidi kuwa kama mkulu wao - kujitoa ufahamu. huwezi kuelewa kwa nini ktk utawala huu watu wanajifanya wamezaliwa bila common sense.
 
Huyu jamaa ni wazi kabisa sasa hivi ana akili ya maiti! Huwa nakumbuka jinsi alivyokufa halafu akafufuka!
 
Ma doctor uchwara, wasomi wetu wanateseka sana, na wenyewe wanajitahidi kuwa kama mkulu wao - kujitoa ufahamu. huwezi kuelewa kwa nini ktk utawala huu watu wanajifanya wamezaliwa bila common sense.
haa haa mkuu njaa mbaya sana...
 
Watu wenye nuru ya ufahamu wa kiakili nchi hii wanateseka sana kuona haya yanayofanyika.

Huwezi amini kabisa Prof mzima anakuwa mtu wa kujikomba?

Sielewi ana hofu gani kusaidia hii nchi. Tuna bahati mbaya sana kama Taifa
labda bado hajajijenga
 
Siasa ni kama msumeno hukata pande zote. Aliye madarakani leo kesho atakuwa mtawaliwa, na vivyo hivyo. Siku ipo na inakuja, wanadai Katiba ya nchi inavunjwa, watakuwa madarakani tukashuhudia wakivunja Katiba waziwazi.

Kuna ushahidi dhahiri kwa sasa, viongozi wa upinzani wanavunja Katiba ya Chama chao (rejea mada kuu) na Katiba ya nchi badala ya kwenda mahakamani (kifungu cha 30(3)) wanahamasisha mikutano ya hadhara na maandamano yasiyo na mwisho.
Mkuu Mwengeso nimekusoma vizuri. Lakini unajua kuwa, "Two wrongs don't make a right" CDM ikivunja katiba yao haihalalishi walioko madaralani nao wavunje katiba ya nchi. CDM ina wanachama wake na washabiki wake, lakini katiba ya nchi ni ya Watz wote bila kujali chama wala ushabiki. Tuwe wakweli na tuseme kile tunachoamini ni kweli bila kuangalia kuwa kuna mtu jana kadanganya kwa hiyo na sisi tufanye kama yeye.
 
Mmepigwa za uso na mswaada umepita mengine yote yamepita.
Sawa umepita, kwani wewe ulitegemea usipite mbele ya wabunge wengi wa chama dola? Hata ungepelekwa mswaada wa kuzuia watu kupumua utapita tu, baadaye ndio watakuja kugundua kuwa nao ni watu unawahusu. Miswaada inapitishwa kama vile kukomoa wapinzani kumbe inatuhusu wote. Unakumbuka ule wa mifuko ya jamii? Nani waliokuja kupiga kelele kama sio hao hao walioupotisha? Utadhani pale wanaposaini kuingia ndani ya bunge na akili zao wanaziacha hapo hapo nje, bure kabisa...!!
 
Aisee Dr mwakyembe upo vizuri hawa jamaa wao tu katiba yao waliivunja ......et Leo wanamshtumu Rais wetu.


.si wamuombe msamaha Dr slaa
 
Back
Top Bottom