Mwingereza
JF-Expert Member
- Jan 21, 2014
- 1,110
- 2,736
Kinachoendelea sasa hivi kinaogopesha. Maafisa wa TRA wameanza kuvamia makampuni. Wanataka ripoti ya mapato yako yote, Bank Account, malipo ya VAT, Rekodi ya manunuzi ya miaka 5 chini ya masaa 72 etc…
Maafisa hawa wa TRA wanafanya mahesabu yao na kurudi kwako kwamba umekuwa ukikwepa kodi kwa maana hiyo wanafanya estimate ya kiwango unachodaiwa. Matajiri wanaulizwa chanzo cha utajiri wao, mwisho wa siku wanaomba watoe hela au account zao zizuiliwe.
Kampuni moja ndogo sana hapa Temeke wanadaiwa million 350 wakati hata kwa mwezi hawaingizi million 60.
Makampuni mengi sana na matajiri wanalalamika kwa uvamizi huu. Hali ni mbaya. Na hii ni uhujumu uchumi maana hawa watu wanaenda kufunga bila shaka.
Sasa, swali langu: Haya makamuni yakifungwa, serikali itapata wapi mapato, na waajiriwa wataenda wapi?
Maafisa hawa wa TRA wanafanya mahesabu yao na kurudi kwako kwamba umekuwa ukikwepa kodi kwa maana hiyo wanafanya estimate ya kiwango unachodaiwa. Matajiri wanaulizwa chanzo cha utajiri wao, mwisho wa siku wanaomba watoe hela au account zao zizuiliwe.
Kampuni moja ndogo sana hapa Temeke wanadaiwa million 350 wakati hata kwa mwezi hawaingizi million 60.
Makampuni mengi sana na matajiri wanalalamika kwa uvamizi huu. Hali ni mbaya. Na hii ni uhujumu uchumi maana hawa watu wanaenda kufunga bila shaka.
Sasa, swali langu: Haya makamuni yakifungwa, serikali itapata wapi mapato, na waajiriwa wataenda wapi?