Dr. Magufuli anahitimisha Budget ya Wizara ya Ujenzi

Kimbunga

Platinum Member
Oct 4, 2007
14,941
9,947
Wadau,

Namsikiliza Dr., Magufuli akihitimisha uchangiaji wa budget ya wizara yake. Ameanza kupangua hoja moja baada ya nyingine akishuka na data. Anamshangaa mkosamali kwa kuwa hata akipewa anasema hakipo.

Msikilizeni kama mnapenda

TuneIn Web Tuner
 
Anasema fire pale kutakuwa na barabara nane na siyo nne. Anasema barabara zinazojengwa hapa Tanzania zingepelekwa Rwanda basi wanyarwanda wasingepata mahala pa kulima, nchi yote ingekuwa lami.
 
namna anavyoongea utadhani serikali inapiga kazi kweli

we msikilize kwa makini ..kila bara bara anasema TUNATARAJIA si kwamba ndio mpango au azimio ni kuijenga kwa rami. mambo mengi ni wishful thinking ...
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Anakuambia CCM Oyeee,
Chadema Oyeee,
Cuf Oyeeee,
TLP Oyeeee,
Nccr Oyeeee,
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Anakupa historia ya sheria ya hifadhi ya barabara tangia mwaka 1934!
 
mnafiki tu huyo, hana chochote ni mropokaji wa propaganda za ccm
 
Lazima atoe makilometa hapo na mavijiji ya uongo ili watanzania wamuamini,akili ndogo tuu huyo hana lolote
 
mnafiki tu huyo, hana chochote ni mropokaji wa propaganda za ccm

Mkuu lakini naona anakubalika na hata wabunge wengi sana waliochangia hoja yake naona wamemkubali sana.
 
Anamshangaa Rweikiza kutoiunga mkono bajeti, wakati hata wapinzani wameiunga mkono.

Anasema barabara ya bamba bay haitawekwa kwa lami, na huo ndiyo ukweli.
 
Hili lijamaa linachapa kazi tuache utani.
Japo siyo hela yake ya mfukoni lakini amesimamia ipasavyo.

Yupo makini
 
Anakupa historia ya sheria ya hifadhi ya barabara tangia mwaka 1934!

mie nimeshamchoka na mbwembwe zake bara bara haziendi zimesimama zinazofanyiwa kazi ni zile tu tulizo fadhiliwa hata ukisikiliza mchango ya wabunge wengi hata wa ccm wanalalamika pesa na mambo yaliopangwa mwaka jana hayajafanyika

 
Dr. Magufuli bwana anawajua hata wenyeviti wa vijiji! Anamhabarisha Rweikiza! Masikini kumbe Rweikiza kakosea na kudhani mkataba ulikuwa wa Ujenzi kumbe siyo ni wa TAMISEMI! Duh Magufuli mwacheni aitwe Magufuli.

Anaitaja Katerero wabunge wanacheka!
 
Hili lijamaa linachapa kazi tuache utani.
Japo siyo hela yake ya mfukoni lakini amesimamia ipasavyo.

Yupo makini

Kumbe mkuu Mungi nawe unaliona hilo. Jamaa amejipambanua tofauti na wengine. Kwa hakika CCM ingepata mawaziri watano tu kama huyu basi isingekuwa na tabu iliyonayo sasa.
 
Last edited by a moderator:
Anasema fire pale kutakuwa na barabara nane na siyo nne. Anasema barabara zinazojengwa hapa Tanzania zingepelekwa Rwanda basi wanyarwanda wasingepata mahala pa kulima, nchi yote ingekuwa lami.

Mkuu, anasemaje kuhusu kampuni ya Ujerumani Strabag International kuhusu mradi wa mabasi yaendayo kasi?
 
Back
Top Bottom