DOWANS vs TANESCO - Why TANESCO Lost?

DOWANS vs TANESCO - Why TANESCO Lost?

Mpaka sasa naona gemu ni bila bila.
Bado sijaona maoni ya kujinasua kwenye hii tindikali.
Hivi jamani huyu mdudu anayeitwa Rostam Aziz anaishi wapi? HQ ya ofic yake ni wapi? ana familia kama wanaume au binadamu wengine?
NAOMBENI HAYO MAJIBU WAKATI TUNATAFUTA la kumfanya itatusaidia vile vile....IF DEMOCRACY IS FAILED DICTATORSHIP IS RECOMMENDABLE
Kama yeye hatuonei huruma wala aibu kwenye kodi zetu nasi hatuna sababu ya kumwonea huruma wala aibu.!!
 
Wakuu, mkumbuke government negotiating team ndio walioipitisha Richmond iliyoleta dowans na si TANESCO , wataalam wa tANESCO waliikataa na ndio maana waliowajibishwa ni viongozi waandamizi wa serikali

No, kuwajibishwa kwa GNT ni haki lkn pia kama mbuzi wa kafara. Ukweli n kwamba hyo GNT haikuwa na maamuzi yyte,ilikuwa inafanya majadiliano ya agenda flani ambayo kimsingi ilikwisha-amriwa,unadhani GNT wangefanyaje! Alyoiptisha Richmond ni EL na wala syo GNT. Pia Tanesco ilikuwa na wajumbe ktk hyo GNT
 
Mpaka sasa naona gemu ni bila bila.
Bado sijaona maoni ya kujinasua kwenye hii tindikali.
Hivi jamani huyu mdudu anayeitwa Rostam Aziz anaishi wapi? HQ ya ofic yake ni wapi? ana familia kama wanaume au binadamu wengine?
NAOMBENI HAYO MAJIBU WAKATI TUNATAFUTA la kumfanya itatusaidia vile vile....IF DEMOCRACY IS FAILED DICTATORSHIP IS RECOMMENDABLE
Kama yeye hatuonei huruma wala aibu kwenye kodi zetu nasi hatuna sababu ya kumwonea huruma wala aibu.!!

Hayupo nchini kwa sasa yy n familia yke yote! Jamaa hajiwezi naye ujue, i wish he wl die or balalirize b4 2015! Bcz hata serikali kwa sasa haiko upande wake-ameichanganya kabisa. Plz refer hta kauli ya Dr. Bilal alyoitoa huko bongo ktk mkesha. Aaa, bongo no naga bana wacha tuwapkie haluwa wamanga mpka bongo kieleweke!
 
Hayupo nchini kwa sasa yy n familia yke yote! Jamaa hajiwezi naye ujue, i wish he wl die or balalirize b4 2015! Bcz hata serikali kwa sasa haiko upande wake-ameichanganya kabisa. Plz refer hta kauli ya Dr. Bilal alyoitoa huko bongo ktk mkesha. Aaa, bongo no naga bana wacha tuwapkie haluwa wamanga mpka bongo kieleweke!

Mkuu kwani yuko nchi gani? inamaana hapa bongo hana makazi maalumu? Naomba anayejua vizuri please!!!!
 
Mkuu Invisible! Heri ya Mwaka mpya.

Kwanza nikupongeze kwa jitihada zako ktk kutumegea yaliyojiri kati ya Tanesco na Dowans. Mashaka yangu ni kwamba document uliyopost haijakamilika and in order for the one to make a proper and an informed argument should have gone through the whole document. Tafadhali kama hutojali weka part ''A'' na ''B'' ili kuweza kuisoma kwa ukamilifu wake na kutoa maoni.

Nawasilisha!!
 
Part II ipo mkuu invisible ameshawajibika kazi kwako mkuu.

Kaka nimeiona baada ya kurejea! Invisible big up to yourself.

Please confirm kwamba kuna page haziko (inasema page empty intentionally)

Mimi sio mwana sheria lakini kwa elimu yangu ndogo na usomaji wa mikataba hata ya kuuziana magari naona mkataba wa Tanesco/Dowans/RichMondul ulikuwa wa kifisadi na wanasheria waliousoma kabla ya kuasainiwa naamini walimalizia ujenzi wa vighorofa vyao maana siamini kama walitoka bila mikono yao kushika grisi (greasing of hands).

Kumbe Tanesco walishindwa mapema kwenye POA walosign. I bet this contract was drafted by RA accomplices because where on earth would one confine to a single justice executing organ as it is on (641) Settlement of Disputes 14.1 (e,f)

NO APPEAL WHATSOEVER, na jamaa wa ICC wamecopy na kupaste tu kwenye ruling yao (enclosure '2'). what a joke!

Naomba kujua kama mwekezaji naye aliorodhesha fascimile numbers manake doc yangu haionyeshi.

Nakubaliana na wenye mawazo kuwa hata hawa arbitrators watatu wana bei ambayo kina RA ni rahisi kufikia. Hebu soma kwenye Tribunal's Award (641 (4) Respondent kumlipa Claimants legal costs ..maneno yanasema ...One million Six hundred Ninety One thousand Four Hundred Thirty Six wakati tarakimu (US$ 1,708,521). Tribunal ilokula $750,000 haikuliona hili au mimi ndio sisomi vizuri jamani???

Hebu piga picha siku traffic police alipokukamata then ukamshikisha, ghafla gari lako linaonekana halina makosa na ghafla unakuita "mzee". Vitabu vya dini vinasema rushwa hupofusha macho meaning rushwa hukufanya usiwe makini tena.

Mie nabaki na wazo la kugoma kulipa tu maana mkataba umetubana sana kila kipengere. Otherwise kwa vile wenye Dowans wanajulikana na ni washikaji wa JK, basi JK awaombe kiungwana/kishkaji tu kwamba jamani mnaniharibia chonde chonde tulimalizeni hili pembeni. Asipofanya hivyo kila mtu ataamini kwamba na yeye yumo kwenye mgao pindi zikilipwa (kama hazijalipwa bado).

Just a quick one: Hivi wakilipwa mitambo watapeleka wapi au ndio litaundwa zengwe jingine tuinunue au watuuzie umeme kwa bei yao tena??
 
Kaka Invisible,

Asante sana kwa hii document manake nilikua naumiza kichwa ntaipataje ili niweze kuchukua hatua husika nikiwa kama mdau wa karibu wa sekta hii ya umeme.

Nimeiosoma hii Award kwa umakini mkubwa sana mno. Kwa wale wanaofahamu Arbitration hii inaitwa "Speaking Award" yaani Arbitration award ambayo inatoa na kuchambua sababu ya kufikia uamuzi (Award). Award kama hizi ni nzuri sana kwani inatoa nafasi kwa parties to the Award to take necessary actions against the award basing on the conclusion reached by the Arbitration Tribunal.

Mambo nilioyaona ndani ya hii Arbitration Award ni haya yafuatayo:

1. Kwanza suala la Mkataba POA: Ukisoma ile Arbitration Clause (Arbitration Agreement) kwa kweli imekaa vibaya sana mno haswa ukizingatia inasema kwamba the decision of the Arbitrators is final and conclusive and no party can appeal or annul (challenge) the decision of the Arbitrators. Yaani hapa ndio pigo kubwa lilipo. Kwa sasa Serikali imefungwa mikono yake kwa sababu hakuna njia ya kuweza kupinga Award hii.

2. Kiutaalam kuna njia chache za kuweza kufanya ili kupinga hukumu hii kwa mfano kutumia njia ya kuipinga mahakamani kwamba Award is against public policy, hata hivyo kwa kweli however much you do, bado hata ukienda mahakamani najua Dowans will stand firm kushikilia msimamo wa hio Arbitration Clause na hivyo uwezekano wa Tanesco kuchomoka ni mdogo na ni finyu sana mno mno...!

3. Suala la Void and Voidable contract. Inoanekana wazi kabisa kwamba Upande wa Serikali haukuweza kuipresent its self mahakamani au ilishindwa kuargue convincingly kuhusu hili suala kwa kweli.

4. Suala la Assignment Contract...! Naona Hapa Tanesco hawakuweza kulizungumzia ipasavyo haswa ukizingatia kwamba Richmond was a non existing company, so ilikua haina uwezo wa ku assign or transfer anything as a company since it was a fictitious company...!

Kwa kweli kwa uchambuzi huo haswa kwa kuangalia kifungu cha Arbitation clause sisi kama taifa kwa kweli hatuna njia ya kuweza kukwepa hukumu hii kwa kweli. Hata hivyo endapo Mwanasheria mkuu atakubali maoni ambayo tutampelekea kutakua na uwezekano wa kuweza kuipinga Award hii (Vacation of the Award) lakini bado nafasi itakua ni ndogo sana ya kushinda...!

Ukweli ndio huo, usishangae kuona Mwanasheria mkuu au Serikali imetulia kimya kwa sababu Mkataba uliosainiwa ulituingiza kichwa kichwa kwenye janga hili...!

Ushauri wangu:

Kuna haja ya Mwanasheria mkuu wa Tanesco kujiuzulu au kufukuzwa kazi kwa kweli kwa kukubali kuingia mkataba kama huu ambapo Tanesco haina uwezo wa kupinga au kukata rufaa dhidi ya hukumu inayotokana na mogogoro wowote uliopo kwenye mkataba...!
 
mbona watu wapo kimya tayari....??? au hii ishakuwa yesterdays news kama kawaida yetu wabongo??? Invisible naomba Part III ili tuendelee na debate
 
KULA TANO MKUU....

Na hili ndilo tatizo kubwa sana tulilonalo... yaani mijitu iko madarakani MIVIVU YA KUFIKIRI anakuja mtu average kama RA na akili kidogo tu.... anatugalagaza mpaka basi... trust me Tanzanians wenye asili ya Kiasia wametumia sana udhaifu huu na kufaidika sana sana....... halafu wakikutana na MIJITU MICHOYO ,MIBINAFSI kama Lowassa.....ndio basi tena.....

Hivi watu walifikiri JKN RIP alikuwa mjinga eeehh...........

Mkuu hata ukiwa mjinga kiasi gani, kama ukiwa na kisu kikali lazima utawahi kula nyama. RA ana visu vya kutosha na wala siyo kimoja. Bahati mabaya anaturushia sisi tumkatie nyama wakati akiendelea ku-sip wine yake... Jamaa anastahili Nobel Prize.


You are quite right Mkuu.......................unajua watu wanafikiri wanamfahamu RA vizuri.............kumbe hawafahamu kisawasawa.............kuna mtu alilia kuwa yeye ni BANGUSILO TU.................watu wanafikiri alikuwa mjinga ehh.............

Nadhani tuache kabisa kumwandama baba wa watu RA. The guy is my hero for the last decade. What else can I say?

Kaka Invisible,

Kuna haja ya Mwanasheria mkuu wa Tanesco kujiuzulu au kufukuzwa kazi kwa kweli kwa kukubali kuingia mkataba kama huu ambapo Tanesco haina uwezo wa kupinga au kukata rufaa dhidi ya hukumu inayotokana na mogogoro wowote uliopo kwenye mkataba...!

Huu ushauri utatekelezwaje wakati hata maazimio ya Bunge hayakufua dafu? Kama kuna uwezekano, ningeshauri TANESCO wakate rufaa huku wakijua watashindwa ili walau tusogeze muda karibia na 2015. Labda wakati huo tutakuwa tumeshapata akili ya kumpigia magoti RA ili atupe extendede period ya kulipa. Vinginevyo jamaa atataka kulipwa leo leo au kutuacha tumlimbikizie 7.5% interest pa!
 
Invisible tuwekee part III pia.

A quick one mzee: Part II ina page 10 tu au zaidi?? maana kuna page zimejifuta
 
Wakuu, hii kitu nimeshindwa kabisa kuifungua! au imeshatolewa?
any help will be appreciated!
 
nashukuru kwa doz hii , nakuomba utoe vipande vilivyobaki vinavyo wataja wamiliki ya Dowans
 
Wamesha ichakachua mkuu haikubali. Mungu wangu alicho sema doctor slaa ni kweli kabisaaa.
 
Wamesha ichakachua mkuu haikubali. Mungu wangu alicho sema doctor slaa ni kweli kabisaaa.

bado zipo nadhani sababu unatumia simu ila angalia post za nyuma kuna mtu alishauri jinsi ya kudownload kama unatumia simu
 
ukweli utajulikana siku kikwete atakapotoka madarakani
mimi naamini kabisa RA ni lefthand man wa kikwete, nina imani kabisa kwenye hizi hela kikwete ndio mfaidika mkubwa
 
nimeisoma niliyofanikiwa kuipakua -kifupi ngoma hii inataka watu wanaoweza kufikiri na kujipanga sawa sio werema, lazima werema achanje mbuga lakini subiri tutakupa valid arguements ambazo zinaenda kumfanya werema kujiuzulu kabisa bila hata kumshinikiza. Asante Mkuu
 
lakini mtu yoyote mwenye akili huwezi kwenda kwenye abitration ambayo mwisho wa siku haikupi chance ya ku-appeal . sema kwa sababu serikali kupitia hiyo tanesco walijipanga kushindwa ndio maana wakajipeleka kichwa kichwa na utetezi goi goi ili kufanikisha walicho kuwa wanata. nacho ni kuilipa dowans
 
Back
Top Bottom