DOWANS vs TANESCO - Why TANESCO Lost?

DOWANS vs TANESCO - Why TANESCO Lost?

OP uko vague sana kwenye swali lako na nini haswa unachotaka kutufahamisha hapa

Nimesoma lakini inaonekana kuwa doc iko incomplete. Sidhani kama kuna mtu anaweza akaja na proper legal arguments on this kwa document iliyokuwa posted na kama akija na hoja then atakuwa ana mislead wasomaji wa JF. If anything itakuwa ni ngumu hata mtu kuwa na bias (either way) kwa kuwa kilichopo hakijakamilika na kwa kuelewa types za watu wa humu ni kuwa out of 100 or so watakao download maybe ni watu 6 tu ndio watakao kuwa wameisoma the whole thing na kati ya hao maybe ni watu 4 au 3 ndio watakao kuja na proper legal arguments ambazo hazina bias na walio baki wote itakuwa yale yale ambayo tumezowea humu nayo ni:

a) CCM ni mbaya

b) JK hafai

c) DR SLAA is the right person

d) ROSTAM ashitakiwe


USHAURI:

Weka nondo nzima then watu (hatakama wachache ) waingie kazini kuja na arguments or counter arguments on this document

unataka na utangulizi pia? mbona hilo lajitosheleza?
 
DHSA
PORTEK ... name aslo noted in the story of the billion plus shiliings purchase of a house in London
CRDB
RDEVO
DOWANS Tanzania Ltd
PRO ENERGY

... and before...
EPA
BOT
MEREMETA
HERITAGE
BARRICK
RESOLUTE
CRDB
RADAR
GULF STREAM JET FOR PRES
THOSE GOLD ASSAYERS
IPTL
KAGODA!!!

...AND..

rA
eL
tUNITUNI
nJAAKAYA
vIJISENTI, vICENTI
.
.
et al

WAJAMENI KATULOGA NANI???
 
Hizi comments ni za mtu mwenye ubongo unaofanya kazi? Na cha kusikitisha ni kwamba hii listi ya watu wenye mawazo ya kifisadi kama huyu ni ndefu ... Wareboya, Kasheshe, Zitto, Uwiano maalumu....... Hawa wote wanamsifia Zitto. Kwa ushauri feki aliotoa wa kununua zile genereta. Wanataka kutuaminisha mwizi akikupora mali suluhisho lake ni kumbembeleza na kwenda kuinunua ili asikuibie tena.

Hongera kwa akili zako 100. Lipi bora kunegotiate na Mwizi au kumlipa mwizi.

Ni hivi, mwizi anakuibia, unamshtaki kwenye baraza la usuluhishi, anakushinda (kwa sababu hilo baraza la usuluhishi liko under control ya mwizi wako) halafu unatakiwa kulipa. .

Mhh... Tanzania lazima u-negotiate na mwizi wako kama ulifanya uzembe at first place. Nasema ni lazima.
Scenario: Umefanya uzembe ukapaki gari yako maeneo ya sinza usiku pasipo ulinzi ukaenda kulala, vibaka wakapitia powerwindows, windscreen, taa zote etc, jamaa yako akakuambia nenda pale "gerezani" kaviona vile vifaa. Hivyo vifaaa ukienda dukani utavipata kwa bei mara mbili ya bei utakayouziwa vile vyako pale gerezani. In this case unafanya nini, ni ku-negotiate na mwizi wako una nunua vifaa vile vile vyako kwa bei nafuu, unakaa kimya umhadithii mtu lakini next time hutafanya uzembe wa kupark gari pasipo ulinzi.

Ukisoma kwa makini hizi docs za invicible unagundua this country (tz) stinks!
 
Wizi ni wizi tuu, uwe wa kukwapua mkononi au kutumia ujanja wa mikataba na sheria. Wanaoshiriki yote hayo wanaitwa wezi, na kama wizi huo una athari kwa jamii nzima unaitwa uhujumu. Nchi kama China wahujumu adhabu yao ni kifo tuu. Hata kule Kariakoo wakwapuaji wanapata hukumu kama hiyo (ambayo siiungi mkono).

Sasa sisi kama taifa inakuwaje? Mbona wezi katika hili tunawafahamu na badala ya kuwaadhibu sie tunapoteza muda kujibishana tuu? tena tunafanya kufuru mbaya kwa baadhi yao kuwaingiza kwenye jengo lile eti wawe watunga sheria? Wakipita tunainamisha vichwa na kusema "Habari Mheshimiwa!"

Huu uzoba utatuisha lini sie? Tunahitaji mwenda wazimu mmoja tuu, alianzishe ili kieleweke.
 
Ni nani wa kuwashtaki wezi/mafisadi kama JK ameshawakingia kifua?

Mfumo mzima wa kisheria uko ICU, na hii inatokana na kuwa na rais mfalme asiyeambilika, maana kashfa zote kubwa duniani huwa zinahusisha watu walio karibu na ikulu, na kwa rais mwenye absolute powers kama wa kwetu ni ngumu kuwabana wahusika!

Kimsingi ili tuweze kuwabana wezi lazima mamlaka na madaraka ya rais yapunguzwe hasa kumzuia kuweka kinga kwa wahalifu, kumpunguzia watu wa kuwateua nk! Pia baraza la mawaziri litenganishwe na bunge, pia mtu yeyote mwenye kashfa awekewe kizingiti cha kugombea uongozi mpaka asafishwe na vyombo vya kisheria!

Haya kwa sasa na mengine mengi hayawezekani mpaka iandikwe KATIBA MPYA ITOKANAYO NA WANANCHI NA SIYO ITOKANAYO NA SERIKALI!
 
Nilichojifunza kwa kusoma kurasa za hii document ya dowans,watu wako smart sana kwenye namna wanavyoibia nchi hii.

A smart move from the very beginning from people we consider stupid.

JK si mjinga,anajua anachofanya na anachotumiwa kukifanya kwa maslahi yake na waliomweka hapo.
 
hii kesi tumpe mr. sitta na wenzake wakate rufaa. walikuwa wanashinda kwenye tv wakisema tuvunje mkataba.

gafla wamepotea. wanasiasa wetu walisikiliza hoja za akina mwanakijiji. kampuni ya briefcase tuvunje mkataba. tunasahau sheria ni taaluma inayosomewa darasani na sio kwenye google.
 
Nilichojifunza kwa kusoma kurasa za hii document ya dowans,watu wako smart sana kwenye namna wanavyoibia nchi hii.

A smart move from the very beginning from people we consider stupid.

JK si mjinga,anajua anachofanya na anachotumiwa kukifanya kwa maslahi yake na waliomweka hapo.
I concur with u
 
legally basing the argument put forward by TANESCO I think the award reflect the proper position of the matter. It is my considered view that TANESCO advanced a weak arguments against the case by DOWANS. I will come back later with a more analysis of the award.
 
Hivi kweli mnaamini Wanasheria wa Tanzania walioshiriki kupelekwa huko ICC na kukubali mapema kuwepo vipengele hivyo vya arbitration wakati Tanzania yenyewe inayo Mahakama ya Biashara na utaratibu wa kutatua migogoro ya kibiashara walifanya hivyo kwa sababu hawajui au hawana uwezo?

Mkuu wameenda huko nadhani kwasababu ya urahisi ila ndio at the expense ya kutojiandaa vizuri na matokeo ndio haya. Na tukichelewa kulilipa deni litakuwa maana kuna interest pale kama umeisoma vizuri.
 
patriotism nchi hii hamna kabisa! nalia na wanasheria waliotuletea hili janga najua njaa tu ndo zinawasumbua na ubinafsi
 
Asante sana Mkuu Mdondoaji kwa ufafanuzi zaidi..................Naomba maoni/mtizamo y/wako kuhusu the argument ya kununua ile Mitambo ya DOWANS

Unajua Ogah,

Hii kitu hatuna jinsi tumejikoroga wenyewe na kusema ukweli wanasheria wa Tanesco na management ya Tanesco needs to go. Kwasababu wameshindwa kuishauri serikali vizuri.

Kuhusu mitambo kulikuwa na loophole pale Dowans walipotaka kutuuzia mitambo yao (sijui kama sasa wanaweza kutuuzia hiyo mitambo hasa baada ya wao kupata christmas present ya bilioni 185 sidhani kama tuko katika position nzuri ya kunegotiate nao kuhusu hilo).

Ninachokiona mie ni kufungua kesi nyengine ya udanganyifu kwa Dowans which I am sure Tanzania wanaweza kushinda kwa information zilizopo hapa JF na hiyo ikatumika kama bargaining power kwa Tanesco kutaka shauri nje ya mahakama.

Wakikubali shauri nje ya mahakama then deni la Tanesco linaweza kupungua kutegemea na Serikali ilidai kiasi gani kule katika kesi ya udanganyifu. Kwasasa mkuu kununua hiyo mitambo is not a wise option maana serikali yetu haina bargaining power ya kunegotiate a better deal.
 
najaribu kuisoma lakini kunaelekea some pages missing hasa pages za mwanzo. can we have a complete set.
 
Hili suala ninalifanyia kazi na nitalibandika humu jamvini kwa kushauriana zaidi................................
 
Hili suala ninalifanyia kazi na nitalibandika humu jamvini kwa kushauriana zaidi................................

Ndugu, lets take action...! We need to do so...! Le me know your strategy and see how we can unite and team up...! Walau tuwaonyeshe watu kwamba we are tired of this kind of shit...!
 
Back
Top Bottom