Kiranja,
Mitambo ya Dowans inaweza kuzalisha megawatt 100, hivyo fuatilia kama kununua mitambo ya kuzalisha umeme wenye megawatt hizo unagharimu pesa nyingi kiasi hicho.
Unajua mkuu hawa wanasiasa wanataka kutuchezea akili zetu wakati sisi wengine hapa biahsra ndio zinatuweka duniani..
Swala lka kufikiria gharama hadi kesho nitalipinga sana na sababu nitazitoa kutoka mfano mdogo wa biashara zetu za nyumbani..
Mathlan mtu unakodisha bus (lease) la Scandinavia kufanya biashara ya safari za kwenda Mbeya..
1. Tatizo linalojitokeza ni ubovu wa mkataba wa awali, kwanza unagundua kuwa bus hilo hata hao Scandinavia wamelikodisha hviyo hawana gharama zaidi ya kucheza mchezo ya kati, mchezo ambao unakuigharimu ulipe shilingi 80 kwa kila 100 unayotengeneza...
Hivyo unapoamua kuvunja mkataba huo ni ujinga kufikiria kununua bus la Scandinavia kwani utakuwa unalipia gharama zao + interest...na pili ni lazima wataweka chochote mbali na kwamba umewaponyesha kurudisha deni lao..+ interest ya kila mwezi au mwaka ambayo wamekubaliana na financer (mtoa mkopo)..
Kwa mfanya biashara yeyote atafahamu kwamba huhitaji middleman ikiwa unaweza ku lease bus wewe moja kwa moja kutokana na sababu zilizotangulia., In this case nitarudi kwa ktk utata wa Richmond deal..
2. Tatizo jingine sio ukubwa wa bus kuweza kuchukua abiria 50 isipokuwa ni hali ya bus lenyewe!.. huwezi kuacha kununua bus jipya kwa kigezo kuwa hili bus linachukua abiria 50 kisha ukatazama gharama yake wakati kuna ma bus yanayoweza chukua abiria chini au zaidi ya hizo 50..kwa hiyo kigezo cha uwezo na gharama ya bus sio chanzo kinachoweza kutumika kama sababu..
Unataka kununua hilo bus kwa sababu nje kabisa ya uwezo na gharama kwani ni ujinga kufikiria gharama au kupoteza asilimia 80 ya pato la awali kwa Scandinavia ikiwa pato hilo linaweza patikana pia ukinunua bus jipya ambalo vipengele vyake kuhusiana na interest, guarantee, maintanance, spareparts (vipuli) vyote utavipata under Your name badala ya mafundi wa kubabaisha wa Scandinavia..
3. Kama kuna sababu ya kunyang'anywa bus tusiponunua, hii wazi inatokana na kuchachamaa kwa Scandinavia sio uwezo wa mnunuzi!.hii ndio point yangu, ina maana tu Scandinavia wanataka ununue bus lao kutokana na mkataba wa awali hasa pale kisheria unaposhindwa kumsimamisha ndugu yako aliweka sahihi mahakamani kama mkosa!..Kama msahihi hana makosa kisheria iweje mkataba wa Richmond au Dorwans uwe na makosa ya kughushi!
Wakuu hapa hakuna hadithi, Lowassa na Karamagi walituingiza mkenge, na sababu kubwa ya kutowasimamisha hawa watu mahakamani wakaonekana kuwa na makosa ndicho kinachoweza kutumika na Dorwans kuwa mkataba wao ni halali na sasa hivi tunataka kujificha nyuma ya madhambi yetu wenyewe..
Kama Dorwans wamefikisha kesi hii ktk mahakama za kimataifa, kilichotakiwa sisi kufanya ni kuwaweka Lowassa, Rostam, na Karamagi hatiani kisha ushahidi huo ukatumika kuvunja mkataba wa Richmond.
Sisi tumechukua sheria mkononi kuvunja mkataba, tunametaka kuwapiga bao Dorwans bila kutumia vyombo vya sheria kutengua mkataba kwa sababu ya kinga kwa baadhi viongozi wetu, well ndio malipo yake haya!..
Sasa wasije na hadithi za SIASA kutufungia kanya boya hapa..maamuzi mabaya yametokana na siasa nyingi ktk utekelezaji...