Double Standard Kuhusu Kauli ya "Zanzibar Sio Nchi!"

Double Standard Kuhusu Kauli ya "Zanzibar Sio Nchi!"

Mkuu inawezekana na mimi nina mapungufu yangu lakini sidhani kama ni vibaya kusema kile ninachoamini! Tushindane kwa hoja sio ku-attack personalities!
Nimeona sasa hivi mmeshaanza kugeuza mjadala na kunijadili mimi badala ya hoja iliyoko mezani! Jadili hoja yangu zaidi ili tusaidia kujenga nchi yetu! Who knows? Unaweza kunishawishi nikabadili mawazo niliyo nayo na kuwa na mtizamo mpya, na ndio maana tuko hapa Jukwaani!
Na huo "undumila kuwili wa Watanganyika" unaousema ndio upi? Unasema hivyo kwa ajili ya "ku-balance equation" au namna gani? Mbona hutoi detail? Au ndo juhudi za ku-divert mada?

Tukianzia kwa wakati wa Utawala wa Abeid Karume hamkuwahi kumuuliza namna gani aliiendesha nchi yake ambayo mnadai kuwa si nchi wakati ikitawaliwa na mwenye nchi atakavyo.
Tatizo lenu wengi mliomo humu hamuujuwi muungano ulivyokuwa huko nyuma. Huko nyuma Mtanganyika akijijuwa Mtanzania tu bila ya kujuwa kuwa neno Tanzania limetokana na muungano na ndio maana wengi wenu mnashindwa kutofautisha uwepo wa mataifa haya mawili, Tanganyika na Zanzibar
Undumila kuwili wa Watanganyika unajionyesha pia katika wakati wa chama kushika hatamu, hamkuwahi hata siku moja kuuliza wala kudai kuwa mnanyimwa haki Zanzibar kwa vile Nyerere aliwafadhili wahafidhina wa Zanzibar chini ya CCM. Ni wakati huu ambao SMZ iliunda vikosi mbali mbali vya ulinzi chini ya Rais wa Zanzibar. Undumila kuwiliwa Watanganyika ulionekana mlipoungana na serikali ya SMZ kwenye mauwaji ya Zanzibar kwa kupeleka vikosi na viongozi wa Tanganyika kupongeza mauwaji hayo ambapo harakati zilipobadilika sasa mnalaani vitendo kama hivyo. Sijui unataka undumilakuwili gani zaidi ufahamishwe?
 
CHAMVIGA

Kitu gani kilichonyonywa huko Zanzibar? Wana madini au yale "mafuta ya kujipaka?"

Hivi wewe ndie huyu huyu Buchanan tunaembiwa ati ndo mmojawapo ya Mods humu-JF!?

Sasa mbona unataka kuharibu hali ya afia ya huu mjadala uliouanzisha wewe mwenyewe!?

Jaribu kujifunza lugha za staha/kitaaluma japo kiduchu...punguza chuki na tashtit kwa Wazanzibary!

Najua si kosa lako,maana ndivyo mlivyokaririshwa kwa myka mingi mno,na mangi mno hamuyajui na wala hamutaki kuyasikia!

Nitakurejea pindi nikapata fursa japo kiduchu!

Ahsanta sana.
 
Mtakuja kutukumbuka tuliokuwa na msimamo wa serikali moja.It's a simple philosophy kwamba nyumba moja haiwezi kuwa na baba zaidi ya mmoja.Hapatakalika.Kila mmoja atataka kulea watoto anavyojua yeye,hawa watoto watakua kwa malezi tofauti,ukubwani hawataweza kukaa nyumba moja.Baba ni serikali,watoto ni wananchi.
 
Mtakuja kutukumbuka tuliokuwa na msimamo wa serikali moja.It's a simple philosophy kwamba nyumba moja haiwezi kuwa na baba zaidi ya mmoja.Hapatakalika.Kila mmoja atataka kulea watoto anavyojua yeye,hawa watoto watakua kwa malezi tofauti,ukubwani hawataweza kukaa nyumba moja.Baba ni serikali,watoto ni wananchi.
Kwani nyie Watanga-Nyikwa ndo si ndio kinamama/Dada zetu myaka yoote ya huu Muungano,au hamulijui hili!?Au hamuitaki "hadhi"hiyo siku hizi!?

Ahsanta
 
Mie sidhani kama CCM wanaogopa fear of the unknown kukubali serikali 3.Mie nadhani wanaogopa "fear of the known".Nadhani wanajua the real motive behind uzanzibari.Kwamba huenda ikawa ndio tayari muungano umevunjika hapo.Chonde tu yasije yakatokea ya Jerusalem na Palestina,mkaja kuidai Dar na Mombasa baadae manake hata kule Mombasa kuna harakati za kutaka kuitenga Mombasa from Kenya!haya mambo ukiyatazama juu juu unaona ni rahisi,lakini ndani ni mazito!msishangae watu kuja kudai Zenj empire ya Sultan huko mbele.
 
Tabia ya kuwadharau na kuwakejeli wazanzibar itaishia lini? Kwanini ndgu zangu watanganyika hatuachi dharau hizi tulizoachiwa na Nyerere?
 
Kwani nyie Watanga-Nyikwa ndo si ndio kinamama/Dada zetu myaka yoote ya huu Muungano,au hamulijui hili!?Au hamuitaki "hadhi"hiyo siku hizi!?

Ahsanta

kuwa dada yake mtu haimaanishi huyo mtu ni lazima awe mwanaume.Unaweza kuwa dada au mama wa mwanamke mwingine,ahsanta!
 
Sioni wa kulitatua kwasababu waliolianzisha hili tatizo hawapo na bahati mbaya wanaotakiwa kulitatua hawako tayari kwasababu kwanza wanaangalia maslahi yao ya kisiasa zaidi hasa uchaguzi wa mwaka 2015 badala ya kuangalia suala la muungano katika maono ya muda mrefu hasa ukitilia maanani EAF.
Nakubaliana nawe kwa kiasi fulani. Bahati mbaya mitazamo na misimamo ya wajumbe wa Bunge la Katiba inatia shaka ikiwa kweli watakuweza kuleta mwafaka wa kitaifa kwenye suala hili. Kila mmoja anatafasiri uzalendo kwa mtazamo wake. Wale wenye msimamo wa CCM wana tafasiri uzalendo kwa kuunga Serikali mbili. Walio kinyume nao wana tafasiri uzalendo kwa kuunga Serikali tatu! Sijui mwafaka utapatikanaje. Nafikiri mchakato huu wa Katiba unaweza kutuacha na maker aha zaidi.
 
wao wanasema kila siku bara imewabana hawapumui vizuri, wanadanganywa sana na waarabu pasipo wao kujijua

Muungano ukivunjika kama mnavyotaka mnafikiri mtabaki Tanganyika? Anzeni kufanya land reclamation sasa hivi ili eneo liwatoshe huko baadaye! Just an advice!
 
Nafikiri unapaswa kubeba lawama za hayo matusi ya nguoni kwa Wazanzibary!

Khalaf mnataraji sisi wenye akili zetu timamu tujechangia hapa ili muzidi kutukashif,sio!? Daah!

Ahsanta

Sistahili kubeba lawama yoyote kwa niaba ya mtu mwingine!
 
Tabia ya kuwadharau na kuwakejeli wazanzibar itaishia lini? Kwanini ndgu zangu watanganyika hatuachi dharau hizi tulizoachiwa na Nyerere?

Mkuu una taarifa kuwa kuna watu wanaitwa "machogo" huko Zanzibar? Tuseme hizo ni dharau walizoachiwa na Karume? Usimwingize mzee wa watu kwenye vitu visivyomhusu, plse!
 
Mie sidhani kama CCM wanaogopa fear of the unknown kukubali serikali 3.Mie nadhani wanaogopa "fear of the known".Nadhani wanajua the real motive behind uzanzibari.Kwamba huenda ikawa ndio tayari muungano umevunjika hapo.Chonde tu yasije yakatokea ya Jerusalem na Palestina,mkaja kuidai Dar na Mombasa baadae manake hata kule Mombasa kuna harakati za kutaka kuitenga Mombasa from Kenya!haya mambo ukiyatazama juu juu unaona ni rahisi,lakini ndani ni mazito!msishangae watu kuja kudai Zenj empire ya Sultan huko mbele.

Ndio tunakoelekea huko nadhani!
 
Context ni ile ile mkuu, PM alipozungumza "Zanzibar sio nchi" aliweka suala la uhaini pembeni? Tunapozungumzia nchi tunajumuisha mambo yote na sio kumega vitu kidogo kidogo!

Sasa kama "kiuhaini" Zanzibar sio nchi, itakuwa nchi kwa jambo lipi? "Nchi" ikikosa sifa moja zingine zinaweza kusimama?

Ni sasa na pombe ikitolewa alcohol haibaki tena kuwa pombe!

Tuki-assume kuwa Zanzibar ni nchi kama unavyolazimisha wewe kwa nini mnataka "kurudishiwa nchi" yenu wakati kumbe mnayo? Mbona Kenya, Uganda, nk hawalii "kurudishiwa" nchi zao, japokuwa wako kwenye EAC?

Nionavyo mimi ni double standard, tena kauli hiyo ingewafanya mkasirike sana kwa kuwa ilimshusha hadhi Rais wenu na kumfanya kuwa hana tofauti na Mkuu wa Mkoa ambaye hawezi kupinduliwa! Afadhali tu Pinda alidai kuwa Zanzibar Sio Nchi tu basi kuliko yule aliyegusa hata Kiongozi wa nchi!

Wazanzibari wanaposema wanataka nchi yao wanamaana kuwa kwa sasa wanatawaliwa na mkoloni mweusi aliyejivisha joho la muungano.

Muungano wa EAC na Tanzania ni vitu viwili tofauti, Zanzibar chini ya Karume ilikasimisha mamlaka yote kisheria kwa Tanganyika ndio maana leo hii tuko hapa tulipo.

Kizazi hiki tulichonacho ndicho kitakachoamua hatma ya muungano. Kama mamlaka ya Zanzibar hayatakuja kwa njia ya katiba mpya basi tusubiri lazima mabadiliko yatatokea kwa njia nyingine.

Siku moja itakuwa kweli.... by Nabwa

Tanzania ni muungano wa nchi mbili huru, Tanganyika na Zanzibar.
 
Hivi wewe ndie huyu huyu Buchanan tunaembiwa ati ndo mmojawapo ya Mods humu-JF!?

Sasa mbona unataka kuharibu hali ya afia ya huu mjadala uliouanzisha wewe mwenyewe!?

Jaribu kujifunza lugha za staha/kitaaluma japo kiduchu...punguza chuki na tashtit kwa Wazanzibary!

Najua si kosa lako,maana ndivyo mlivyokaririshwa kwa myka mingi mno,na mangi mno hamuyajui na wala hamutaki kuyasikia!

Nitakurejea pindi nikapata fursa japo kiduchu!

Ahsanta sana.

Sijaona cha ajabu hapa, maana wenyewe walidai kuwa mafuta hata kama yapo kidogo watajipaka! Kwa hiyo sijasema kipya hata kidogo!

Na hayo mengi unayodai sijui ndo yapi tusiyoyaju? Hebu yataje uone kama hatuyajui!
 
Wakuu,

Si mara ya kwanza kwa Pinda kutamka kuwa "Zanzibar Sio Nchi" halafu kukazua mtafaruku mkubwa sana hadi tukaona purukushani za kubadili Katiba ya Zanzibar, 1984 ili ku-create "nchi" iitwayo "Zanzibar!"

Ni siku za nyuma tuliona aliyekuwa Jaji Mkuu, Augustino Ramadhan, pamoja na Majaji wengine wakitamka katika Hukumu ya Mahakama ya Rufani-Kesi ya Uhaini (Machano Hamis and others vs R case) kuwa "Zanzibar Sio Nchi" na kwamba "Uhaini hauwezi kufanywa dhidi ya Rais wa Zanzibar" kwa kuwa "Zanzibar Sio Nchi!" Hukumu hiyo haikuleta hasira yoyote kwa Wazanzibari lakini aliponyanyua mdomo "Mtoto wa Mkulima" kukawa na mzozo mkubwa sana ambao kila mmojawetu anaujua!

Swali ni kwamba kwa nini Wazanzibari hawakukasirishwa na kauli ya Jaji Mstaafu Agustino Ramadhan wakaja kukasirishwa na kauli ile ile lakini ikasemwa na Pinda? Why double standard? Au ni chuki tu kwa watu wa bara/ Tanganyika? Juzi tena Pinda "kazungumzia kuwa wanaotaka Tanganyika waeleze ni Tanganyika ipi waitakayo!"

Hili nalo limeleta "hasira" kwa Wazanzibari hapa JF utafikiri alikuwa anazungumzia kuhusu "nchi" yao! Hawa watu huwa siwaelewi kabisa! Ila wakipewa vyeo huku Bara kwenye Wizara ambazo si za Muungano wako kimya kama wamemwagiwa maji ya baridi! Lakini utasikia eti "Waziri Mkuu Pinda mwisho wake ni kisiwa cha Chumbe!" Hatusikii wakisema Makamu wao wa Kwanza wa Rais ambaye hata Katiba ya JMT, 1977 haimtambui mwisho wake wapi!

Wao wenyewe wame-acquire ardhi na kuishi Tanzania Bara bila bughudha yoyote! Hao ndo Wazanzibari bwana!!!
inategemea tendo lilitendeka kabla ya mabadiliko ya katiba 2010? ambayo ndio Warioba anadai inaifanya Zanjibari kuwa Nchi
 
Rohoni hawautaki muungano ila kwa sababu ya mafao wanayopata humo wanaogopa kujiondoa. So, wakifika mahali pa kumdhuru mtu mmoja wanasema huyo ni Mzanzibari, wakifika mahali pa kuwajibishwa kwa ujumla wanakataa kuwa sio Wazanzibari. Nadhani mtanielewa tu.
 
nyerere aliamua kutanua mipaka bila kutumia nguvu, wazungu wanasema kuconquer, alitumia saikolojia ya kuita muungano, tangu lin mto na bahar ikaungana? ikiungana hyo bahar cyo mto tena ni bahar hyo, zanzibar ni kama mikoa mengine tu, kamwe aina sauti katika Tanzania
 
"Zanzibar is NOT a Sovereign State" maana yake ni nini? Juzi juzi nimemsikia Jaji Mstaafu akirudia kauli yake kuwa "Zanzibar Sio Nchi" na akadai kuwa wa kulaumiwa hakuwa PM Pinda bali ni yeye mwenyewe Jaji Ramadhan kwa kutangulia kusema kuwa "Zanzibar Sio Nchi" na si PM Pinda!


Je unajua maana ya Sovereign State kwa kiswahili?

Je hiyo Sovereign State ni Doula ay Nchi?

Lakin suala langu lipo pale pale TOFAUTI YA NCHI NA DOLA NI NINI?

 
Back
Top Bottom