Buchanan
JF-Expert Member
- May 19, 2009
- 13,192
- 1,976
Wakuu,
Si mara ya kwanza kwa Pinda kutamka kuwa "Zanzibar Sio Nchi" halafu kukazua mtafaruku mkubwa sana hadi tukaona purukushani za kubadili Katiba ya Zanzibar, 1984 ili ku-create "nchi" iitwayo "Zanzibar!"
Ni siku za nyuma tuliona aliyekuwa Jaji Mkuu, Augustino Ramadhan, pamoja na Majaji wengine wakitamka katika Hukumu ya Mahakama ya Rufani-Kesi ya Uhaini (Machano Hamis and others vs R case) kuwa "Zanzibar Sio Nchi" na kwamba "Uhaini hauwezi kufanywa dhidi ya Rais wa Zanzibar" kwa kuwa "Zanzibar Sio Nchi!" Hukumu hiyo haikuleta hasira yoyote kwa Wazanzibari lakini aliponyanyua mdomo "Mtoto wa Mkulima" kukawa na mzozo mkubwa sana ambao kila mmojawetu anaujua!
Swali ni kwamba kwa nini Wazanzibari hawakukasirishwa na kauli ya Jaji Mstaafu Agustino Ramadhan wakaja kukasirishwa na kauli ile ile lakini ikasemwa na Pinda? Why double standard? Au ni chuki tu kwa watu wa bara/ Tanganyika? Juzi tena Pinda "kazungumzia kuwa wanaotaka Tanganyika waeleze ni Tanganyika ipi waitakayo!"
Hili nalo limeleta "hasira" kwa Wazanzibari hapa JF utafikiri alikuwa anazungumzia kuhusu "nchi" yao! Hawa watu huwa siwaelewi kabisa! Ila wakipewa vyeo huku Bara kwenye Wizara ambazo si za Muungano wako kimya kama wamemwagiwa maji ya baridi! Lakini utasikia eti "Waziri Mkuu Pinda mwisho wake ni kisiwa cha Chumbe!" Hatusikii wakisema Makamu wao wa Kwanza wa Rais ambaye hata Katiba ya JMT, 1977 haimtambui mwisho wake wapi!
Wao wenyewe wame-acquire ardhi na kuishi Tanzania Bara bila bughudha yoyote! Hao ndo Wazanzibari bwana!!!
====================================
ADDITIONAL
====================================
Hivi ndivyo alivyosema Jaji AGUSTINO RAMADHANI, pamoja na Majaji wenzake katika Kesi ya SMZ v. Machano Hamisi and 18 others:
"After the above exposition, we have no difficulty at all to answer that question in the negative. The International Persons called Tanganyika and Zanzibar ceased to exist as from 26[SUP]th[/SUP] April, 1964 because of the Articles of Union. The two states merged to form a new international person called the United Republic of Tanzania.
The Rt. Hon. The Earl of Birkenhead has said at page 36: "A nation cannot indefinitely surrender the treaty-making power to another, and at the same time retain its existence as a sovereign state". We concur with this contention and we wish to point out that both Tanganyika and Zanzibar, and not Zanzibar alone, surrendered their treaty-making powers to the United Republic of Tanzania.
Thus, Zanzibar, just like its sister Tanganyika, is neither a state nor is it sovereign. The state and the sovereign is the United Republic of Tanzania."
Si mara ya kwanza kwa Pinda kutamka kuwa "Zanzibar Sio Nchi" halafu kukazua mtafaruku mkubwa sana hadi tukaona purukushani za kubadili Katiba ya Zanzibar, 1984 ili ku-create "nchi" iitwayo "Zanzibar!"
Ni siku za nyuma tuliona aliyekuwa Jaji Mkuu, Augustino Ramadhan, pamoja na Majaji wengine wakitamka katika Hukumu ya Mahakama ya Rufani-Kesi ya Uhaini (Machano Hamis and others vs R case) kuwa "Zanzibar Sio Nchi" na kwamba "Uhaini hauwezi kufanywa dhidi ya Rais wa Zanzibar" kwa kuwa "Zanzibar Sio Nchi!" Hukumu hiyo haikuleta hasira yoyote kwa Wazanzibari lakini aliponyanyua mdomo "Mtoto wa Mkulima" kukawa na mzozo mkubwa sana ambao kila mmojawetu anaujua!
Swali ni kwamba kwa nini Wazanzibari hawakukasirishwa na kauli ya Jaji Mstaafu Agustino Ramadhan wakaja kukasirishwa na kauli ile ile lakini ikasemwa na Pinda? Why double standard? Au ni chuki tu kwa watu wa bara/ Tanganyika? Juzi tena Pinda "kazungumzia kuwa wanaotaka Tanganyika waeleze ni Tanganyika ipi waitakayo!"
Hili nalo limeleta "hasira" kwa Wazanzibari hapa JF utafikiri alikuwa anazungumzia kuhusu "nchi" yao! Hawa watu huwa siwaelewi kabisa! Ila wakipewa vyeo huku Bara kwenye Wizara ambazo si za Muungano wako kimya kama wamemwagiwa maji ya baridi! Lakini utasikia eti "Waziri Mkuu Pinda mwisho wake ni kisiwa cha Chumbe!" Hatusikii wakisema Makamu wao wa Kwanza wa Rais ambaye hata Katiba ya JMT, 1977 haimtambui mwisho wake wapi!
Wao wenyewe wame-acquire ardhi na kuishi Tanzania Bara bila bughudha yoyote! Hao ndo Wazanzibari bwana!!!
====================================
ADDITIONAL
====================================
Hivi ndivyo alivyosema Jaji AGUSTINO RAMADHANI, pamoja na Majaji wenzake katika Kesi ya SMZ v. Machano Hamisi and 18 others:
"After the above exposition, we have no difficulty at all to answer that question in the negative. The International Persons called Tanganyika and Zanzibar ceased to exist as from 26[SUP]th[/SUP] April, 1964 because of the Articles of Union. The two states merged to form a new international person called the United Republic of Tanzania.
The Rt. Hon. The Earl of Birkenhead has said at page 36: "A nation cannot indefinitely surrender the treaty-making power to another, and at the same time retain its existence as a sovereign state". We concur with this contention and we wish to point out that both Tanganyika and Zanzibar, and not Zanzibar alone, surrendered their treaty-making powers to the United Republic of Tanzania.
Thus, Zanzibar, just like its sister Tanganyika, is neither a state nor is it sovereign. The state and the sovereign is the United Republic of Tanzania."