Double Standard Kuhusu Kauli ya "Zanzibar Sio Nchi!"

Double Standard Kuhusu Kauli ya "Zanzibar Sio Nchi!"

Punguza jazba na chuki za kuwazushia mambo wa Znz.

Zanzibar hawahitaji Serikali 2 au 3 au hata 10. Kinachotakiwa ni kuwa na Znz huru kwa maana nchi yenye mamlaka kamili. Kama Znz itaweza kuyapata haya katika Serikali Moja au Mbili au Tatu au hata 7 hiyo sio Tatizo.

Jaribu kuwasoma nini wa Znz wanachotaka na sio kuendeshwa na hisia na chuki dhidi yao.

Lakin japo ni Mod naweza kukuuliza suala hapa. JE UNAJUA TOFAUTI ZA DOLA NA NCHI?

Naomba jibu lako ili tukupe mwanga kama upo kizani.

He wont give you an aswer

He is so weak
 
Undumilakuwili kama unaouonyesha wewe wa kuwaita wenzako wazanzibar double standard wakati nawe ni walewale.
Undumilakuwili wa watanganyika ni kuwa ng'ang'ania wazanzibar waliojipambanua wazi hawataki muungano. Unataka detail ya wanaong'ang'ania muungano au detail gani mkuu!?

Hakuna anayeng'ang'ania muungano bana....Muungano kwetu sio tatizo. Naomba jibu swali moja tu; KUNA WAZANZIBARA NA WAZANZIBARI, WE UKO UPANDE GANI?
 
kesi ile ya uhaini ilikuwa inawahusu wazanzibari wenyewe na jaji alikuwa mzanzibari, sasa mtanganyika akisema zanzibar sio nchi wanakuja juu kwa sababu hawautaki muungano, mimi kwa maoni yangu tuvunje muungano maana kuna baadhi wanatuita sisi watanganyika kuwa ni wakoloni weusi na wao wazanzibari ni watumwa wetu jambo ambalo halina ukweli wowote, hivi tukivunja muungano kuna hasara gani?.
 
Mkuu wangu wazanzibar tumewalea,tumewabeba,tumewavumilia kwa vituko vingi imefika wakati watanganyika wameanza kuhoji huu muungano ni agizo la Mungu au ni binadamu wawili walikaa wakakubaliana wengine hawawezi kurekebisha chochote sawa na misahafu ?.

Ukweli ni kwamba Zanzibar si nchi hilo halina ubishi tatizo liko kwa mkuu wa nchi kakimbilia magogoni lakini ameshindwa kusimamia katiba aliyoapa kulinda.Rais Kikwete wakati waziri mkuu anaandamwa na wabunge wa Zanzibar alitakiwa kusimama na kuipa nguvu hoja ya waziri wake mkuu.

Mabadiliko yaliyofanywa na baraza la wawakilishi yalikuwa yakivunja katiba ya JMT badala ya amiri jeshi mkuu kuchukua hatua za haraka za kukemea na kuhakikisha mabadiliko hayo yanakuwa batili alibaki akicheka cheka kana kwamba hakuna jambo baya limetendeka.

Wapo wanasheria makini akina Tindu Lissu walipaza sauti lakini serekali badala ya kujibu hoja ikawa inafanya juhudi za kufunika funika.

Kwa nini Wazenj wana "Double Standard," linapokuja suala la "Zanzibar Sio Nchi?"
 
He wont give you an aswer

He is so weak

Nataka nimdarsishe kidogo hapo kwani Hata Mahakama katika kesi hiyo haijatamka kuwa Znz sio nchi bali walisema Znz sio Doula.

Nafikiri anajichanganya na kukurupuka mwenyewe katika maneno hayo na ukiongezea na chuki na hisia zake ndio zinampeleka pabaya.

Tuvute subra kusubiri jibu lake.

 
Wazanzibari ni vipanga kuliko watanganyika. Kwa kutumia mbinu ya kulalamika na kukosoa muungano wa sasa wameweza kututawala na kunufaika na muungano kuliko watanganyika. Wao wanaweza kuongoza wizara za Tanganyika, wanamiliki ardhi na biashara huku Tannganyika lakini bado wanalaumu muungano. CHETU CHA WOTE CHAO CHA KWAO PEKE YAO.

Hii mbinu imewasaidia sana mkuu.Na kwa hali ilivyo,sidhani kama kuna familia Zanzibar haifaidi moja kwa moja mapato ya serikali!Maana hatua chache tu unakuta yupo mbunge wa JMT,ama mwakilishi,ama balozi,waziri,naibu waziri,katibu mkuu nk!Katika jumuia yenye uwiano mzuri wa viongozi wanaolipwa kifisadi kila siku,lazima wananchi wake watafaidika zaidi kuliko ilivyo huku bara.

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Mkuu wangu wazanzibar tumewalea,tumewabeba,tumewavumilia kwa vituko vingi imefika wakati watanganyika wameanza kuhoji huu muungano ni agizo la Mungu au ni binadamu wawili walikaa wakakubaliana wengine hawawezi kurekebisha chochote sawa na misahafu ?.

Ukweli ni kwamba Zanzibar si nchi hilo halina ubishi tatizo liko kwa mkuu wa nchi kakimbilia magogoni lakini ameshindwa kusimamia katiba aliyoapa kulinda.Rais Kikwete wakati waziri mkuu anaandamwa na wabunge wa Zanzibar alitakiwa kusimama na kuipa nguvu hoja ya waziri wake mkuu.Mabadiliko yaliyofanywa na baraza la wawakilishi yalikuwa yakivunja katiba ya JMT badala ya amiri jeshi mkuu kuchukua hatua za haraka za kukemea na kuhakikisha mabadiliko hayo yanakuwa batili alibaki akicheka cheka kana kwamba hakuna jambo baya limetendeka.Wapo wanasheria makini akina Tindu Lissu walipaza sauti lakini serekali badala ya kujibu hoja ikawa inafanya juhudi za kufunika funika.

Ngongo,

Achana kabisa na hawa wanasheria unaowataja kwani wote ni wachumia tumbo na wanafiki wakubwa.JIULIZE KWANINI WALISHINDWA KWENDA MAHAKAMANI KUDAI HAKI YAO YA KIMSINGI KABISA YA UVUNJWAJI HUO WA SHARIA NA KATIBA YA NCHI.

Ndio maana tunaita wachumia tumbo na wanafiki tu.

Pole sana.

 
Bwana Buchanan, sijui ulitaka kuelimishwa au kujibiwa shutuma zako juu ya haki a Wazanzibari. Nitajaribu kufanya yote mawili.

1. Fahamu kuwa matamshi mawili unayoyanukuu yana sababu tofauti, La kwanza ni jitihada ya Wazanzibari katika hizo harakati za kuigombea hiyo Zanzibar kutokana na dola la Zanzibar chini ya SMZ ilipokuwa ikipingana na jitihada hizo za kudai Utaifa wa Zanzibar. Waliokuwa mahakamani hawakuwa na kesi bali walikuwa wakipinga maovu ya kutawaliwa. Hivyo basi lolote ambalo lingesaidia katika harakati hizo ingekuwa rahisi kupotelezewa kama ilivyofanywa kwa kauli ya Jaji Augustino

2. Kauli ya Pinda ni muendelezo wa kuidhalilisha Zanzibar, jambo lililofanya Wazanzibari wapinge. Harakati ni zile zile kama hapo mwanzo ni kutaka uhuru wa Zanzibar.

Kuhusu swali la ktukejeli, nafikiri akili ya mtu alie sawa itamwambia kuwa mtu ujivune na upiganie chako na hivyo Wazanzibari kupigania nchi yao si vibaya ubaya ni kukukatalieni nyie kuwa na nchi yenu, lakini kwa vile hamuitaki isiwe lazima tutuburuza mnavyotaka. As far as hili la utambuzi, hiyo ni hiyari yenu mnapoona kuwa muwape rushwa baadhi ya Wazanzibari ili iwe kigezo cha kutafuta uhalali wa kutumeza. Rushwa ni rushwa ni si Wazanzibari tu bali hata nyinyi tunawaona Makamanda wanaingizwa kwenye kamati za POSHO na kutoka na maazimio ya muafaka na CCM.

Hili la Makamo wa pili kufika Tanganyika huwa hafiki Kiserikali na hahudumiwi na SMT na hivyo si vibaya na Pinda nae kuambiwa mwisho Chumbe.

Kama nimekuelewa vizuri kauli ya Jaji Mstaafu Augustino Ramadhani ni ya "kizalendo" wakati ile ya Pinda ni ya "kejeli" japokuwa maana ni ile ile! Kama hivi ndivyo safari ndefu bado tunayo juu ya huu Muungano wetu!
 
Kama nimekuelewa vizuri kauli ya Jaji Mstaafu Augustino Ramadhani ni ya "kizalendo" wakati ile ya Pinda ni ya "kejeli" japokuwa maana ni ile ile! Kama hivi ndivyo safari ndefu bado tunayo juu ya huu Muungano wetu!

Hakuna safari ndefu kwani sasa mambo yapo katika ncha. LAAZIMA ZNZ HURU YENYE MAMLAKA KAMILI IPATIKANE. Na waZnz wanataka kupumua sasa.

Laazima kieleweke huko Dodoma
.
 
Huu Muungano ulikuwa na walakini toka mwanzo. Huwezi unganisha nchi mbili kuwa moja na wakati huo huo ukaacha upande mmoja ukiwa na serikali zake kama kawaida, huku upande mwingine ukipoteza kila kitu.

Zanzibar kama wanataka mamlaka yao kamili waachiwe, maana sioni kama tuapata hasara yeyote wakiondoka maana hata hivyo hamna walichotuongezea. Ukienda kwao hawataki umilika hata kaploti kakuweka kioski tu wakati wao huku kwetu wamamiliki ardhi kwa mahekari na hakuna anayewabugudhi.
 
Buchanan unaendeshwa na hisia

Haya mkuu! Mimi "nahisi" kuwa Pinda aliwahi kudai kuwa "Zanzibar Sio Nchi" pia "nahisi" kuwa Jaji Mstaafu aliwahi kuandika Hukumu inayodai kuwa "Zanzibar Sio Nchi!" Umefurahi sasa?
 
Last edited by a moderator:
Mimi ni mtanganyika.

PERFECT! Kiukweli hakuna mzanzibar anayetamani uzanzibar kihalisia, midomo inataka muungano uvunjike lkn mioyo yaoinawasuta na wengi wataukana uzanzibar na kuchukua uraia wa tanzanyika. Hivi ulilia Zanzibar kwa kitu gani hasa jamani?
 
Huu Muungano ulikuwa na walakini toka mwanzo. Huwezi unganisha nchi mbili kuwa moja na wakati huo huo ukaacha upande mmoja ukiwa na serikali zake kama kawaida, huku upande mwingine ukipoteza kila kitu.

Zanzibar kama wanataka mamlaka yao kamili waachiwe, maana sioni kama tuapata hasara yeyote wakiondoka maana hata hivyo hamna walichotuongezea. Ukienda kwao hawataki umilika hata kaploti kakuweka kioski tu wakati wao huku kwetu wamamiliki ardhi kwa mahekari na hakuna anayewabugudhi.

Mnaweza kuunganisha nchi mkafanya vyovyote mtakavyo! Ndio maana Watanzania tunakataa Ardhi isiwe "Suala la Muungano" katika EAC wakati wengine wanakubali!

Muungano ni "how you make it!" Ndio maana kuna ndoa mitara, mutta (za muda mfupi kwa waislamu wa madhehebu ya Shia), mke mmoja, mkeka, nk. Zote ni ndoa japokuwa setting na makubaliano ni tofauti!
 
Mfungue akili huyo.

Anaonesha yupo ndotoni sana,tena nina mashaka sana na Thinking Capacity yake

Mbona umeanza kejeli? Umeishiwa hoja? Kama umeishiwa unaweza ukakaa pembeni ukawaachia wengine wakachangia!
 
Mnaweza kuunganisha nchi mkafanya vyovyote mtakavyo! Ndio maana Watanzania tunakataa Ardhi isiwe "Suala la Muungano" katika EAC wakati wengine wanakubali! Muungano ni "how you make it!" Ndio maana kuna ndoa mitara, mutta (za muda mfupi kwa waislamu wa madhehebu ya Shia), mke mmoja, mkeka, nk. Zote ni ndoa japokuwa setting na makubaliano ni tofauti!

Umejitahidi sana kuuhalalisha ubovu wa muungano tulionao lakini ukweli utabaki kuwa jinsi ulivyo, kwamba Muungano uliundwa ukiwa na kasoro zake tokea mwanzo. Huwezi ua nchi moja kabisa halafu nyingine ukaiacha kama ilivyokuwa na ukadai kwamba mmeungana kwa usawa na sasa nchi yenu ni moja. Kama ni kufa zife zote ndipo izaliwe nchi hiyo moja mnayotaka kuiunda, kama ni kubaki zibaki zote ili mjue hamjaungana bali mmeunda Jumuiya kama zilivyo SADC, EAC, etc.
 
Tangu lini mikoa idai kuwa nchi? basi dar, mwanza, arusha, mbeya, moro, tanga nk, wadai kuitwa nchi, wasinyonyane
 
Back
Top Bottom