CHAMVIGA
JF-Expert Member
- Oct 5, 2012
- 7,687
- 2,240
Juzi juzi kuna mtu kavuliwa uanachama na Wazanzibari kwa kutaka Serikali 3! Msiwachukie watu wengine bure jamani wakati nyie wenyewe ndo mnang'ang'ania mambo huku mkifanya kama hamtaki!
Niwape changamoto wang'ang'ania Muungano wa Zanzibar: ukipewa Cheo chochote na JK, whether kwenye Taasisi ya Muungano au la ukatae kwa kuwa wewe hutaki Muungano! Otherwise ni unafiki hutaki samaki huku unakunywa mchuzi wake!
Buchanani.
Mkuu wangu hivi nani asiejua kuwa viongozi wengi wa zanzibar ni vibaraka wa serikali yetu? Kifupi hakuna anaepewa cheo kama zawadi bali hao ni viongozi walioandaliwa kutumikia na kuulinda muungano na maslahi yetu(tanganyika) na yawakubwa/external katika huu Muungano. Tangulini nchi ya watu millioni moja ikaungana na nchi ya watu milioni 45? Huruma hiyo Nyerere ameipata wapi? Wasiojua wanapaswa kujua kuwa moja ya masharti ya kuwa mwanaCcm anaepewa cheo katika serikali kutoka Zanzibar ni kuwa mhafidhina wa muungano! Akina Shekh Abedi Amani karume waliuliwa na Nyerere pale walipotaka kuvua koti lilianza kuwa zito la muungano. Akina Jumbe alipopachikwa na Nyerere kama Rais wazanzibar alipokwenda kinyume si unajua kilichompata? Akina Mansour, Jussa, Moyo nao si unaona kilichowapata walipojaribu kuutikisa muungano? So nani ni nani hapa mkuu? Kiukweli wanafiki ni Tanganyika na zanzibar ni wakuburutwa tu.