Double Standard Kuhusu Kauli ya "Zanzibar Sio Nchi!"

Double Standard Kuhusu Kauli ya "Zanzibar Sio Nchi!"

Kwa nini Jaji Mstaafu Agustino Ramadhan alipodai kuwa Zanzibar sio nchi hamkukimbilia kubadili Katiba ya Zanzibar?

Thats Too Low & Its Ridiculous

Hiyo inazuia nini au vipi watu kudai zanzibar yao huru?au taifa lao kamili??

Acheni kupindisha pindisha hoja,inshort acheni unafiki,waachien zanzibar,tafuteni tanganyika yenu
 
Kwa hiyo wanaodai "nchi" yao waache mara moja, right?


JK alishasema ZNZ si nchi nje ya TZ

hilo linajulikana....

kabla ya kujadili ni nchi au sio nchi ni bora kwanza ujiulize nchi ni nini? nchi inaundwa na nini? components zake ni Zipi? then unakuja kufanya comparison kwa ZNZ ndo upate jibu ni nchi au laa...

Haya malumbano nafikiri ni kutafuta Faraja tu lakini kwa mtu mwenye akili na mwelewa anaelewa kipi ni kipi
 
Muungano unalazimishwa na wahafidhina ndani ya ccm kwa manufaa yao siyo kwa waTanganyika wala waZanzibar. Waliungana Nyerere na Karume na baadae 1977 wakaunganisha vyama vyao vya TANU na ASP.

Sasa katika era hii ya vyama vingi muungano hauswikhi, kwani ule ulikuwa wa wana ccm, siyo wa nchi hizi mbili, ndiyo maana CCM wanaulazisha. Hawana nia nyingine ni kuendelea kutawala na kutunyonya. Mafisadi wakubwa.

Ccm wana nia ya nchi hizi mbili wananchi wake wafanye vurugu za kuukataa huu muungano fake, ili wahalalishe utawala wao wa kidikteta ie they want to legalize their dictatorial regime!!

Mungu ilaani CCM na viongozi wake kwa mateso wanayotuletea wkt wanatumia pesa nyingi kwa kisingizio cha muungano wkt watoto wakikaa chini mashuleni, mahospitali hamna madawa kama zipo basi ni fake etc
 
Muungano unalazimishwa na wahafidhina ndani ya ccm kwa manufaa yao siyo kwa waTanganyika wala waZanzibar. Waliungana Nyerere na Karume na baadae 1977 wakaunganisha vyama vyao vya TANU na ASP.

Sasa katika era hii ya vyama vingi muungano hauswikhi, kwani ule ulikuwa wa wana ccm, siyo wa nchi hizi mbili, ndiyo maana CCM wanaulazisha. Hawana nia nyingine ni kuendelea kutawala na kutunyonya. Mafisadi wakubwa.

Ccm wana nia ya nchi hizi mbili wananchi wake wafanye vurugu za kuukataa huu muungano fake, ili wahalalishe utawala wao wa kidikteta ie they want to legalize their dictatorial regime!!

Mungu ilaani CCM na viongozi wake kwa mateso wanayotuletea wkt wanatumia pesa nyingi kwa kisingizio cha muungano wkt watoto wakikaa chini mashuleni, mahospitali hamna madawa kama zipo basi ni fake etc
Huu Muungano haulazimishwi na CCM pekee mkuu, kuna mkono wa CIA!

Muungano huu ukivunjika Marekani hawatakubali kuwe na "Somalia" nyingine Afrika Mashariki! Al Qaeda/Al Shabaab nao ndo hao wanasubiri kama fisi anayemfuata binadamu kwa nyuma akidhani atadondosha mkono ili aule! Piga ua garagaza Zanzibar haitakuwa huru milele!

CCM knows exactly what they are doing!
 
Tunajadili juu ya "double standard" wewe unajadili juu ya "ung'ang'anizi!" Tutafika kweli?

hatuwezi kuamini hicho unachokisema kwamb ni "double standard" Wazanzibar kauli yao tumeiona kweny takwimu za Jaji Warioba, na huo ndio msimamo wao unaotambulika kisheria!!
 
Kwa nini tuiachie Zanzibar wajukuu wa sultani! Mnadhani Watanganyika wajinga waache ndugu zao warejeshwe kwenye utumwa?

ni kweli ila sio ndugu zenu Wazanzibar maana kamwe hatujapata kusikia Wazanzibar kufanywa watumwa na kama unawajua hebu tuwekee majina ya Wazanzibar waliokuwa watumwa wa Sultan, hizo ni propaganda na kukosa fikra za kuona mbali.
 
Buchanan

Kwa ninavyoona hapa swala la U-Zanzibari au U-zanzibara, kuwa ipi ni nchi au mkoa hii imefikia sehemu imewachosha wananchi kwa kuwa imepelekwa kihunihuni tu tangu awali. Hata pale kulipotokea migogoro chanya voingozi walihodhi mamlaka na kulitolea majibu mepesi kama kitu baki tu. Ila kwa lilipofikia sasa ni lazima serikali zote zilizopo zikubali kuwa huu siyo muungano wa serikali ni muungano wa nchi, na kuwa nchi siyo mali ya viongozi ni ya wananchi. Kwa hiyo kama tunataka hili liamuliwe mpaka wote waridhike ni tufikie tuwatengenezee wananchi hao "MEZA YA MAZUNGUMZO" ili waone kama:

(a) Bado wanautaka huo Muungano na
(b) Kama wanautaka wanaotaka ni wa aina gani

Kama watasema hawautaki ndiyo wao walioutaka wamesema sasa inatosha. Siyo dhambi. Hatuhitaji kuelekea kwenye watu flani kuanza kupigana vita ya kudai uhuru wao humuhumu na hapahapa. Ni aibu.

Kuhusu double standards hili swala la kukosa subira tu. Ni swala la ubinafsi la wengine kuona kina flani hawana haki ya kuongelea hili. Mi nadhani kuna mtu aliwadanganya sehemu. Hivi ni kweli tunaamini kuwa Muungano ukivunjika, Tanganyika ikazaliwa upya, kuna Mtanganyika atakayeathirika. Kwamba kuna msaada unaotokea Visiwani? Au "Machogo" yakiongelea Zanzibari ndo kilichosemwa kinakuwa siyo sawa? Mbona kuna wengine wanaongoza wizara nje hata ya makubaliano na siwasikii wapige kelele kwamba mwenzao kashika visivyomhusu? Mbona?

Nimalizie kwa kuishauri Serikali. Haya yanayowahusu Watanganyika na Wazanzibari tuwaache wao waamue. Tusiwaamulie.
Na kwa siye wengine, tuwe na subira. Mtengeneza janga hula na wa kwao. Tusikimbilie kunako vurgu ilihali tunaweza kufikiria njia nyinginezo. Niwakumbushe kuwa walipounganisha ile hati ya ndoa waliipeleka UN wakaweka wazi. Kama kuna mmojawapo katika ndoa hiyo hajaridhika na amejiridhisha kuwa hakuna suluhu anaweza kulipeleka kule "KISHERIA" na kusema "siye twadai talaka yetu ati". Naamini watasikilizwa vizuri. Hakuna haja ya kusarandiana na kujazana mitusi ya uso kisha tunakaa chini tena.
 
Last edited by a moderator:
KUEPUKANA NA KUFUATWA FUATWA NA NZI ONDOA CHAKULA ULICHOBEBA UBAVUNI.

Wazanzibar mmewanyonya vyakutosha na kuwadhulumu kwakiwango kisichoelezeka. Wanataka sasa nchi yao yenye mamlaka kamili nyie mwalalamikia udouble standard wao. Wenye double standard ni sisi watanganyika/serikali isiyotaka kuwaacha wazanzibar na taifa lao.

Kwanini tunaendelea kuwanyonya na kuiharibu Zanzibar yao huku twajifanya eti wao ndio wananufaika? Mnaogopa nini kuwapa taifa lao? Au mnaogopa nchi kuongozwa na sheria za dini ndio maana gharama kubwa yatumika kuulinda muungano/ukoloni kwa wazanzibar?
 
hatuwezi kuamini hicho unachokisema kwamb ni "double standard" Wazanzibar kauli yao tumeiona kweny takwimu za Jaji Warioba, na huo ndio msimamo wao unaotambulika kisheria!!

Sijazungumzia suala "Takwimu" zilizotolewa kwenye Tume ya Warioba bali ni kauli ya "Zanzibar Sio Nchi" ilipotolewa na Jaji Agustino Ramadhan hatukuona pilikapilika za Kubadili Katiba ya Zanzibar, 1984 ili Zanzibar iwe "nchi" lakini PM Pinda, mtoto wa Mkulima aliponyanyua tu mdomo, unajua kilichotokea!mbona unataka ku-divert mada kwa makusudi?
 
CHAMVIGA

Kitu gani kilichonyonywa huko Zanzibar? Wana madini au yale "mafuta ya kujipaka?"
 
Last edited by a moderator:
Thats Too Low & Its Ridiculous

Hiyo inazuia nini au vipi watu kudai zanzibar yao huru?au taifa lao kamili??

Acheni kupindisha pindisha hoja,inshort acheni unafiki,waachien zanzibar,tafuteni tanganyika yenu

Sijazungumzia Zanzibar "kudai nchi yao," bali "Double Standard!" Kweli nimeamini Mulugo na Kawambwa wameharibu elimu yetu, kama suala dogo kama hili linakushinda kulielewa!

Halafu hilo la "kudai nchi" mbona mnadai kuwa "Zanzibar ni nchi" kama Ibara ya 1 ya Katiba ya Zanzibar, 1984 inavyosema? Sasa mnadai nini exactly? Au ndo mwendelezo wa u-double standard?
 
Huu Muungano haulazimishwi na CCM pekee mkuu, kuna mkono wa CIA! Muungano huu ukivunjika Marekani hawatakubali kuwe na "Somalia" nyingine Afrika Mashariki! Al Qaeda/Al Shabaab nao ndo hao wanasubiri kama fisi anayemfuata binadamu kwa nyuma akidhani atadondosha mkono ili aule! Piga ua garagaza Zanzibar haitakuwa huru milele! CCM knows exactly what they are doing!
Hapa ndugu unaimba wimbo moyo wako unapenda kabisa. Hapa nawe umekuwa mwanaCCM kwakuwa inaulinda muungano ambao upo kwa ajili ya kupambana na uislamu kama maelezo yako yanavyojieleza.

Wewe ni CHADEMA damu lakini hapa unaiunga mkono CCM kisa CIA inaisapoti ili kuhakikisha muungano haufi ili kupambana na uislamu usijefanya zanzibar dola ya kidini huoni wewe pia ni double agent mkuu!!? Hapa unajifanya kuibebesha CCM majukumu/responsibility kuwa ndio inajua pekee inachokifanya na kumbe nawe ndio ngoma unapenda CCM iendelee kucheza.

Huu ndio unafiki ambao mimi ninauchukia kwasababu nyie chadema hata serikali tatu mwazitaka kwa makusudio ya kisiasa tu lakini hampo tayari muungano kuvunjwa. Nyie mwataka kuja endeleza utawala wa ki imla kama aliokuwa akiuendesha Nyerere.
 
KUEPUKANA NA KUFUATWA FUATWA NA NZI ONDOA CHAKULA ULICHOBEBA UBAVUNI.

Wazanzibar mmewanyonya vyakutosha na kuwadhulumu kwakiwango kisichoelezeka. Wanataka sasa nchi yao yenye mamlaka kamili nyie mwalalamikia udouble standard wao. Wenye double standard ni sisi watanganyika/serikali isiyotaka kuwaacha wazanzibar na taifa lao.

Kwanini tunaendelea kuwanyonya na kuiharibu Zanzibar yao huku twajifanya eti wao ndio wananufaika? Mnaogopa nini kuwapa taifa lao? Au mnaogopa nchi kuongozwa na sheria za dini ndio maana gharama kubwa yatumika kuulinda muungano/ukoloni kwa wazanzibar?
Angalia sana mkuu, ukisema ukweli sana juu ya hili utaitwa mwana Chadema. Imefika mahali watu hawataki tena kufikirisha ubongo wao bali kurukia mambo ya itikadi za vyama tu.
 
Kitu gani kilichonyonywa huko Zanzibar? Wana madini au yale "mafuta ya kujipaka?"

Kwa hiyo wewe fikra zako zinaishia hapo kwenye mafuta au ndio muendelezo wa kejeli kwa wazanzibar? Zanzibar ni taifa lenye kila utajiri na zanzibar ni taifa ambalo kwa hadhi yake halikupaswa kuwa ombaomba kwa Watanganyika. Leo hii Zanzibar ndio inategemea eti iwezeshwe na watanganyika ili kuendesha nchi wakati Zanzibar inautajiri wa kuweza kuindesha serikali bila kuwa ombaomba. Maliasili zinabebwa kinyemela kutoka Zanzibar na kuja kuinufaisha Tanganyika kisha Twasema Zanzibar inategemea Tanganyika.
 
Back
Top Bottom