Buchanan
JF-Expert Member
- May 19, 2009
- 13,192
- 1,976
- Thread starter
- #101
Punguza jazba na chuki za kuwazushia mambo wa Znz.
Zanzibar hawahitaji Serikali 2 au 3 au hata 10. Kinachotakiwa ni kuwa na Znz huru kwa maana nchi yenye mamlaka kamili. Kama Znz itaweza kuyapata haya katika Serikali Moja au Mbili au Tatu au hata 7 hiyo sio Tatizo.
Jaribu kuwasoma nini wa Znz wanachotaka na sio kuendeshwa na hisia na chuki dhidi yao.
Lakin japo ni Mod naweza kukuuliza suala hapa. JE UNAJUA TOFAUTI ZA DOLA NA NCHI?
Naomba jibu lako ili tukupe mwanga kama upo kizani.
Mkuu sina jazba yoyote wala chuki, niko fiti kwa kile ninachosimamia, wala usinipe pole kwa kuwa sijakwazwa au kuumia popote kwenye mjadala huu! Unaposema Wazanzibari hawataki Serikali 2 au zaidi umenukuu kauli ya nani? Mimi nimewanukuu akina Amani, Jumbe na kuhusu Sera za CUF.
Kwa kuongezea tu CCM Zanzibar walimvua uanachama Mbunge kwa kudai Serikali 3, akanyang'anywa Kadi na kuambiwa kuwa hiyo sio Sera ya CCM! Sasa wewe uko nchi gani mwenzetu?
Kwa habari ya Dola vs Nchi, mimi sijazungumzia Dola, kama unataka mjadala wa kama Zanzibar ni Dola au la anzisha tu tutatoa mawazo yetu!