Dkt. Mwigulu Nchemba aunga mkono ununuzi wa jezi halisi (original), anunua jezi 200 za Simba

Dkt. Mwigulu Nchemba aunga mkono ununuzi wa jezi halisi (original), anunua jezi 200 za Simba

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
3,177
Reaction score
7,472
WhatsApp Image 2025-10-13 at 10.55.14_1057db2c.jpg

WhatsApp Image 2025-10-13 at 10.55.24_adcb71d3.jpg

Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba ameunga mkono kampeni ya kununua jezi halisi (original) za timu ya Simba SC, akitoa rai kwa wapenda soka wote kuepuka jezi bandia (feki).

Dkt. Mwigulu ameunga mkono kampeni ya kuhamasisha mashabiki kukataa jezi feki na kununua orijino kwa kununua jezi 200.
WhatsApp Image 2025-10-13 at 10.55.17_c32b6297.jpg
Amesema jezi feki zinaikosesha timu mapato muhimu kwa ajili ya usajili wa wachezaji bora, na pia zinaikosesha serikali mapato ya kodi.

Ameyasema hayo nyumbani kwake Misigiri Iramba Mkoani Singida, alipotembelewa na ugeni wa timu ya mauzo ya simba ukiongozwa na Msemaji wa Timu hiyo Ahmed Ally.
WhatsApp Image 2025-10-13 at 10.55.18_e8757b36.jpg
 
Yeye aweke mambo sawa kitaa ili watu tubakia na disposable income hizo jezi tutanunua tu (unadhani yale matozo kwenye simu waliyoweka tungekuwa na hizo chenji ni sawa na jezi ngapi ) !????

 
Hatimaye timu ya simba yaingia kwenye payroll ya Mwigulu! Na wenyewe wameanza kufaidi matunda ya kodi zetu.
 
Sielewi mantiki ya msemaji wa Simba kuzunguka na kushugurika na swala la jezi feki wakati Simba imeshatoa tenda kwa Jayruti.
 
Siku zinaenda kasi sana mwigulu sasa hiv ataitwa dr. Mzee mwigulu nchema
 
Back
Top Bottom