Dkt. Bashiru Ally ''amkaanga'' Lazaro Nyalandu

Dkt. Bashiru Ally ''amkaanga'' Lazaro Nyalandu

Hilo ni tatizo lako kwa sababu hukulazimishwa kufungua thread na kusoma.
Hili ndio tatizo la vijana wengi hapa JF, hawasomi mada wakaelewa wao wanakimbilia kuweka comment ndio waonekane wao ni wakwanza ku-comment.
 
Kinachonifurahisha nikwamba,Daktari huyu Bashiru Ali 1995 alisema serikali yenye dira lakini ndiyo iliyoingia mikataba mibovu kwa nini hakuisema?. 2005 Serikali hiyohiyo aliunga mkono na kusema serikali ya kasi zaidi na nguvu zaidi ni safi,lakini ndiyo iliyokuwa ikiporomoka kwa kila aina ya ufisadi ,cha ajabu kama msomi hatukumsikia akiishauri hata kuionya ,leo anasema wanaohama ccm hawakufanikiwa kwa kuwa ccm nidora ndio kiburi kada huyu msomi anafagilia?,atambue kuwa serikali za namna hii hazikuweza kudumu zilifika wakati zikaferi kabisa
 
Haya majibu ya Dr Bushiru si ya mtaaluma,tena mwalimu wa chuo kikuu. Hakuna uchambuzi wa kifikra. Amejibu kama Slowslow
ha ha haaaa... kisa amejibu usivyotaka wewe. Sisi wanafunzi wake tunaona amejibu vizuri sana na kiuweledi. Ukisoma political science ambalo ndo somo analofundisha kuna kitu kinaitwa "checks and balances" katika serikali. ukimsoma Aristotle na Greek historians anaitwa polybius wameelezea vizuri sana suala la 'separation of power' na "checks and balances" katika serikali. chimbuko la theories zao zinatokana na huo mwingiliano kati ya vyombo vya serikali (Bunge, Mahakama na Utawala). kwahiyo ni kweli kabisa kwamba hili suala mihimili ya serikali kuingiliana lilianza kabla Nyalandu na sisi hatujazaliwa.
 
Kwani ndugu hauwezi kumjibu mtu mpaka utumie lugha za matusi.......

Kama una amini katika uhuru wa kutoa maoni kwanini unakereka na maoni ya wengine.....je huo si udikteta.....!!?
Professor of mathematics ukisema 1+1=3 katika normal/natural mathematics, tutaku label kama Rubbish, your professorship!
Dr. mzima na PhD.. Doctor of Philosophy, kusema kuwa mihimili kuingiliana ilikuwepo hata kabla ya yeye kuzaliwa, ni rubbish statement from a Doctor of philosophy degree holder! Kama ilikuwepo , watu wasiikemee kwa vile ilikuwepo kabla hajazaliwa (Nyarandu)!
 
Ukweli ni dhana tu kulingana na fikra zako!

Upungufu wa fikra unaweza kusababisha ukadhani suala/jambo fulani ni kweli wakati kwa wenye fikra pana wanajua sio kweli.
Inaonekana hujaisoma hiyo nukuu ya Oliver Tambo: "...kuwa mkweli dhidi ya tuhuma kwa watawala sio jambo rahisi...." sasa hiyo hoja yako kwamba "ukweli ni dhana tu kulingana na fikra zako" wewe unaipata wapi? Kuna wengi ambao wanaunga mkono utawala kwa sababu ya msimamo wao. lakini wanaounga mkono utawala kwa sababu ama ya woga ama ya kulinda nafasi zao ama kujipendekeza, ni wengi zaidi. ndio maana ni rahisi sana kumkandamiza maskini au asiye nacho, na ni vigumu kumtuhumu aliyenacho. hizo ni simple facts of life. Mkono mtupu haulambwi, wanasema wahenga. na kwa sababu hiyo, ni ngumu sana kuwa mpinzani. inabidi uwe na roho ngumu kweli. utazushiwa hiki na kile. utadhulumiwa hata haki zako wazi wazi. JK kasema upinzani siyo uadui, angalia alivyoandamwa. utawala una dola, na unaitumia dola kufanya utakavyo. very unfair battle.
 
Pamoja na kuwa na katiba wanayo isifia sana hapo Kenya, Uhuru Kenyata kaingilia mihimili yote ili abaki madarakani (mahakama, tume ya uchaguzi, bunge)
Na aliapa kuwa akirudi madarakani hao majaji watakiona. Ngoja tusubiri tuone. Karudi.
 
Chama Cha Mapinduzi ni genge la wezi, wala rushwa na wabadhirifu wakubwa nchi hii! Ni genge ndani msitu mnene uliojaa muumiani na monsters!!

Ndani ya genge hili hatari duniani, wanahakikisha kuna vikaragosi wao wa kutosha nje ya msitu huo wa mafedhuli! Vikaragosi hivyo vitakuwa vitapewa kwa vipipi na vibiskuti na wakati mwingine kuishia kudanganywa kwa kauli na baada ya hapo, wataingia duniani kuwatetea mafedhuli na manduli wanaoiangamiza nchi!!

Ni kweli, kwavile ni msitu mnene uliojaa majahiri wa kila aina, haishangazi wengine kujikuta wamezaliwa kwenye hilo limsitu la waovu na kujikuta wakitenda kama manduli mengine yaliyomo humo yanavyotenda!! Hata hivyo, wapo miongoni mwao ambao hatimae wanakuja kupata maono kwamba udhalimu na uovu unaofanywa na jamii yao haukubaliki, sio dunia tu bali hata akhera!

Hawa ni wale wanaoamua kuukumbia msitu huku wakirushiwa kila aina ya silaha kutoka kwa mafedhuli wao ambao hawataki kuona watu wakiungama... wanachotaka ni kuona kizazi chao cha majahiri kikiendelea kushikamana!!!
Mumiani na monsters. Mkuu hili ni povu bilashaka!
 
Kwani mnafikiri Bashir Ally yeye hataki uteuzi! Huyu jamaa siku nyingi alishakuwa kitu kingine kabisa baada ya kuamua kuwa msemaji wa CCM.
Kama kila msomi mnasema ni CCM, sasa vyama vya upinzani vitaendeshaje nchi bila kuwa na wasomi kama wasomi wote ni CCM.
 
Awe amekaangwa au hajakaangwa, awe ametoka kwa sababu za maana au za hovyo the point remains ameamua kuondoka CCM na ameshafanya hivyo.
Haya mengine ni umbea na ufukunyuku tu kwa masuala binafsi ya mtu. It's not gonna put food on your table or pay your next salary.
Inashangaza unatoa lawama kwa wale wanaomjadili Lazaro Nyalandu wakati na wewe umeungana katika majadiliano!

Kutoa mchango wako hapa ni kuendeleza ''umbea na ufukunyuku'' ambao unaupiga vita.
 
Walimu wa chuo kikuu wamekuwa makada wa ccm, wanajipanga kupokea rushwa ya vyeo toka kwa pombe. Namshukuru M/Mungu kwa kuninyima nafasi ya kwenda kupoteza muda kwenye vyuo hivi
Mkuu lazima ujiulize kwann wasomi wanaunga mkono mambo mengi anayofanya Magufuli, na wale activist kama Mange na wewe mnapinga??
Kiukweli kwa mtu yeyote mwenye akili sawa sawa na kumbukumbu sahihi lazima ataunga mkono matendo yote ya serikali hii.

Ni ajabu sana kuona Nyarandu huyu huyu leo anaitwa Kamanda na watu kama akina Wema.

Jiulize tu mtu aliewahi kuwa Waziri mkuu leo anagombea uenyekiti wa mkoa akishindana na akina Kubenea halafu anaitwa Kamanda!!!

Inamaana sisi hatuna hata kumbukumbu kuwa huyu mtu anahitajika kutoa mchango mkubwa zaid sio kwa level ile,

Nyarandu huyu huyu aliekuwa anashinda Marekan na warembo kisa kutangaza utalii, tukapiga kelele, anauza wanyama mchana kweupe mpaka tukaanza kutabiri kuwa miaka kumi ijayo iwapo ataendelea kuwa waziri tutakuwa hatuna wanyama lakin leo tunamtetea kwa nguvu hivi!!! Tatizo ni nini??? Tumelogwa sisi. Hebu tuamke watanzania,

Tusiwaendekeze hawa wezi wa mali zetu kirahisi hivi. Huyu ameona anataka kukamatwa anaenda chadema kujificha na sisi tunamuona shujaa. Huyu Nyarandu huyu!!! Haiwezekani kabisa!!!!

Nyarandu huyu huyu ambae alienda kuwaleta maseneta ili waje wamtishe Magufuli ampe uwaziri wa utalii bwana Nyarandu!! Huyu Nyarandu huyu ndo leo tunamshangilia kama shujaa, Kisa yule mwanamke Mange kasema!!!

Ama kweli sisi tumelogwa. Ndo maana watu na elimu zao wakiona gari lake limepigwa chain mjin sabb ya wrong parking anapiga picha anamtumia Mange et tusaidie dada Mange, hide my id!!!!! Watu na elimu zao. Amefokewa na bosi wake kazin ana muandikia Mange amsaidie. Ukicheki mtu mwenyewe ana Masters, Phd , graduate wa first class. Yaan ni majanga, alieturoga kafa kazikwa baharini kama osama.

Hakuna aliekuwa hasikii uchafu wa Nyarandu wakati wa uwaziri wake. Alikuwa mchafu kias cha kupandisha twiga kwenye ndege mchana kweupe. Tukapiga kelele sana halafu leo et tumesahau, Dah! Mpaka inatia hasira .
 
Na aliapa kuwa akirudi madarakani hao majaji watakiona. Ngoja tusubiri tuone. Karudi.
....malizia cha mtemakuni ! Sasa hapo muhimili mkubwa uliojikita mpaka chini utaujua tuu.
 
ha ha haaaa... kisa amejibu usivyotaka wewe. Sisi wanafunzi wake tunaona amejibu vizuri sana na kiuweledi. Ukisoma political science ambalo ndo somo analofundisha kuna kitu kinaitwa "checks and balances" katika serikali. ukimsoma Aristotle na Greek historians anaitwa polybius wameelezea vizuri sana suala la 'separation of power' na "checks and balances" katika serikali. chimbuko la theories zao zinatokana na huo mwingiliano kati ya vyombo vya serikali (Bunge, Mahakama na Utawala). kwahiyo ni kweli kabisa kwamba hili suala mihimili ya serikali kuingiliana lilianza kabla Nyalandu na sisi hatujazaliwa.
Tatizo ndio liko hapo. kusema kwamba tatizo limeanza kabla Bashiru na Nyalandu hawajazaliwa, ni fact, lakini siyo hoja hapa. Hoja hapa ni kwamba katika awamu zetu tano za utawala, suala la muingiliano wa mihimili limekuwa ajenda kubwa sana hivi sasa kwa sababu za msingi kabisa. kwamba tunaye rais ambaye haoni ubaya wa kuchanganya mihimili apendavyo, na anaamini kabisa kwamba hakuna mhimili wala nini. kuna mhimili mmoja tu. ufalme wake.

JPM haoni tatizo kufanya siasa chafu katika tukio la Kijeshi. Awamu zote zilizopita, kamisheni kwa wanajeshi zilitolewa Monduli na ni zoezi la wanajeshi na Amiri jeshi mkuu wao. sasa hii kashfa ya juzi, mpaka Rais anapokea wanachama wa upinzani wanaohamia CCM, katika shughuli ya kijeshi, hiyo ni kashfa kubwa haijawahi kutokea. Hapa nataka kusema kwamba Rais JPM anajiona yeye ni mfalme kabisaaaa. hana kikomo cha madaraka, hakuna checks and balances unazosema. kwake kila kitu kinawezakana tu. hakuna katiba hakuna sheria. ndio maana amediriki kupiga marufuku mikutano ya vyama vya upinzani (siyo mikutano ya vyama vya siasa - CCM ni tofauti), kwanza ya nje, na baadaye hata ya ndani, kinyume cha sheria, with impunity.

Katika awamu hii, Rais wa nchi anadiriki kusema watu fulani wasibomolewe nyumba zao kwa sababu "walinipa kura nyingi". anataka kusema nini hasa? kwamba maeneo ambayo hawakumpa kura wataisoma namba? na kweli, angalia maeneo ambayo kitakwimu hawakumpa kura nyingi, wanaisoma namba. Bukoba, maeneo ya Dar ambapo Bomoa Bomoa ya kufa mtu inaendelea. Anabomoa hata nyumba ambazo Mahakama imezuia zisibomolewe. Hiyo hatujawahi kuiona katika taifa letu. Serikali ina-ignore mahakama wazi wazi namna hii, tena kwa matukio ambayo yanawaumiza raia wake yenyewe? Hapo kuna mihimili?

Rais ambaye anadiriki kuiambia mahakama kwamba kama kesi zikihukumiwa haraka na serikali ikapata fedha, basi robo ya mapato yatapelekwa kwa mahakama. Rushwa ya wazi. lugha kama hizo zina utata mkubwa sana.

Bunge ambalo Naibu Spika siyo mbunge wa kuchaguliwa, ni wa kuteuliwa na Rais. na Rais anaagiza Spika afanye hiki na kile, moja kwa moja. Anaagiza hata wajumbe wa kamati za Bunge. hayo yote ni mapya ya utawala huu. na inafikia hatua anaagiza spika awashughulikie wapinzani. hapo tuna haki ya kujiuliza hata hiyo concept ya separation of powers siyo tu kwamba ina matatizo, bali haipo kabisa as far as awamu hii is concerned

Kwa hiyo uchambuzi wa Dr. Bashiru umejikita katika ukada wake wa CCM, na kuogopa kuuchambua utawala. anatumia theory za Political Science kama nyenzo za ku-advance sentiments zake kwa utawala. sasa huo siyo uchambuzi wa kitaaluma. huo ni utetezi tu, tena usio na hoja za kisomi
 
Mkuu lazima ujiulize kwann wasomi wanaunga mkono mambo mengi anayofanya Magufuli, na wale activist kama Mange na wewe mnapinga??
Kiukweli kwa mtu yeyote mwenye akili sawa sawa na kumbukumbu sahihi lazima ataunga mkono matendo yote ya serikali hii.

Ni ajabu sana kuona Nyarandu huyu huyu leo anaitwa Kamanda na watu kama akina Wema.

Jiulize tu mtu aliewahi kuwa Waziri mkuu leo anagombea uenyekiti wa mkoa akishindana na akina Kubenea halafu anaitwa Kamanda!!!

Inamaana sisi hatuna hata kumbukumbu kuwa huyu mtu anahitajika kutoa mchango mkubwa zaid sio kwa level ile,

Nyarandu huyu huyu aliekuwa anashinda Marekan na warembo kisa kutangaza utalii, tukapiga kelele, anauza wanyama mchana kweupe mpaka tukaanza kutabiri kuwa miaka kumi ijayo iwapo ataendelea kuwa waziri tutakuwa hatuna wanyama lakin leo tunamtetea kwa nguvu hivi!!! Tatizo ni nini??? Tumelogwa sisi. Hebu tuamke watanzania,

Tusiwaendekeze hawa wezi wa mali zetu kirahisi hivi. Huyu ameona anataka kukamatwa anaenda chadema kujificha na sisi tunamuona shujaa. Huyu Nyarandu huyu!!! Haiwezekani kabisa!!!!

Nyarandu huyu huyu ambae alienda kuwaleta maseneta ili waje wamtishe Magufuli ampe uwaziri wa utalii bwana Nyarandu!! Huyu Nyarandu huyu ndo leo tunamshangilia kama shujaa, Kisa yule mwanamke Mange kasema!!!

Ama kweli sisi tumelogwa. Ndo maana watu na elimu zao wakiona gari lake limepigwa chain mjin sabb ya wrong parking anapiga picha anamtumia Mange et tusaidie dada Mange, hide my id!!!!! Watu na elimu zao. Amefokewa na bosi wake kazin ana muandikia Mange amsaidie. Ukicheki mtu mwenyewe ana Masters, Phd , graduate wa first class. Yaan ni majanga, alieturoga kafa kazikwa baharini kama osama.

Hakuna aliekuwa hasikii uchafu wa Nyarandu wakati wa uwaziri wake. Alikuwa mchafu kias cha kupandisha twiga kwenye ndege mchana kweupe. Tukapiga kelele sana halafu leo et tumesahau, Dah! Mpaka inatia hasira .
Vile vile tukumbuke hawa unaowaita wasomi ndio hao hao waliotengeneza mikataba mbalimbali ya ovyo inayotia kinyaa ya rasimali tulizonazo yakiwemo madini ambayo huyo anayejiita rais mzalendo anajifanya kuirekebisha.

Labda kama awamu hii kuna kundi jipya la wasomi ambao awamu zilizopita hawakuwepo.
Ila kama wasomi wenyewe ndio hao wakina Profesa waliotolewa ACT wazalendo na kupewa u general secretary basi Tanzania hatuna wasomi.

Huwezi kujiita msomi wakati huna msimamo, ukiwa upande huu unakemea ujinga , ukiitwa upande ule unatetea ujinga ule ule ulioukemea mwanzoni.

Hii imepelekea hadi mtu anayewatuhumu watu kwa chuki binafsi kwamba wanatumia drugs kuitwa MSOMI na huyu magufuli wenu.

kama wasomi unaowaongelea ni wale wenye akili kama za DAB basi awamu hii wapo wengi sana.
 
Kwa kasi ya teuzi za wanazuoni wa Mlimani naamini Bushiru muda si mrefu atapingana na mengi aliyowahi yasema na kuyaamini.
 
Falsafa,mahitaji na muelekeo mpya unahitaji dr wako amekalia upuuzi tuu
 
Doctorial rubbish....
Kama huu ndiyo uchambuzi wa kidaktari basi hizo awards zao zinamashaka mengi sana na namna zinavyopatikana.
Mkuu;
Onyesha wewe uchambuzi wako ambao sio wa ''kidaktari'' badala ya kupiga kelele ambazo hazina hoja.
 
vyeo vinatafutwa kwa nguvu zote.sawa dr ..!!
 
Hawa wasomi siku hizi wamekaa mkao wa kusubiri uteuzi. Ukisoma maoni yao changanya na za kwako.
 
Back
Top Bottom