Mimi sijaongelea "speculation za wanasiasa" bali nimetoa nukuu ya yale ambayo ameyaongea yeye mwenyewe JPM tena hadharani, na mambo ambayo yameandikwa na kushuhudiwa na watu mbalimbali. mfano kuhusu kubomoa nyumba ambazo Mahakama iliagiza zisibomolewe, katika eneo la Kimara. ishu hiyo imeandikwa sana magazetini, wahusika walilalamika mahakamani na mahakama ikatoa onyo, lakini bomoa bomoa inaendelea, na ukiongea na wahanga wanakuambia kabisa kama unabandika ile STOP ORDER kwenye nyumba yako, ndiyo watabomoa na hutaondoa kitu ndani. hiyo nimeshuhudiwa na wahanga kadhaa. Rais mwenyewe kule Mwanza amesikika live akitamka kwamba watu wa Mwanza wasibomolewe kwa kuwa walimpa kura nyingi. hapo hakuna speculation.
Hiyo ni theory. lakini alichokwepa Dr. Bashiru ni kuongelea kinachoendelea sasa hivi vs awamu zilizopita vs theory. ndio ninachosema kujificha katika theory. ni kweli head of state ndiye anasimamia vyombo vya kukusanya kodi na kugawa mafungu. lakini kuna checks and balances. kwamba ukimteua Jaji, au CAG, huna uwezo wa kumtoa. sasa kwa kawaida msimamizi wa wabunge ni Spika. lakini tunaona utawala huu, hata ruhusa ya wabunge kwenda nje ya nchi inatolewa ikulu. sasa hapo ni kuingilia mhimili. ni kuvuka mstari kabisa
Nimekupa mifano ya serikali ime-ignore amri ya mahakama, kwa kuvunja nyumba ambazo mahakama imeagiza zisivunjwe kwanza. lakini kuingilia uhuru wa mahakama siyo lazima iwe hivyo unavyosema, bali inaweza kuwa more subtle. mfano kitendo cha kuahidi kutoa fedha zitakazotokana na maamuzi ya kesi, tayari ni kuingilia uhuru wa mahakama.
Ndugu unaishi Tanzania hii au uko nje ya nchi?? mara ngapi wabunge wa upinzani wamelalamika serikali inatumia fedha nje ya bajeti? na hili lilianza mara tu JPM alipoingia madarakani. na tena huwa anaongea waziwazi: "tutachomoa chomoa fedha hapa na pale". kumbuka KUB Mbowe aliwahi kuuliza swali kwa waziri mkuu kuhusu hongo iliyotolewa kwa wabunge wa CCM, milioni 10 nadhani. sasa tungetarajia spika amtake Mbowe athibitishe hilo au afute kauli hiyo. lakini Naibu Spika alikataa tu kuruhusu swali lijibiwe na ikawa mwisho wa stori hiyo. maana yake serikali wala haikutaka kukanusha hayo. huko ni kuingilia uhuru wa bunge kwa kiasi kikubwa mno. ni rushwa ya hali ya juu, ni kejeli kwa serikali inayojinadi kupambana na Rushwa.
Sasa hapo unapingana hata na kauli ya JPM mwenyewe. aliulizwa swali na Pascal Mayalla siku alipoongea na waandishi wa habari kule Ikulu, kuhusu mihimili. alijibu wazi kabisa kwamba mihimili hailingiani, kuna mihimili iko juu. hapo alikuwa anakiri kabisa kwamba hata akiingilia, ni sawa tu. na huwa anaingilia.
Ni hoja nzuri tu na yenye logic. counter-hoja ni kwamba, kama JPM haheshimu hata hii katiba tuliyonayo, katiba inayotoa uhuru wa kukutana, kuongea. anapiga marufuku mikutano ya vyama vya siasa, kinyume kabisa cha sheria na katiba. anasema ngoja kwanza niinyooshe nchi. nchi siyo familia ya mtu. sasa kama haheshimu hii katiba yenye mapungufu, ataheshimu hiyo mpya?? sawa anaweza kusema fine. let us draw up a new constitution. lakini kwa jinsi alivyo na anavyoonekana kuwa, hakutakuwa na tofauti yoyote katika utendaji wake. and not many people will shout at him.