Dkt. Baruani Mshale: Usiposhiriki uchaguzi utachaguliwa Kiongozi usiyemtaka

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,120
Mshale.jpg

Baruani Mshale ambaye ni Mkurugenzi wa Mikakati na Mafunzo kutoka TWAWEZA amesema kitendo cha Watu na hasa Vijana kutoshiriki katika masuala ya Uchaguzi kinasababisha maamuzi yanayofikia kuchaguliwa kwa Viongozi ambao hawawataki.

Amesema "Tuchukulie mfano wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa pale mtaani kwenu au kijijini kwako mnatakiwa kuchagua viongozi. Kipindi cha Uchaguzi kimefika ukaona wanaogombea watafanya yaleyale tu, ukaamua usishiriki, kitakachotokea ni kwamba wale wachache watakaoshiriki watakwenda kukuchagulia wewe Kiongozi".

Akizungumza kupitia PowerBreakfast ya CloudsFM , Baruani ameongeza kuwa "Hukushiriki halafu yule atakapokuja kuwa Kiongozi ndio utaanza sasa kuona matokeo ya yule Kiongozi atakapofanya vitu ambavyo havikufurahishi wewe".

"Tuchukue miaka 10 iliyopita wakati wa mchakato wa katiba mpya Watanzania wengi sana walikuwa wakifuatilia, walikuwa wanajua kinachoendelea kuhusu mijadala ile na walikuwa wanajua kuna bunge la katiba mpya limekaa na linajadili kwa sababu ilikuwa linaoneshwa katika vyombo vya habari.

"Baada ya uchaguzi wa mwaka 2015 ilitamkwa wazi kwamba hata bunge live halikuwepo kwahiyo wananchi wasingeweza kuona bunge lao linajadili nini, masuala muhimu sana kwao. Pia ilitamkwa na Kiongozi aliyekuwepo kwamba uchaguzi ulikuwa umekwisha siasa ziwekwe kando tushughulike na shughuli za maendeleo"

"Watu wengi wanaogombea nafasi za uongozi wanatuaminisha kwamba wao ndio watakuwa mwarobaini wa matatizo ambayo yapo pale, wakati ushiriki thabiti wa mwananchi ni kitu muhimu sana katika hayo maendeleo.

"Bila ushiriki wa mwananchi unaweza ukafikiri wewe hivi ulivyoviweka ndio vipaumbele vya kero hasa zinazowakabili wananchi wa lile eneo lakini kumbe Wana kero zao.Ili kuleta maendeleo ya kweli ni muhimu kuchagiza ushiriki mzuri wa wananchi"

"Mfano wa uchaguzi wa serikali za mitaa pale mtaani kwenu au kijijini kwako manatakiwa kuchagua viongozi kipindi cha uchaguzi kimefika ukaona kwamba hao wanaogombea wataleta yaleyale tu, ukaamua wewe usishiriki kitakachotokea ni kwamba wale wachache watakaoshiriki watakwenda kukuchagulia wewe Kiongozi"


 
View attachment 2867250
Baruani Mshale ambaye ni Mkurugenzi wa Mikakati na Mafunzo kutoka TWAWEZA amesema kitendo cha Watu na hasa Vijana kutoshiriki katika masuala ya Uchaguzi kinasababisha maamuzi yanayofikia kuchaguliwa kwa Viongozi ambao hawawataki.

Amesema "Tuchukulie mfano wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa pale mtaani kwenu au kijijini kwako mnatakiwa kuchagua viongozi. Kipindi cha Uchaguzi kimefika ukaona wanaogombea watafanya yaleyale tu, ukaamua usishiriki, kitakachotokea ni kwamba wale wachache watakaoshiriki watakwenda kukuchagulia wewe Kiongozi".

Akizungumza kupitia PowerBreakfast ya CloudsFM , Baruani ameongeza kuwa "Hukushiriki halafu yule atakapokuja kuwa Kiongozi ndio utaanza sasa kuona matokeo ya yule Kiongozi atakapofanya vitu ambavyo havikufurahishi wewe".

"Tuchukue miaka 10 iliyopita wakati wa mchakato wa katiba mpya Watanzania wengi sana walikuwa wakifuatilia, walikuwa wanajua kinachoendelea kuhusu mijadala ile na walikuwa wanajua kuna bunge la katiba mpya limekaa na linajadili kwa sababu ilikuwa linaoneshwa katika vyombo vya habari.

"Baada ya uchaguzi wa mwaka 2015 ilitamkwa wazi kwamba hata bunge live halikuwepo kwahiyo wananchi wasingeweza kuona bunge lao linajadili nini, masuala muhimu sana kwao. Pia ilitamkwa na Kiongozi aliyekuwepo kwamba uchaguzi ulikuwa umekwisha siasa ziwekwe kando tushughulike na shughuli za maendeleo"

"Watu wengi wanaogombea nafasi za uongozi wanatuaminisha kwamba wao ndio watakuwa mwarobaini wa matatizo ambayo yapo pale, wakati ushiriki thabiti wa mwananchi ni kitu muhimu sana katika hayo maendeleo.

"Bila ushiriki wa mwananchi unaweza ukafikiri wewe hivi ulivyoviweka ndio vipaumbele vya kero hasa zinazowakabili wananchi wa lile eneo lakini kumbe Wana kero zao.Ili kuleta maendeleo ya kweli ni muhimu kuchagiza ushiriki mzuri wa wananchi"

"Mfano wa uchaguzi wa serikali za mitaa pale mtaani kwenu au kijijini kwako manatakiwa kuchagua viongozi kipindi cha uchaguzi kimefika ukaona kwamba hao wanaogombea wataleta yaleyale tu, ukaamua wewe usishiriki kitakachotokea ni kwamba wale wachache watakaoshiriki watakwenda kukuchagulia wewe Kiongozi"


View attachment 2867252

Siyo kweli.Kinachotufanya sisi wananchi tusishiriki uchaguzi ni kwa sababu ya udhaifu wa mchakato wa uchaguzi wenyewe.Kama hakuna usawa katika kusimamia upigaji na uhesabuji wa kura mimi mwanchi ninachojua watakaopita ni wale ambao msimamizi wa uchaguzi anataka wapite.Si tuliona masanduku ya kura.Usisahau Dr.Mshale Serikali iliwahi kutamka kwamba kama Unalipwa mshahara na serikali ole wako apite wa upinzani kwenye jimbo lako.

Cha kufanya ni kurejesha kwanza imani kwa kusimamia mifumo ya uchaguzi kuwa huru.

By the way kwa sasa INAHISIWA kwamba msimamizi mkuu wa uchaguzi siyo tume ya uchaguzi bali ni yule anayewaweka hao watendaji wa tume kwenye nafasi
 
Huyo Baruani aache upotoshaji, anyooshe maelezo kuwa kushiriki uchaguzi ni upuuzi kama upuuzi mwingine, maana watu wanashiriki, kisha matokea batili ndio yanatangazwa.

Aendelee kushiriki yeye na familia yake, uoga utakapotutoka watanzania tutatafuta namna nyingine ya kupata viongozi, bila kujali hiyo njia itakuwa madhara kiasi gani.
 
Siyo kweli.Kinachotufanya sisi wananchi tusishiriki uchaguzi ni kwa sababu ya udhaifu wa mchakato wa uchaguzi wenyewe.Kama hakuna usawa katika kusimamia upigaji na uhesabuji wa kura mimi mwanchi ninachojua watakaopita ni wale ambao msimamizi wa uchaguzi anataka wapite.Si tuliona masanduku ya kura.Usisahau Dr.Mshale Serikali iliwahi kutamka kwamba kama Unalipwa mshahara na serikali ole wako apite wa upinzani kwenye jimbo lako.

Cha kufanya ni kurejesha kwanza imani kwa kusimamia mifumo ya uchaguzi kuwa huru.

By the way kwa sasa INAHISIWA kwamba msimamizi mkuu wa uchaguzi siyo tume ya uchaguzi bali ni yule anayewaweka hao watendaji wa tume kwenye nafasi
Lazima ushiriki kuondoa tatizo, hii nchi lazima tupambanie sisi wenyewe hakuna mwingine atatusaidia
 
Huyu Mshale Ni mgeni hapa Tanzania?
Korogwe vijijini alichaguliwa Mndolwa kwa kura nyingi, wakapelekewa MTU mwingine.
2015 kule Zanzibar vijana walishiriki kwa kumchangia Seif. Mkafuta matokeo.
Haya Kawe mlitaka vijana wafanyeje ikiwa masanduku yaliyojaa kura za wizi tuliyaona.

Mshale aache kudhihaki vijana.
TWAWEZA Ni CCM Kama uvccm na UWT.
 
Huyu Mshale Ni mgeni hapa Tanzania?
Korogwe vijijini alichaguliwa Mndolwa kwa kura nyingi, wakapelekewa MTU mwingine.
2015 kule Zanzibar vijana walishiriki kwa kumchangia Seif. Mkafuta matokeo.
Haya Kawe mlitaka vijana wafanyeje ikiwa masanduku yaliyojaa kura za wizi tuliyaona.

Mshale aache kudhihaki vijana.
TWAWEZA Ni CCM Kama uvccm na UWT.
Anaipamba CCM ili ionekane haiibi kura kama panyarodi.
 
Tutashiriki uchaguzi pale tu wakurugenzi ambao ni makada wa CCM watakapoacha kusimamia.... Vinginevyo HAKUNA uchaguzi Tz siwezi kupoteza huo muda.
 

Dkt. Baruani Mshale: anajifanya hakuwahi kumsikia balozi Karume aliyesema ukweli kuwa CCM haijawahi kushinda uchaguzi Zanzibar, wenzake kiliwauma sana japo wanajua huo ndio ukweli.​

 

Baruani Mshale ambaye ni Mkurugenzi wa Mikakati na Mafunzo kutoka TWAWEZA amesema kitendo cha Watu na hasa Vijana kutoshiriki katika masuala ya Uchaguzi kinasababisha maamuzi yanayofikia kuchaguliwa kwa Viongozi ambao hawawataki.

Amesema "Tuchukulie mfano wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa pale mtaani kwenu au kijijini kwako mnatakiwa kuchagua viongozi. Kipindi cha Uchaguzi kimefika ukaona wanaogombea watafanya yaleyale tu, ukaamua usishiriki, kitakachotokea ni kwamba wale wachache watakaoshiriki watakwenda kukuchagulia wewe Kiongozi".

Akizungumza kupitia PowerBreakfast ya CloudsFM , Baruani ameongeza kuwa "Hukushiriki halafu yule atakapokuja kuwa Kiongozi ndio utaanza sasa kuona matokeo ya yule Kiongozi atakapofanya vitu ambavyo havikufurahishi wewe".

"Tuchukue miaka 10 iliyopita wakati wa mchakato wa katiba mpya Watanzania wengi sana walikuwa wakifuatilia, walikuwa wanajua kinachoendelea kuhusu mijadala ile na walikuwa wanajua kuna bunge la katiba mpya limekaa na linajadili kwa sababu ilikuwa linaoneshwa katika vyombo vya habari.

"Baada ya uchaguzi wa mwaka 2015 ilitamkwa wazi kwamba hata bunge live halikuwepo kwahiyo wananchi wasingeweza kuona bunge lao linajadili nini, masuala muhimu sana kwao. Pia ilitamkwa na Kiongozi aliyekuwepo kwamba uchaguzi ulikuwa umekwisha siasa ziwekwe kando tushughulike na shughuli za maendeleo"

"Watu wengi wanaogombea nafasi za uongozi wanatuaminisha kwamba wao ndio watakuwa mwarobaini wa matatizo ambayo yapo pale, wakati ushiriki thabiti wa mwananchi ni kitu muhimu sana katika hayo maendeleo.

"Bila ushiriki wa mwananchi unaweza ukafikiri wewe hivi ulivyoviweka ndio vipaumbele vya kero hasa zinazowakabili wananchi wa lile eneo lakini kumbe Wana kero zao.Ili kuleta maendeleo ya kweli ni muhimu kuchagiza ushiriki mzuri wa wananchi"

"Mfano wa uchaguzi wa serikali za mitaa pale mtaani kwenu au kijijini kwako manatakiwa kuchagua viongozi kipindi cha uchaguzi kimefika ukaona kwamba hao wanaogombea wataleta yaleyale tu, ukaamua wewe usishiriki kitakachotokea ni kwamba wale wachache watakaoshiriki watakwenda kukuchagulia wewe Kiongozi"


View attachment 2867252
Kama Sanduku la kura haliheshimiwi,

Kura ya nini?
 
hivi Watu wanaoongea haya maneno hua wanaongea kwa kutokujua au ni just kujizima data tu ?

toka lini kura ikaamua nani awe kiongozi na nani asiwe kiongozi au kila kitu kinapangwa na system ?
 
Ni kweli lakini sio jambo la kufurahia.

Kama utaitwa kiongozi wa watu wasiokutambua kuwa ni kiongozi wao utakuwa na tija gani kwao? Utaongoza misitu, milima, madini na mbuga za wanyama? Toka lini soka lisilo na watazamaji likawa na tija kwa vilabu,kocha, refa, wachezaji au mashabiki?

Ni wazi kuwa nchi itaendelea kuporomoka na kudumaa kwenye kila nyanja ya maisha.
 
Kwani viongozi wote tuna mamlaka ya kuwachagua!!! Tunachagua WAWAKILISHI / REPRESENTATIVES TU ambao ni Wabunge na madiwani wasio na mamlaka yeyote ya kuamuru hata barabara ijengwe ikajengwa.
 
Back
Top Bottom