Dk. Nchimbi tulia! Mwosha huoshwa

network ya wazinzi wa CCM wakiwa dodoma inaongozwa na wabunge na wafuatao; nchimbi, ngereja, mwan'gonda,na mbunge mmoja wa majimbo ya DSM nakamilisha data zangu nitawamwagia
cheche!sasa hawa si ndio wanotegemewa kuongoza sisiemu ya kesho?au ndio vijana damu inachemka?EL anamchukua kigori gani..teh teh
 
Simshangai Nchimbi kudai Slaa hana, uzalendo. Hivi uzalendo ni nini? Mzalendo ni Karamangi aliyeenda ku sign mkataba hotelini? au ni Balali ni mafisadi wenzake wanaoibiia nchi hii mabilion ya $? Au ni Midhihiri alyetoa hoja ya kufukuzwa bungeni Zitto akitetea maslahi ya nchi.

Zama hizi, kwa tafsiri ya SISIEM mzalendo ni yule FISADI na mwenye degree fake km Nchimbi. Ukiwa msafi na muadilifu wewe sio mzalendo.

Ni bora misaada isije kwani hata ikija inaishia kwenye mifuko ya mifasadi. Slaa Endeleeea!!!!!!!!!

Nafikiri hii serikali ya JK imejaa wasanii tupu hawajui wanachoongea kwani maneno yao wanayotoa yanawasuta wao wenyewe.
 
Wazee heshima yenu wakuu!
Najua huyu minister anapita hapa jamvini kila siku.So mimi namshauri kutumia opportunity anazozipata za kufunga domo lake kuliko kupayuka ovyo.He's a public figure now so asije akawaacha watu wanaomuita Idiot wakaendelea kufanya conclussion hiyo kitu ambacho angekaa kimya na kufunga domo lake asingedharaulika.WATCH OUT!
 
source mwananchi
RAIS Jakaya Kikwete, jana aliwasili nchini akitokea Marekani na kuwahoji mawaziri waliofika kumpokea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere akimtaka kila mmoja, kueleza mkoa aliotembelea kuwaeleza wananchi kuhusu utekelezaji wa bajeti ya serikali ya mwaka wa fedha wa 2007/2008.

Rais ambaye alikuwa nchini Marekani kwa ziara ya wiki tatu ambapo pamoja na mambo mengine alihudhuria Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, aliwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam saa 8:00 mchana jana kwa ndege ya Shirika la Ndege la Emirates.

Baada ya kuwasili uwanjani hapo, alianza kuwauliza mawaziri hao, mmoja baada ya mwingine ambapo kila mmoja alimjibu kulingana na mkoa aliotembelea.[/

Baadhi ya mawaziri hao ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge), Dk Batilda Burian, Waziri wa Fedha, Zakhia Meghji, Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano), Dk Hussein Mwinyi, Naibu Waziri wa Miundombinu, Dk Maua Daftari, Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Omar Yusuf Mzee.

Baada ya mahojiano hayo, alikwenda moja kwa moja kwa wananchi na kuwapungia mkono kabla ya kupanda katika gari lake na kuondoka uwanjani hapo.

kama muungwana alifanya hivyo (kama sio propaganda za magazeti),
hakuna mabadiliko yatakayotokea,
Nahisi hesabu zake ni 2+2=22.
tunasafari ndefu kuelekea utawala bora.nguvu ya wananchi inahitajika (tukatae tuseme hapana pale kwenye uongo)
Ndio maana kina nchimbi wanakiburi na jeuri kwani wanaridhaa ya muungwana,
 
wewe kumbe unajua magazeti ni propaganda! huna nafasi dunia ya leo, gazeti la mwananchi sio la udaku acha unafiki wa CCM
una ushahidi,sio la CCM ila waanadishi wanaweza kutumiwa na kina Rostam na EL(BA theatre Arts) kuandika habari za kuwapamba hawa wasanii,
 
Ukiijua Vyema Background Ya Nchimbi Huwezi Shangaa Hayo Anayoyaongea.
At Once Tulikuwa Nae Chuo Uyo.
 
1. Tulisema ziara za raisi zipunguzwe ili kuokoa gharama, sio kwamba zisitishwe kabisa. CAG alionyesha gharama halisi ambazo raisi angeweza ku save kama angepunguza safari hizi. Sasa kwa nini huyu Nchimbi anakuwa nunda wa kushindwa kuelewa suala la mantiki ndogo kama hili? Huyu ni Dk kweli?

2. Nilikuwa sijajua kuwa Kikwete huwa akiwa Ikulu "analinda Njiwa". Nchimbi kanifumbua macho! Sie wadanganyika tunashinda mashambani yeye anashinda ikulu kulinda njiwa? Kwa nini asiungane na sie katika kuchimba mitaro ya kunyweshea mashamba yetu? Ama Nchimbi hapa aliropoka? Naomba jibu wanakijiji!

3. Kasi ya maendeleo anayoiongelea Nchimbi ni ipi? Kama ni ndege haijapaa na wala hata uwanjani haipo! Hizi shule za kata anazozisema tumejenga sisi wavuja jasho kwa nguvu zatu na michango yetu. Na shule hizi bado hazina walimu wa kutosha, hazina maabara za kisasa, hazina vitabu vya kutosha, na nyingine madarasa hayajakamilika. Tuwasifu wao kwa lipi? Hapa napo kachemsha!

4. Barabara anazozisema Nchimbi zilianza ujenzi wake awamu ya tatu enzi za Magufuli, ujenzi ukasuasua baada ya awamu ya nne kuingia madarakani. Kwa nini? Kama barabara ya Sam Nujoma tu iliyo Dar es Salaam, yenye kilometa zisizozidi sita inachukua karibu mikaka miwili kukamilika, na zile za mikoani zenye mamia ya kilometa anatarajia zitakamilika? Kwa nini wananchi wa Mwanza na Bukoba hulazimika kupita nchi jirani ili kwenda mikoani kwao, kama barabara anazozisema ziko njema? Kwa nini Rukwa haijaunganishwa kwa lami na mikoa jirani yake hadi leo, kama barabara zinajengwa kwa kasi anayoisema?
Wakati mwingine kama hana cha kuongea no bora akakaa kimya, kuliko kuropoka.

5. Tumesema, na tunarudia kusema kuwa, kama wao sisiemu wanasema Slaa ni mzushi, basi watupatie takwimu za hali ya uchumi ambazo ni sahihi, na watuonyeshe mikataba yote ili tuamini kuwa anachosema Slaa sio sahihi. Kwa nini wao wanaona hili gumu? Eti mikataba ni mali ya sirikali. Aibu!
Tunamsubiri Nchimbi afike kwetu aone atakavyozomewa.
Mungu Ibariki Tanzania.
 
Na Nkuzi Mhango Nkwazi
Source; Tanzania Daima


KWANZA nampa pole Profesa Juma Kapuya, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, kwa ajali iliyompata.

Hata hivyo binafsi napenda kusema wazi kwamba Oktoba 3 nilifumbuka macho baada ya vyombo vya habari kuripoti kuwa Waziri Juma Kapuya aliibwa mali fulani. Viliendelea kuelezea kuwa wizi huo ulitokea huko Longido kwenye mgodi wake wa rubi.

Binafsi nilishtuka kusikia kuwa kumbe Kapuya ni milionea anayemilki mgodi. Japo sheria zetu hazizuii waziri kuwa na mali, kuna maswali yalijitokeza kutokana na taarifa hii inayoweza kuonekana ya kawaida.

Swali la kwanza, je, Waziri Kapuya alipataje mgodi huu hata bila kuwapo matangazo? Je, ni mawaziri au vigogo wengine wangapi kama yeye wanaomilki migodi hata mali nyingine kimsingi zinazopaswa kujulikana zilivyopatikana?

Je, hii inaweza kuwa ndiyo staili ya watawala wetu kutumia uwekezaji na ubinafsishaji kujipatia na kumiliki mali nyingi na za thamani binafsi? Je, aliwezaje kumiliki mgodi iwapo kila siku wachimbaji wetu wadogo wadogo wanatimuliwa?

Je, ni yale yale ya Kiwira? Je, wananchi wanaichukuliaje hii hali wakiangalia jinsi maslahi yao yanavyozidi kuhujumiwa na baadhi ya watawala ama wawekezaji kutokana na kutamalaki kwa rushwa na kulindana hasa kwenye sekta ya madini?

Kwa anayekumbuka tume iliyoundwa na Mzee Benjamin Mkapa kuhusiana na kadhia ya ugomvi baina ya wachimbaji wadogo wadogo na wawekezaji kule Mirerani, atakuwa anakumbuka kulivyozuka tuhuma kuwa mkuu wa zamani wa majeshi ya ulinzi, Jenerali Robert Mboma, hakufaa kuwa mwenyekiti wa tume hiyo kutokana kuwa na vitalu vya madini huko. Uvumi ulikwenda mbali hata kuhusisha maofisa wengine waandamizi wa Serikali ya Awamu ya Tatu na familia zao.

Kutokana na wananchi kuchukulia mambo kijuujuu, kombe lilifunikwa na mwanaharamu akapita. Pia kuna gazeti la kila siku lililowahi kuripoti juu ya hujuma kwa jeshi la wananchi wakati jenereta kubwa ilichukuliwa na kigogo wa jeshi hilo wa zamani, kiasi cha kuwa analitumia kwenye miradi yake binafsi. Tunakumbuka ilikuwa ni gazeti la ‘Tazama’ la mwaka 2004. kutokana na ubabe na ukosefu wa uwazi na uhuru wa kweli wa vyombo vya habari, suala hili nalo liliuawa kimya kimya!

Turejee kwa Kapuya na kumilki mgodi wa rubi.

Kwa mtu anayechambua kila kitu kwa kina, habari kuwa Kapuya anamilki mgodi si ndogo wala ya kawaida. Inaamsha maswali mengi kuliko majibu. Hasa ikizingatiwa kuwa mwezi Septemba kuliripotiwa habari kuwa sekta ya utalii inamilikiwa na vigogo na familia na kampuni zao binafsi. Walitajwa Waziri Muhammed Seif Khatib na kampuni yake, Rashidi Kawawa na wengine wazito.

Hii haikuwa habari nyepesi wala ya kupuuzia bali kungoja kuona mengine yatakayoibuka kama hili la Kapuya na kumiliki mgodi.

Ukiongeza na taarifa za hivi karibuni juu ya kampuni mizengwe na yenye kila aina ya utata ya Tangold na mali na fedha za umma zinamilikiwa na watu binafsi kiasi cha kuweza hata kuruhusiwa kisheria kuhamishia hisa zao kwa wake na watoto zao, unajenga shaka. Ukiunganisha na madudu kama Meremeta na upuuzi mwingine unazidi kuhoji kuhoji na kuhoji bila kupata jibu bali kuzidi kuuliza!

Ukichanganya na ugumu wa watawala kutaja mali zao, unaweza hata kufikia hitimisho kuwa kuna kitu tena kikubwa ambacho kimsingi ni hatari kwa maslahi ya umma.

Kama tulivyoeleza hapo juu kuwa si vibaya wakubwa kumiliki mali. Lakini wanapozifanya kuwa kificho lazima mtu ajiulize inakuwa hivyo kwa kuogopa nini kama siyo jinai nyuma ya upatikanaji wa mali hizo?

Rais Mwai Kibaki na familia yake wana makampuni yapatayo 64. Makamu wa Rais Moody Arthur Awori na familia yake wana viwanda. Kila Mkenya anajua hivyo na hana shaka wala pingamizi. Lakini inapokuja kwetu ambako ukweli ni kwamba tulikuwa wajamaa jana, maswali na mashaka yanakuwa mengi.

Je, hawa wanaotuaminisha kuwa uwekezaji na ubinafsishaji unalipa ni kwa sababu wamejihudumia wao kwanza? Unalipa kwao au kwetu? Je, hii haiwezi kuathiri maslahi ya umma inapotokea kukawa na mgongano wa kimaslahi baina ya mali hizi na za umma?

Juzi juzi ulitoka uvumi kuwa Benki ya M ni ya Mkapa. Waliokanusha walikanusha na umma ukanyamaza! Waliokanusha hata hivyo walituachia faida kuwa Benki ya M ni mpangaji kwenye jumba la Mkapa.

Hapo maswali ndipo yaliopanza kujengeka. Je, Mkapa alijenga lini jumba hilo? Alikuwa ameliorodhesha kwenye mali zake alizotangaza wakati wa mkwara wa kutangaza mali? Alilipata alipoingia madarakani kwa kutumia urais? Je, ana majumba mengine mangapi kama haya? Kwa nini ayapate kisirisiri? Kuna nini hapa? Je, ni mawaziri na maofisa wengine wa serikali wana majumba hata mahoteli ambayo umma hauyajui ili upime kama yanalingana na mishahara yao? Je, wanaficha kwanini?

Kuna haja ya serikali kukubali haraka maofisa watangaze mali zao umma uzijue kuepusha kutumia uficho huu kutuibia wakijinufaisha sisi tukiendelea kuteseka. Pia kuna haja ya kubadili katiba yetu itamke wazi kuwa tunajenga taifa la kichuuzi badala ya kijamaa. Maana mtu anaweza akatoka siku moja akataka hizi mali za kificho zitaifishwe kwa sababu nchi ya kijamaa hairuhusu watendaji wake kujilimbikizia mali.

Umma ungetaka kujua licha ya jinsi walivyopata mali hizi, kama mali zao zinaingiliana na shughuli zao za kiserikali. Kwa mfano, mhusika huwa anatembelea zilipo mali yake kwa gharama za serikali? Je, kuna miundombinu kama barabara hata visima vya maji alivyoelekeza huko kutokana na kuwapo mali zake? Je kuna magari au vitendea kazi hata watumishi wa umma vilivyopo au waliopo chini yake anavitumia kwenye miradi yake? Na mambo mengine kama hayo.

Umma ungetaka kujibu maswali haya. Maana wahusika ni binadamu sawa na wengine. Mfano mmoja rahisi ni nchini Kenya. Rais Kibaki alipoingia madarakani alitoa tenda ya kujenga barabara kwenda kwenye jimbo lake. Hii ilichukuliwa na Wakenya kama kujihudumia kwa mgongo wa umma.

Hata nchini mwetu kuna waziri mmoja kutoka mkoa mmoja wa kaskazini aliyeshutumiwa kupeleka umeme milimani kwao kwa sababu tu alikuwa anatokea huko na hii ilimsaidia kuchaguliwa mbunge wa eneo hili kwa muda mrefu.

Lakini alifanya yote kwa kuwahujumu wengine. Hata kuna baadhi ya mikoa, wilaya hata majimbo ya uchaguzi yamepewa hadhi yake kutokana na kujuana au kulinda nafasi za watu kisiasa. Hivyo kama hali hii inaweza kufanyika hata kwenye mambo ya siasa, inakuwaje kwenye miradi ya wakubwa? Je, hii ni mojawapo ya usiri unaozunguka mali za watawala wetu?

Je, hawa wanaposema ubinafsishaji una manufaa kwa taifa tuwaamini kwa vile wamefanikiwa wao wakati sisi tunaendelea kuangamia? Je, huu si ubinafsi na ufisi unaopewa jina zuri la ubinafsishaji na urekebishaji wa mashirika ya umma?

Kapuya na wengine kama hawa watoe maelezo. Vyombo vya habari vianze kuziwinda mali za namna hii na kuzianika. Pia wananchi wasiwe wanachukulia kwa wepesi au ukawaida habari kama hizi ambazo zina maslahi kwao.

nkwazigatsha@yahoo.com
 
Dk. Nchimbi tulia, mwosha huoshwa

Irene Mark

ALHAMISI ya wiki hii, Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Dk. Emmanuel Nchimbi, alinukuliwa na vyombo vya habari akitoa tamko zito, tamko la kuonya, la kuwachukulia hatua viongozi wa chama na serikali wanaojaribu kuingiza mikono yao katika uchaguzi wa chama hicho.

Dk. Nchimbi, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, alielekeza kauli yake hiyo kwa viongozi wote wa juu ndani ya CCM na serikali walio nje ya umoja huo wenye nia ya kuvuruga demokrasia wakati wa uchaguzi wa umoja huo.

Katika kile kinachoonyesha kukerwa kwa kiongozi huyo na vitendo vya wenzake, serikali na ndani ya chama, alionya kuwa atawaaibisha wote watakaotia dosari kwa namna moja ama nyingine uchaguzi huo ulioanza juzi katika ngazi ya mashina nchini kote.

Dk. Nchimbi, Mwenyekiti anayemaliza muda wake mwezi Desemba mwaka huu, alisema kwa kujiamini, namnukuu: "Tunawapa tahadhari bila kujali ni viongozi wa serikali au wa chama, waache tabia ya kuingilia uchaguzi na wasithubutu kufanya hivyo. Huu ni ushauri wa hisani, wasije wakatembea macho chini kutokana na aibu watakayoipata."

Hili ni onyo zuri kwa wenye nia hiyo hasa linapotolewa na kiongozi wa aina ya Dk. Nchimbi ambaye baadhi ya wachambuzi wa mambo walitafsiri kuwa ni sawa na Dk. Nchimbi kujinyooshea kidole mwenyewe; wengine wanasema ni kauli ya ‘mfa maji asiyeisha kutapatapa.'

Ninakubaliana na wachambuzi hawa. Kwanza, kwa sababu sitaki kuamini kuwa Dk. Nchimbi ni mwepesi wa kusahau kiasi hicho. Historia ya kisiasa ya Dk. Nchimbi inaonyesha kuwa katika kipindi chake miaka kumi ya uongozi ndani ya umoja huo, Dk. Nchimbi amekuwa na makundi na ni muasisi wa makundi ndani ya umoja huo na katika CCM kwa ujumla.

Tafsiri ya haraka inayojitokeza kwa historia yake kisiasa na kauli yake hii ni kwamba aliokuwa akicheza nao ngoma moja sasa wamemgeuka, wamemzidi kete, wamemuacha akiwayawaya.

Tujikumbushe usemi huu: ‘Ukiua kwa upanga, utakufa kwa upanga.' Hili linajidhihirisha kwa Nchimbi ambaye zipo kumbukumbu zinazoonyesha kuwa siku chache kabla na baada ya kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Vijana (UVCCM), hayati Amina Chifupa, alituhumiwa kuwa chanzo cha kusambaratika kwa ndoa ya mbunge huyo kijana. Kisa siasa!

Zilikuwa tuhuma mbaya kwa Dk. Nchimbi lakini alikataa kuzijibu. Tuhuma zilionyesha kuwa aliiona dhamira ya Amina ya kuwania uongozi wa juu ndani ya UVCCM, hivyo aliamua kwa makusudi kumuundia zengwe litakalomwondoa kwenye ulingo wa siasa kijana mwenzake.

Tukiipitia historia isiyokuwa rasmi kuhusu matukio yaliyoambatana na kifo cha Amina, inaonyesha kuwa ni Dk. Nchimbi aliyeelezwa kumbeba Amina katika hatua zake za mwanzo kuingia katika siasa. Hili hajawahi kulikanusha.

Inaelezwa zaidi kwamba ni yeye Dk. Nchimbi aliyehakikisha Amina anasimikwa kuwa kamanda wa vijana kabla ya kumwingiza kwenye mchakato mgumu wa kuwania uwakilishi wa kundi hilo huku akimpigia kampeni za chini kwa chini akishirikiana na Kapteni mstaafu, John Komba.

Kwa waliowashuhudia wanasiasa hao vijana, siku za mwanzo baada ya kuapishwa Amina kuwa mbunge, walikuwa bega kwa bega katika kupiga hatua kadhaa za kisiasa.

Haikuwa siri, Dk. Nchimbi alijitolea kuwa ‘Godfather' wa Amina huku wengi tukiamini kuwa, alifanya hivyo kwa nia njema kutokana na ukweli kwamba alikuwa kiongozi wake katika UVCCM.

Historia hiyo hiyo inaonyesha kuwa Dk. Nchimbi ni mmoja wa wanasiasa walioongoza mbinu za hila za kumwingiza Amina na kumfanya akubalike ndani ya UVCCM katika kipindi kifupi.

Katika hatua nyingine, inaonyesha kuwa kwa sababu anazozijua mwenyewe, Dk. Nchimbi aliamua kumpoteza Chifupa kutoka katika anga za siasa kwa kumtengenezea zengwe. Kweli, alifanikiwa.

Kilichomponza Amina ni nguvu alizopata katika medani za siasa, nguvu hizo zilimwogofya mwenyekiti wake, akaamua kumshughulikia. Hata hilo, mbali na kuandikwa kwa mapana na marefu, Dk. Nchimbi hakulikanusha, jambo lililothibitisha kuwa kweli alimshughulikia mwanafunzi wake huyo kisiasa.

Wakati haya yakiwa bado katika kumbukumbu za wengi, Dk. Nchimbi anaibuka akilalamika kuhusu kuwapo kwa mbinu chafu za kuwabeba wapendwa wa viongozi wa ndani na nje ya UVCCM, kwa lengo la kuwapa madaraka huku akisisitiza kuwa vijana hawapendi viongozi wa ‘kuchongwa'. Kilio cha ajabu!

Maneno mengine ya Dk. Nchimbi yanaduwaza. Kwamba upo uwezekano wa uchaguzi huo kugubikwa na vitendo vya rushwa, kupakana matope na kuingilia uchaguzi kwa masilahi binafsi. Ni maneno yanayoacha maswali mengi kuliko majibu.

Kimsingi, Dk. Nchimbi ameanza kushughulikiwa na wanamtandao wenzake wanaoendekeza siasa za makundi na kuua demokrasia ya kweli ndani ya CCM na taifa zima.

Kwa wafuatiliaji wa siasa za hapa nyumbani, watakubaliana na mimi kuwa CCM ni kinara wa propaganda, kashfa, siasa za mizengwe na kupakana matope, hasa katika vipindi vya chaguzi mbalimbali.

Dk. Nchimbi ni mmoja wa wanamtandao, kundi linaloaminika kuwa kinara wa siasa za kuchafuana na kupakana matope, hivyo si rahisi kuamini kwamba hivi sasa anachukizwa na siasa hizo. Kinachoingia akilini ni kwamba amezidiwa nguvu na kundi jingine la wanasiasa linalompinga ndani ya chama chake.

Na kama anavyowalalamikia sasa wanasiasa na viongozi wenzake wanaotaka kuharibu uchaguzi wa UVCCM, ni hivyo hivyo alivyolalamikiwa yeye na wanachama wenzake ndani ya UVCCM hadi ikamlazimu Mwenyekiti wa zamani wa CCM, Benjamin Mkapa, kumtenganisha na wana UVCCM kwa kumpa wadhifa wa mkuu wa wilaya.

Aidha, dhambi anayoikemea sasa Dk. Nchimbi aliwahi kuhusishwa nayo wakati akitetea nafasi ya uenyekiti kwa awamu ya pili, baada ya kutuhumiwa mambo mazito hadharani na aliyekuwa mgombea mwenzake, Jane Mihanji.

Kwa kauli hii ya Dk. Nchimbi, mwanasiasa asiyependa kuzungumza na vyombo vya habari, ni wazi kwamba sasa anaelekea ukingoni, siku zake katika jukwaa la siasa zinahesabika baada ya kujijengea maadui wengi ndani na nje ya chama chake.

Dhambi aliyoshiriki kuifanya kwa muda mrefu sasa imemgeukia yeye, ameamua kukimbilia katika vyombo vya habari, ambako nafasi ya ukombozi ni finyu zaidi, kwa sababu iwapo mabingwa wenzake wa siasa za kupakana matope na kuchafuana wataamua kumshambulia kupitia vyombo vya habari, basi siku za uhai ndani ya siasa za kibabe na kuchafuana sitazidi kupungua.

Source: Tanzania Daima

Maswali ya kizushi: Hivi Mh. Nchimbi siku hizi yuko kundi gani? Maana Mtandao ndiyo huo umeishayoyoma, na kinachoandaliwa ndani ya UVCCM kwenye huu uchaguzi wa mwaka huu ni "Focus 2010" au "Focus 2015"! Kuna mtu yeyote ambaye ameishaonyesha nia ya kutaka kumrithi Nchimbi? Kuna kipindi ilisemekana kwamba alikuwa na mtu wake, ni yupi huyo aliyeandaliwa kumrithi?
 
Dk. Nchimbi tulia, mwosha huoshwa

Irene Mark

ALHAMISI ya wiki hii, Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Dk. Emmanuel Nchimbi, alinukuliwa na vyombo vya habari akitoa tamko zito, tamko la kuonya, la kuwachukulia hatua viongozi wa chama na serikali wanaojaribu kuingiza mikono yao katika uchaguzi wa chama hicho.

Dk. Nchimbi, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, alielekeza kauli yake hiyo kwa viongozi wote wa juu ndani ya CCM na serikali walio nje ya umoja huo wenye nia ya kuvuruga demokrasia wakati wa uchaguzi wa umoja huo.

Katika kile kinachoonyesha kukerwa kwa kiongozi huyo na vitendo vya wenzake, serikali na ndani ya chama, alionya kuwa atawaaibisha wote watakaotia dosari kwa namna moja ama nyingine uchaguzi huo ulioanza juzi katika ngazi ya mashina nchini kote.

Dk. Nchimbi, Mwenyekiti anayemaliza muda wake mwezi Desemba mwaka huu, alisema kwa kujiamini, namnukuu: “Tunawapa tahadhari bila kujali ni viongozi wa serikali au wa chama, waache tabia ya kuingilia uchaguzi na wasithubutu kufanya hivyo. Huu ni ushauri wa hisani, wasije wakatembea macho chini kutokana na aibu watakayoipata.”

Hili ni onyo zuri kwa wenye nia hiyo hasa linapotolewa na kiongozi wa aina ya Dk. Nchimbi ambaye baadhi ya wachambuzi wa mambo walitafsiri kuwa ni sawa na Dk. Nchimbi kujinyooshea kidole mwenyewe; wengine wanasema ni kauli ya ‘mfa maji asiyeisha kutapatapa.’

Ninakubaliana na wachambuzi hawa. Kwanza, kwa sababu sitaki kuamini kuwa Dk. Nchimbi ni mwepesi wa kusahau kiasi hicho. Historia ya kisiasa ya Dk. Nchimbi inaonyesha kuwa katika kipindi chake miaka kumi ya uongozi ndani ya umoja huo, Dk. Nchimbi amekuwa na makundi na ni muasisi wa makundi ndani ya umoja huo na katika CCM kwa ujumla.

Tafsiri ya haraka inayojitokeza kwa historia yake kisiasa na kauli yake hii ni kwamba aliokuwa akicheza nao ngoma moja sasa wamemgeuka, wamemzidi kete, wamemuacha akiwayawaya.

Tujikumbushe usemi huu: ‘Ukiua kwa upanga, utakufa kwa upanga.’ Hili linajidhihirisha kwa Nchimbi ambaye zipo kumbukumbu zinazoonyesha kuwa siku chache kabla na baada ya kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Vijana (UVCCM), hayati Amina Chifupa, alituhumiwa kuwa chanzo cha kusambaratika kwa ndoa ya mbunge huyo kijana. Kisa siasa!

Zilikuwa tuhuma mbaya kwa Dk. Nchimbi lakini alikataa kuzijibu. Tuhuma zilionyesha kuwa aliiona dhamira ya Amina ya kuwania uongozi wa juu ndani ya UVCCM, hivyo aliamua kwa makusudi kumuundia zengwe litakalomwondoa kwenye ulingo wa siasa kijana mwenzake.

Tukiipitia historia isiyokuwa rasmi kuhusu matukio yaliyoambatana na kifo cha Amina, inaonyesha kuwa ni Dk. Nchimbi aliyeelezwa kumbeba Amina katika hatua zake za mwanzo kuingia katika siasa. Hili hajawahi kulikanusha.

Inaelezwa zaidi kwamba ni yeye Dk. Nchimbi aliyehakikisha Amina anasimikwa kuwa kamanda wa vijana kabla ya kumwingiza kwenye mchakato mgumu wa kuwania uwakilishi wa kundi hilo huku akimpigia kampeni za chini kwa chini akishirikiana na Kapteni mstaafu, John Komba.

Kwa waliowashuhudia wanasiasa hao vijana, siku za mwanzo baada ya kuapishwa Amina kuwa mbunge, walikuwa bega kwa bega katika kupiga hatua kadhaa za kisiasa.

Haikuwa siri, Dk. Nchimbi alijitolea kuwa ‘Godfather’ wa Amina huku wengi tukiamini kuwa, alifanya hivyo kwa nia njema kutokana na ukweli kwamba alikuwa kiongozi wake katika UVCCM.

Historia hiyo hiyo inaonyesha kuwa Dk. Nchimbi ni mmoja wa wanasiasa walioongoza mbinu za hila za kumwingiza Amina na kumfanya akubalike ndani ya UVCCM katika kipindi kifupi.

Katika hatua nyingine, inaonyesha kuwa kwa sababu anazozijua mwenyewe, Dk. Nchimbi aliamua kumpoteza Chifupa kutoka katika anga za siasa kwa kumtengenezea zengwe. Kweli, alifanikiwa.

Kilichomponza Amina ni nguvu alizopata katika medani za siasa, nguvu hizo zilimwogofya mwenyekiti wake, akaamua kumshughulikia. Hata hilo, mbali na kuandikwa kwa mapana na marefu, Dk. Nchimbi hakulikanusha, jambo lililothibitisha kuwa kweli alimshughulikia mwanafunzi wake huyo kisiasa.

Wakati haya yakiwa bado katika kumbukumbu za wengi, Dk. Nchimbi anaibuka akilalamika kuhusu kuwapo kwa mbinu chafu za kuwabeba wapendwa wa viongozi wa ndani na nje ya UVCCM, kwa lengo la kuwapa madaraka huku akisisitiza kuwa vijana hawapendi viongozi wa ‘kuchongwa’. Kilio cha ajabu!

Maneno mengine ya Dk. Nchimbi yanaduwaza. Kwamba upo uwezekano wa uchaguzi huo kugubikwa na vitendo vya rushwa, kupakana matope na kuingilia uchaguzi kwa masilahi binafsi. Ni maneno yanayoacha maswali mengi kuliko majibu.

Kimsingi, Dk. Nchimbi ameanza kushughulikiwa na wanamtandao wenzake wanaoendekeza siasa za makundi na kuua demokrasia ya kweli ndani ya CCM na taifa zima.

Kwa wafuatiliaji wa siasa za hapa nyumbani, watakubaliana na mimi kuwa CCM ni kinara wa propaganda, kashfa, siasa za mizengwe na kupakana matope, hasa katika vipindi vya chaguzi mbalimbali.

Dk. Nchimbi ni mmoja wa wanamtandao, kundi linaloaminika kuwa kinara wa siasa za kuchafuana na kupakana matope, hivyo si rahisi kuamini kwamba hivi sasa anachukizwa na siasa hizo. Kinachoingia akilini ni kwamba amezidiwa nguvu na kundi jingine la wanasiasa linalompinga ndani ya chama chake.

Na kama anavyowalalamikia sasa wanasiasa na viongozi wenzake wanaotaka kuharibu uchaguzi wa UVCCM, ni hivyo hivyo alivyolalamikiwa yeye na wanachama wenzake ndani ya UVCCM hadi ikamlazimu Mwenyekiti wa zamani wa CCM, Benjamin Mkapa, kumtenganisha na wana UVCCM kwa kumpa wadhifa wa mkuu wa wilaya.

Aidha, dhambi anayoikemea sasa Dk. Nchimbi aliwahi kuhusishwa nayo wakati akitetea nafasi ya uenyekiti kwa awamu ya pili, baada ya kutuhumiwa mambo mazito hadharani na aliyekuwa mgombea mwenzake, Jane Mihanji.

Kwa kauli hii ya Dk. Nchimbi, mwanasiasa asiyependa kuzungumza na vyombo vya habari, ni wazi kwamba sasa anaelekea ukingoni, siku zake katika jukwaa la siasa zinahesabika baada ya kujijengea maadui wengi ndani na nje ya chama chake.

Dhambi aliyoshiriki kuifanya kwa muda mrefu sasa imemgeukia yeye, ameamua kukimbilia katika vyombo vya habari, ambako nafasi ya ukombozi ni finyu zaidi, kwa sababu iwapo mabingwa wenzake wa siasa za kupakana matope na kuchafuana wataamua kumshambulia kupitia vyombo vya habari, basi siku za uhai ndani ya siasa za kibabe na kuchafuana sitazidi kupungua.

Source: Tanzania Daima

Maswali ya kizushi: Hivi Mh. Nchimbi siku hizi yuko kundi gani? Maana Mtandao ndiyo huo umeishayoyoma, na kinachoandaliwa ndani ya UVCCM kwenye huu uchaguzi wa mwaka huu ni "Focus 2010" au "Focus 2015"! Kuna mtu yeyote ambaye ameishaonyesha nia ya kutaka kumrithi Nchimbi? Kuna kipindi ilisemekana kwamba alikuwa na mtu wake, ni yupi huyo aliyeandaliwa kumrithi?

Nchimbi anataka kumpaya kiongozi ambaye atakuwa anawajibika kwake. Kwa maana nyingine anataka kuifanya Kin Maker wa vijana na baadaye kutumia remote kuwageuza anavyo taka kwa masalhi yake siku zijazo .Hili liko wazi na Nchimbi hawezi kutoa tamko kama hili labda yeye akiandikiwa akawa anasoma kwa mara ya kwanza bila ya kutafakari .
 
Inabidi aachie ngazi maana ana vyeti vya elimu ya kubabaisha.

Mkuu KJ unakumbuka kama ile tume iliundwa kuchunguza vyeti hivi vya waheshimiwa imefikia wapi au hata kama imekufa imefia wapi? It is disgusting kuona watu wanaendelea kupeta kwa kutumia vyeti wasivopata kutoka vyuo vinavotambulika..na hivyo kutia shaka uwezo wao kitaaluma
 
Mkuu KJ unakumbuka kama ile tume iliundwa kuchunguza vyeti hivi vya waheshimiwa imefikia wapi au hata kama imekufa imefia wapi? It is disgusting kuona watu wanaendelea kupeta kwa kutumia vyeti wasivopata kutoka vyuo vinavotambulika..na hivyo kutia shaka uwezo wao kitaaluma

Kwenye kundi la Nchimbi kuna Asha Kigoda ambaye kila Spika bila aibu anakazana kwa sauti kumwita Dr.Asha Kigoda .
 
kubwajinga bwana, unapenda ishu tata kama hizi.......ebu fafanua hilo suala la vyeti.

Nchimbi ana Online degree mbili toka kwenye chuo cha matapeli cha Commonwealth Open University. Ndio maana amefanya hiyo Ph.D anayojiitia Dr. kweye wakati ambao alikuwa Mzumbe akifanya Masters yake. A Genius???
 
Nchimbi ana Online degree mbili toka kwenye chuo cha matapeli cha Commonwealth Open University. Ndio maana amefanya hiyo Ph.D anayojiitia Dr. kweye wakati ambao alikuwa Mzumbe akifanya Masters yake. A Genius???

Hivi kwa nini huwsa hawabandiki tafiti zao kwenye tovuti ya bunge?
 
Back
Top Bottom