Dini ya Uislam iliwezaje kuenea kwa wingi "Sub Saharan Africa" ilhali waarabu hawakuwa na makoloni huko? Ni biashara pekee ama kuna njia nyingine?

Infantry Soldier

JF-Expert Member
Feb 18, 2012
15,893
16,317
Habari za wakati huu kaka na dada zangu wote wa humu jamiiforums.

Ndugu zangu watanzania;

Dini ya Uislam iliwezaje kuenea kwa wingi "Sub Saharan Africa" ilhali waarabu hawakuwa na makoloni huku? Ni kupitia biashara pekee ama kuna njia nyingine za ziada zilitumika?

Orodha ifuatayo ni baadhi tu ya nchi zilizopo katika eneo hilo la "Sub-Saharan Africa";

Angola, Benin, Botswana, Burkina Faso, Burundi, Cameroon, Central African Republic, Chad, Congo, Cote d'Ivoire, Eritrea, Namibia, Niger, Nigeria, Rwanda, Senegal, Sierra Leone, Somalia, South Africa pamoja na Tanzania.

1.jpg


Ninaomba kuanza kwa kusema kwamba, kwa msio nifahamu mimi Infantry Soldier ni mkristo mkatoliki ila ninafahamu fika ya kuwa dini ya uislamu ni dini safi sana tena ya watu waungwana kweli inayohubiri amani na upendo kama ilivyo dini ya kikristo. I love and respect all my muslim brothers and sisters out there.

KWA UFUPI KUHUSU UKOLONI NA KUENEA KWA UKRISTO BARANI AFRIKA
=====
Ushahidi wa kihistoria unaonyesha ya kuwa Waafrika walikuwa na mila nyingi za kitamaduni na kidini ambazo zilichangia pakubwa katika kuenea kwa haraka kwa dini ya Ukristo katika bara letu.

Wamishionari wa Magharibi waliamua kukataa au kuweka pembeni mila hizi, ambazo ilikuwa msingi wa imani zetu tangu zamani. Mifumo hii ya msingi ya mila na tamaduni ya Waafrika ilitoa msingi thabiti ambao Ukristo ulifikishwa (kwa kiingereza changu kibovu ninaweza kusema upon which Christianity was conceived), kueleweka na kupokelewa.

2.jpg


Hata hivyo, wamishionari wengine walijaribu kuaminisha watu kwamba hakuna mila na wala tamaduni za urithi kama huo wa kidini uliokuwepo kabla ya kuwasili kwao katika bara la Afrika miaka hiiiyoooo ya zamani.

Ukristo na ukoloni mara nyingi huhusishwa kwa karibu kwa sababu Uprotestanti (wasabato, anglikana, Lutheran) na Ukatoliki walishiriki kama dini za serikali/kidola za mamlaka ya kikoloni ya Ulaya na kwa njia nyingi zilitumika kama "matawi ya udini" ya tawala hizo za kikoloni.

Wakati Wazungu walipokuja kuitawala Afrika, hawakufanya hivyo tu kwa nguvu waliyoitumia dhidi ya Waafrika. Hapana. Ukoloni ulifanywa vema pia kwa matumizi ya dini, na haswa Ukristo na ndio maana mpaka sasa, Waafrika wengi hujitambulisha kama Wakristo.

3.jpg


Inaonekana dini imetumika zaidi kuathiri utambulisho wa mtu mweusi barani Afrika. Dini za jadi za Kiafrika zimetupiliwa mbali na zinaonekana kama za kipagani na za kishamba kwa asili.

Wakati kila mtu anastahili kuwa imani katika dini yake, ni dini hiyo hiyo ambayo imetumika kuvuruga historia ya Afrika haswa na ujio wa ubeberu na ukoloni ambao umejengwa juu yake.

Dini zilifanikisha jambo moja kubwa sana barani Afrika: kuwafundisha Waafrika weusi kuachana na mila zao zote na kuwezesha kuenea kwa tawala za kikoloni.

SWALI KUU: Dini ya Uislam iliwezaje kuenea kwa wingi "Sub Saharan Africa" ilhali waarabu hawakuwa na makoloni huko? Ni kupitia biashara pekee ama kuna njia nyingine ya ziada ilitumika?

4.jpg


USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
 
Kwani waarabu na wakoloni wapi walianza kuja??

Tuchukulie hapa bongo kama mfano;kati ya kiarabu,kijerumani na kiingereza kipi kimeinfluence kiswahili zaidi?

Ukijua hilo jibu basi utajua hao watu ndo wamekaa sana na kutawala sana Africa(ex. Zanzibar)

Lakini pia biashara ilichangia pakubwa
Lakini pia kwa nchi za North Afrika Upanga ulihusika
 
Kabla ya biashara ya utumwa
Kulikuwa na biashara za bidhaa nyingi sana
Usisahau biashara ya utumwa ilichangiwa na vita za makabila
Walioshindwa ndio walikamatwa wakauzwa..
Kabla ya baadae kuvurugika..

Lakini kulikuwepo na biashara mbalimbali nyingi
 
Kabla ya biashara ya utumwa
Kulikuwa na biashara za bidhaa nyingi sana
Usisahau biashara ya utumwa ilichangiwa na vita za makabila
Walioshindwa ndo walikamatwa wakauzwa..
Kabla ya baadae kuvurugika..

Lakini kulikuwepo na biashara mbalimbali nyingi
Ni kweli
kuna yale ma caravan routes and trades.

Hata mtume Muhammad alikuwa trader wa Caravan kabla hajawa mtume..Although alipokuwa mtume na kupata wafuasi alianza kuvizia hawa traders na kuwapokonya mali.
 
Njia kuu zilikuwa ni biashara pamoja na utawala na ilikuwa ukizingua kuwa arabized/islamized kirahisi; na ukang'ang'ania "ukafiri" wako basi walikuwa wanatumia maguvu tu - upanga! Waliichakaza karibu Ulaya nzima wakati wa Ottoman Empire na isingekuwa Jangwa la Sahara hata Sub Saharan Africa huku tungekuwa tunaongea Kiarabu tu
untitled-design-321.jpg
 
Aliyekwambia Muhammad (SAW) alikuwa trader wa caravan nani? Acha chuki zako za kijinga, unajitahidi kuonesha chuki zako za wazi kabisa dhidi ya uislam kila sehemu ilimradi uonekane, sijui ndivyo ulivyotumwa kufanya hivyo na mabasha wako!?

Sent from my Infinix X573 using JamiiForums mobile app
Ndo ulivyofundishwa huko kanisani
Ndugu zanguni Samahani kama ninawakwaza mkisikia jina muhammad..lakini hapa sio msikitini na wote tupo kwa ajili ya kujifunza So napomtaja Muhammad(saw) Simtaji kama nabii au religional figure bali namtaja kama historical figure..na ndiyo muktadha wa hii mada.

Nashangaa mnakasirika kusikia Muhammad alikuwa trader kuliko kusikia alivamia traders.

Furthermore kama hamjui Hata mke wake wa kwanza Bi Khadija(aliyemzidi miaka 15) alikuwa boss wake kwenye biashara ya trade.Bi khadija alimuajiri Muhammad kwasababu alisikia story zake kuwa ni muaminifu na alipewa nickname "Al-amin" baadae Muhammad akaongeza ukaribu akamuoa.
Muhammad alisafiri nchi mbalimbali(Syria,Yemen etc.) na ngamia akiuza na kununua bidhaa(ikiwemo watumwa).
Anko wake Muhammad,Abu Talib ndio alimuingiza kwenye biashara akiwa na umri mdogo kabisa(12yrs) na maisha yake mengi alikuwa trader kuliko nabii.Kwani nyie huwa mnadhani kabla hajawa nabii akiwa na miaka 40 alikuwa anafanya kazi gani?

Muhammad years as a trader-25 years
Muhammad as a prophet-23years

For references Check this article


For further reading
Afriza Hanifa,27 April 2013,Prophet(Rasulullah SAW) A True Entrepreneur[online]
Available at http://warwir.com/forumj/printthread.php?tid=1376

Ryan Novrian,31 January 2009,Concept Of Islamic Business Ethics[online]
Available at

Dr. Muzammil H. Siddiqi,17 December 2004,Religion[online]
Available at Religion

Sidmskhan,20 May 2012,Summary of Seerah[online]
Available at

Amanullah,15 January 2012,Manhood of Prophet Muhammad PBUH[online]
Available at

Majelis Ilm, 27 July 2011, 11 Principles for Islamic Living (4) Sunnah. Follow the Model of
Prophet Muhammad (PBUH)[online]
Available at
sunnath-follow-the-model-of-prophet-muhammad-pbuh
Ahmad Afiq Al-Kelantani,20 Januari 2013,Contohilah Akhlak Rasulullah S.A.W Ketika
Berniaga[online]
Available at

Dr. Sabahuddin Azmi,2010,An Islamic Approach To Business Ethics[online]
Available at http://www.renaissance.com.pk/Mayviewpoint2y5.htm

Rosli Baharuddin,2012,3 Akhlak Menjual Cara Rasulullah[online]
Available at http://www.majalahniaga.com/3-akhlak-menjual-cara-rasulullah.html

Zahid Isa (2010), TPR - Tips Pemasaran Rasulullah Sesuai Untuk Peniaga Online &
Offline.[online]
Available at http://www.wangcyber.com/forum/archive/t-36252.html
 
Ndugu zanguni Samahani kama ninawakwaza mkisikia jina muhammad..lakini hapa sio msikitini na wote tupo kwa ajili ya kujifunza So napomtaja Muhammad(saw) Simtaji kama nabii au religional figure bali namtaja kama historical figure..na ndiyo muktadha wa hii mada.

Nashangaa mnakasirika kusikia Muhammad alikuwa trader kuliko kusikia alivamia traders.

Furthermore kama hamjui Hata mke wake wa kwanza Bi Khadija(aliyemzidi miaka 15) alikuwa boss wake kwenye biashara ya trade.Bi khadija alimuajiri Muhammad kwasababu alisikia story zake kuwa ni muaminifu na alipewa nickname "Al-amin" baadae Muhammad akaongeza ukaribu akamuoa.
Muhammad alisafiri nchi mbalimbali(Syria,Yemen etc.) na ngamia akiuza na kununua bidhaa(ikiwemo watumwa).
Anko wake Muhammad,Abu Talib ndio alimuingiza kwenye biashara akiwa na umri mdogo kabisa(12yrs) na maisha yake mengi alikuwa trader kuliko nabii.Kwani nyie huwa mnadhani kabla hajawa nabii akiwa na miaka 40 alikuwa anafanya kazi gani?

Muhammad years as a trader-25 years
Muhammad as a prophet-23years

For references Check this article


For further reading
Afriza Hanifa,27 April 2013,Prophet(Rasulullah SAW) A True Entrepreneur[online]
Available at http://warwir.com/forumj/printthread.php?tid=1376

Ryan Novrian,31 January 2009,Concept Of Islamic Business Ethics[online]
Available at

Dr. Muzammil H. Siddiqi,17 December 2004,Religion[online]
Available at Religion

Sidmskhan,20 May 2012,Summary of Seerah[online]
Available at

Amanullah,15 January 2012,Manhood of Prophet Muhammad PBUH[online]
Available at

Majelis Ilm, 27 July 2011, 11 Principles for Islamic Living (4) Sunnah. Follow the Model of
Prophet Muhammad (PBUH)[online]
Available at
sunnath-follow-the-model-of-prophet-muhammad-pbuh
Ahmad Afiq Al-Kelantani,20 Januari 2013,Contohilah Akhlak Rasulullah S.A.W Ketika
Berniaga[online]
Available at

Dr. Sabahuddin Azmi,2010,An Islamic Approach To Business Ethics[online]
Available at http://www.renaissance.com.pk/Mayviewpoint2y5.htm

Rosli Baharuddin,2012,3 Akhlak Menjual Cara Rasulullah[online]
Available at http://www.majalahniaga.com/3-akhlak-menjual-cara-rasulullah.html

Zahid Isa (2010), TPR - Tips Pemasaran Rasulullah Sesuai Untuk Peniaga Online &
Offline.[online]
Available at http://www.wangcyber.com/forum/archive/t-36252.html
Hapa humkwazi mtu ila usizue uongo
 
Back
Top Bottom