Wewe huna macho ya akili, Mtukufu mtume (saw) amesema mitume waliikuja kabla yake ni 124,000. Akili yako haikutoshi kujua kwamba hawa ni mitume waliokuja kwa dunia nzima???
Allah katika sehemu kadhaa ndani ya Qur'an anasema; katika kila umma alituma mtume.
Huku kwetu Africa na sehemu zingine za dunia kulikuwepo na watu mbalimbali katika mahaki mbalimbali (nyimati), kwa msingi huo, kwa mujibu wa Qur'an ni lazima mitume walitumwa kwa ajili yao.
Hatujui habari zao kwasababu Allah hakuona umuhimu kumsimulia Mtukufu mtume (saw), almuhimu Mitume Walikwepo na huku kwetu, wazee wetu nao walikuwa watu kama wazee wa Mashariki ya kati hivyo walihitaji Muongozo wa kiroho, wazee wetu hawakuwa hayawani, hawakuwa na laana kiasi kwamba Allah asiwape neema ya Mitume.
Haiingii akilini kwamba kwama toka Nabii Adam (as) hadi Muhammad (saw), mitume 124,000 watokee Mashariki ya kati tu, walikuja kucheza mpira au zilikuwa ni timu za Basket ball!!!??, Wakati mtume kasema wametokea duniani kote wewe umasema hapana wametokea mashariki ya kati tu!!!-- wewe ni "Mmmanga" na unajivunia umanga wako ukijiona kwamba nyinyi ndio mlistahiki kuletewa mitume peke yenu huko Mashariki ya kati na wengine hawakustahili.
kaka acha kunywa Alkasusu, upende kula Samaki sana uongeze omega 3 في ريسك.