Dini ni Utamaduni wa watu fulani

Dini ni Utamaduni wa watu fulani

Unakubali kuwa waafrika walikuwa ni katika hizo nyumati ?

Nimeona twende kifupifupi...
Umati kwa maana kufikiwa na ujumbe au umati kwa maana ya kimaumbile, ama kimaumbile nakubali. Ila kama kiijumbe unatakiwa utupe ushahidi.
 
watu hao hawakufikiwa na mjumbe,haina maana ya kuwa mtume hakuwepo.
Unaweza kututhibitishia ya kuwa mjumbe anae kusudiwa hapo siyi mtume bali ni mtu yoyote ? Lakini pia unaweza kututhibitishia ya kuwa mtume alikuwepo zama za hao?
Hapa unapingana na mtume kwa kile kilicho simuliwa na Imaam Ahmad katika musnad yake na imaam al Bayhaaq katika kitabu chekae "al 'Itiqaad" juu ya watu aina nne watakao pewa mtihani siku ya Kiyama,kwa maana wapo watu ambao hawakufikiwa na mtume kabisa na mtums amewataja watu hao na kwa istilahi huitwa "ahlul Fitrah". Al muhimu unapo kata kwa kusema kulikuwa na mjumbe unatakiwa utupe ushahidi juu ya mjumbe huyo.

Lakini swali lingine, ni kuwa kimepita kipindi kirefu baina ya nabii Issa na mtume Muhammad,unaweza kutupa hshahidi ya kuwa katikati hapa palikuwa na mtume ?
 
Kwa sababu hao watu unaowasema walikuwa katika umma fulani na huo ummah ulikuwa na mjumbe,ila ujumbe wa huyo mjumbe haukuwafika hao watu.
Bhyo mjumbe unamjua wewe au umejuaje kama kuna mjmbe ?
 
Si

Simulizi gani ambazo hazirejei kwenye vitabu vya hilo jambo ?

Hujajibu swali langu bado.

Simulizi ipi ambayo haiarejei kwenye vitabu ?
mkuu wangu kwani fasihi simulizi lazima irejee kwenye fasihi andishi?

simulizi ya mtu/kitu haiwezi kutoka kizazi hadi kizazi bila kupitia kwenye maandishi?

kabla ya uwepo wa maandishi watu walikua hawapati taarifa za nyuma?
 
Nadhani unafahamu kuwa watu na ummah ummah ni mkubwa zaidi ya watu.

Kwa sababu hata leo hii kuna watu ambao hawajapata ujumbe wa uislamu,wako maporini huko hawwajui lolote lakini watu hao wapo katiuka ummah huu huu tunaoishi sisi.

Hivyo kutaka kuweka sawa watu fulani kuwa ummah ni makosa.

Na kama ukisema kuwaa kuna watu hawakupata mjumbe kwa kumaanisha kuwa watu hao ni ummha,basi je Qurani inajikanyaga kwa kusema kuwa ilipeleka mjumbe katika kila ummah ?
Mbona ummah wako bwana zurri haukupata mjumbe kama Qurani inavyodai ?

Utaona kuwa kuna pahala umeenda kombo,ni pale pakushikilia kuwa hao watu ni ummah pia.kumbe hao watu ambao hawakupata ujumbe wako ndani ya ummah wenye mjumbe tayari.
Usichanganye watu hawa ambao tuko nao lakini hawajapata ujumbe bali kuna wale ambao mtume hakushushwa katika kipindi chao, hao ni kati ya wale watu wa aina nne watakao jaribiwa siku ya Qiyama, kwa mujibu wa kilicho pokelewa toka kwa Imaam Ahmad na al Imaam al Bayhaaq katika kitabu chake.

Bado nasisitiza ya kuwa aya ile hukuielewa vizuri, sababu mtume amekuja kuweka wazi juu ya aya hiyo na ukisoma tafsiri ya Imaam Ibn Kathiri ameliweka wazi hizi. Kwahiyo usichanganye mambo.
 
Usichanganye watu hawa ambao tuko nao lakini hawajapata ujumbe bali kuna wale ambao mtume hakushushwa katika kipindi chao, hao ni kati ya wale watu wa aina nne watakao jaribiwa siku ya Qiyama, kwa mujibu wa kilicho pokelewa toka kwa Imaam Ahmad na al Imaam al Bayhaaq katika kitabu chake.

Bado nasisitiza ya kuwa aya ile hukuielewa vizuri, sababu mtume amekuja kuweka wazi juu ya aya hiyo na ukisoma tafsiri ya Imaam Ibn Kathiri ameliweka wazi hizi. Kwahiyo usichanganye mambo.
Wewe ndo ulete huo ufafanuzi wa hiyo aya kuwa huo umma ni upi uliokusudiwa ni upi ambao lazima ashushwe mjumbe na huo umma ambao ulikosa mjumbe ni upi ?
 
mkuu wangu kwani fasihi simulizi lazima irejee kwenye fasihi andishi?

simulizi ya mtu/kitu haiwezi kutoka kizazi hadi kizazi bila kupitia kwenye maandishi?

kabla ya uwepo wa maandishi watu walikua hawapati taarifa za nyuma?
Basi umekosa uadilifu.

Hapa hatubishani yunazungumza vitu hakika.

Unapokataa kuwa haya mambo hujayapata katika vitabu vyenyr vyanzo hivyo ni kukosa uadilifu.

Sasa labda nikuambie kuwa,msingi wa uislamu hasa kwa zama hizi zetu
mkuu wangu kwani fasihi simulizi lazima irejee kwenye fasihi andishi?

simulizi ya mtu/kitu haiwezi kutoka kizazi hadi kizazi bila kupitia kwenye maandishi?

kabla ya uwepo wa maandishi watu walikua hawapati taarifa za nyuma?
Kwa hiyo unataka kuniambia kuwa hujui kitu chochote kuhusu uislamu kwa kupitia chanzo chochote cha vitabu vya kiislamu ?

Kama ni hivyo basi naomba nikuambie kuwa mambo ya kiislamu yameshahifadhiwa katika vitabu mpaka kwa zama zetu hizi hakuna mambo ya kusimuliana simuliana alafu yasirejeshwe kwenye vitabu.

Kama wewe ni muislamu ukisema jambo lolote lile kuhusu uislamu hatutajali kuwa umesimulia bali tutataka ushahidi wa maandiko ya vitabu kuhusu jambo hilo.

Kama ambavyo leo ni ngumu historia ya bwana newton kuipata kwa simulizi wee mswahili pasi na kaurejea vitabuni basi na huku ndo hivyo hivyo lazima urejee vitabuni.

Kwa hiyo nadhani kukimbia kwako vitabu na kudai ni masimulizi hakun amashiko kwa sababu uislamu wenyewe mpaka sasa ni dini ya maandiko na sio dini ya kusikia sikia.

Kwa hiyo tunakubaliana kuwa wewe umetumia fasihi simulizi kujua hayo unayojua kuhusu uislamu ?
 
Bhyo mjumbe unamjua wewe au umejuaje kama kuna mjmbe ?
Nimejua kwa sababu Qurani inasema kila umma umepewa mjumbe na huo umma pia lazima uwe na mjumbe.

Hao mitume wote zaidi ya laki moja ndo wapo humo katika hizo nyumati ambazo Allah hatuona umuhimu wa kututajia.

Kutokuwajua hao mitume sio hoja kuwa ati hawakuwa na mitume hizo nyumati.

Kama ambavyo kutokuwajua majina hiyo mitusme zaidi ya laki moja sio hoja kuwa ati haipo...ipo ila Allah kwa hekima zake hakutaka kututajia.

Unachotaka kulazimisha kuwa Allah angetaja kila kitu na kila tukio jambo ambalo sio sawa kuna mambo yameachwa tele tu ambayo Allah kaona hayatufaidishi.
 
Wewe ndo ulete huo ufafanuzi wa hiyo aya kuwa huo umma ni upi uliokusudiwa ni upi ambao lazima ashushwe mjumbe na huo umma ambao ulikosa mjumbe ni upi ?
Reja Tafsiri Ibn Kathiri ameelezea hilo, na nimekupa marejeo katika musnad ya Imaam Ibn Hanbal Abuu Abdillah na kwa Imaam al Bayhaaq katika kitabu chake cha "al 'Itiqaad" amenukuu hadithi juu ya watu aina nne watakao pewa mtihani siku ya hukumu.

Lingine nilikuuliza swali, lakini hukujibu bali ukajibu kwa kile ambacho kipo hata kwetu sisi, kwa maana wapo watu leo hii japo mtume alikuwepo lakini hawajafikiwa na ujumbe, sasa kuna wale ambao hapakuwa na mjumbe kabisa, nikakutolea mfano kipindi cha kina Socrates,Plato,Aristotle na mfano wao, na Shaykhu Islam ana maneno mazuri sana kuhusu wao, rejea kitabu chake "Naswaht ahlul Imaan fi Raadd al Mantiq al Yuunani" au "Dar Ta'arudh 'aql wa naql" au "al Majmu'i al Fatawah" vyote vitabu vyake Shaykuhl Islam.
 
Unaweza kututhibitishia ya kuwa mjumbe anae kusudiwa hapo siyi mtume bali ni mtu yoyote
Mimi sijasema mtu yeyote bali nimesema Mtume yule wa kuchaguliwa hasa afikishe ujumbe katika kila umma.

Wewe kama unasema njumbe ni mtu yeyote hiyo sio mimi ni wewe,mimi nasema mjumbe kusudiwa katika aya ni Mtume hasa.
Lakini pia unaweza kututhibitishia ya kuwa mtume alikuwepo zama za hao?
Kuna zama na umma.mfano sisi zama hizi ni umma wa mtume muhammad lakini zama ni tofauti kabisa ukiangalia zama za Mtume muhammad na zama zetu ni tofauti kabisa.

Lakini tofauti hizo za zama sio tofauti za ummah.sisi ni UMMA MMOJA WA ZAMA TOFAUTI.

Kutofautiana kwa zama sio kutofautiana kwa umma.

Zama zetu kuna mambo mengi ya maendeleo,lakini zama za mtume hakukuwa na mambo hayo.

Ila mimi na wewe tunakubaliana kwamba zama zile na zama hizi wote ni ummah mmoja japokuwa tofauti zama zetu.

Kwa hiyo kama unataka kusema kuwa tofauti za zama pia zinatofautisha umma ulete ushahidi wenye mashiko pia kwa sababu zama zinaweza kuwa tofauti na umma ukawa ni mmoja ule ule.
Hapa unapingana na mtume kwa kile kilicho simuliwa na Imaam Ahmad katika musnad yake na imaam al Bayhaaq katika kitabu chekae "al 'Itiqaad" juu ya watu aina nne watakao pewa mtihani siku ya Kiyama,kwa maana wapo watu ambao hawakufikiwa na mtume kabisa na mtums amewataja watu hao na kwa istilahi huitwa "ahlul Fitrah". Al muhimu unapo kata kwa kusema kulikuwa na mjumbe unatakiwa utupe ushahidi juu ya mjumbe huyo.
Kwani hao watu umeambiwa ni ummah au ni watu ndani ya ummah ?

Unajua mkuu unashindwa kuelewa makusudio,tumia ufahamu wa kawaida tu hapo kuelewa.

Ahlul fitrah sio umma hao ni baadhi ya watu ndani ummah wenye zama nyingiii.

Mtume alisema kauli ya ummah au watu fulani ndo hawakupata mjumbe ?

Unapoambia ahlul fitrah na ummah basi ummah ni mkubwa kuliko ahlul fitrah,hivyo hao ahlul fitrah walikuwa ndani ya ummah wenye mtume.

Allah alisema kila ummah ameuletea mjumbe,na Wala hakusema kila mtu kamletea ujumbe.

Allah kusema Ummah sio mjinga.

Kama amabo sisi ummah huu mtume wetu ni Muhammad ila wapo watu mpaka leo hawaujui uislamu wako maporini huko hawaelewi dini kabisa.

Hawa huwezi kusema ni ummah,hao ni watu walioko ndani ya ummah huu wa Mtume muhammad.

Ila hao sasa kwa sababu hawabebi ummah bali umma ndo unawabeba hao ati.

Kwa hiyo huwezi kusema ati kuna nyumati hazikupewa Mtume huo ni ufahamu wa kimakosa.

Wale ambao hawakufikiwa ujumbe katika zama zetu hizi hao mtume wao ni Muhammad japo kuwa huo ujumbe waMuhammad hawajaupata,ila hatuwezi kusema kuwa hawana mtume ati kwa sababu kimepita kipindi kirefu baina yetu na yao.
 
Nimejua kwa sababu Qurani inasema kila umma umepewa mjumbe na huo umma pia lazima uwe na mjumbe.

Hao mitume wote zaidi ya laki moja ndo wapo humo katika hizo nyumati ambazo Allah hatuona umuhimu wa kututajia.

Kutokuwajua hao mitume sio hoja kuwa ati hawakuwa na mitume hizo nyumati.

Kama ambavyo kutokuwajua majina hiyo mitusme zaidi ya laki moja sio hoja kuwa ati haipo...ipo ila Allah kwa hekima zake hakutaka kututajia.

Unachotaka kulazimisha kuwa Allah angetaja kila kitu na kila tukio jambo ambalo sio sawa kuna mambo yameachwa tele tu ambayo Allah kaona hayatufaidishi.
Mtume maisha yake yote alikuwa anafasiri Qur'aan yeye akaja kuwatoa na kueleza ya kuwa wapo ambao hawakufikiwa na ujumbe, na ni katika watu wa aina nne, hawa watu watapewa mtihani siku hiyo hiyo ya hukumu, katika hao wapo ambao hawakufikishiwa mjumbe kabisa, soma katika Musnad ya Imaam Ahmad na al Imaam al Bayhaaq amenukuu hadithi hiyo.

Nanukuu :

Imam Ahmed Ben Hanbal narrated in his “Musnad” and Al-bayhaqi in his book “Al- I’tiqaad”, and classed as Saheeh by Al-Aswad Ben Saree’ that the prophet (PBUH) said:
“Four types of people will be tested on the day of judgement: a deaf man who cannot hear anything, a mad man, an old aged man and a man who died during fatrah (a period of time when no messenger was sent to people). The deaf man will say: “Oh Allah, Islam came while I cannot hear anything!”. The mad man will say: “Oh Allah, Islam came while the boys throw animals’ excrement on me!”. The old aged man will say: “Oh Allah, Islam came while I can understand nothing”. And the man who died during a fatrah will say: “Oh Allah, I witnessed no messenger from You”. Then Allah takes a promise from them to obey Him. Then He will command them to enter hell, and who enters it will find it peace and cool, and who disobeys will be dragged to hell”

Mwisho wa nukuu.
 
Mtume maisha yake yote alikuwa anafasiri Qur'aan yeye akaja kuwatoa na kueleza ya kuwa wapo ambao hawakufikiwa na ujumbe, na ni katika watu wa aina nne, hawa watu watapewa mtihani siku hiyo hiyo ya hukumu, katika hao wapo ambao hawakufikishiwa mjumbe kabisa, soma katika Musnad ya Imaam Ahmad na al Imaam al Bayhaaq amenukuu hadithi hiyo.
Hao watu ni ummah bossi ?
 
Kwani hao watu umeambiwa ni ummah au ni watu ndani ya ummah ?
Unajua kwamba mjumbe wapo walikuwa wanakuja kwa ajili ya mji au koo fulani, huo ni umma mzee, hata nabii Issa alitumwa kwa Wana wa Israeli na si katika umma wote wa dunia nzima, na ndiyo maana ule pia unaitwa umma, umma siyo lazima uwe dunia nzima mzee, hili unatakiwa uelewe, mtume pakee aliye tumwa kwa ajili ya ulimwengu mzima ni mtume Muhammad pekee.
 
Hao watu ni ummah bossi ?
Umma, ukisoma aya katika matini yake, imekuja "Rasula" kwa maana ya mtume kilugha kama alivyofasiri Shaykhul Islaam katika majmui al Fatawa unawatoa manabii, lakini aya inajumuisha na manabii kadhalika, hii uone ya kuwa linalo kusudiwa hapo ni wingi wa watu.

Soma Kamusi uone maana ya umma, kwamba siyo lazima uwe wote duniani, ndiyo maana hata nabii Ibrahiim aliitwa "Ummah" japokuwa alikuwa peke yake, lakino aliitwa vile sababu alikuwa kwenye haq.
 
Wewe kama unasema njumbe ni mtu yeyote hiyo sio mimi ni wewe,mimi nasema mjumbe kusudiwa katika aya ni Mtume hasa.
Na mimi sikusudii mjumbe ni mtu yoyote, mimi namkusudia yule aliyezungumziwa katika aya.

Almuhimu unatakiwa usome fasiri za Qur'aan hasa zile za "Maathuri" zinazofasiri aya kwa hadithi, na soma kitabu cha Imaam Muhammad al Amin ash Shanwitwy kiitwacho "Da'fu Ihaam adh Twirasb 'an ayaat al Kitaab",uone namna wanavyo oanisha aya kwa aya au aya hadithi na kupata jibu moja.
 
Kuna zama na umma.mfano sisi zama hizi ni umma wa mtume muhammad lakini zama ni tofauti kabisa ukiangalia zama za Mtume muhammad na zama zetu ni tofauti kabisa.
Sasa nana unatoka kwenye lengo na kuingiza mambo ambayo hayapo, hakuna sehemu iliyo gusiwa na aya kuhusu zama, hapa aya inaongelea umma,yaano watu.

Zama ni tofauti ila aya imegusa umma, haijalishi ni zama gani, na suala la zama hapa haliingii, hapa ni umma na ujumbe.
Lakini tofauti hizo za zama sio tofauti za ummah.sisi ni UMMA MMOJA WA ZAMA TOFAUTI.
Na ujumbe wetu ni mmoja, na naongelea ujumbe, na umma huu mtume ni Muhammad, sasa kuna ummat hazikupelekewa mtume kabisa.
Ahlul fitrah sio umma hao ni baadhi ya watu ndani ummah wenye zama nyingiii.
Soma matini ya hadithi nimekupa marejeo, mtume amesema umma na akasema baadhi ya watu ndani ya umma, soma hadithi, imegusia watu wa aina nne, sasa usingie mlango ambao umeshafungwa tayari, utazidi kuharibu.

Unapingana na mtume siyo ?
Unapoambia ahlul fitrah na ummah basi ummah ni mkubwa kuliko ahlul fitrah,hivyo hao ahlul fitrah walikuwa ndani ya ummah wenye mtume.
Tuambie sasa walikuwa katika umma wa mtume gani, maana mtume habari hizi amefunuliwa na ndiyo maana akasema watu wa aina nne, na angetuambia ni mtume gani.

Naona hata hadithi hujaisoma, embu kasome hadithi, kisha uje kujenga hoja. Nikikuuliza mathalani nabii Swalehe huyu alichaguliwa kufikisha ujumbe lakini ujumbe ni kwa watu wake wa Mad'yaan, vipi ule siyo umma ? Rejea kitabu cha Imma Ibn Kathir, kiitwacho "Qasas al An'biyaa".Kadhalila nabii Issa alikuwa katika umma gani, mbona ni mtume lakini kwa watu wa Israeli ule nao ni umma mzee.
Unapoambia ahlul fitrah na ummah basi ummah ni mkubwa kuliko ahlul fitrah,hivyo hao ahlul fitrah walikuwa ndani ya ummah wenye mtume.
Naona unalazimisha jambo ambalo halipo, ndiyo maana nikasema hivi aya hujaielewa. Nani alikwambia umma lazima uwe mkubwa kama ummat Muhammad ? Umma huwa hata kwa kijiji au mji. Sasa soma historia ya kina Plato uone kama walikuwa wachache, magharibi yote ile.
 
Sasa nana unatoka kwenye lengo na kuingiza mambo ambayo hayapo, hakuna sehemu iliyo gusiwa na aya kuhusu zama, hapa aya inaongelea umma,yaano watu.

Zama ni tofauti ila aya imegusa umma, haijalishi ni zama gani, na suala la zama hapa haliingii, hapa ni umma na ujumbe.

Na ujumbe wetu ni mmoja, na naongelea ujumbe, na umma huu mtume ni Muhammad, sasa kuna ummat hazikupelekewa mtume kabisa.

Soma matini ya hadithi nimekupa marejeo, mtume amesema umma na akasema baadhi ya watu ndani ya umma, soma hadithi, imegusia watu wa aina nne, sasa usingie mlango ambao umeshafungwa tayari, utazidi kuharibu.

Unapingana na mtume siyo ?

Tuambie sasa walikuwa katika umma wa mtume gani, maana mtume habari hizi amefunuliwa na ndiyo maana akasema watu wa aina nne, na angetuambia ni mtume gani.

Naona hata hadithi hujaisoma, embu kasome hadithi, kisha uje kujenga hoja. Nikikuuliza mathalani nabii Swalehe huyu alichaguliwa kufikisha ujumbe lakini ujumbe ni kwa watu wake wa Mad'yaan, vipi ule siyo umma ? Rejea kitabu cha Imma Ibn Kathir, kiitwacho "Qasas al An'biyaa".Kadhalila nabii Issa alikuwa katika umma gani, mbona ni mtume lakini kwa watu wa Israeli ule nao ni umma mzee.

Naona unalazimisha jambo ambalo halipo, ndiyo maana nikasema hivi aya hujaielewa. Nani alikwambia umma lazima uwe mkubwa kama ummat Muhammad ? Umma huwa hata kwa kijiji au mji. Sasa soma historia ya kina Plato uone kama walikuwa wachache, magharibi yote ile.

Kwa ufupi sana ili tusizongane..

Kwa mujibu wa uislamu umma ni nini na uweje ili uwe umma ?
 
Back
Top Bottom