"Je yule mbwa wa vijana wa Pangoni, alikuwa jike au dume au alikuwa ana rangi gani ?" kisha ujione kwamba una akili, aisee Qur'aan haitutaki tuhoji ujinga bali tuhoji vya maana.
Hii ndiyo nature ya akili yako, hii inaonyesha wewe unaweza kuuliza maswali ya aina hiyo.
Angalia maswali na hoja zangu zilivyo na sio huo ujinga wa maswali yako ya kitoto unayotaka kuninathibisha kwangu.
1----Kipindi manabii wanashushwa huko mashariki ya kati kwa ajili ya watu wa huko katika sehemu mbalimbali za dunia watu (nyimati) zilikuwepo.
2----- Qur'an inasema katika kila umma (katika kila watu duniani) waonyaji walitumwa kwao. (Ushahidi wa aya 4 nilikupa)--- Allah jambo hili kalieleza katika aya 4 kama msisitizo, na ni watu wenye akili tu ndio wanaweza kujua hilo. Watu wenye akili (albaaab), here I am talking of the people who can exercise well their mental faculties and not people like you.
3----Allah akasema kwamba kuna mitume aliomsimulia mtume (saw) na kuna wale hajamsimulia, (nikikupa ushahidi wa aya pia).
Hoja yako ikawa je mitume walitumwa mashariki ya kati pekee, mimi nikapinga na ninapinga, na ninasema kwamba mbali na mashariki ya kati pia mitume walituma sehemu mbalimbali za dunia ambapo zama hizo watu walikuwepo, Maeneo ya Africa, China, America zote, Mashariki ya mbali, Australia na Newzealand nk.
Mungu anasema na kila umma alitumwa Muonyaji, mpuuzi mmoja anasema kwa kibri na jeuri eti; "toa ushahidi !!!" Kama kwamba haoni hizo aya za Qur'an, kama kwamba hakusoma historia kujua kwamba sehemu zingine za dunia kulikuwepo na watu, kama kwamba haoni umuhimu wa hizo aya za Allah anaposema katika kila umma alitumwa mwonyaji, kama kwamba anaona fahari kusema mababu zetu huku Africa nk, hawakustahili kupewa mitume (muongozo wa kiroho) na hivyo walikuwa Washenzi kwani bila Muongozo wa kiroho mtu huwa nshenzi na mshirikina.
Ninachopinga kwako ni kauli zako za kijinga bila Ushahidi kwamba mitume hawakutumwa huku nje ya mashariki ya kati, mimi nimekupa ushahidi wa Maneno ya Allah, na wewe toa ushahidi wa maneno ya Allah kutetea "ujinga wako".
Soma pia hapa ufute ujinga kumuhusu Sage Luqman.