Dhana ya wasomi tu kuwa wabunge Tanzania kwa kigezo cha kutunga sheria imepitwa ma wakati

Dhana ya wasomi tu kuwa wabunge Tanzania kwa kigezo cha kutunga sheria imepitwa ma wakati

HAKI KWA WOTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 30, 2022
Posts
2,691
Reaction score
2,303
Kazi ya mbunge siyo kutunga sheria tu pia siyo sheria zote hutokana na wabunge hasa ukizingatia wabunge wasomi ndiyo wameifikisha Tanzania hapa tulipo kwa kukosa uzalendo kwa nchi yao.

SHERIA NA VYANZO VYA SHERIA TANZANIA
MAANA YA SHERIA

Sheria ni kanuni zinazoongoza shughuli na mahusiano ya watu waishio katika jamii fulani. Sheria inaelezea haki na wajibu wa wanajamii hao, inaweka masharti juu ya mambo fulani, kuelezea makosa na adhabu iwapo makosa ama masharti yaliyotajwa na sheria yatakiukwa.

AINA ZA SHERIA
Kuna aina mbili za sheria Tanzania;-
1. Sheria za madai
2. Sheria za jinai

VYANZO VYA SHERIA TANZANIA
1. KATIBA
Katiba ni chanzo kikuu cha sheria, ni wajibu wa haki za wananchi kubainishwa katika katiba husika. Sheria zote za nchi hupata nguvu kutoka katika katiba ya nchi, hivyo basi kama kuna sheria ambayo haikubaliani na Katiba basi itakataliwa na Mahakama kuu kwani sheria zote ni lazima zifuate Katiba ya nchi.
2. SHERIA ZILIZOANDIKWA
Ni sheria ambazo zimeandikwa na kupitishwa na bunge au chombo kingine cha kutunga sheria. Sheria hizi huwa katika madaraja mawili; sheria kuu na sheria ndogo au sheria ya uwakilishi
1. SHERIA KUU
Kwa Tanzania, sheria hutungwa na bunge. Sheria ambazo hutungwa na bunge lenyewe huitwa sheria kuu; Mfano wa Sheria Kuu ni; Sheria ya Ardhi za Vijiji, 1999. Hata hivyo, bunge laweza kutunga sheria inayoruhusu chombo kingine au mtu kutunga sheria.
2. SHERIA NDOGO AU SHERIA YA UWAKILISHI
Sheria ndogo au sheria ya uwakilishi ni ile ambayo hutungwa na mtu, chombo au mamlaka yoyote ile ambayo imeruhusiwa kutunga sheria hiyo kwa mujibu wa Sheria kuu iliyopitishwa na Bunge. Mfano mmojawapo wa sheria ndogo ni ile inayotungwa na Halmashauri za Wilaya/Manispaa au Waziri.

3. SHERIA ZINAZOTOKANA NA MAAMUZI YA MAHAKAMA
Vyanzo vingine vikuu vya sheria ni maamuzi ya Mahakama ya rufaa au Mahakama kuu ambazo hufuatwa na mahakama za chini katika kuamua kesi za aina hiyo. Kwa hiyo, maamuzi yanayotolewa katika Mahakama hizi ni chanzo kingine cha sheria kwa mahakama za chini haswa katika kesi au mashauri yanayofanana. Hali kadhalika, Mahakama kuu haina budi kufuata maamuzi ya Mahakama ya Rufaa kwani majaji wa mahakama hizi huitafsiri na kuzifafanua zaidi sheria.
4. SHERIA ZA KAWAIDA
Sheria ya Kawaida ni sheria ya kitamaduni ya Uingereza ambazo baadaye ziliingizwa katika mahakama. Sheria hizi zinafanana na sheria zetu za kimila kwa vile hata sheria hizi zimetokana na misingi iliyofuatwa na watu.
Asili ya sheria za kawaida katika mfumo wa kisheria wa Tanzania ni baada ya kutumiwa nchini India wakati wa utawala wa kikoloni wa mwingereza. Kwa mfano kanuni za adhabu za India, kanuni za madai za India, Sheria ya ushahidi ya India n.k. Mahakama za kikoloni za Tanganyika (kama Tanzania ilivyojulikana zama hizo) zilitumia kanuni hizi ambazo zilitungwa Uingereza katika utoaji haki kwenye mahakama zetu.

5. SHERIA ZA KIMATAIFA
Sheria za kimataifa huongoza mahusiano kati ya mataifa, zinaunda haki na majukumu ya mataifa kwa raia na inaweza pia kuunda haki za watu binafsi. Sheria za Kimataifa pia zinaweka kiada na viwango ambavyo vinatakiwa kuheshimiwa na kufuatwa na wananchi, mfano sheria ya kimataifa za mazingira, sheria za Kimataifa za bahari n.k
HATA HIVYO, kwa Tanzania sheria za kimataifa haziwezi kutumika nchini Tanzania bila utaratibu maalumu wa kuziingiza na kuzitumia ufanyike. Lazima zipitishwe na Bunge na zijumuishwe kwenye sheria za ndani ya nchi

6. SHERIA ZA MILA
Sheria za Mila zinaweza kutafsiriwa kama kanuni za kimila au jadi ambazo zinatumika, zinatambulika na kukubaliwa na jamii yoyote na kupata nguvu ya kisheria kupitia katika serikali na katiba ya nchi.
HATA HIVYO, Ili kutumiwa, ni lazima zithibitishwe na kuhalalishwa katika mahakama za kisheria pale ambapo kuna kesi zinazohitaji kutumika kwa kanuni hizo ili kuamuliwa
 
Huu ni mkakati wa CCM kuhakikisha bunge linakuwa na watu wenye akili ndogo
 
Huu ni mkakati wa CCM kuhakikisha bunge linakuwa na watu wenye akili ndogo
Hao wenye akili nyingi ni akina nani na wamefanya nini cha maana?

Yaani kwa akili hiyo ya kuona aliyesoma ndiyo mwenye akili ni wazi waTanzania wenye akili kama hii yako ni maiti
 
Jenga hoja yako unazani kwanini Mbunge ambae sio msomi ni bora kulikoa ambae amesoma.

Yaani ukiwa hujasoma, Una advantage gani kuwa mbunge kuliko alie soma.

Ukijenga hoja, bila kelele ntarudi
 
Jenga hoja yako unazani kwanini Mbunge ambae sio msomi ni bora kulikoa ambae amesoma.

Yaani ukiwa hujasoma, Una advantage gani kuwa mbunge kuliko alie soma.

Ukijenga hoja, bila kelele ntarudi
Mbunge ambaye hajasoma kwanza anahofu na jamii na ni mzalendo wa kweli ukilinganisha mbunge msomi hana hofu na anatumia elimu yake kama kinga na kibali ktk bunge kupindisha ukweli wakati huohuo uongozi hauangalii ELIMU bali karima ya uongozi na hofu ya Mungu.

Je,hao wabunge wasomi mara ngapi wameliingiza taifa kwenye kashifa za mikataba feki na ufisadi wa kupindukia????

Acheni unafiki tumeona wabunge na watumishi wasomi wangapi wametuhumiwa au wamefikishwa mahakamani kwa ufisadi na kashifa nzito ikiwemo ubadhirifu wa fedha na mali za umma i.e:chenge,mahalu,tibaijuka,nk?

Je,imekuwaje baadhi ya wabunge wasomi i.e:kimei wameachwa kwenye majimbo yao na baadhi ya wabunge wasio wasomi wamebaki kwenye majimbo yao i e:msukuma.

Huu siyo wakati wa kuangalia usomi wa mtu bali uzalendo wa mtu kwa taifa lake hao wasomi ndiyo wameliingiza taifa kwenye mikataba mibovu na wizi mkubwa kwa kisingizio cha elimu na kurefusha mambo ili tu kujipatia mali.

Sasa kama elimu au usomi ndiyo chanzo cha maendeleo na ufanisi ktk ubunge basi hakuna haja ya ya wasiosoma kupiga kura wajipigie haohao wasomi wenye uwezo na uelewa,haiwezekani kuwe na kundi la wasomi wapigiwa kura na kundi la wasiosoma wapiga kura.

Kama kweli elimu ndiyo kigezo cha uongozi basi hata viongozi wa. chini i.e:wenyeviti wa vijiji na mitaa,madiwa,nk wawe maprofesa ili nchi iendelee kwa kasi ya ajabu.

Haiwezekani kuwe na tabaka la wapiga kura tu i.e:wasiosoma na tabaka la wapigiwa kura/wabunge tui.e:wasomi wote wana haki sawa za kuwa wagombea na kuwa wapiga kura.
 
Mbunge ambaye hajasoma kwanza anahofu na jamii na ni mzalendo wa kweli ukilinganisha mbunge msomi hana hofu na anatumia elimu yake kama kinga na kibali ktk bunge kupindisha ukweli wakati huohuo uongozi hauangalii ELIMU bali karima ya uongozi na hofu ya Mungu.

Je,hao wabunge wasomi mara ngapi wameliingiza taifa kwenye kashifa za mikataba feki na ufisadi wa kupindukia????

Acheni unafiki tumeona wabunge na watumishi wasomi wangapi wametuhumiwa au wamefikishwa mahakamani kwa ufisadi na kashifa nzito ikiwemo ubadhirifu wa fedha na mali za umma i.e:chenge,mahalu,tibaijuka,nk?

Je,imekuwaje baadhi ya wabunge wasomi i.e:kimei wameachwa kwenye majimbo yao na baadhi ya wabunge wasio wasomi wamebaki kwenye majimbo yao i e:msukuma.

Huu siyo wakati wa kuangalia usomi wa mtu bali uzalendo wa mtu kwa taifa lake hao wasomi ndiyo wameliingiza taifa kwenye mikataba mibovu na wizi mkubwa kwa kisingizio cha elimu na kurefusha mambo ili tu kujipatia mali.

Sasa kama elimu au usomi ndiyo chanzo cha maendeleo na ufanisi ktk ubunge basi hakuna haja ya ya wasiosoma kupiga kura wajipigie haohao wasomi wenye uwezo na uelewa,haiwezekani kuwe na kundi la wasomi wapigiwa kura na kundi la wasiosoma wapiga kura.

Kama kweli elimu ndiyo kigezo cha uongozi basi hata viongozi wa. chini i.e:wenyeviti wa vijiji na mitaa,madiwa,nk wawe maprofesa ili nchi iendelee kwa kasi ya ajabu.

Haiwezekani kuwe na tabaka la wapiga kura tu i.e:wasiosoma na tabaka la wapigiwa kura/wabunge tui.e:wasomi wote wana haki sawa za kuwa wagombea na kuwa wapiga kura.

Najitahidi Nikuelewe, Sasa unataka kutuambia Tukiweka la saba B au Form four Failure wote pale bungeni, Kutakua na maendeleo kuliko sasa ambapo 80+ ya wabunge wamesoma.
 
Najitahidi Nikuelewe, Sasa unataka kutuambia Tukiweka la saba B au Form four Failure wote pale bungeni, Kutakua na maendeleo kuliko sasa ambapo 80+ ya wabunge wamesoma.
Soma machapisho yangu humu utahnielewa kama una akili ya kunielewa kama huna hiyo akili ni bure tu unapoteza muda wako humu,je ni wapi nimesema bunge liwe na 80+ la f4 failure au la saba failure ndiyo kuwtakuwa na maendeleo?je kwa sasa ambapo kuna wabunge 80+ waliosoma kuna maendeleo?

Fikirisha ubongo wako siyo kwamba wabunge wasomi ndiyo wanaoleta maendeleo kwa usomi wao na wabunge wasio wasomi ndiyo hawaleti maendeleo,unataka kusema familia za wasomi ndizo zina maendeleo kuliko za wasiosoma,jiongeze!!
 
Ngoja tuanzie hapa.
Kwa hiyo mleata mada unataka kusema, hata kile kigezo cha mbunge kutakiwa kujua kusoma na kuandika kifutwe maana usomi huanzia hapo.
 
Ngoja tuanzie hapa.
Kwa hiyo mleata mada unataka kusema, hata kile kigezo cha mbunge kutakiwa kujua kusoma na kuandika kifutwe maana usomi huanzia hapo.
Soma mada yangu uielewe acha kikirupuka ni wapi nimesema kigezo cha kujua kusoma na kuandika kiondolewe?je wanaojua kusoma na kuandika wote ni wasomi au wameenda shuleni?
 
Minaona nisawa tu, kama ni sheria hata kwenye vitabu vya dini vitatuongoza mazee....
Na kama ni taraibu na kanuni tutazitungia hata hapa Waswanu bar...
 
Minaona nisawa tu, kama ni sheria hata kwenye vitabu vya dini vitatuongoza mazee....
Na kama ni taraibu na kanuni tutazitungia hata hapa Waswanu bar...
Ndiyo,kwani hao manabii mnaowasoma kwenye biblia na quruan na waliotunga vitabu vya dini walikuwa wasomi kiasi gani hadi bunge liwe la wasomi?quruan na biblia ziliandikwa na wasomi hadi bunge liwe la wasomi tu?
 
Back
Top Bottom