Denis Msacky, Zitto Kabwe waungana kumjulia hali Kibanda

Denis Msacky, Zitto Kabwe waungana kumjulia hali Kibanda

Kwani Kibanda kapelekwa Afrika Kusini lini? Msacky alikuwa anamsubiri Zitto atoke Jeshini ndio waende kumjulia hali Kibanda, au?
 
Kuna wana siasa wengine watafukuzwa wakienda kumuona Kibanda hakuna haja ya kuwataja wanajijua wenyewe.

Kikwete mbona alijikosha akaenda kumwona kana kwamba hahusiki? Mambo ya Ramadhani Ighondu hayo.
 
Yaani wewe hujui jinsi Slaa anavyohusika na kutekwa kwa Kibanda?

duh hiyo kali kwa hiyo uko south africa na msacky kumpasha Kibanda kwamba Dr Slaa akimteka ,haya bwana tutauona mwisho wako tunakufuatilia na tutakuja kukwambia unafiki wako utakapokutumbukiza baharini
 
Mh. Zitto bana,
Ni wale wanasiasa ambao wao wako tayari kwa lolote. Either, YOU LOVE HIM or LOATHE HIM.

Jana ametema cheche hapa ambazo watu bado wanazijadiri, leo yuko South Africa kwa Kibanda.

He keeps on turning CHADEMA stomach.
Mzizi wa ufitini umefika mwisho Zitto analingia kitu fulani lakini anatusaidia wananchi kumfahamu alipo, nina uhakika mawakiri wa Lwakatare watamuunganisha kama mtoa ushahidi si bure ile video ya Lwakatare Zitto,Msacky,Ludovicky na Mwigulu na Nape wanaijua syndicate
 
duh hiyo kali kwa hiyo uko south africa na msacky kumpasha Kibanda kwamba Dr Slaa akimteka ,haya bwana tutauona mwisho wako tunakufuatilia na tutakuja kukwambia unafiki wako utakapokutumbukiza baharini
Duh tumefika huko?
 
Kuna wana siasa wengine watafukuzwa wakienda kumuona Kibanda hakuna haja ya kuwataja wanajijua wenyewe.

Jembe (lao) Ritz

Umeanza lini uoga. Unashindwa kumtaja Mwenezi wa taarifa na propaganda zenu, ambaye alifukuzwa pale hospitalini na vyombo vya habari vikaripoti na hajawahi kukanusha. Kwa ujasiri ambao wengi hapa huwa wanafikiri unao, kamilisha kumtaja usiogope.

Wataje na wale wengine wenzenu ambao wanakwenda kwa kuvizia, wakiambiwa wasubiri kidogo yule mwandishi mahiri tuliyemwamini aende na Kibanda, aje pale awatambue, wanakumbuka enzi zao za UMITASHUMITA na UMISSETA walipokuwa wanakimbia riadha. Wanakula mbio, ulimi hapa, kisigino hicho, kwenye ngazi za hospitali. Wataje tu usiogope mkuu, jembe lao.

Kwani mlivyomfanyia Dkt. Ulimboka si pia jamaa zenu walikuwa wanatuma watu pale. Sema wale madaktari nao walikuwa makini. Wanahabari pia katika hili wako sawa sawa tangu mwanzo. Ndiyo maana jamaa alifukuzwa na unaogopa kumsema!
 
Siku zito akawa rais jk atakuwa cha mtoto katika uzururaji
 
Na uko Twitter aliandika hivi...."@zittokabwe: Offf to Jburg to see my brother and advisor #Kibanda .""@zittokabwe: Kaka yangu, ndugu yangu na rafiki yangu absakibanda anaendelea vizuri sana http://t.co/NV58vaq6ly""@zittokabwe: Ni lazima watu waliofanya unyama huu kwa absakibanda wapatikane. Sisi rafiki zake tusipohakikisha hilo tutakuwa tunamsaliti""@zittokabwe: Mola ashukuriwe sana, sikuamini kama nitamkuta Absalom Kibanda mzima na anapata nafuu."Anaendelea hiviii...."@zittokabwe: Demokrasia ni dhana. Kwenye demokrasia, watu wanapopishana mawazo ndio dhana inakomaa. Wanapopishana na kudhuriana dhana inauwawa"
Simameni kidedea, msipende kukanusha vitu kwa sababu vtawaua kisiasa ... kama hampendi mambo fulani, semeni kuwa hampendi. Mkiitwa wanafiki poa tu!!

Tunajua hampendi mambo yanavyoenda .... simamieni hilo kwanza, mkikanusha mnaonekana waongo mbele ya watanzania makini ... tushaanza kuchoka malumbano ya kinafiki.
 
Ah naogopa hata ku coment mara unapuigwa ban ya nguvu ah hawa mods bana wanatunyima uhuru wa kuongea
 
Mh.Zitto anaanza
kuwafunulia Viongozi wa CHADEMA maana ya ujumbe wake wa jana na vile
vile kuwasuta pale aliposema,
Mh. Zitto, kumbuka pia, JASUSI Lwakatare anatumia nyenzo za CHADEMA
kwenye kesi yake na huku Dr. Slaa akimkumbatia.
Ningeshangaa usingemtaja Dk Slaa maana ndiye target yenu.
 
Kwani Kibanda kapelekwa Afrika Kusini lini? Msacky alikuwa anamsubiri Zitto atoke Jeshini ndio waende kumjulia hali Kibanda, au?

One of Great Thinker wetu wa JF! unapiga pale pale bila soni! inatosha sihitahi kuchangia lolote!
 
Back
Top Bottom