DCI Manumba: Mwakyembe hajalishwa sumu!

DCI Manumba: Mwakyembe hajalishwa sumu!

Hii ni kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na vyombo vya habari mchana wa leo. Katika maelezo yake, DCI anasema kwamba:

"Kutokana na uchunguzi wa kipolisi ulioshirikisha Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, hakuna ushahidi juu ya hilo".

Alipoulizwa na waandishi wa habari:

Je, Dr. Mwakyembe anasumbuliwa na maradhi gani?


DCI alijibu kwamba:

"Kazi ya Jeshi la Polisi sio kuchunguza maradhi bali kuchunguza tuhuma, na baada ya uchunguzi wake kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Jeshi la Polisi limebaini kwamba tuhuma kwamba Dr. Mwakyembe amelishwa sumu hazina ukweli
."

Kwa watu waliotazama taarifa ya habari ya saa mbili usiku atakubaliana na mimi ya kuwa DCI Ametoa taarifa za uongo.

Kwanza alipoanza kuzungumzia swala la Dr . Mwakyembe hata SURA yake ilibadilika, ilidhahirisha machungu ambayo moyo wake ulikuwa unayapata hasa anapotoa maneno yale kwa taifa.(hapa inaonesha wazi alikuwa anasema kitu ambacho hata yeye anajua anapindua agano kwa kuzungumza uongo)

Wataalamu wa saikologia wanaweza kututolea ufafanuzi jinsi DCI Alivyokuwa na fake face,kuhusiana na Ugonjwa wa DR mwakyembe.
 
Wanajamvi,
Kuna jambo naomba tuliweke sawa.
Kwa baadhi yetu hatusemi kuwa Dr Mwakyembe kalishwa sumu au hakulishwa sumu.
Hoja ni kuwa madai yaliyotolewa kuhusu sumu ya Dr ni makubwa, mazito na yanatisha.
Majibu yaliyotolewa na serikali hayakidhi kabisa majibu ya tuhuma hizo kama yalivyowekwa.

Wasi wasi unatokana na jinsi serikali ilivyoshughulikia upande wa utetezi. Kwanza kulikuwa na kurushiana mpira kana kwamba serikali ni genge la watu wa kijiweni waisojua nani aseme nini na kwanini.
Hili halijitokezi katika mambo mengi tu isipokuwa kwa Dr Mwakyembe na pengine ingekuwa rahisi kama kungekuwa na ushirikiano wa pande husika.

Dr Mwakyembe hajakanusha madai yaliyotolewa na mzee Sitta. Maana yake ni kuwa hili jambo ni kama linavyoelezwa vinginevyo anafahamu lingeleta sintofahamu na uchonganishi mkubwa. Dr ni msomi aliyeerevuka kutambua hili hata kabla ya kusemwa.

Dr Mwakyembe ameshatoa madai kuhusiana na hatari ya maisha yake ambayo hayajashughulikiwa.
Hili linaonekana kuwa la muhimu zaidi serikali kujibu kuliko mpango wa 'kigaidi' wa kumuua kule Morogoro. Kuna nini?
Hatuna sababu ya kutafuta CIA kutujuza kuwa kuna kundi linalindwa iwe limefanya au halijafanya. Hapa ndipo panaondoa kabisa Imani juu ya jeshi la polisi. Nina maana ile integrity ,ethics and moral authority ya jeshi imekuwa compromised beyond repair.

Ndio maana tunahoji, kama si sumu ni nini? na je maelezo 'si sumu' yanatosha kuondoa mtitiriko wa matukio yanayoyaambana na uhai wa mtu. Ni kwanini serikali ichague masuala ya kujibu kuhusiana na mtu yule yule na matukio yanayoweza kuunganishwa kwa kamba moja. Kwanini sumu na si mauaji ya Morogoro

Mwisho, niwakumbushe kuwa Waziri mkuu aliyejiuzulu, Mkurugenzi wa PCCB waliwahi kutuambia kuwa uchunguzi umeonyesha kuwa hakuna uchafu Richmond. Kwasababu Watanzania tunapenda jibu noja 'hakuna' na tunaamini kuwa serikali imesema basi tukaimba wimbo huo kwa masham sham na nderemo. Ni hadi pale wanaojua kudadasi walipokuja na njia mbadala tumegeundua kuwa tumeingizwa chaka.

Hili la Mwakyembe litashindikana vipi!!!!! au hatujajifunza kusema ndio kwa jibu rahisi la 'hakuna'?
 
Mkuu Pasco,

Mtu akiwekewa sumu hawezi kujua kabla hajaambiwa na wataalam wa tiba. Unaweza kuwekewa sumu na usijue kwamba umewekewa sumu ila utaona unaanza kuugua na vipimo vya hospitali ndio ambavyo vinaweza kuthibitisha kwamba huyu mtu aliwekewa sumu na wanaweza ku-identify hata aina ya sumu aliyowekewa kama wana utaalam wa kutosha na vifaa vinavyoweza kugundua.
Litvinenko-aliwekewa Polonium-210, hakujua mpaka alipoenda hospitali na baadaye kuanza ku-trace alipita wapi na wapi na watu gani aliokutana nao. Kama unakumbuka vyema kwenye hilo sakata sehemu zote ambazo alipita siku hiyo ziliwekwa under investigation na kuzuwia watu wasiende. Sasa Mwakyembe ange-ripoti vipi bila kuwa na uhakika wa kulishwa/kuwekewa sumu?

Zama za Mkapa, Mh. John Pombe Magufuli aliwahi kuwekewa sumu na hakujua sumu hiyo aliipata wapi, alipelekwa haraka sana Ujerumani kwenda kutibiwa na baada ya hapo Mh. Pombe alipewa ulinzi na Jeshi la Polisi, walimpa bila kuomba. Maelezo ya Polisi yalikuwa kwamba mtu akishakumbwa na msukosuko kama huo huwezi kujua mtu aliyemfanyia hayo alikuwa na nia gani. Sikumbuki ulinzi huo ulidumu kwa muda gani.

Kwa kufuatilia mtiririko wa matukio ambayo Mwakyembe aliya-report, la kuhusu ajali kule Iringa na kutaka kuuawa Morogoro, kama jeshi la polisi linafanya kazi inavyotakiwa basi lingeweza kuanza kufuatilia nyendo zake hata bila kutangaza na hiyo ingewapatia jibu.

Tatizo la Jeshi la Polisi, linafanya kazi kwa maslahi ya kundi fulani la watu. Kibaya zaidi ni kwamba kwenye tuhuma za Mwakyembe, polisi na gari la polisi walikuwa ni wahusika/watuhumiwa. Sasa unapokuta kwamba Jeshi la Polisi linatuhumiwa, polisi inapoteza sifa ya kufanya uchunguzi ambao unaweza kutoa majibu sahihi. "Dili" kama hizo za kutumia magari ya polisi na polisi wenyewe kufanya jinai, mara nyingi huwa zina baraka za wakubwa wa Jeshi hilo, refer, case ya Zombe na askari wake.

Kwa hiyo Mwakyembe asingeweza kujua kabla hajaenda India kutibiwa. Muhimu ni kile ulichokisema kwamba as long as Manumba amesema Mwakyembe hajalishwa sumu, basi Mwakyembe akirejea kutoka India aje aseme kwamba report ya madaktari inasema nini.
!.
Mkuu Keil, asante kwa hii, umezama deep sana sina cha kuongeza. Media yetu ingekuwa serious ingetuma wato Appollo kuzungumza na Mwakiyembe na madaktari wake, na sio kumsubiri mpaka atakaporudi!.
 
Ngoja tusubiri kitakachosemwa na lile kundi la wabunge wanaojiita wapigania haki za wanyonge na wapinga ufisadi, waliahidi kutembea makanisani kutoa ushuhuda wa kuponywa kwa MWAKYEMBE lakini sijawaona tena!
 
Bora kukaa kimya kuliko kusema mapema hakulishwa sumu. Eti uchunguzi umefanywa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii!!!!!!! ha ha ha ileile ya blandina nyoni au mpya?
 
Nchi yetu bado inasafari ndefu sana, majibu kama haya yananipa imani kubwa kuwa hakuna utawala wa kisheria,

kwanza yapo mambo ya msingi ya kujiuliza kabla ya kujadili report ya manumba,

(1) dr. Mwakyembe ni nani katika taifa hili?

(2) kazi zipi ambazo amezifanya na zinatija ktk taifa letu?

(3)upi wajibu wa serikali kwa wana nchi wake?

(4)zipi ni kazi za police wa tanzania?

(5)majibu ya report tatu za dr. Mwekyembe alizopeleka police ni yapi?

(6)tangu mwanzo dr. Ametowa vielelezo na majina ya wahusika, je wangapi wamehojiwa juu ya swala hili?

(7)kama wapo wangapi wamefunguliwa mashtaka?

(8)kanumba anasema nn juu ya vyombo vya serikali vilivyotumika kwenye vielelezo juu ya malalamiko ya dr.?



Haya maswali ukiyatazama vizuri yanaweza kutufikisha kwenye point yetu kuu,kuwa hakuna utawala wa sheria,kanumba katowa majibu. Ningepata muda wa kuonana na kanumba swali langu kwake ni hili,je mpaka sasa dr. Mwakyembe anaimani na police?.
 
Kwani MWAKYEMBE ni tahira? Anashindwa nini kuueleza ukweli umma wa Tanzania? we unategemea muharifu akajiukumu au mtuhumiwa akajituhumu? Let him get what he diserves..................Je akiwa BUBU apoapo na ulemavu wa mikono yote apo tungeliweza msemea apart from that DCI manumba yupo sawa.....
 
Aibu tupu. Kwanza wao ndio watuhumiwa,watafanyaje uchunguzi tena.Tulitegemea jibu hili.Isipokuwa natoa angalizo,leo wameshika mpini,kesho watashika makali.
Hii ni kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na vyombo vya habari mchana wa leo. Katika maelezo yake, DCI anasema kwamba:

"Kutokana na uchunguzi wa kipolisi ulioshirikisha Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, hakuna ushahidi juu ya hilo".

Alipoulizwa na waandishi wa habari:

Je, Dr. Mwakyembe anasumbuliwa na maradhi gani?


DCI alijibu kwamba:

"Kazi ya Jeshi la Polisi sio kuchunguza maradhi bali kuchunguza tuhuma, na baada ya uchunguzi wake kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Jeshi la Polisi limebaini kwamba tuhuma kwamba Dr. Mwakyembe amelishwa sumu hazina ukweli
."
 
Mwakyembe, si alitibiwa India!!, nilitegemea kuletewa ripoti ya Uchunguzi na majibu ya vipimo kutoka India na siyo Wizara ya Afya ambao walishindwa: na muda wote walikuwa wapi mpaka wanakuja kutoa taarifa leo??
 
Hebu ngojeni; hivi nyi Mwakyembe mnamjua au mnamsikia tu?! Mwakyembe si mtu wa kusemewa na wana-JF wala huyo Sitta! Mwakyembe ni mwanasheria aliyekomaa, jasiri na asiyeogopa chochote kwa kile anachoona ni haki! Wakari Mkapa anauza NMB, Mwakyembe alikuwa ni mjumbe wa bodi na kv hakutaka kuhusika kwenye dhambi ile, Mwakyembe alichukua uamuzi wa kujiudhuru kama ambavyo alifanya CEO wa wakati wakati ule. Mwakyembe ni mpiganaji awezae kupigana mwenyewe bila ya kuhitaji msaada wowote! Endapo angelishwa sumu; Mwakyembe asingeogopa kusema ukweli!!! Kwa ujasiri alionao Mweakyembe; nitashangaa kwanini asifungue mashitaka dhidi ya washukiwa!!! By the way; hivi nyie watu mwaijua sumu au mwafanya mchezo?! Kwa upako gani alionao Mwakyembe hata sumu ishindwe kumwondoa?! Kama ambavyo wadau wanasema walitarajia kauli hii toka kwa jeshi la polisi; hiki ndicho hasa alichokuwa anakitaka Sitta! Kwamba, auaminishe umma kwamba Mwakyembe amelishwa sumu; ili hata pale itakapotolewa ripoti rasmi kwamba hakulishwa sumu, basi watu waamini kwamba ripoti hiyo imechakachuliwa kwavile tayari walishajengwa kisaikolojia kwamba alilishwa sumu!! By the way, kama issue ni Richmond; Mwakyembe alikuwa Mwenyeketi tu wa ile kamati na kama kuna watu ambao wamekuwa wakipiga kelele sana kuhusu Richmond, Mwakyembe si mmoja wao! Role ya Mwakyembe kwenye suala la Richmond iliisha pale aliposoma ripoti ile bungeni na siku chache baadae tena pale alipolazimika kufanya hivyo. Hata hivyo, bado kulikuwa na watu ambao waliendelea kuishupalia zaidi issue ya Richmond kuliko huyo Mwakyembe! Ole Sendeka, Anne Killango, Samuel Sitta (ingawaje huyu alikua anazumgumzia kimaslahi yake zaidi), Zitto na Mnyika ndio watu ambao naweza kusema hakuacha issue ile itulie na wala sio Mwakyembe! Ni kweli, Mwakyembe ndie alikuwa Mwenyekiti, lakini mwiba uliokwama shingoni mwa wana-Richmond ni ule uliotokana na wapiganaji kutotaka kuiacha issue hiyo iishe hivi hivi....!!! So, WHY MWAKYEMBE?! Hapa hakuna cha sumu wala nini, na kama ni sumu wala si ya kwamba kuna mtu alitaka kumwua....!!!!!

Pamoja na hayo, shime kwa Rais Kikwete.....juzi kwenye salamu zangu za Valentine nilikueleza kuhusu ni namna gani viongozi wa serikali yako wanavyotoa kauli tata kiasi naweza ku-conclude kwamba ni WAONGO, WAZUSHI, WAFITINI......List yangu iliwataja tu Anna Makinda, Mizengo Pinda, Salva Rweymamu bila kukusahau wewe mwenyewe. Kwamba, angalau mmoja katika listi hiyo atakuwa ni mwongo mkubwa na mzushi. List hiyo sasa imeongozeka....Ama Samuel Sitta au DCI Manumba, lazima mmoja wapo hapo atakuwa ni mzushi na mwongo wa kutupwa!!! NI hatari kuwa na watendaji wakuu ambao ni waongo na wazushi wasio na mfano. Katika list hiyo, ni lazima angalau mmoja awajibike ama kuwajibishwa kutokana na dhambi ya ya uongo na uzushi wa kupitiliza.
 
Hahaha, huyu mwalimu wa Pasco ni mnafiki sana:-

1. Alipika report na kujifanya kuwa ameisoma nusu bungeni na nusu ni siri ya kamati, kumbe kamba tupu
2. Alidai kuwa once akirudi kutoka India ataweka mambo hadharani lakini kaja kakaa kimya, huyu ni mnafiki hatari...

`sasa nadhani watanzania wote tuko kwenye page moja, safi sana Manumba na Wizara ya Afya....hahahhaha....

Hahahahaaaa,...unachezea sirikali ww....sita sasa apelekwe segereaa kwa kosa la uchochezi
 
Serikali makini itamshughulikia Sitta haraka iwezekanavyo, scrap him his ninisterial positions na kumpandisha kizimbani kwa kosa la "uchochezi"!.
Mkuu Nguruvi3 kwenye hili la sumu, mwisho wa uwezo wa serikali kusema sio sumu ndio hapo. Serikali haipaswi kusema ilichunguza nini na ni kwa vigezo gani waliend up kuhitimisha sio sumu, japo pia nina doubt na uwezo wa kiteknolojia kufanya uchunguzi wa sumu kama polonium!.
Ile hoja kuwa alishalalamika huko nyuma bali polisi hawakufanya chochote its still valid, polisi walipaswa wauambie umma wa Watanzania why ili wengi wenu msio mwelewe vizuri Mwakyembe what he is really is!.
Tuhuma za Mwakiyembe kutishiwa kuuwawa,sasa hizi tuhuma za sumu si angalau wamejibu!, si wangeweza kukaa kimya na wasiulizwe chochote kama kawaida yao!.
Kuusema ukweli sisi waandishi wa Tanzania ni wavivu na sio wachokonozi!. Waandishi wanaoripoti issues za polisi, kazi yao ni kumeza tuu kila wanacholishwakwenye zile daily press co. zao badala kuuliza serious issues.
Mkuu Pasco, kwa kusema serikali itamshughulikia Sitta huoni hapo tayari umeshakua upande! (Quote 1). Na kwanini imshughulikie Sitta kwa uchochezi na si Dr Mwakyembe kwa madai 'fake'(Quote yako 2). Halafu unasema waandishi wa Tanzania si wachokonozi, sasa mkuu kwa jinsi ulivyofikia conclusion ya uchochezi wa Sitta na 'fake' ya mauaji ya Mwakyembe huoni una ji-limit kuchokonoa kama waandishi wa Tanzania?

Bila kuliangalia jambo hili kwa mizania iliyo sawa tutaishia kuchukua upande na kusahau kuwa sisi ni watanzania na kama hatutajenga utamaduni wa kuambizana ukweli, kutafuta ukweli na kuweka wazi ukweli, ipo siku sisi au nduguze watakuwa victims kwa namna moja au nyingine
 
Haya Bwana naona unajitahidi kweli.
Pasco, nadhani huko serious. Unafanya mzaha nadhani, unadhani ingekuwa rahisi hivyo hata yeye mwenyewe angesema sema ovyo? Tafadhali Mkuu ila tuombeane uzima tu. Bahari imechafuka, tsunami iko njiani.
Mimi ninawaombea wale tu walio na nia nzuri na nchi yetu, walio na nia ya kuoikoa nchi kutoka kwenye makucha ya MAFISADI, basi!
 
Ukiona watu wanaanza kujisafisha hivyo ujue ndio kiyama yao iko jirani!
Mzee 6 hawezi kukubali kudhalilishwa na maneno ya uwongo hivyo!
Hivi wakuu mnaweza kuweka KAULI YA SITA hapa, ili tuende sambamba katika hili?
 
kuna kitu kinafichwa na pande zote mbili.Kuna kitu kinamkwamisha Mwakyembe asiseme kuhusu ugonjwa wake na vilevile kuna kitu kinaikwamisha serikali isiseme kila kitu kuhusu ugonjwa wa Mwakyembe
ni muda pekee ndiyo utatufumbulia mlinganyo huu
 
Back
Top Bottom