Aliyewekewa sumu ni Mwakyembe hajaripoti polisi kuhusu kuwekewa sumu. Aliyepayuka hadharani kuhusu jinai ya sumu ni jirani (Sitta). Polisi wamechukua maelezo ya Sitta na kufanya uchunguzi, wakakuta hakuna jinai ya sumu!. Mwakyembe mwenyewe wala familia yake hawajalalamikia sumu!. Kama ambavyo mkeo hajalalamikia polisi kuhusu kichapo alichokula!.
Mwakiyembe anaumwa, hajalalamikia kupewa sumu. Jirani ndio anae eneza uvumi wa simu ili kuwanyooshea kidole mahasimu wake wa kisiasa!. Sasa kwa vile issue ilikuwa ni kupewa sumu, imethibitika sio sumu!. Mwambieni jirani sasa na atoe uthibitisho, ila its high time Dr. akirudi toka matibabu ya India awaambie Watanzania ukweli wa anachoumwa!.
Mkuu Pasco,
Mtu akiwekewa sumu hawezi kujua kabla hajaambiwa na wataalam wa tiba. Unaweza kuwekewa sumu na usijue kwamba umewekewa sumu ila utaona unaanza kuugua na vipimo vya hospitali ndio ambavyo vinaweza kuthibitisha kwamba huyu mtu aliwekewa sumu na wanaweza ku-identify hata aina ya sumu aliyowekewa kama wana utaalam wa kutosha na vifaa vinavyoweza kugundua.
Litvinenko-aliwekewa Polonium-210, hakujua mpaka alipoenda hospitali na baadaye kuanza ku-trace alipita wapi na wapi na watu gani aliokutana nao. Kama unakumbuka vyema kwenye hilo sakata sehemu zote ambazo alipita siku hiyo ziliwekwa under investigation na kuzuwia watu wasiende. Sasa Mwakyembe ange-ripoti vipi bila kuwa na uhakika wa kulishwa/kuwekewa sumu?
Zama za Mkapa, Mh. John Pombe Magufuli aliwahi kuwekewa sumu na hakujua sumu hiyo aliipata wapi, alipelekwa haraka sana Ujerumani kwenda kutibiwa na baada ya hapo Mh. Pombe alipewa ulinzi na Jeshi la Polisi, walimpa bila kuomba. Maelezo ya Polisi yalikuwa kwamba mtu akishakumbwa na msukosuko kama huo huwezi kujua mtu aliyemfanyia hayo alikuwa na nia gani. Sikumbuki ulinzi huo ulidumu kwa muda gani.
Kwa kufuatilia mtiririko wa matukio ambayo Mwakyembe aliya-report, la kuhusu ajali kule Iringa na kutaka kuuawa Morogoro, kama jeshi la polisi linafanya kazi inavyotakiwa basi lingeweza kuanza kufuatilia nyendo zake hata bila kutangaza na hiyo ingewapatia jibu.
Tatizo la Jeshi la Polisi, linafanya kazi kwa maslahi ya kundi fulani la watu. Kibaya zaidi ni kwamba kwenye tuhuma za Mwakyembe, polisi na gari la polisi walikuwa ni wahusika/watuhumiwa. Sasa unapokuta kwamba Jeshi la Polisi linatuhumiwa, polisi inapoteza sifa ya kufanya uchunguzi ambao unaweza kutoa majibu sahihi. "Dili" kama hizo za kutumia magari ya polisi na polisi wenyewe kufanya jinai, mara nyingi huwa zina baraka za wakubwa wa Jeshi hilo, refer, case ya Zombe na askari wake.
Kwa hiyo Mwakyembe asingeweza kujua kabla hajaenda India kutibiwa. Muhimu ni kile ulichokisema kwamba as long as Manumba amesema Mwakyembe hajalishwa sumu, basi Mwakyembe akirejea kutoka India aje aseme kwamba report ya madaktari inasema nini.